Kwa kichwa cha habari cha gazeti la MWANANCHI la leo Aprili 1, 2022 unajifunza na kugundua nini?

Kwa kichwa cha habari cha gazeti la MWANANCHI la leo Aprili 1, 2022 unajifunza na kugundua nini?

Mwananchi nawakubali sana kwenye kufikisha "Ujumbe Makhsusi" kwa jamii lakini kwa njia Isiyo moja kwa moja mpk utumie Akili mingi na yenye interpretations tofauti tofauti... Ndipo Upate Jibu rasmi na kusepa zako. 'Mwananchi Aisee'..... [emoji38][emoji38][emoji38][emoji122][emoji122][emoji122][emoji122]
 
Inaweza kumaanisha, (wale waliotaka kupotezwa kwa hila na maguvu makuu) wamerudia aiseee (kwa uwezo wa Muumba)!
Inamaana Jiwe, a.k.a bludoza alishindwa kuwabluza hawa pamoja na ujangili wao, ujambazi wao, u-land load wao?

Nikijiulipa hapo ndipo hapo nionapo kuwa aidha nae Jiwe alikuwa wale wale au alikuwa ana uonevu kwa baadhi ya wanyonge.

Nakumbuka kipindi cha Jk Bwana Bazir Mramba alishitakiwa na kuhukumiwa kwa sababu ya matumizi mabaya ya madaraka.
 
Ukimuuliza Musiba na Ally Hapi watakupa majibu mujarabu na wanajisikiaje saa hizi.

Ni heri ya kuwa ma viongozi watoto wa mjini kuliko kuongozwa na washamba.

Tawala zote tumeziishi, ogopa mtu anayetaka watu wawe maskini yeye peke yake ndio awe na pesa, halafu kuna wajinga wakaaminishwa kuitwa wanyonge na maskini ndio sifa na uzalendo.

Hawa hawa ndio wanafaa, acha malalamiko, jipange kwenye channel, tengeneza connection na wewe ule mema ya nchi.
Zaidi ya hapo tutaishiaa Kulalamika tu
Kwikwi

Ova
 
Operesheni rejesha wahuni, hahaaa hiki chama bana , waliowaponda sasa wanawasifia, kimsingi wanakua kama benderra tuuuuuu fuata upepo hakuna wanachokiamini hawa. Mtu akifukuzwa wanashangilia, akirudishwa wanashangilia, wakimwita muhuni msaliti, wanashangilia heeeeeeeeeeeeee , sasa hawa wanaamini kwenye nini?
 
Kuna uwezekano mkubwa Sana sheli za mafuta kujengwa ata kwenye open space na pengine kwenye mlango wa ikulu maana waliorudi wizar ya aridhi wanaimiliki
Sasa hivi njia ya tandale ina "sheli tatu au nne. Na pale Mgabe kuingia simu 200 kwenye kona pale nyumba 2 zishavunjwa, nadhani ni sheli.
WAMERUDI AISEE.
 
Operesheni rejesha wahuni, hahaaa hiki chama bana , waliowaponda sasa wanawasifia, kimsingi wanakua kama benderra tuuuuuu fuata upepo hakuna wanachokiamini hawa. Mtu akifukuzwa wanashangilia, akirudishwa wanashangilia, wakimwita muhuni msaliti, wanashangilia heeeeeeeeeeeeee , sasa hawa wanaamini kwenye nini?
Hakuna utofaiti na vyama confine, ni act peke yake bado sijajua au sijaona undumilakuwili wake. Lkn chadema wasiongee kabisaaaa,.....walishangilia lowassa alivyoitwa fisadi, wakashangilia na kudeki barabara alipokinunua chadema. Tena km kuna chama chafaa kuogopwa ni chadema......Kwa unafiki hapo ndo nyumbani
 
Wakati tembo wanaisha kwa kuuliwa , kuna meli ya aliyekua kigogo wa chama ilikamatwa na meno ya tembo. Tukaambiwa meli ni yake ila meno ya tembo sio yake. Nasikia karudi tena kwenye usukani. Zamu hii tembo watabaki historia
 
Nimeshaanza kuamini JPM aliuwawa mbona kasi kubwa ninayoishuhudia na mipasho mingi kwa marehemu kila kona kwa Maembe kwa mzee marope , Jk nae anachekelea mpaka na chifu Hanga mpaka anainama kuchekea chini kufuatia mipasho ya wazee wanayoitoa huko Idodomya. Lakini tusisahau there is no permanent condition / situation vijana wapo huwezi kujua mawazo yao
 
Kuelewa mbongo anataka nini ni kazi kwelikweli.
Kipindi cha JK tulikua tunamponda na kumtukana kwelikweli, majina yote ya hovyohovyo tukampachika tukafikia mpaka kutamani siku moja nchi yetu itawaliwe kidikteta.
Mungu si Athumani akasikia kilio chetu akatuletea Jiwe tena Jiwe kwelikweli hacheki kabisa na kima yoyote, Wabongo tukaanza vilio na kusaga meno, tukampachika majina ya hovyohovyo lakini Mwamba alifunga macho na akaziba kabisa masikio yake.
Kelele zikaanza mpaka mjengoni za kummisi JK na kila sifa nzuri akapewa na walewale waliokua wanambeza, wanamkebehi na kumtukana.
Leo hii baada ya Mwamba kutangulia mbele za haki walewale waliokua wanambeza, wanamkebehi na kumtukana JPM ndio haohao wamekua wapiga zumari wa kumsifia na kumuona yeye ndie alikua haswa mkombozi wa hii nchi, wamegeukia upande wa pili kumtukana na kumsimanga Mama pamoja na viongozi waliopita wa awamu ya nne.
Mimi ninachosema Mama aendelee tu kuupiga mwingi asisikilize kelele za chura maana chura akiwa majini analalamika maji ni ya baridi sana halafu pia ni machafu yanamsababishia ngozi yake kushambuliwa na wadudu ndio maana mwili wake unapata mabaka mabaka,
Chura huyohuyo akiwa nchi kavu pia analalamika nchi kavu jua ni kali sana linamchoma mpaka ngozi yake inababuka na mwili wake wote unajaa mabaka mabaka.h
Kila mtu anauziri na ubaya wake. Uzuri ukimpamba na kuonyesha umuhimu wake ubaya ukionyesha ushetwani wake. Kuna mambo jiwe asingeyaingiza kwenye siasa zake kila mtu angemkubali. Ubaguzi, kunyanyasa wapinzani,mauaji ya raia, utekaji wa waziwazi ilikua ukiona noa nyeusi mtu unakimbia, kubambikia watu kesi, upendeleo na matakataka mengi yataendelea kumchafua huyo jamaa hata huko aliko
 
Kuna watu humu wanawaita waizi ila hapohapo utakuta nae ni mla rushwa mkubwa au hata jizi la kuku ambapo akipiga hela hatuzioni

Acha waingie tu tuishi kwa amani
Ibeni sana ila msiuwane na kutupa watu kwenye viroba

Naona hata uhuru wa kuandika chochote umerudi [emoji1431][emoji23]
Watu wanaishi kwa furaha hata kama hakuna Hela mfukoni
 
acha warudi ,watakutana na mzimu wa MAGUFULI,mzimu haukufagi
 
Nani asiyejua kinana ni mwizi na Jangili wa taifa? Tutegemee biashara ya meno ya tembo na faru ikirudi kwa kasi ya ajabu.

Biashara ya nyala za serikali Kikwete aliyofanya na waziri wake Nyalandu ilimnogea kiasi kwamba ; sasa imebidi afanye mbinu amuweke chawa wake mwingine pale awe ndio waziri wa Maliasili ili wafufue ile Biashara yao ya wanyama pori na pembe za ndovu!! Enzi ya Jiwe Kikwete alikuwa hafurukuti hivyo asingeweza kuendelea na ufisadi ule!
 
Huyu mwamba atarudi lini 'aisee'?😁😁😁
 
Me sijui, ninachojua Kinana ni gwiji wa siasa za Tanzania

Hujui hata kuwa Kinana ni MSOMALI?
Ngoja tukufamishe basi KUWA huyu Kinana alipokuwa katibu Mkuu wa ccm kwa kushirikiana na rafiki yake Kimbisa ndiyo waliouza mashine za kupiga chapa za magazeti ya Uhuru na Mzalendo. Akiwa katibu mkuu wafanya kazi wa magazeti hayo ya ccm walikuwa na malimbikizo ya mishahara kwani walikuwa hawalipwi kwa wakati!!
 
Back
Top Bottom