Kwa madereva: Tuliowahi kutokewa na mauzauza barabarani tupeane uzoefu

Kwa madereva: Tuliowahi kutokewa na mauzauza barabarani tupeane uzoefu

Mimi mkasa wangu ulinitokea bwawani eneo la darajani, ilikuwa kama saa 6 usiku alitokea mwanamke mrefu

kavaa gauni jeupe na kuingia
barabarani. kwa ghafla na kisha kuanza kunisimamisha huku

akiingia barabarani mwili wangu pamoja na nywele ulisisimka huku nikikumbuka

hapa nikiyumbishwa ni ajali mbaya maana mbele kuna gari zinakuja kwa kasi nyuma yangu pia gari zinakuja kwa kasi

Baada ya hapo wala sikuona kama nimemgonga au kukimbilia upande wa pili wa barabara


Ukitaka kuona haya mambo tembea sana safari za usiku na pia huwa kuna maeneo yanajulikana kwa visa hivyo

Pia kuna baadhi ya vitu huwa vinakutokea lakini uhalisi wake huwa unatokana na uchovu (fatigues)

Barabarani kuna mambo mengi mengine ni tabia za watu hupenda kusifiwa hata kama kitu kipo nje ya uwezo wake, atalazimisha kufanya ili ionekane huyu jamaa ni kiboko
 
Mimi ni mzoefu wa safari za usiku na sikuwahi kuona maluelue yoyote! Mimi nadhani ni imani tu. Wengi wanakutana na watu kama walevi, viziwi au vichaa wakivuka barabara na kuoanisha na imani za kishirikina. Hofu yangu ni kuona watu wanahamasishana kuua kwa kugonga bila kujali ni binadamu wenzetu.
Hivi ukutane na mlevi au chizi katikati ya mbuga ya mikumi au Yale mapori ya maeneo ya ruaha ukiwa unatoka mikumi kweli...

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Trople Kiss!? Maimuna huyo!

Sent using Jamii Forums mobile app
Habari wana JF,

Nimekua nikisikia kwamba barabarani Kuna vitimbwi vya mauza uza nikawa siamini, sasa ni juzi nilikua natoka Arusha kuelekea Kibaha. Nilifika sehemu jina silifahamu, ni kijiji baada ya kutoka Mombo.

Ni kwamba nikiwa kwenye mwendo alitokea mtu upande wa kushoto akawa anaingia barabarani Kama vile haioni gari nikapunguza mwendo na kupiga honi, nikitumaini jamaa atasimama ama kustuka, badala yake akaongeza spidi na kuliingia gari upande ule ule wa kushoto mimi na jamaa yangu tukasikia kishindo, side mirror ikavunjika ikaweka na kreki mbaya sana kwenye kioo cha mlango wa kushoto.

Nilisimamisha gari fasta tukashuka na kuangalia tunamuona yule mtu anakwenda tu kwa spidi ile ile, kama vile hakikutokea chochote. Tukawa tunashangaa basi yule mtu akaingia kama kwenye kichochoro Kati ya nyumba mbili, hii nyumba ya kulia Kuna jamaa alikua ameketi kibarazani amepaki pembeni gari aina ya vitz.

Tukamfuata jamaa yangu akamuuliza, Ndugu huyu mtu amekatiza hapa unamfahamu ? Maana tumemgonga na gari tumesimama ili tumtazame lakini cha kushangaza jamaa hakuanguka wala kuyumba ameelekea huku. Cha kushangaza tena, Jamaa akatuambia, nyie mpo salama? Tukamjibu ndio. Akasema basi shukuruni nyie endeleeni na safari. Nikamuuliza mbona hatuelewi?

Badala ya kujibu akabaki ametukazia macho jamaa yangu akanishika mkono na kunivuta tukaondoka. Lakini mpaka sasa hivi tumebaki na maswali vichwani mwetu.

Ni nini hasa kilitokea....

Asanteni
nakumbuka nilipokuwa dreva wa basi moja linaitwa Tanganyika bus kule MWANZA nilipokuwa ktk route za kwenda Mara ipo siku njiani majira ya saa 3 nikiwa ktk shughuli zangu za udereva nilionana ghafla na jamaa akiwa ana Ng'ombe wawili akikatisha katkati ya barabara tena ni babu kavaa lubega,nilichosema ni kwa jina la Yesu ,Mungu wangu nisaidie sikuwa hata na akili ya kushika breki niliachia mikono na gari ilivuka pale,shukrani kwa utingo jirani yangu baada ya kuona ile hali utingo yule alikanyaga breki huku tukiwa tumevuka lile eneo,baada ya hapo sikuweza tena kuendesha,gari liliendehswa na utingo hadi tukafika nahc ni Mungu tu alisaidia si mimi,tokea siku ile sijaedesha tena gari usiku mwisho ni saa 12 jioni
 
Wakija na wavuvi hapa...nahisi patachimbika'
[emoji2] [emoji2] [emoji2] wakija wavuvi na stori zao wanayoyaona baharini usiku,, nyinyi mtajihisi mnaona midoli tu barabarani. kote nime experience najua udereva mpaka uvuvi,, maana kwetu ni karibu na bahari tangu nina miaka kumi na tatu nilikua navua samaki baharini,, nikaanza kwenda na usiku pia na makarabai,, tunayoyaona huko baharini usiku,, nafkiri barabarani tunaona tom n jery[emoji2] tu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna siku ilikuwa 2007. Nikitoka Arusha kwenda Dar saa Saba Nane usiku nilikuwa napita maeneo ya kwedikwazu. Kuna mahala Barbara imenyooka Sana Basi nikawa natembea speed 100-120.
Kuna mrembo mmoja mdada akawa anasimamisha gari akiomba lift. Nikapiga taa kubwa kumwona vizuri mrembo haswaa, sikusimama nikanuoosha goti, huku najiuliza huyu anaenda Wapi saa hizi,. Bwana ile nampita kwa speed ile alinipiga busu Mara tatu hapo dirishani. Maana sikuwa nimefunga madirisha ili nipigwe upepo nisilale. Nilifika dar Sina raha kutwa nzima.

Sent using Jamii Forums mobile app
Napafahamu mkuu pale ni wilaya ya Handeni kwa Wazigua, Ni noma

Sent using Jamii Forums mobile app
 
[emoji2] [emoji2] [emoji2] wakija wavuvi na stori zao wanayoyaona baharini usiku,, nyinyi mtajihisi mnaona midoli tu barabarani. kote nime experience najua udereva mpaka uvuvi,, maana kwetu ni karibu na bahari tangu nina miaka kumi na tatu nilikua navua samaki baharini,, nikaanza kwenda na usiku pia na makarabai,, tunayoyaona huko baharini usiku,, nafkiri barabarani tunaona tom n jery[emoji2] tu

Sent using Jamii Forums mobile app
Ya baharini ndio nilikua nayasubiria kwa hamu mnoooooooo
 
[emoji2] [emoji2] [emoji2] wakija wavuvi na stori zao wanayoyaona baharini usiku,, nyinyi mtajihisi mnaona midoli tu barabarani. kote nime experience najua udereva mpaka uvuvi,, maana kwetu ni karibu na bahari tangu nina miaka kumi na tatu nilikua navua samaki baharini,, nikaanza kwenda na usiku pia na makarabai,, tunayoyaona huko baharini usiku,, nafkiri barabarani tunaona tom n jery[emoji2] tu

Sent using Jamii Forums mobile app
Tupe stori angalau mbili tatu Mkuu. ili na sie tusio wavuvi tufahamu kidogo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ndoto, usingizi na imani za kishirikina.

Hakuna kitu. Why usiku na si mchana??

Why barabarani tu na si njia ya train, Angani au Majini??.

Story za abunwasi na changamsha genge.

Nishasafiri Barabara nyingi, masaa yote kuspan 24 hours sijashuhudia hayo.

Ulongo tu na kutiana woga, kuwapa ulaji waganga wa kienyeji wafanye zindiko.
Usikatae ndugu mimi Nisha kutana. Mambo kama hayo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ndoto, usingizi na imani za kishirikina.

Hakuna kitu. Why usiku na si mchana??

Why barabarani tu na si njia ya train, Angani au Majini??.

Story za abunwasi na changamsha genge.

Nishasafiri Barabara nyingi, masaa yote kuspan 24 hours sijashuhudia hayo.

Ulongo tu na kutiana woga, kuwapa ulaji waganga wa kienyeji wafanye zindiko.
Usikatae

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Enzi hizo nimetoka moshi naenda mbeya nimepanda hood tumefika mikumi basi ikasumbua.tukasubiri ipone kwa mda wa saa tatu,tumekuja kuondoka Giza limeanza,tumefika kitonga SAA NNE usiku.abiria wawil MTU na mkewe wakaomba kushuka eti wamefika.gari ikawashusha,ilibaki gumzo wanaenda WAP na kipindi hicho hata hakujajengwa kituo cha polisi na pana Giza totoro.
Habari wana JF,

Nimekua nikisikia kwamba barabarani Kuna vitimbwi vya mauza uza nikawa siamini, sasa ni juzi nilikua natoka Arusha kuelekea Kibaha. Nilifika sehemu jina silifahamu, ni kijiji baada ya kutoka Mombo.

Ni kwamba nikiwa kwenye mwendo alitokea mtu upande wa kushoto akawa anaingia barabarani Kama vile haioni gari nikapunguza mwendo na kupiga honi, nikitumaini jamaa atasimama ama kustuka, badala yake akaongeza spidi na kuliingia gari upande ule ule wa kushoto mimi na jamaa yangu tukasikia kishindo, side mirror ikavunjika ikaweka na kreki mbaya sana kwenye kioo cha mlango wa kushoto.

Nilisimamisha gari fasta tukashuka na kuangalia tunamuona yule mtu anakwenda tu kwa spidi ile ile, kama vile hakikutokea chochote. Tukawa tunashangaa basi yule mtu akaingia kama kwenye kichochoro Kati ya nyumba mbili, hii nyumba ya kulia Kuna jamaa alikua ameketi kibarazani amepaki pembeni gari aina ya vitz.

Tukamfuata jamaa yangu akamuuliza, Ndugu huyu mtu amekatiza hapa unamfahamu ? Maana tumemgonga na gari tumesimama ili tumtazame lakini cha kushangaza jamaa hakuanguka wala kuyumba ameelekea huku. Cha kushangaza tena, Jamaa akatuambia, nyie mpo salama? Tukamjibu ndio. Akasema basi shukuruni nyie endeleeni na safari. Nikamuuliza mbona hatuelewi?

Badala ya kujibu akabaki ametukazia macho jamaa yangu akanishika mkono na kunivuta tukaondoka. Lakini mpaka sasa hivi tumebaki na maswali vichwani mwetu.

Ni nini hasa kilitokea....

Asanteni
 
Enzi hizo nimetoka moshi naenda mbeya nimepanda hood tumefika mikumi basi ikasumbua.tukasubiri ipone kwa mda wa saa tatu,tumekuja kuondoka Giza limeanza,tumefika kitonga SAA NNE usiku.abiria wawil MTU na mkewe wakaomba kushuka eti wamefika.gari ikawashusha,ilibaki gumzo wanaenda WAP na kipindi hicho hata hakujajengwa kituo cha polisi na pana Giza totoro.
Mkuu ulishindwa kuwauliza ? au uliogopa wangeshuka na wewe ?[emoji851][emoji851][emoji851]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Dah hata konda alibaki mdomo wazi
Kuna jamaa yangu amenipigia simu anasema, Kuna siku alikua anarudi Nyumbani Area C, saa sita usiku. alikua taxi driver, kufika eneo la round about ya kuelekea Area C akasimamishwa na mdada amevaa ijabu, jamaa anasema alimpa maelekezo sehemu anapotaka kwenda. jamaa anasema alipo fika maili mbili aliuliza ni njia Ipi ili afahamu mapema pa kuingilia, lakini aliona kimya akamuuliza tena akaona kimya, ikabidi apaki pembeni akageuka nyuma akakuta siti tupu. jamaa anasema alifungua mlango na kukimbia, gari aliifuata asubuhi na kwenda kukabidhi kwa mwenye gari. Ndio ikawa mwisho wa yeye ku taxi driver. ni miaka ya tisini kwa mujibu wake. jamaa anaishi Dom.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ni safari moja tu ndio nimewah kufika home late saa saba halaf home sikusema kama nakuja na niko hivo hua wananishtukia tu nipo, lakini sijawah kukumbwa na hiyo kadhia tena napenda sana kufika home usiku sema sio wa manane

Kuna siku pia tulienda shamba la moja la mkonge liko mnazi, ni mbali tulikua kama watu wanne nikiwa mwanamke alone kwenye ule msafara, wakat tunarud dereva akasema tuchanje mbuga kwa mbuga tusipite ya lami tutazunguka sana tulipokua mbugan gari sjui ilikanyaga nn ikaserereka karib iingie kwenye kidaraja tukashuka hatukuona chochote tukaendelea kuja tokea sehem kunaitwa maramba tayar usiku saa mbili hivi, tukatembea hapo hakuna alieku na waswas kuhusu nn tulikanyaga kufika eneo linaitwa gombero alitoka nyoka upande wa dereva anavuka dereva akamkanyaga tena nikapiga kelele nyoka ikabidi tuangalie hatukuona kama amekanyagwa sikua na waswas kabisa leo ninesoma hapa nimerecall hayo matukio maybe yawezekana n hayo mauza uza au ilikua kweli
Ni hayo mauza uza tu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nishakutana na mwanamama,anatembea katikati ya barabara saa 7 usiku ukipita chalinze mjini kama km 15 kwendea dar,nilimkwepa na nilikua zaidi speed 120,niliokua nao kwenye gari wakanilaumu sana kwann sikumgonga eti yule ni jini,nikawaambia mbona nimemkwepa na tunaendelea na safari,kuna wengine wanakua wamerukwa akili tu,unamgonga then unafupisha maisha ya binadamu mwenzio kwa ajili ya kuamini imani za ajabu ajabu!

Sent using Jamii Forums mobile app
Saa 7 mtu anatokea wapi jamani?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom