Kwa hawa Madaktari huko mbeleni tutapata tabu

Kwa hawa Madaktari huko mbeleni tutapata tabu

Sabato NJEMA!

Kuna madaktari waliotokea moja Kwa moja Kidato cha Sita kwenda kusoma MD, na wapo ambao wametokea Diploma(Clinical Officer, CO) kwenda kusomea MD.

Kiukweli nimeshtushwa mno baada ya kukutana na Baadhi ya Madaktari watarajiwa wasomao MD na wengine waliomaliza CO.

Mambo yaliyonishtua;

1. Hawajui Lugha ya kingereza.
Kuna kipindi nilifika Pale Mloganzila ambayo Kwa wasioijua ni sehemu ya Hospitali ya taifa ya Muhimbili ambayo kimsingi madaktari wake inatakiwa wawe vipanga na wenye uwezo Mkubwa.

Madaktari waliomafunzoni walinishtua Sana Kwa kingereza Chao kibovu kilichowafanya mara Kwa mara kucheka CHEKA Kwa aibu.

Sitaki kuzungumzia Ma-CO, ambao wengi wao nao kingereza kinawapiga chenga.

Kuna watu watasema, kingereza sio muhimu kwani ni lugha Kama lugha zingine.
Kumbuka materials nyingi za Taaluma ya Udaktari zipo katika Lugha ya kingereza, kutokujua kingereza kutamfanya Daktari kutokuwa mahiri.


2. Clinical officers wa Zama hizi wengi wao sio mahiri, hawako competent katika Taaluma Yao.

Nikikutana na wahitiu wa Diploma ya Clinical officer katika Stori nikiwasabahi nikawauliza mmoja mmoja aelezee concept ya Physiology, mwingine aelezee concept ya anatomy, na mwingine aelezee jinsi damu inavyozalishwa ndani ya Mwili WA mwanadamu.
Unajua hizo ni concept ndogo Sana ambazo hata mwanafunzi wa Kidato cha nne na sita wanaweza Kueleza.

Lakini wakaishia kubwabwaja.


Ukienda baadhi ya Hospitali, madaktari hawajui ku-take patient History, baadhi Yao wanakulazimishia vitu ambavyo havikuumi.

Na hapa nazungumzia madaktari Vijana. Unakuta kijana CV kubwa lakini uwezo unatia Shaka.

Hakuna kitu kinakera Kama uende Hospitalini alafu ukute Daktari anauwezo mdogo katika Fani yake, yaani ukimsikiliza unagundua kabisa hapa hamna kitu.

Ni Sawa na Mwanafunzi afundishwe na mwalimu kilaza, yaani inakera Sana.

Ushauri wangu, siku hizi ukienda Hospitalini kuwa Makini Sana, madaktari wa siku hizi sio wakuwaamini 💯 hasa hawa Vijana.

Serikali iangalie Kwa umakini hivi vyuo vya Kati ambavyo ongezeko lake limekuwa kubwa.

Kuna watu hawatanielewa.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Dar es salaam
Lakini wote walianza kwa kutokujua kitu ndio wakajua kwa hiyo hakuna hoja hapo.
 
Huu uzi ni wa madaktar najua madaktar mtaingia humu kuusoma ebu naomba madaktar leo mnisaidie kitu

Unaweza kuta mtu anaumwa na ugojwa wake kulingana na kitua cha afya alipo hawez kutibika anatokea daktar anamshauri mgojwa akatibiwe kwa mganga wa kienyeji hii inatokea sana yan unakuta daktar au nesi anamuita mgojwa au ndg ya mgojwa af anamshauri kumtoa mgojwa hospital akatibiwe kienyeji

2) kuna ili suala la uzazi wa mpango unakuta daktar au nesi anamshauri mtumiaji wa dawa za uzazi wa mpango anamwambia sio nzuri zinazala wakiwa pembeni ila wakiwa ofsin daktar anakushauri utumie sasa km ni mbaya kwa nn madaktar hamjazikataa sku zimeletwa

1: Ukiona unashauriwa hivyo, basi ujue mtoa huduma ya afya uwezo wake wa kufikiri ndi umefika kikomi. Ingawa haimaanishi kuwa huwezi kusaidika huko mbele, ndio maana kuna referral systems. Inawezekana kimaarifa kazi imekuwa pevu au kiteknolojia pia. Sasa hao hujiongeza kulingana na ubinadamu na asili yetu na mambo ya imani.

2: Njia za uzazi wa mpango zaweza kutokumfaa mtu kulingana na hali yake ya kiafya aliyonayo. Kila njia inaelezwa uzuri vs ubaya na kiasi cha uhakika. Suala la kuchagua ni la mteja baada ya kuelezwa yote hayo. Hivyo, wakati mwingine ni suala la personality/unafiki ya kutokuwa wazi. Kama A haikufai nitakueleza na kwa nini, kama inasemwa usitumie zaidi ya miaka mitano nitakueleza.
 
Na Mimi nakuambia Kwa uzoefu.

Ukiona moja Kati ya hao hawajui kingereza basi jua wanajua kihispania, kireno au kifaransa.

Zingatia; wengi wao sio wote
Mbona kigeugeu Kama popobawa?, Mara kiingereza mara kireno mara kispain. Tuchukue lipi tuache lipi?. Acha kulimbukia lugha za watu, kwani kiingereza ndiyo kinatibu?. Basi usiende hospitali za Kitanzania katibiwe Uingereza, Ureno au Spain. Ushamba tu unakusumbua.
 
Juzi nilikua hospital, hao vijana wameshindwa choma/ weka ile kanule mara 3, anakuja huyu mara yule. Nilijaa sumu kwa mgonjwa wangu

Hivi ni vitu ambavyo hutokea kwa yeyote:
1: Anaweza kushindwa daktari/MD nesi anaweza na kinyume chake.
2: Anaweza kushindwa daktari bingwa wa usingizi, MD au nesi au ward attendant akakuwekea. Haya mambo yaoneni tu yalivyo, siyo ABCD....
Ni mambo yanahitaji ushirikiano na kuheshimiana sana, thamini mchango wa kila mmoja pale.

NB: Unaweza kusikia, furani angekuwepo tusingepata shida, kumbe ni health attendant. Nawe utasema muiteni basi kumbe hujui ndo huku unaona hana maana.
 
Unaweza
Unalo sema ni kweli ila linaanzia uko chini, mimi binafsi paka leo na shanga mtoto alie maliza f4 na kupata D4 anawezaje kusoma udakitari CO, kwanza vile vitabu vya medicine hawezi kutoa concept hailewi kabisa. Kiingereza hiki cha kawaida cha kuongea ni shida, àtaweza je kusoma na kuelewa vitabu vikumbwa kama atonomiology, kwa kweli mimi naona ni usani kwenye hivyo vyuo vya kati...........

Unaweza kuwaza hivyo, lakini si wote wenye D4 ni uwezo wao wa mwisho. Tunapata matokeo hayo baada ya mambo/factors nyingi. Huwezi kumwona mtu hawezi kwa kuona D4 bila kuhua aliipataje.

Mbona haujajiuliza miaka 60 ya uhuru Tanzania one yeyote aliyefanya kitu cha mfano zaidi ya yale matokeo ni yupi??
 
Hii fani imevamiwa na makanjanja mkuu....hulifahamu hilo watakucheka watu😂😂😂
 
Tufanyaje sasa?
Tuboreshe mfumo wetu wa elimu from the scratch ambapo tuandae vijana wenye uwezo wa kuelewa na siyo Kukariri.
Nakumbuka kipindi niko o level tulikuwa tunaambiwa tukariri ili tufaulu mitihani, that's the problem halafu unapata credit za kwenda chuo kwa matokeo ya Kukariri.
Kwenye kiingereza tuache kuprint dictionary za English to swahili tujikite kwenye English verbs to English translation zile za English - swahili zinakaririsha tu
 
Mbona kigeugeu Kama popobawa?, Mara kiingereza mara kireno mara kispain. Tuchukue lipi tuache lipi?. Acha kulimbukia lugha za watu, kwani kiingereza ndiyo kinatibu?. Basi usiende hospitali za Kitanzania katibiwe Uingereza, Ureno au Spain. Ushamba tu unakusumbua.


Huwezi elewa concept ninayoizungumzia Hapa.

Kingereza ñdio lugha ya kitaaluma na kufundishia na kujifunzia hapa nchini ulitaka nisemeje?
 
Ishu hapo ni uwezo wao kutafsiri maandiko na vitabu vya kitaaluma katika Lugha zao.

Kutafsri nako usidhani ni kazi ndogo,

Nchi hizo na zingine zenye uwezo wa kutafsiri vitabu na majarida ya kitaaluma katika Lugha zao nyingi zipo vizuri Kama vile India.

Kwa muktadha wa Tanzania, machapisho, vitabu na majarida mengi Kam sio yote yapo Kwa lugha ya kingereza na ndio lugha ya kujifunzia, sasa mtu Kama hawezi kingereza unafikiri atakuwa mahiri wa Taaluma husika aliyofundishiwa Kwa lugha asiyoimudu?

Ni Sawa na Malenga wa ushairi wa Kiswahili asiyeimudu lugha ya kiswahili alafu awe mahiri katika Mashairi na Riwaya za Kiswahili.

Ndio maana washairi wengi WA lugha ya Kiswahili wametoka Pwani ya Afrika mashariki Kwa sababu wanamudu Lugha ya Kiswahili.

Huo ni mfano tuu.

Kama Udaktari ungekuwa unafundishwa Kwa lugha ya Kiswahili na vitabu vyake vingi vipo katika Lugha yetu basi ningeungana na wewe

Mkuu unaongea points saana sema wadau wamekaza fuvu hawataka kukubaliana na ukweli
 
Sabato NJEMA!

Kuna madaktari waliotokea moja Kwa moja Kidato cha Sita kwenda kusoma MD, na wapo ambao wametokea Diploma(Clinical Officer, CO) kwenda kusomea MD.

Kiukweli nimeshtushwa mno baada ya kukutana na Baadhi ya Madaktari watarajiwa wasomao MD na wengine waliomaliza CO.

Mambo yaliyonishtua;

1. Hawajui Lugha ya kingereza.
Kuna kipindi nilifika Pale Mloganzila ambayo Kwa wasioijua ni sehemu ya Hospitali ya taifa ya Muhimbili ambayo kimsingi madaktari wake inatakiwa wawe vipanga na wenye uwezo Mkubwa.

Madaktari waliomafunzoni walinishtua Sana Kwa kingereza Chao kibovu kilichowafanya mara Kwa mara kucheka CHEKA Kwa aibu.

Sitaki kuzungumzia Ma-CO, ambao wengi wao nao kingereza kinawapiga chenga.

Kuna watu watasema, kingereza sio muhimu kwani ni lugha Kama lugha zingine.
Kumbuka materials nyingi za Taaluma ya Udaktari zipo katika Lugha ya kingereza, kutokujua kingereza kutamfanya Daktari kutokuwa mahiri.


2. Clinical officers wa Zama hizi wengi wao sio mahiri, hawako competent katika Taaluma Yao.

Nikikutana na wahitiu wa Diploma ya Clinical officer katika Stori nikiwasabahi nikawauliza mmoja mmoja aelezee concept ya Physiology, mwingine aelezee concept ya anatomy, na mwingine aelezee jinsi damu inavyozalishwa ndani ya Mwili WA mwanadamu.
Unajua hizo ni concept ndogo Sana ambazo hata mwanafunzi wa Kidato cha nne na sita wanaweza Kueleza.

Lakini wakaishia kubwabwaja.


Ukienda baadhi ya Hospitali, madaktari hawajui ku-take patient History, baadhi Yao wanakulazimishia vitu ambavyo havikuumi.

Na hapa nazungumzia madaktari Vijana. Unakuta kijana CV kubwa lakini uwezo unatia Shaka.

Hakuna kitu kinakera Kama uende Hospitalini alafu ukute Daktari anauwezo mdogo katika Fani yake, yaani ukimsikiliza unagundua kabisa hapa hamna kitu.

Ni Sawa na Mwanafunzi afundishwe na mwalimu kilaza, yaani inakera Sana.

Ushauri wangu, siku hizi ukienda Hospitalini kuwa Makini Sana, madaktari wa siku hizi sio wakuwaamini 💯 hasa hawa Vijana.

Serikali iangalie Kwa umakini hivi vyuo vya Kati ambavyo ongezeko lake limekuwa kubwa.

Kuna watu hawatanielewa.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Dar es salaam
Kama mtu ni PhD holder anasema taki fosi( task force) unadhani hao form 6 mkuu watakuwaje?
 
Wao darasani walikuwa wanameza nondo tu za kujibia mitihani, wanasemaga Kingereza waachie watu Wa Arts..
 
Materials za Taaluma ya Udaktari nyingi zipo Kwa lugha ya kingereza.

Na kutokana na mabadiliko ya magonjwa na madawa Udaktari kila siku unahitaji ku-update.

Huwezi kuwa Daktari mahiri bila kujua Lugha ya kingereza
Hao madaktari hawajui Kuandika Kiingereza,Kusoma Kiingereza au Kuzungumza Kiingereza?. Kuwa specific tafadhali. Lipi hapo?

Sent from my VF-795 using JamiiForums mobile app
 
Kuhusu Kiingereza, hilo ni janga la kitaifa [endapo kama unaithamini lugha hiyo].

Kiingereza hicho kibovu unachodai, kinaakisi uwezo wa Watanzania walio wengi.

Watanzania walio wengi lugha hiyo inawapiga chenga.

Hivyo hamna cha ajabu hapo. Watanzania kuongea Kiingereza kibovu ni jambo la kawaida sana.

Si ajabu hata wewe mwenyewe huongei Kiingereza kizuri kilichonyooka.

Just sayin’.
Hata jiwe kwake kilikuwa kigumu kukielewa japo cha kibongo bongo kipooooooooooo!!!!!!!!
 
Mbona Mtoa Mada ameweka kila kitu wazi kabisa? sijui kwanini watu wana vichwa vigumu kuelewa... Ngoja nimsaidie

Kwa nchi yetu.. Tanzania, English ndo lugha inayotumika kufundisha, vitabu vyote vipo katika lugha hii, machapisho n.k hivyo kitendo cha kukutana na mtu anaejiita mtaalamu katika fani fulani (Daktari) halafu english inampiga chenga kiukweli kabisa ni swala la kujiuliza na mara nyingi huwa amefika hatua hio kwa kukariri = sio daktari mzuri. Unaongea na daktari hawezi hata kuwasilisha taarifa kwa Kingereza halafu unaamini kabisa kasoma molecular structure akaielewa?? [emoji23][emoji23]

Mataifa yaliyoendelea yana mifumo ya kutafsiri vitabu na machapisho kwa lugha zao. hata waandishi wanaandika kwa lugha zao. Urusi mfano hata "Google" haipo.. wana system zao, china hamna whatsApp n.k nimetaja hivi kuonesha namna walivyo independent.
 
Kama daktari anaweza kuokoa maisha kingereza kinasaidia nini?, Nenda China, urusi, Spain, uarabuni, uone Kama kuna mtu anahusudu kingereza.
Ushaambiwa material zetu za udaktari zimeandikwa kwa kiingereza, hao unaowataja wanavitabu vyao vilivyoandikwa kwa lugha zao, elewa basi.
 
Kama muda karibu wote unaongea Kiswahili (98%), Kiingereza 1%,halafu utegemee uongee English safi kama mganda itakuwa ndoto za mchana, au utegemee mtu anayeishi mjini ambaye muda wote anazungumza Kiswahili hawezi kuongea kilugha kilichonyooka kama mtu wa kijijini, lugha ni kuifanyia mazoezi haipimi kiwango cha elimu
Sijawahi kuona watu wanaongea kiingereza kibovu tena kwa lafudhi mbovu kama waGanda
 
Materials za Taaluma ya Udaktari nyingi zipo Kwa lugha ya kingereza.

Na kutokana na mabadiliko ya magonjwa na madawa Udaktari kila siku unahitaji ku-update.

Huwezi kuwa Daktari mahiri bila kujua Lugha ya kingereza
Mi nadhani mother tongue ndio inaathiri kiiingereza cha mtu!sio kila mtu anaweza kuongea pure english mf.kenyans kile sio kiiingereza bali ni lugha zao za asili the same to Nigerians!!!mfano A sukuma can't speak like an englishman!mi nadhani swala la kiiingereza ni pana Sana kuliko tunavofikiri!!halafu kiiingereza cha kuongea mtu sio sawa na cha kuandika wala cha kuelewa maana halisi ya maneno yenyewe!!inaweza ukawa mzuri kwenye kuandika na kuelewa lakini lafudhi ikawa sio!!!
 
Back
Top Bottom