Kwa hili la mwaka mmoja wa kifo cha Magufuli, Kanisa Katoliki linapaswa kuona aibu

Kwa hili la mwaka mmoja wa kifo cha Magufuli, Kanisa Katoliki linapaswa kuona aibu

Pambana na dhambi zako kanisa halita kusaidia , na kamwe halitaona aibu na maisha yataendelea.
Dini haziwaongozi watu kwenda mbinguni tu bali huwafanya watawalike kirahisi pia watawala hupenda kuona dini zikiwasaidia kutawala na maandiko yanasema tutii mamlaka kwa vile hutoka kwa Mungu.
So complex.
 
Ndugu,
Lakini Wakristo hawatakiwi kuwa WANAFIKI kama walivyokuwa Mafarisayo wa wakati wa Yesu.
Unamuaibisha mwenye jina hilo ambae alikuwa imara na mkweli asiyeyumba.
Ukiniita mimi mnafiki Tundu Lisu na Freeman Mbowe wanaoongea Lugha ya CCM hivi sasa sijui utawaitaje?
 
Hao hawahusiki hapa. Acha kuokoteza cha kuongea. Mwenye jina hilo hakuwa hivyo.
Nimekupa mfano wa Wanafiki HAI.

Mchana Chadema usiku wanaomba " Mafao na Misamaha" CCM

Hahahaaaa........ Endelea kushangilia hapo hapo banda la mkaa jirani na ofisi ya Mange!
 
Mimi ni moatoliki, lakini h

awa maaskofu wetu kwa unafiki siwawezi. Hata askofu Nyaisonga kuwa rais wa tec, hawakuzingatia vigezo vingine zaidi ya kuwa mwendazake alikuwa rafiki mkubwa wa huyu askofu.
Kwani Mwenyekiti wa TEC anapaswa kuwa na vigezo gani? Askofu (Mkuu) Nyaisonga hana hivyo vigezo?
 
Sitaki kuzungumzia madhila ya kisiasa aliyoyafanya kwa Taifa huyu mtu, maana hata ukurasa huu hautatosha, nataka nizungumzie tu madhila aliyowafanyia kanisa Katoliki na Makanisa Mengine, halafu leo hii wanaadhimisha mwaka mmoja tangu kifo chake

Kwanza kabisa kulikuwa na mauaji na watu kupotea kulivyoshamiri mwaka 2017 Kanisa Katoliki lilitoa waraka wa kulaani mambo hayo na kuliombea Taifa lirudi kwenye mstari, alichojibu bwana huyu ni kulikejeli Kanisa katoliki na kusema kuwa halikukemea mauaji ya Kibiti (Kitu ambacho ni uongo, Kanisa lilikemea) na hata kama halikukemea kweli ndio itafanya mauaji ya watu wale kuwa sahihi? Ni mtu muovu namna gani anayeweza kuwaza hivi? Kanisa halioni aibu kumuadhimisha mtu kama huyu?

Pili, Baraza la Maaskofu wa Makanisa ya Kiprotestanti nao wakatoa waraka wa kukemea mauaji yaliyokuwa yameshamiri nchini kipindi kile, lakini mtu huyu alivyokuwa wa ajabu alitoa wa notisi kwa makanisa hayo kufuta waraka huo ama yatafutiwa usajili, hii ilileta sekeseke hadi aliyekuwa waziri wa mambo ya ndani kipindi kile Mwigulu Nchemba kuondolewa

Tatu, Askofu Kakobe, aliposema kuwa Tanzania ni nchi ya vyama vingi na vyama vyote vinapaswa kupewa nafasi, askofu huyu alitukanwa na kudhihakiwa sana na vijana wa kazi wa huyu mzee, na kunyang’anywa paspoti yake na kuambiwa sio raia wa Tanzania, haikuishia hapo askofu Kakobe alitishiwa kufilisiwa mali zake na za kanisa endapo ‘asingeunga juhudi’ . Huytu ndiye mtu Kanisa Katoliki linamuadhimisha?

Nne, Askofu Niwemugizi aliposema kudai katiba mpya sio uchochezi, mtu huyu bila chembe ya aibu alimuundia zengwe kuwa sio raia wa Tanzania na akapokjonywa paspoti, japo Askofu huyu ndio alikuwa Askofu wake tangu kabla hajawa Rais..!

Tano, Kulipokuwa na Wimbi la ugonjwa Corona, mtu huyu kwa siasa zake za kilaghai akasema Corona imeondolewa kwa maombi ya siku 3, Kanisa Katoliki ambalo linajua kuwa Mungu katupa Sayansi ya kukabiliana na majanga, likasisitiza watu kuchukua tahadhari za kisayansi na kushauri Serikali ifuate njia zilizothibitishwa Kisayansi kukabiliana na hili Janga.

Kanisa lilienda mbali na kutoa takwimu za watumishi wake kama maaskofu, mapadri, masista n.k waliokufa wengi kwa kipindi kifupi kwa dalili za ugonjwa wa Covid. Mtu huyu mnakumbuka alifanyaje? Alikejeli vibaya viongozi wa Dini na kusema wanapotosha watu kiimani, kuna kipindi aliingia kanisani na kumkejeli padre mmoja aliyekuwa anazingatia kanuni za kujikinga na Corona. Mtu huyu leo ndio Kanisa..Au linataka kumtangaza Mtakatifuu?

Nimechagua baadhi tu ambayo yalifanyika hadharani na mtu fmfuatiliji wa siasa atayajua, ila yapo mengi sana mtu huyu aliwafanyia viongozi wa Dini kama yale ya akina Mwingira, na kukamata mapadri huko Moshi, ila niishie hapa

Najua baadhi wanaweza kuteta na kusema alikuwa kiongozi mkubwa wa nchi aliyefanya mambo makubwa hivyo lazima wamuadhimishe. Lakini Mkapa, ambaye ni kiongozi aliyekuwa na mapungufu yake pia japo hayakufikia kiwaongo hiki, alifanya mambo makubwa sana na alipofikisha mwaka mmoja tangu kifo chake, Kanisa Katoliki halikufanya chochote
Yesu Amewafundisha Wakatoliki hivi!
[emoji1370][emoji1370]
Mathayo 5
43 Mmesikia kwamba imenenwa, Umpende jirani yako, na, Umchukie adui yako;

44 lakini mimi nawaambia, Wapendeni adui zenu, waombeeni wanaowaudhi,

45 ili mpate kuwa wana wa Baba yenu aliye mbinguni; maana yeye huwaangazia jua lake waovu na wema, huwanyeshea mvua wenye haki na wasio haki.

46 Maana mkiwapenda wanaowapenda ninyi mwapata thawabu gani? Hata watoza ushuru, je! Nao hawafanyi yayo hayo?

47 Tena mkiwaamkia ndugu zenu tu, mnatenda tendo gani la ziada? Hata watu wa mataifa, je! Nao hawafanyi kama hayo?

48 Basi ninyi mtakuwa wakamilifu, kama Baba yenu wa mbinguni alivyo mkamilifu.

Usipo Yafuata na Kuyaishi Mafundisho yake ww sio Mfuasi wake!
 
Suala si kuazimisha kwa ajili yake hapo,......hapo issue ni kuazimisha kumuonyesha aliyopo kuwa 'hatukukubali kiviiile kwa kuwa si mwenzetu'!.
 
Mie nilijua utazungumza kuhusu uwajibikaji serikalini, miundombinu, uzalendo nk. Chacha wange alikufa kwenye ajali ya utata je mbowe alihusika?

Kaka yake mbowe alikufa, je chadema walimuua? Suala la kifo lipo tu ata ungefanya nini.

Alphonse mawazo alikufa kipindi magufuli akiwa madarakani, yule mwandishi wa channel 10 aliyefia iringa je?

Alikufa wakati wa magufuli, kipigo na vifo mtwara wakiandamana kuhusu gesi na mafuta ilikua kipindi cha Magu?

Tuseme kweli, Magu hakuwaita upinzani ikulu kunywa chai, hyo ndio walikasirika. Sasa wameitwa ikulu ni mapambio na kusifu.
 
Ukumbuke kuwa kwa Imani ya katoliki kupokea sakramenti sio kigezo peekee cua kufika Mbinguni. Yesu alisema: 'Aulae mwili wangu bila kustahili anakula hukumu yake mwenyewe'.
Wewe naye kiazi kwelikweli.

Ukiambiwa mtu amepokea Sakramenti kabla ya kufa maana yake amepewa Sakramenti ya Kitubio, Mpako wa Wagonjwa na Ekaristi Takatifu.

In other words, mtu kama huyo ni msafi kwelikweli. Hapo ni mbinguni moja kwa moja unless hapo katikati afanye dhambi ndogo ndio itabidi apitie toharani kwa ajili ya malipizi. considering his health at his death, this is very unlikely.

Nyie ndio Wakatoliki mnaoyumbishwa kwa kutoijua imani yetu vema. Mnatuaibisha sana.
 
Sitaki kuzungumzia madhila ya kisiasa aliyoyafanya kwa Taifa huyu mtu, maana hata ukurasa huu hautatosha, nataka nizungumzie tu madhila aliyowafanyia kanisa Katoliki na Makanisa Mengine, halafu leo hii wanaadhimisha mwaka mmoja tangu kifo chake

Kwanza kabisa kulikuwa na mauaji na watu kupotea kulivyoshamiri mwaka 2017 Kanisa Katoliki lilitoa waraka wa kulaani mambo hayo na kuliombea Taifa lirudi kwenye mstari, alichojibu bwana huyu ni kulikejeli Kanisa katoliki na kusema kuwa halikukemea mauaji ya Kibiti (Kitu ambacho ni uongo, Kanisa lilikemea) na hata kama halikukemea kweli ndio itafanya mauaji ya watu wale kuwa sahihi? Ni mtu muovu namna gani anayeweza kuwaza hivi? Kanisa halioni aibu kumuadhimisha mtu kama huyu?

Pili, Baraza la Maaskofu wa Makanisa ya Kiprotestanti nao wakatoa waraka wa kukemea mauaji yaliyokuwa yameshamiri nchini kipindi kile, lakini mtu huyu alivyokuwa wa ajabu alitoa wa notisi kwa makanisa hayo kufuta waraka huo ama yatafutiwa usajili, hii ilileta sekeseke hadi aliyekuwa waziri wa mambo ya ndani kipindi kile Mwigulu Nchemba kuondolewa

Tatu, Askofu Kakobe, aliposema kuwa Tanzania ni nchi ya vyama vingi na vyama vyote vinapaswa kupewa nafasi, askofu huyu alitukanwa na kudhihakiwa sana na vijana wa kazi wa huyu mzee, na kunyang’anywa paspoti yake na kuambiwa sio raia wa Tanzania, haikuishia hapo askofu Kakobe alitishiwa kufilisiwa mali zake na za kanisa endapo ‘asingeunga juhudi’ . Huytu ndiye mtu Kanisa Katoliki linamuadhimisha?

Nne, Askofu Niwemugizi aliposema kudai katiba mpya sio uchochezi, mtu huyu bila chembe ya aibu alimuundia zengwe kuwa sio raia wa Tanzania na akapokjonywa paspoti, japo Askofu huyu ndio alikuwa Askofu wake tangu kabla hajawa Rais..!

Tano, Kulipokuwa na Wimbi la ugonjwa Corona, mtu huyu kwa siasa zake za kilaghai akasema Corona imeondolewa kwa maombi ya siku 3, Kanisa Katoliki ambalo linajua kuwa Mungu katupa Sayansi ya kukabiliana na majanga, likasisitiza watu kuchukua tahadhari za kisayansi na kushauri Serikali ifuate njia zilizothibitishwa Kisayansi kukabiliana na hili Janga.

Kanisa lilienda mbali na kutoa takwimu za watumishi wake kama maaskofu, mapadri, masista n.k waliokufa wengi kwa kipindi kifupi kwa dalili za ugonjwa wa Covid. Mtu huyu mnakumbuka alifanyaje? Alikejeli vibaya viongozi wa Dini na kusema wanapotosha watu kiimani, kuna kipindi aliingia kanisani na kumkejeli padre mmoja aliyekuwa anazingatia kanuni za kujikinga na Corona. Mtu huyu leo ndio Kanisa..Au linataka kumtangaza Mtakatifuu?

Nimechagua baadhi tu ambayo yalifanyika hadharani na mtu fmfuatiliji wa siasa atayajua, ila yapo mengi sana mtu huyu aliwafanyia viongozi wa Dini kama yale ya akina Mwingira, na kukamata mapadri huko Moshi, ila niishie hapa

Najua baadhi wanaweza kuteta na kusema alikuwa kiongozi mkubwa wa nchi aliyefanya mambo makubwa hivyo lazima wamuadhimishe. Lakini Mkapa, ambaye ni kiongozi aliyekuwa na mapungufu yake pia japo hayakufikia kiwaongo hiki, alifanya mambo makubwa sana na alipofikisha mwaka mmoja tangu kifo chake, Kanisa Katoliki halikufanya chochote
ndugu kanisa halilipi kisasi hata maandiko yanasema kisasi si juu ya mwanadamu.kanisa linaamini katika kusamehe na hukumu anaachiwa Mungu sababu ndiye anyejua yaliyopo ndani ya kila mwanadamu.
 
Hivi nyie Ukatoliki wenu mliupata kwa kufuata hatua zote ikiwemo mafundisho? No wonder mkipata challenges tu kidogo kuwa mnaabudu sanamu, mnamuabudu Bikra Maria, mara ooh sijui Papa ni Freemason mnateteleka. Inasikitisha sana.

Nimeshuhudia kanisa hilohilo likihukumu wafu kwa kudai kwamba hakuwa amefunga ndoa, alikuwa na suria, alikuwa hashiriki jumuiya nk; wakati hapohapo likiwatunuku sakramenti hizohizo walevi na majambazi!
Mama Kanisa hayupo hapa kuhukumu mtu yeyote. Ili mtu ustahili kitu fulani, siyo Kanisani pekee hata katika maisha, lazima uwe na vigezo.

• Ukijinyonga maana yake umemkufuru Roho Mtakatifu kwa kukata kwako tamaa and so automatically umejitenga na Mungu na Kanisa. Hatuwezi kukuzika.

• Ukiishi na mtu kama mke ama mume wako wakati hamjafunga ndoa maana yake umeamua kujitenga na Kanisa, haustahili kupokea Sakramenti yoyote and so hatuji kukuzika.

• Tumeagizwa kuishi kwa umoja na mshikamano. Unapoamua kujitenga na Jumuiya maana yake umejitenga na Kanisa. Unapojitenga na Kanisa automatically unajitenga na Mungu. Hatuwezi kuja kukuzika.

1 Yohane 4:20-21
Mtu akisema,
"Nampenda Mungu,"
naye anamchukia ndugu yake ni mwongo.
Kwa maana asiyempenda ndugu yake ambaye amemwona, hawezi kumpenda Mungu ambaye hakumwona.
Na amri hii tumepewa na yeye:
ya kwamba yeye ampendaye Mungu,
ampende na ndugu yake.


Kwahiyo unapoamua kujitenga na Kanisa maana yake umejitenga na Mungu. Hatuwezi kuja kukuzika.

Hata hivyo, mdhambi akiamua kutubu Kanisa linampokea kwa furaha na mikono miwili, and so atapata huduma na haki zote wazistahilizo watoto wa Mungu na Kanisa.

Kuna walakini kubwa sana katika kuadhimisha uovu na waovu
Magufuli hakuwa mwovu, at least at his deathbed. Tunaamini yupo mbinguni au toharani. Ndio maana tunamuombea yeye pamoja na roho za waamini wengine marehemu waliopo toharani wapate rehema kwa Mungu wafike mbinguni mapema iwezekanavyo.
 
Back
Top Bottom