Kwa dhuluma ambayo Jakaya Kikwete alimfanyia Mzee Lowassa, ataumaliza uzee wake bila amani

Kwa dhuluma ambayo Jakaya Kikwete alimfanyia Mzee Lowassa, ataumaliza uzee wake bila amani

Madaraka makubwa, usipokuwa na hekima, hasa hekima ya Mungu, yanalevya. Na ukikosa hekima unaweza kudhania kuwa wewe ni kila kitu, kwa sababu hakuna wa kukuhoji wala kukuadhibu.

Mathalani madaraka ya Rais wa Tanzania, anaweza kuyatumia vyovyote apendavyo, hata kuua, akitaka, na asihojiwe wala kushtakiwa mahali popote Duniani.

Lakini hawa watawala, kwa kukosa hekima huwa wanaamini kuwa hawawezi kuhojiwa Duniani, ahera wala hata na nafsi zao.

Marehemu Lowasa, aliuishi uaminifu kwa urafiki wake na Kikwete, lakini Kikwete alimsaliti na kumdhulumu rafiki yake.

Lowasa alijitoa kwa nguvu na moyo wake wote katika kuhakikisha Kikwete anakuwa Rais. Hata ndege iliyompeleka Kikwete Dodoma wakati anautafuta Urais, naambiwa iligharamiwa na Lowasa.

Serikali ya Kikwete ipopata msukosuko kutokana na kashfa ya Richmond, huku Msabaha akitamka wazi kuwa zigo la Richmond halikuwa lake kama waziri, kwa sababu wakati wote aliwasiliana na Serikali kupitia Waziri Mkuu, na hivyo kama kuna makosa, basi ni makosa ya Serikali nzima, Lowasa alimwendea Kikwete kumweleza kuwa yeye ameamua kujiuzulu ili kuilinda Serikali. Kikwete alikataa ombi la Lowasa kujiuzulu, lakini marehemu alishikilia msimamo wake, akiamini ndiyo njia ya kuiokoa Serikali ya Kikwete isidondoke, na pengine ipate imani ya aina fulani toka kwaWabunge.

Katikati ya safari yao, tofauti na makubaliano yao ya awali kuwa yeye marehemu amsaidie Kikwete kuwa Rais 2005, halafu Kikwete amsaidie marehemu kuutafuta Urais mwaka 2015, Kikwete alimtosa rafiki yake na kutaka Urais uende kwa mdogo wake.

Kikwete akifahamu wazi kuwa hakukuwa na mgombea yeyote ndani ya CCM na hata nje, wa kumzidi marehemu, akatumia madaraka yake, kuliondoa jina la Lowasa, lisipelekwe kwenye mkutano mkuu wa CCM.

Huku zaidi ya wajumbe 2,000 wa mkutano mkuu wa CCM wakiwa wamejiandaa kumpigia kura Lowasa RIP, kwa mshangao mkubwa wakaambiwa jina la Lowasa halipo.

Wajumbe wa mkutano mkuu, baada ya kuujua ukweli namna Kikwete alivyodhulumu haki ya rafiki yake wa awali ili Urais uende kwa mdogo wake, wakaitana nje, wakaambizana kuwa wale wote waliokuwa wamejiandaa kumchagua Lowasa, kura zao wampe mgombea aliyeonekana dhaifu kuliko wote, na ambaye amewekwa na Kikwete kama chambo. Ndipo ushindi ulipomwangukia Magufuli RIP.

Lowasa hakukata tamaa, aliamua kugombea nafasi ile ile kupitia CHADEMA. Sote tunayakumbuka mafuriko ya Lowasa. Lakini Kikwete akiwa amefunga mkataba wa kudumu wa kumdhulumu marehemu, huku majumuisho ya kura kutoka vituoni yakionesha wazi kuwa Lowasa alikuwa anaongoza kwa kura nyingi, aliwatuma Polisi kwenda kuvamia kituo cha ujumlishaji kura za Lowasa, wakapora computers zote, na kuwaweka mahabusu wajumlishaji wa kura.

Watanzania, nyakati hizi, tunaombeleza msiba wa Edward Lowasa, ambaye kiuhalisia ndiye aliyechaguliwa na wananchi kuwa Rais wa JMT mwaka 2015.

Lakini ni Kikwete pia, ndiye aliyemdhulumu ushindi wa Urais wa Zanzibar, Maalim Seif RIP.

Dhuluma ya Kikwete kwa marehemu hawa, itaitafuna nafsi yake mpaka siku yake ya mwisho. Madaraka yalimlevya, akaisahau haki. Akasahau kuwa madaraka ni kitu cha kuja na kupita, lakini haki huamua maisha yako ya leo na ya umilele.

Nina hakika, hata wakati huu wamsiba, watu watamtazama Kikwete kwa kujiuliza maswali mengi sana. Je, anaupenda sana na kuisikitikia mwili wa marehemu kuliko nafsi ya marehemu ilipokuwa hai?

Ndugu zangu, tutendeni haki ili tuwe na amani hadi siku za uzee wetu.

Kwa heri Lowasa, mtu uliyependwa na Watanzania walio wengi, ukadhulumiwa na wachache.

Mungu wa rehema, tunakuomba umtuze mja wako kwa raha ya milele kwani aliyathamini uhai wa wengine kuliko madaraka yake binafsi.
Dua la Kuku. Elewa kuwa watu wabaya ndio hudumu muda mrefu na kula nchi sana kuliko watu wema
 
Madaraka makubwa, usipokuwa na hekima, hasa hekima ya Mungu, yanalevya. Na ukikosa hekima unaweza kudhania kuwa wewe ni kila kitu, kwa sababu hakuna wa kukuhoji wala kukuadhibu.

Mathalani madaraka ya Rais wa Tanzania, anaweza kuyatumia vyovyote apendavyo, hata kuua, akitaka, na asihojiwe wala kushtakiwa mahali popote Duniani.

Lakini hawa watawala, kwa kukosa hekima huwa wanaamini kuwa hawawezi kuhojiwa Duniani, ahera wala hata na nafsi zao.

Marehemu Lowasa, aliuishi uaminifu kwa urafiki wake na Kikwete, lakini Kikwete alimsaliti na kumdhulumu rafiki yake.

Lowasa alijitoa kwa nguvu na moyo wake wote katika kuhakikisha Kikwete anakuwa Rais. Hata ndege iliyompeleka Kikwete Dodoma wakati anautafuta Urais, naambiwa iligharamiwa na Lowasa.

Serikali ya Kikwete ipopata msukosuko kutokana na kashfa ya Richmond, huku Msabaha akitamka wazi kuwa zigo la Richmond halikuwa lake kama waziri, kwa sababu wakati wote aliwasiliana na Serikali kupitia Waziri Mkuu, na hivyo kama kuna makosa, basi ni makosa ya Serikali nzima, Lowasa alimwendea Kikwete kumweleza kuwa yeye ameamua kujiuzulu ili kuilinda Serikali. Kikwete alikataa ombi la Lowasa kujiuzulu, lakini marehemu alishikilia msimamo wake, akiamini ndiyo njia ya kuiokoa Serikali ya Kikwete isidondoke, na pengine ipate imani ya aina fulani toka kwaWabunge.

Katikati ya safari yao, tofauti na makubaliano yao ya awali kuwa yeye marehemu amsaidie Kikwete kuwa Rais 2005, halafu Kikwete amsaidie marehemu kuutafuta Urais mwaka 2015, Kikwete alimtosa rafiki yake na kutaka Urais uende kwa mdogo wake.

Kikwete akifahamu wazi kuwa hakukuwa na mgombea yeyote ndani ya CCM na hata nje, wa kumzidi marehemu, akatumia madaraka yake, kuliondoa jina la Lowasa, lisipelekwe kwenye mkutano mkuu wa CCM.

Huku zaidi ya wajumbe 2,000 wa mkutano mkuu wa CCM wakiwa wamejiandaa kumpigia kura Lowasa RIP, kwa mshangao mkubwa wakaambiwa jina la Lowasa halipo.

Wajumbe wa mkutano mkuu, baada ya kuujua ukweli namna Kikwete alivyodhulumu haki ya rafiki yake wa awali ili Urais uende kwa mdogo wake, wakaitana nje, wakaambizana kuwa wale wote waliokuwa wamejiandaa kumchagua Lowasa, kura zao wampe mgombea aliyeonekana dhaifu kuliko wote, na ambaye amewekwa na Kikwete kama chambo. Ndipo ushindi ulipomwangukia Magufuli RIP.

Lowasa hakukata tamaa, aliamua kugombea nafasi ile ile kupitia CHADEMA. Sote tunayakumbuka mafuriko ya Lowasa. Lakini Kikwete akiwa amefunga mkataba wa kudumu wa kumdhulumu marehemu, huku majumuisho ya kura kutoka vituoni yakionesha wazi kuwa Lowasa alikuwa anaongoza kwa kura nyingi, aliwatuma Polisi kwenda kuvamia kituo cha ujumlishaji kura za Lowasa, wakapora computers zote, na kuwaweka mahabusu wajumlishaji wa kura.

Watanzania, nyakati hizi, tunaombeleza msiba wa Edward Lowasa, ambaye kiuhalisia ndiye aliyechaguliwa na wananchi kuwa Rais wa JMT mwaka 2015.

Lakini ni Kikwete pia, ndiye aliyemdhulumu ushindi wa Urais wa Zanzibar, Maalim Seif RIP.

Dhuluma ya Kikwete kwa marehemu hawa, itaitafuna nafsi yake mpaka siku yake ya mwisho. Madaraka yalimlevya, akaisahau haki. Akasahau kuwa madaraka ni kitu cha kuja na kupita, lakini haki huamua maisha yako ya leo na ya umilele.

Nina hakika, hata wakati huu wamsiba, watu watamtazama Kikwete kwa kujiuliza maswali mengi sana. Je, anaupenda sana na kuisikitikia mwili wa marehemu kuliko nafsi ya marehemu ilipokuwa hai?

Ndugu zangu, tutendeni haki ili tuwe na amani hadi siku za uzee wetu.

Kwa heri Lowasa, mtu uliyependwa na Watanzania walio wengi, ukadhulumiwa na wachache.

Mungu wa rehema, tunakuomba umtuze mja wako kwa raha ya milele kwani aliyathamini uhai wa wengine kuliko madaraka yake binafsi.
Nitakuunga mkono kwa dhuluma ya uaminifu lakini si dhuluma ya kura za 2015. 2015 Lowasa alipigwa na CCM ilishinda kwa kishindo. Ingawa ushindi ulikuwa wa magine ndogo. So acha kupotosha. Maswala ya urafiki wao hapo nakuunga mkono. Ila kura za 2015 Dr John Pombe Joseph Magufuli alishinda kwa kishindo.
 
Hata JK kwenda Dodoma na majina matano na Lowassa kutokuwepo ni mpango wa Mungu pia, labda hujui namna Mungu anavyofanya kazi kupitia sisi katika maisha yetu ya kila siku.

Hujawahi kusikia hadithi mbalimbali za namna Mungu anavyowaokoa watu wanaotaka kusafiri na ndege wanakutana na vikwazo mbalimbali kutoka kwa familia zao wenyewe halafu baada ya ndege kuanguka ndio wanaanza kumshukuru Mungu kwa kuwaokoa na kifo?.

Baadhi ya watu walikwepa kifo siku ile ya September 11 kule New York wakiwa wamekwenda kwanza kuwaacha shuleni watoto wao saa mbili asubuhi na wakati ndege ya kwanza inalipuka saa mbli na dakika 48 asubuhi walikuwa bado wapo njiani wakienda ofisini, hivyo ndivyo Mungu anavyofanya kazi.

Apumzike kwa amani Lowassa, amefanya mengi lakini hakuna sababu ya kuhuzunika kuukosa Urais, hii ni nchi yenye watu milion 63 haupo uwezekano kila mwenye ndoto za kuingia ikulu aje siku moja aitimize ndoto yake hiyo.
Uliyoyasema ni sahihi, kuwa Mungu hutenda kazi kwa namna ambayo wakati fulani hata hatuifikirii. Ndiyo maana tunaambiwa tushukuru katika kila jambo.

Siamini kama kuna anayesikitika kwa nini Lowasa hakuwa Rais, bali watu wanasikitikia unafiki na dhuluma. Na Mungu kutenda kazi kwa namna tofauti tofauti, haiondoi ukweli kuwa unafiki na dhuluma ni ushetani. Na pia tukumbuke kuwa hata shetani hutenda kazi kwa namna tofauti tofauti kwa kuangalia udhaifu wako ulipolala. Kama udhaifu wako ni tamaa ya madaraka, basi unaweza kukuingia kupitia hiyo tamaa yako, ndiyo maana wengine wanafanya dhuluma mbalimbali ikiwemo hata kuua. Wanawaua wapinzani wao kisha kwa unafiki na ushetani wao, wanakimbilia kusema ama ni mapenzi ya Mungu, ama Mungu hakupenda awe kiongozi, n.k.
 
Uliyoyasema ni sahihi, kuwa Mungu hutenda kazi kwa namna ambayo wakati fulani hata hatuifikirii. Ndiyo maana tunaambiwa tushukuru katika kila jambo.

Siamini kama kuna anayesikitika kwa nini Lowasa hakuwa Rais, bali watu wanasikitikia unafiki na dhuluma. Na Mungu kutenda kazi kwa namna tofauti tofauti, haiondoi ukweli kuwa unafiki na dhuluma ni ushetani. Na pia tukumbuke kuwa hata shetani hutenda kazi kwa namna tofauti tofauti kwa kuangalia udhaifu wako ulipolala. Kama udhaifu wako ni tamaa ya madaraka, basi unaweza kukuingia kupitia hiyo tamaa yako, ndiyo maana wengine wanafanya dhuluma mbalimbali ikiwemo hata kuua. Wanawaua wapinzani wao kisha kwa unafiki na ushetani wao, wanakimbilia kusema ama ni mapenzi ya Mungu, ama Mungu hakupenda awe kiongozi, n.k.
Any way labda kwasababu humu hatujuani status zetu za wasifa wa maisha yetu.
Kiuhalisia huenda haya makubaliano yanayo semwa hata haya kuwepo bali ni hear say tu za kutengenezwa ili kuongeza umaarufu wa mtu flani.
Na hata kama ni kweli nadhani watu hawa wawili walifahamiana kiundani zaidi kuliko sisi tunavyo Dhani.
Pia maisha yetu sisi binadamu tuna pambana sana kufikia mafanikio lkn ukweli unabaki kuwa muamuzi wa Mwisho ni Mwenyezi Mungu pekee ndio huamua wapi tufikie
 
Kwamba Lowassa 'Urais ulikuwa ni Haki yake kutoka Kwa Mungu' kwahiyo kadhulumiwa?

Cha ajabu wanaolia Lia na hili ni Chadema. Kama Lowassa aliona CCM wamemdhulumu why alirudi CCM?
Kama alisamehe why Chadema inawauma sana?

Lowassa hii Haki ya kuwa Rais ilitoka wapi?si na Kambona nae watoto wake watadai Nyerere alimdhulumu Urais?watoto wa Sokoine je waseme Baba Yao aliuwawa ili asiwe Rais?

Mijitu mizima inalialia na consipiracy theory za kitoto kabisa
Hivi mlutheri anaweza kuwa rais wa tanzania mkuu
Maana naona ni wakatoliki na waislam kutoka bakwata tu ndy marais

Ova
 
Waswahili wa Pwani sio watu wakuwaamini.

Lowasa alifanya kosa kubwa kumuamini mswahili.
Wale washkaji kitambo na wanajuana
Mbona nakumbuka kijiwe chao kilikuwa pale peace bar mwananyamala miaka hiyo na walikuwa wanakutana sana pale

Ova
 
JK kama mtu ana mapungufu yake, hawezi kukosa. Huwezi kuongoza mamilioni ya watu ukakosa matatizo.

Lakini, haya mambo mengi hatuna hata uhakika kama yametokea hivyo yanavyosemwa yalitokea, na kama yametokea kweli, ni JK aliyeamuru ama watu wa chini yake tu wamejipendekeza kufanya mambo bila amri.

Sitaki kuongea mengi, lakini nataka kusema kwamba ukiongea katika network za kifamilia, halafu ukisikiliza stories za kwenye magazeti na vijiweni, stories nyingi ni tofauti sana. Tatizo viongozi wa Bongo hawana uwazi. Mimi saa nyingine naongea na hao watoto wa kina Warioba na Lowassa, naona dah, kazi yetu kupata story straight ni kubwa sana.

Kuna mambo nashindwa hata kukubishia kwa sababu sitaki kutengeneza mzozo ambao hauwezi kuwa settled one way or another hapa.

Ukweli utabaki kuwa, kipindi cha JK ni kipindi ambacho watu walikuwa huru sana kusema. Kipindi pekee cha kukilinganisha na kipindi cha JK ni kipindi cha Mzee Mwinyi cha Ruksa.

Mambo mengine mtamlaumu JK wakati JK hahusiki moja kwa moja na wala hajaagiza mtu.

Nitakupa mfano mmoja ninaoujua binafsi unaoonesha mambo mengine mnaweza kumpa lawama JK kuwa kaamuru, wakati hata hakuamuru na in fact yupo against nayo.

Kipindi cha JK Jamiiforums ilikuwa moto sana. Kipindi hicho FMES (RIP) na wenzake waliokuwa serikalini walikuwa wanapata sana nondo za ndani ya serikali na kuzimwaga hapa, watu wakawa wanachambua mambo na kuinanga serikali kwa style ya "Kumkoma Nyani Giladi". Wakongwe wa JF watakumbuka.

Sasa, ikatokea Polisi fulani wakubwa wakawa wanataka sifa, wakamkamata mkuu Maxence Melo. Wakamfunga.

Kusikia hivyo, tukalianzisha bonge la timbwili kimataifa. Tukawatafuta "The Committe to Protect Jouranalists" www.cpj.org , tukawatafura Human Rights Watch, wakalianzisha timbwili kwenye vyombo vya habari vya kimataifa. Shout out to Mimi Mwanakijiji kwa kazi kubwa aliyoifanya.

Tanzania ikawa ina trend vibaya kwamba inaminya uhuru wa habari.

JK kusikia hivyo, akasema kwa nini mnawasumbua hawa vijana wa dotcom ambao hawana hata impact kwenye utawala wangu? Waachieni tu, msiwabugudhi. Msinichafulie jina la nchi yangu bila sababu.

Mara moja Max akaachiwa.

Sasa, kwa mtu ambaye hakuwa karibu na ile story, angeweza kujua kuwa JK aliamuru Max ashikwe, halafu ikaonekana issue imeleta negative press kimataifa, akaamuru Max aachiwe.

Kumbe, Max alivyoshikwa hata JK hakujua.

Mambo mengine tunaweza kumlaumu JK kwa sababu watu wa chini wamejipendekeza tu. JK mwenyewe hata hakuyapenda.


Hii ni Kama nimeiona ikijirudia 2016-2021.


Inawezekana kabisa anaekalia kiti kikuu kutokua na taarifa ya mambo mengi na mengi mengine akasaidiwa “kuamua na outcome ya mwisho kabisa kwetu sisi watazamaji ikaonekana vyovyote vile iwavyo muhusika mkuu ni mkaaji wa kiti kikuu.

Yawezekana pia ndicho kilimkuta Nyerere mpaka akatangaza “kung’atuka, vijana walimchezea rafu za gizani nyingi.

Mwinyi yeye aliona isiwe tabu, “Ruksa era ikazaliwa wakati wake.

Pia inaweza kutoa mwanga ni kwanini Mkapa hakucheka na nyani. (Alikaa mbele mwenyewe)
Ukweli na Uwazi.
 
Mleta mada una ushahidi wa hilo? Ukikamatwa utaenda mahakamani kujibu nini haliyakua ushahidi huna!
 
Hoja ya kuwa Kikwete alikataa Lowassa asijiuzulu sio kweli. Lowassa alijiuzulu baada ya kuona hana support ya Rais!!
Hata kama asingejiuzuru na kuendelea na uwaziri mkuu lile doa la ile kashfa lisingeondoka !
Hata hivyo uzito wa kashfa ile na jinsi ingeathiri chama ungeamuliwa kwa kura za wanachama na sio kiongozi mmoja kwa kutumia mamlaka ya uenyekiti! Kikwete angeacha kura za wajumbe ziamue kama Lowassa angefaa kupeperusha bendera au la!’ Mkwere kwa fitina zake akaingia na majina aliyetaka yeye wakiwemo Chawa wake watatu ; January Makamba, Asha Rose Mtengeti na Membe!!
Hao wengine Magufuli na Amina kwake walikuwa wasindikizaji!
Amina should have been the de facto vice presidential pick but in her campaign speech she alluded to be pro Lowassa hence again Kikwete used his influence to pick Samia instead of Amina as is always the case! Amina missed the Vice presidential slot simply by mentioning Lowassa’s name.


Hapa inadhihirisha nguvu za Mwenyekiti wa Chama Mwaka huo 2014.


Ila sasa nashangaa jambo moja, hawa wanachama wa Wanamtandao mbona hili la presidential candidates wa 2015 ni Kama lilifanyika kwa zima moto?!

Kwanini na wakati “masterplanner na “kingmaker walikua na more than 5 yrs za kujiandaa na walikua jikoni kabisa na wao ndio walikua wapishi rasmi wa mambo mengi nyakati hizo?

Ama hiyo Richmond scandal na kujiuzulu kwa member muhimu wa wanamtandao kulipindua meza na plans zote?

Hivi kipi kilitangulia, kujivua Gamba ama Kujiuzulu uwaziri mkuu?

Lowassa aliposema “mheshimiwa speaker, tatizo ni uwaziri mkuu..” alimaanisha nini haswa?
 
mkuu unamwonea imani Lowasa vp ufisadi wake alioufanya kutajirisha familia yake...hutuonei huruma sisi watanzania!!!
au na wewe family member
Kuna aliye msafi kwenye huo mfumo? Humo kila mtu anakula kulingana na urefu wa kamba yake humo.
 
Back
Top Bottom