Kwa mambo kama haya Dada zangu mnajiharibia sana kisha baadaye mnatulaumu

Kwa mambo kama haya Dada zangu mnajiharibia sana kisha baadaye mnatulaumu

Ndio walivyohao, juzi kuna mmoja tulikutana Makao makuu ya nchi nikampeleka Royal tumefika anamuuliza mhudumu ampe menu ya vyakula vyakizungu nilivyoona hvyo nikakumbuka alishawahi nisumbua kuagiza pizza na milk shake ambayo aliiacha akisema ni mbaya inasukari nyingi, basi mm nikaagiza makange ya kuku yakaja akaonja akasema yana chumvi, mm nikala nikamaliza na pepsi baada ya hapo akasema anataka bites tena za supermarket usiku wa saa 7 nikaona poa kwa nje kuna maduka lakini chakushangaza akanunua chocolate zile kubwa mbili na maziwa.
Kesho yake nikampeleka sehemu pale wanaita oven....akaagiza pizza na milk shake alivyoanza kula akaniambia hajapenda hiyo ladha hivyo abadili na mm nikamkata jicho.
Kesho yake tena nikampeleka Mwambao tukaagiza but yeye aliagiza vitu vingi nikamwambia cha msingi umalize ila mwisho wa siku aligusa kila kimoja akasema ameshiba
Jioni akasema anataka sehemu iliyotulia, pale mwambao kwa juu kulia kuna mgahawa flani kama wakihindi umetulia. Tukafika akapewa menu alivyochagua akaambiwa hamna kwa sasa ikabd achague upya.
Baada ya hapo kwakuwa kesho tulisafiri kurudi makwetu akaniambia tutafute maduka ya nguo nikamwambia tayari tumeshatumia zaidi ya 300k so imetosha

Nilichogundua baadhi ya wanawake wanakuwa single mother kwa sababu ambazo huwa wanajitakia wenyewe kwasababu huyu alikuwa anachagua chakula chenye gharama kubwa kuliko chochote kwenye menu. Ukiachana na dread alizotaka kusuka kwa 100,000
Swali la msingi...mbususu ulikula?
 
Hiyo ndo shida ya kujifanya good samaritan. Kwanin usinyooshe maelezo? Mwambie wazi kua mnaenda hosp but una 50k te atajua atapimaje? Af kupima kwan lazma iwe "hospital anayoipenda?" Rapid tests ni zile zile kila hospital mayb kama anafanya CT Scan.
Af na we pia mjomba uwe mkweli tu wacha udomo zege. Kama umeenda kupiga kwa gia ya hospital mwambie mapema kabisa. Tena mshauri achukue na panadol ukimueleza wazi kua utakapomaliza kumshughulikia atazihitaji kupoza maumivu.
 
Ameshakuonyesha tabia yake iliyofanya wenzako wamkimbie, wewe unasubiri nini [emoji23][emoji23][emoji23]
 
Wewe ndio Hazimo bora hata huyo Mdada. Wanaume watatu wamemkimbia ww unahisi unaweza kukaa naye. Tatizo la Wanaume wengi Huruma zinawasumbua sana.

Achana na Huyo Akili hana. Na sometimes Huko kwao keshalaaniwa. Wazazi washamshundwa.. Ndugu washamlaani ww unapeleka pua yako
 
Kwenye kikao Hatujakubaliana kuwaita mademu wetu Dada hata kama Hatuwakubali ..Heshima ibaki palepale ni mademu wetu wanatulinda sana sema sisi hatuna shukrani.
 
Huko sio kushiba ni kufuru. Kwanza akishiba sana hiyo shughuli yenyewe aweza iona kero
🤣🤣🤣🤣 Labda yeye anaoend kula sana akishaingia ulingoni anapanua mapaja kazi kwako wewe mwanaume. Yeye kashapata raha yake huko kwenye chakula
 
Ndio matatizo ya ku-date singo mazaz!! Yaani huwa wanaona wanaume kuwa ni ATM zao tu. Dawa yao ni hii akikuomba pesa we mwambie huna. Kata nae mawasiliano utafute mwanamke anaejielewa na kujua thamani ya pesa za mwanaume. Ukiona mwanamke ana watoto wawili na kuendelea, tena kwa wanaume tofauti jua kuwa ni kimeo ,usirushe ndoano yako hapo ,utavua miba tu
 
Kwa sema wako huo alipaswa alipe fadhila kwa kukupatia mtoto mmoja miongoni mwa nao alionao!
 
Nakumbuka ilikuwa Jmosi fulani hivi, dada mmoja ambaye ni rafiki yangu alinipigia simu. J uko wapi? Nikamwambia niko getho. Nimeboreka home bana, tunaweza kutoka? Nikasema poa.

Tukaenda kijiwe fulani hivi, mi nilibeba 50,000.00. Tulikaa kuanzia saa 10 hadi saa 6 usiku. Nilitumia kama 23,000.00 tu, maana situmii wine, sijui bia. Labda Maji. Mwenzangu sasa, anakula hiki anaacha, mara sijui mbona ladha yake, sijuii nini, mara ili Mradi tu anikomoe!

Mara nifungieni niwapelekee watoto, ana watoto wawili, na msichana wake wa kazi + mdogo wake. Bill inakuja napewa Mimi kulipa 129,000.00/=

Nikamwambia mhudumu, naomba unipe ya kwangu kwanza! Akarudi akaniletea 23,000.00, then akampa yule dada 106,000.00. Nikatoa 30,000.00 nikaomba Chenji yangu. Akanipa 7,000.00 yangu nikatulia.

Namwambia lipa twende, anasema hana hela. Nikamwambia naondoka. Mhudumu nafikir mi sidaiwi naondoka. Akasema hudaiwi kaka, nikanyanyuka. Hivi kweli J ndo unaondoka bila kulipa, mi nishalipa wee ndo hujalipa! Lipa twende!

Akainuka akaenda pembeni, akaongea na simu, baada ya maongezi yale akamuuliza mhudumu unaweza kupokea kw M-pesa! Mhudumu sawa tu, ila uweke na ya kutolea. Mhudumu alivosema tu, nimeiona. Akanyanyuka bila kuniaga!

Tuko nae ofisi moja, hadi Leo hata nikimwambia tukanywe, chai naona anachungulia kwenye wallet yake kwanza, ndo ananyanyuka.
 
Huyu dada ni rafiki yangu kiasi flani maana tuliwahi kuwa karibu kipindi cha nyuma. Nmekuja kutana naye this time ana watoto watatu wana baba tofauti.

Na hawa baba zao wote wamemwachia yeye watoto. So anahangaika nao sana. Nilipokutana naye tukaongea nilimwonea huruma sana.nikawaza how to help her. Sikumwambia lolote lakini.

Juzi kaniambia anaumwa UTI nikaona leo nimpeleke Hosp. Kwa roho safi kabisa. Pamoja na kuwa najua ana Bima maana anafanya kazi Serikalini.

Akanitajia jina la Hosp flani ndo anapenda aende huko. Nikampeleka.... Tumeenda amepima kila ugonjwa mwilini na kuchukua dawa nyingi sana. Yaani alikuwa anaomba tu apimwe kitu flani,apimwe na hiki, apimwe na kile....

Mwishowe akawa anaomba apewe dawa na nyingine anazo kwenye simu anaomba aandikiwe apewe. Analeta Bill Tsh 378,000. Nilipe. Kweli nimelipa. But ameni disappoint sana. Anaonekana hana utu au hajui thamani ya pesa ya mwenzie.

Wakati mimi nlidhani ataangalia tu UTI ,Typhoid na Malaria. Then tutoke twende fanya shopping ya vyakula awapelekee watoto. Yeye kaona watoto wake wataenda kula madawa.

Tunatoka ananambia "sasa tunaelekea wapi My?" Nimemjibu tu nyumbani kwako.

Anaonekana hajafurahi. Tunarudi ananiambia 'yaani hapa sijui hata nachowaza My.... Nyumbani nimeishiwa kila kitu" nimejisikia uvivu hata kumjibu. Nimeona tu huyu dada akili hana.

Last week tumetoka out akawa anaagiza vinywaji vya gharama na kuku mzima ambaye hakummaliza nikadhani atabeba apeleke nyumbani. Akaacha. Nlimwambia basi si bora angeagiza nusu. Akajibu tu hakutegemea kuku angekuwa mkubwa kiasi kile. Simple like that.

Nimeshindwa namna ya kuendelea kuwaza msaidia. Maana naona hasaidiki. Sijui anawaza nini. Dada mzuri sister du but kichwani mweupe kabisa. Huku analalamika kuwa wazazi wenzie wamemwachia tu watoto ahangaike nao peke yake.

Imeniumiza sana. Akina dada muwe na subra, uvumilivu na upendo. Usimkatishe tamaa mtu anayetaka kukusaidia.

Ujinga ni kudhani wanaume walioshindwa single mother hawajui kujali,hakuna mwanaume mwenye akili timamu anayemwacha Mwanamke anayejitambua
 
Yaani katika Mambo ya chakula mtu akiacha chakula huwa namuona mshamba na limbukeni wa kupitiliza,kwa Nini uagize kitu hujawahi kula lakini?sijui huwa wanawaza Nini hata!
Nyumbani kwangu ukipakua sahani hairudi nyeupe hata Kama mgeni ukishashika ukasema Asante nauliza hiki nikakitupe??anaona aibu
[emoji23][emoji23][emoji23]
 
Back
Top Bottom