Uchaguzi 2020 Kwa hali hii, Membe anaweza kurudi CCM kabla hata kampeni hazijaisha

Uchaguzi 2020 Kwa hali hii, Membe anaweza kurudi CCM kabla hata kampeni hazijaisha

Kumbuka vyama vya upinzani havina rasilimali vya umma . Kwa hiyo udhaifu unaouona ni hali halisi ya nchi .
Wanazo resources ambazo haziko organized. Dawa yao ni kuungana,ila kwa style hii ya kila mtu kugombea minofu michache kwenye sinia watasubiri Sana.
 
Yaani nashukuru cdm waligoma kuungana na huyu mzee wa ccm, vinginevyo hii idadi ya watu anaopata Lisu, ccm wangesema cdm ilikuwa imekufa, lakini uwepo wa Membe ndio umeleta watu. Kuna watu huwa ninawaambia kabisa hata mafuriko ya Lowassa hayakumfuta Lowassa, bali Lowassa ndio alifuata kundi la mabadiliko ambalo liko cdm. Iwapo Lowassa angekosea ile 2015 aende chama kingine nje ya cdm, angepata aibu kuliko hii ya Membe. Hata sifa wanayopata ACT ni kwa ajili ya uwepo wa Maalim Seif huko Zanzibar. Wafuasi wa upinzani wa kweli wako cdm kwa huku bara. Ile nyomi ya Membe kule Zanzibar alitembelea nyota ya Seif, ukweli huu Zito alikuwa anaujua ndio maana alikuwa anang'ang'ania muungano na cdm huku bara.
Umeongea point mkuu, nimekuwa nikiwauliza ACT wana nini cha kunganisha na CDM hata bendera tuu mtaani hakuna, vilevile malengo ya kuanzishwa kwa ACT nacho ni kikwazo tosha.
 
Wanazo resources ambazo haziko organized. Dawa yao ni kuungana,ila kwa style hii ya kila mtu kugombea minofu michache kwenye sinia watasubiri Sana.
Angalia; unaposikia nchi flani vyama vimeungana na kukitoa chama tawala madarani hesabu zao huwa hivi, chama A kina wanachama wengi mfano mikoa ya kusini, chama B kiko zaidi Mikoa ya magharibi, chama C kiko mikoa ya kati na chama D kiko mikoa ya kasikazini na chama tawala chenyewe kinajitapata kwa kuwa na wanachama nchi nzima, sasa hivyo vyama ABCD vikiungana ni rahisi sana kukitoa chama tawala, kwa nchi yetu mazingira hayako hivo.Haya niambie unadhani ACT au CUF ni wapi imekita mizizi??
 
Mmmmm mbona kama nyepesi nae katoka mkuku alfajiri kweupe kamuacha Mzee jasusi mbobezi hana hata jukwaa. Sijui wameliunda faster 😺😺
 
Sijaelewa Ni kuwa ACT hawampi support ya kutosha au VIP?

Yaani Hili ndio Liwe jukwaa la mgombea Urais kweli? Tena aliwahi kuwa Waziri wa mambo ya nje?
Haya maisha yanaweza kumshinda kabla hata kampeni hazijaisha

View attachment 1559836View attachment 1559837
Huyu naye simwelewi kabisa, tamaa ya madaraka, alivyoona Lissu amekuja na amepita alitakiwa tu kumpisha waungane, ila tamaa inamponza
 
Basi asingehamia Upinzani Kama alikuwa analijua Hilo au wangeungana na wenzao wa Chadema, Ila naona ego yake kubwa ndio imemponza
Heee we mmama vp. Kwa hiyo tusiwe na vyama vingi
Maana kila mtu ataenda ccm kwenye pesa
 
Membe alifikiri Tanzania ni Kijiji chake Cha Rondo. Alijidanganya sana. Alipenyeza vibaraka wake humu jf kitambo tu na kuwa very aggressive. Akadhani ameshakuwa Rais. Hakujitambua. Mwache sasa aaibike. Hana mvuto. ACT WAZALENDO wamelamba galasa.
 
Wafuasi wa Chadema ndani ya JF wanachuza sana. Kwenye harakati zao za kutafuta hero wanaweza kumuaminisha mtu anauwezo wa kupaa, usipokuwa makini unaweza kujikuta unapanda juu ya ghorofa za PSPF uruke; mwisho wake sio mzuri.

Ndio kilichomkuta Membe, baada ya CDM kupata hero mpya kutoka ubelgiji hawana habari nae. Membe mwenyewe ata kuongea majukwaani kushawishi hawezi.

Sasa hivi Lissu yeye anaaminishwa na wafuasi wa CDM ni malaika fulani hakuna anaemuweza Tanzania kila mtu anamuhofia sijui anaweza amrisha jeshi la raia wanaomuunga mkono wakinukishe anytime.
 
ukigombea urais yakupasa uwe na fweza lasivyo inakula Hakuna atayekuamini. Alipaswa Kuwadai ACT program na bajeti ya kampeni Kabla hajajitokeza kugombea.
 
Back
Top Bottom