Wakati Mama Samia anatangaza mkakati wake wa kuwapanga upya machinga kwenye maeneo mbalimbali, nilibarikiwa kuwa mmoja wa watu wa mwanzo kabisa kutoa ushauri wangu humu!
Huna hoja wala mchango wa msingi kwenye hili, hujielewi, hulijui tatizo wala huwezi kuwa na suluhu unaongeaongea tuu sababu ya chuki zilizokujaa, choyo, roho mbaya na ubinafsi. Ukipunguza roho mbaya na kufurahia maumivu ya wengine utaweza kujenga hoja za msingi na zenye maendeleo kwako na...
www.jamiiforums.com
Wakati naandika hii thread nilitoa haya Mawazo nikiamini kuwa yakifanyiwa kazi yataleta matokeo!
Baadae Waziri Mkuu wa JMT Ndug Kassim Majaliwa alifanya kikao na Wakuu wa Mikoa na akatoa maagizo ambayo nashukuru Mungu Kwa sehemu fulani yalitoka kwenye thread niliyoiandika hapa JF
Nirudi kwenye mada!
Watu wengi walipoona Rais Samia anatoa yale maagizo walifikiri kuwa kamwe hayatofanikiwa, Kuna wengine walidhani kuwa ndo Kama maagizo ya siku zote ya wanasiasa wa Tanzania ambayo hayazingatiwi, Kuna wengine walidhani as long as ni mwanamke basi ni dhaifu hivyo maagizo yake hayawezi kufanyiwa kazi, Kuna kundi lingine ni kwa chuki zao tu walimkatisha tamaa Mama samia na kuongea maneno ya kejeli kumdhihaki ili kumfanya aone tu hatoweza!
Nimekuwa jijini Dar es Salaam kwa wiki sasa na nimetembea sana Jiji la posta na hata maeneo ya Ubungo na mwenge, napenda kusema kwa sauti kuu na moja HONGERA MAMA SAMIA, ZOEZI LINAKWENDA VIZURI NA SURA YA MJI WETU WA DAR UNAOJENGWA KWA GHARAMA KUBWA NA SERIKALI IMEANZA RASMI KUONEKANA.
Nilisema humu na ninasema tena, suala la machinga kamwe, haliwezi kuwa mfupa mgumu kwa serikali, kilichokuwa kunasababisha kutokea yale tuliyokuwa tunayaona awamu ya tano kurudi nyuma ni
1. Viongozi kukosa commitment ya kushughulikia mambo ya msingi
2. Siasa ya kijinga, uvivu na uzembe kwa viongozi hasa Wakuu wa Mikoa, Wilaya na Wakurugenzi wa Majiji na Halmashauri
3. Ushamba na kukosa exposure
Kwa mwezi sasa tumeona viongozi wakikomaa kushughulikia suala la machinga na sasa imeanza kuonekana kuwa kumbe inawezekana Kwa machinga kupangwa na kufanya biashara kistaarabu
Kwa Mafanikio haya niliyoanza kuyaona sasa napenda kuishauri Serikali ya Awamu ya Sita kuzingatia haya
1. Msibweteke kwa mafanikio mliyoanza kuyapata hasa baada ya machinga wenyewe kukubali kupangwa baada ya serikali kuweka msisitizo! Maeneo Yaliyokuwa wazi sasa yawekewe ulinzi na utaratibu maalum ili kutoruhusu hali ya huko nyuma kujirudia tena
2. Kuwe na by laws za faini na hata kufanya kazi za kijamii kwa watu wanaokiuka taratibu na kurudi kwenye maeneo waliyoondolewa
3. Ziundwe kamati za wafanyabiashara wenyewe kusimamiana wenyewe ili kutoruhusu sheria kuvunjwa tena na hali kurudi Kama ilivyokuwa.
Mf. Kwa kariakoo Wafanyabiashara wa pale waunde kamati zao na vikundi vyao vya kusimamia usafi na ufanyaji biashara kwa kuzingatia taratibu . Kamati hizi sipewe meno na mamlaka ya kuadhibiana wenyewe kwa wenyewe pale taratibu zilizowekwa zinapokiukwa
4. Kwa maeneo wanayopelekwa machinga! Naomba sasa mkazo uwekwe huko, miundombinu Bora na ya kisiasa ijengwe huko. Wafanyabiashara hawa wapangwe na kusimamiwa vizuri chini ya kamati za wao wenyewe watakaoziunda. Wapangwe kisasa na kistaarabu kwa kuzingatia aina ya biashara wanayofanya
Wafanyabiashara hawa wawekewe utaratibu mzuri wa kulipa kodi kidogo kidogo na jamii ielekezwe kwenye kununua bidhaa kwenye maeneo hayo walikopangiwa wafanyabiashara hao. Vijengwe vituo vya mabasi kwenye maeneo hayo ili ununuzi wa bidhaa uwe rahisi
Wakati Mama Samia anatangaza mkakati wake wa kuwapanga upya machinga kwenye maeneo mbalimbali, nilibarikiwa kuwa mmoja wa watu wa mwanzo kabisa kutoa ushauri wangu humu!
Huna hoja wala mchango wa msingi kwenye hili, hujielewi, hulijui tatizo wala huwezi kuwa na suluhu unaongeaongea tuu sababu ya chuki zilizokujaa, choyo, roho mbaya na ubinafsi. Ukipunguza roho mbaya na kufurahia maumivu ya wengine utaweza kujenga hoja za msingi na zenye maendeleo kwako na...
www.jamiiforums.com
Wakati naandika hii thread nilitoa haya Mawazo nikiamini kuwa yakifanyiwa kazi yataleta matokeo!
Baadae Waziri Mkuu wa JMT Ndug Kassim Majaliwa alifanya kikao na Wakuu wa Mikoa na akatoa maagizo ambayo nashukuru Mungu Kwa sehemu fulani yalitoka kwenye thread niliyoiandika hapa JF
Nirudi kwenye mada!
Watu wengi walipoona Rais Samia anatoa yale maagizo walifikiri kuwa kamwe hayatofanikiwa, Kuna wengine walidhani kuwa ndo Kama maagizo ya siku zote ya wanasiasa wa Tanzania ambayo hayazingatiwi, Kuna wengine walidhani as long as ni mwanamke basi ni dhaifu hivyo maagizo yake hayawezi kufanyiwa kazi, Kuna kundi lingine ni kwa chuki zao tu walimkatisha tamaa Mama samia na kuongea maneno ya kejeli kumdhihaki ili kumfanya aone tu hatoweza!
Nimekuwa jijini Dar es Salaam kwa wiki sasa na nimetembea sana Jiji la posta na hata maeneo ya Ubungo na mwenge, napenda kusema kwa sauti kuu na moja HONGERA MAMA SAMIA, ZOEZI LINAKWENDA VIZURI NA SURA YA MJI WETU WA DAR UNAOJENGWA KWA GHARAMA KUBWA NA SERIKALI IMEANZA RASMI KUONEKANA.
Nilisema humu na ninasema tena, suala la machinga kamwe, haliwezi kuwa mfupa mgumu kwa serikali, kilichokuwa kunasababisha kutokea yale tuliyokuwa tunayaona awamu ya tano kurudi nyuma ni
1. Viongozi kukosa commitment ya kushughulikia mambo ya msingi
2. Siasa ya kijinga, uvivu na uzembe kwa viongozi hasa Wakuu wa Mikoa, Wilaya na Wakurugenzi wa Majiji na Halmashauri
3. Ushamba na kukosa exposure
Kwa mwezi sasa tumeona viongozi wakikomaa kushughulikia suala la machinga na sasa imeanza kuonekana kuwa kumbe inawezekana Kwa machinga kupangwa na kufanya biashara kistaarabu
Kwa Mafanikio haya niliyoanza kuyaona sasa napenda kuishauri Serikali ya Awamu ya Sita kuzingatia haya
1. Msibweteke kwa mafanikio mliyoanza kuyapata hasa baada ya machinga wenyewe kukubali kupangwa baada ya serikali kuweka msisitizo! Maeneo Yaliyokuwa wazi sasa yawekewe ulinzi na utaratibu maalum ili kutoruhusu hali ya huko nyuma kujirudia tena
2. Kuwe na by laws za faini na hata kufanya kazi za kijamii kwa watu wanaokiuka taratibu na kurudi kwenye maeneo waliyoondolewa
3. Ziundwe kamati za wafanyabiashara wenyewe kusimamiana wenyewe ili kutoruhusu sheria kuvunjwa tena na hali kurudi Kama ilivyokuwa.
Mf. Kwa kariakoo Wafanyabiashara wa pale waunde kamati zao na vikundi vyao vya kusimamia usafi na ufanyaji biashara kwa kuzingatia taratibu . Kamati hizi sipewe meno na mamlaka ya kuadhibiana wenyewe kwa wenyewe pale taratibu zilizowekwa zinapokiukwa
4. Kwa maeneo wanayopelekwa machinga! Naomba sasa mkazo uwekwe huko, miundombinu Bora na ya kisiasa ijengwe huko. Wafanyabiashara hawa wapangwe na kusimamiwa vizuri chini ya kamati za wao wenyewe watakaoziunda. Wapangwe kisasa na kistaarabu kwa kuzingatia aina ya biashara wanayofanya
Wafanyabiashara hawa wawekewe utaratibu mzuri wa kulipa kodi kidogo kidogo na jamii ielekezwe kwenye kununua bidhaa kwenye maeneo hayo walikopangiwa wafanyabiashara hao. Vijengwe vituo vya mabasi kwenye maeneo hayo ili ununuzi wa bidhaa uwe rahisi
Swala la machinga nampongeza Rais kwa kutoa maamuzi magumu machinga walishakuwa kero pia vibanda na uchafu ilikuwa aibu kwa majiji makubwa ilifanya tuonekane nchi ka ya vichaa, pia nimpongeze Makele jiji limeanza kuwa safi kuanzia Mwenge, ustawi na kwingine aisee vile vibanda plus mbao ulikuwa uchafu uliokubuhu Hadi nawaza kwanini machinga hawana aibu na hawajali usafi?
Swala la machinga nampongeza Rais kwa kutoa maamuzi magumu machinga walishakuwa kero pia vibanda na uchafu ilikuwa aibu kwa majiji makubwa ilifanya tuonekane nchi ka ya vichaa, pia nimpongeze Makele jiji limeanza kuwa safi kuanzia Mwenge, ustawi na kwingine aisee vile vibanda plus mbao ulikuwa uchafu uliokubuhu Hadi nawaza kwanini machinga hawana aibu na hawajali usafi?
Inaonekana viongozi wa mikoa wamepewa maagizo,maana Makala kasema Machinga endapo itafika tarehe 30 halafu wakarudi katika maeneo yao basi ye atakuwa kaehindwa kazi.Kwa sentensi nawashauri waleachinga wabishi wajiondokee wenyewe wasishupaze shingo.Muda huu watumie kutafuta sehemu nyingine za fursa
Serikali ya Samia ni serikali ya watoto wa mjini,hiyo michezo yote naamni Samia anaijua.Na serikali yake haina mchezo na kodi.Soon atawafikia,ngoja aweke sawa hili la wamachinga.In short mama anataka kila mtu alipe Kodi
Mimi nina mtazamo binafsi kuwa asilimia fulani ya Machinga ni watu wa mfumo. Wanatumika kufanya surveillance, kukusanya data na kusambaza propaganda. Hili zoezi ni geresha tu, ndiyo maana maeneo hayo hayo wanapoondolewa, kuna vibanda bado vimebaki.
Hauwezi kuniambia Serikali haikuwa inaliona hili tatizo hadi limekuwa kubwa hivi. Kuna maeneo kabisa wanajenga vibanda hadi unajiuliza haiwezekani huyu kufanya hivi bila kuwa na baraka za mamlaka husika.
Mnamlaumu tu Magufuli kwenye hili. Machinga na mauchafu yao wamekuwepo hata kabla ya Magufuli kuwa Rais. Labda useme ruhusa yake ilifanya hali kuwa mbaya zaidi ila tatizo tayari lilikuwepo na tayari lilikuwa kubwa.
Hivi mandate ya kusema Kwa kuwa Rais ni nwanamke mnaitoa wapi .to be honest hii kauli binafsi inanikera na inanikera hata pale inaposenwa na mama mwenyewe it's disgusting to hear such statement .
Alaumiwe aliyekuza utamaduni kuwa, katika wazazi wawili, mtoto abebe jina la mwenye uume hata kama mwenye uume ni dhaifu na hana mchango katika malezi na mafanikio ya mtoto. Sisi wenye uume tunatembelea hiyo nyota na hatutaki ife.
Hongera kwa kazi nzuri, miji kwa kweli ilikuwa michafu, nakumbuka kuna wakati Makonda alijitahidi kuisafisha kariakoo lakini jiwe akaamuru waachwe wajinafasi, kwa hili jiwe was absolutely wrong.
Ila kumbuka, umetatua tatizo kubwa...umeibua tatizo kubwa, the jobless.. the kipatoless, soon ukabaji, udokozi na wizi utaanza. Unless measures za uhakika zichukuliwe kunusuru hii hali.
Tusirudie kumpa nchi tena mfuga mifugo mshamba mtu mwenye nongwa. Magufuli kaenda Na aoze kabisa. Ila kuna Antipas Lissu huyo ni wa hovyo zaidi ya Magufuli anaweza ingia Na machungu yake akaruhusu biashara ya umalaya mpaka misikitini Na makanisani.
Tusifanye hilo kosa Kwa watu hao. Lissu ni HOVYO kuliko Magufuli.
Povu [emoji3475] [emoji3476] RUKSAAAA
Mi nafikiri hata somo la usafi na haiba liludishwe mashuleni ili kujenga tabia ya watu kupenda usafi, tabia ikijengwa angali watu wana umri mdogo hakika itaendelea. Tuna barabara zinajengwa kwa gharama kubwa sana lakini unakuta mitaro yake imegeuzwa kuwa majalala, mitaani ni wachache sana wanaojali usafi. Hili tatizo ni zaidi ya kuweka sheria, kuna ustaarabu na tabia ambayo kama taifa inabidi tuanzie kwenye msingi wa malezi ya watoto wadogo
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.