Kwa hili la Ommy Dimpoz na Babake wee uliye biological mother/father ukimkataa/kumtelekeza mtoto wako ujue umemuumiza sana kisaikolojia na makuzi yake

Kwa hili la Ommy Dimpoz na Babake wee uliye biological mother/father ukimkataa/kumtelekeza mtoto wako ujue umemuumiza sana kisaikolojia na makuzi yake

Mama wa ommy Dimpoz alifariki ommy ukiwa mdogo sana primary school. Huyu baba hakutokea msibani japo kumpa faraja mwanae, wala hakuwahi kumtafuta mwanae kujua anaishi au amekufa
Mmh hii kweli ya duniani basi akapigwe vipimo ili ajue zaidi maana km ni hivyo hata mimi naweza nikaibuka na kujimwambafyi kwamba huyu ni mwanangu hapo unaona imekaaje mkuu?
 
Mmh hii kweli ya duniani basi akapigwe vipimo ili ajue zaidi maana km ni hivyo hata mimi naweza nikaibuka na kujimwambafyi kwamba huyu ni mwanangu hapo unaona imekaaje mkuu?

Wazazi wa aina hii ni wazazi matapeli
 
Kabisa mkuu
Bibi yangu aliwahi kunihusia kwamba hata awe na hasira vipi kamwe usimfanyie ubaya mtoto mdogo maana siku moja utakua mzee nae atakua kijana mtu mzima mwenye hatma yake
Na pia kuna tabia tunazo wa Africa kwamba mtoto wako ni lazima akusaidie, kitu ambacho hakina ulazima. Ni vema wazazi wakaandaa uzee wao vizuri na siyo kuja kutegemea fadhila za watoto wao, unless watoto wamependa wenyewe kuwasupport wazazi wao hata kama wazazi waliwalea ama hawakuwalea.

Kwa mfano huyu mzee asingekuwa na tamaa za mafanikio ya mwanae ama asingekuwa anamtafuta mwanae kwa sababu ya mafanikio, bali tu kumaliza tofauti zao, hii ingekuwa rahisi sana kusamehewa na mwanae, kuliko kumtafuta mtoto wako kisha kuanza kudai fadhila kitu ambacho si busara na hekima.
 
Wazazi wa aina hii ni wazazi matapeli
Mama ndie anaemjua baba wa mtoto hivyo ndivyo ilivyo

Km ommy aliambiwa na mama yake kua huyo ndio baba yake basi hapo hakuna shida wamalizane tu kiutu uzima ila km hakuambiwa na mama yake kua huyu ndio baba yako basi hapo kuna walakini
 
Na pia kuna tabia tunazo wa Africa kwamba mtoto wako ni lazima akusaidie, kitu ambacho hakina ulazima. Ni vema wazazi wakaandaa uzee wao vizuri na siyo kuja kutegemea fadhila za watoto wao, unless watoto wamependa wenyewe kuwasupport wazazi wao hata kama wazazi waliwalea ama hawakuwalea.

Kwa mfano huyu mzee asingekuwa na tamaa za mafanikio ya mwanae ama asingekuwa anamtafuta mwanae kwa sababu ya mafanikio, bali tu kumaliza tofauti zao, hii ingekuwa rahisi sana kusamehewa na mwanae, kuliko kumtafuta mtoto wako kisha kuanza kudai fadhila kitu ambacho si busara na hekima.

Mtoto kukuheshimu ni shurti
Ila mtoto kukusaidia ni upendo unaotokana na ulichokijenga wakati wa makuzi yake
Mtoto anaweza kukusaidia lakini asikuheshimu
 
Mama ndie anaemjua baba wa mtoto hivyo ndivyo ilivyo

Km ommy aliambiwa na mama yake kua huyo ndio baba yake basi hapo hakuna shida wamalizane tu kiutu uzima ila km hakuambiwa na mama yake kua huyu ndio baba yako basi hapo kuna walakini
Umesikiliza alichoongea huyo mzee na alichoongea ommy au umesoma comments tuu?
 
Kadri siku zangu za maisha zinavyozidi kusonga mbele nazidi kutambua maisha hayana maana.

Maisha yanahitaji kuwa mnyenyekevu, kusamehe, kuwa mwema, kukubaliana na hali husika, na kuwachukulia wengine kwa upole.

Maisha hayana jipya, hasa ukiwaona waliolala huko ocean Road, hvyo tunapopata muda wa kusamehe, tusamehe tu bila ya kutafuta justification, ni ngumu ila inawezekana.

Mwisho wa siku tulivyonavyo tutaviacha.
 
Aisee, siwezi kumthamini mtu ambaye anasahau na kutelekeza uzazi wake, hata kama ni marafiki nikijua na urafiki unaishia hapo, kama unaweza kumfanyia hivyo damu yako,vipi kuhusu mimi?QUESTION MARK????
 
Umesikiliza alichoongea huyo mzee na alichoongea ommy au umesoma comments tuu?
Ndio ila mama wa mtoto hajasikilizwa kwa hio hapo bado kuna gap mwenye ukweli halisi kua huyu mtoto ni wa nani ni mama wa mtoto
 
Aisee, siwezi kumthamini mtu ambaye anasahau na kutelekeza uzazi wake, hata kama ni marafiki, kama unaweza kumfanyia hivyo damu yako,vipi kuhusu mimi?QUESTION MARK????

MITHALI 22:6​

"Mlee mtoto katika njia impasayo, Naye hataiacha, hata atakapokuwa mzee."​

 
Mama wa ommy Dimpoz alifariki ommy ukiwa mdogo sana primary school. Huyu baba hakutokea msibani japo kumpa faraja mwanae, wala hakuwahi kumtafuta mwanae kujua anaishi au amekufa
Ulikwepo msibani na kuthibitisha ni kweli hakutokea?
 
Back
Top Bottom