Kwa mara ya kwanza nimeona mwanaume analia kwa sababu isiyohusisha msiba wala mapenzi

Seems na wewe umesapoti rafiki yako kuzaa na binamu yake

Mshauri atoke hapo akatafute kazi
Akiwa na pesa itafuta aibu zake zote
Anakaa hapo anaendelea kulia Lia itamsaidia nini
 
Hawa wazazi ukifanikiwa ndio wanakupenda

Wazazi wachache sana hasa wakina mama ndio wanampenda mtoto ata akiwa situation gani, wazee wanazinguaga sana. Yalishanikuta
Wamama wa hivi ndio wanafuga vibaka, panya road na majambazi. Hongera mshua wako kukukazia huenda ungekuwa kipanya road kikuu sasa hivi
 
Hawa wazazi ukifanikiwa ndio wanakupenda

Wazazi wachache sana hasa wakina mama ndio wanampenda mtoto ata akiwa situation gani, wazee wanazinguaga sana. Yalishanikuta
Kina mama ndio wanaoharibu vijana wao kwa kuwatetea na kuwafichia Siri, Tena baba akisema mama anapanda juu ya meza kumtetea mtoto mavuno ndio hayo, miaka 28 nyumbani anatafuta nini?
 
Kina mama ndio wanaoharibu vijana wao kwa kuwatetea na kuwafichia Siri, Tena baba akisema mama anapanda juu ya meza kumtetea mtoto mavuno ndio hayo, miaka 28 nyumbani anatafuta nini?
Anapanda juu ya meza😃😃
 
Hawa wazazi ukifanikiwa ndio wanakupenda

Wazazi wachache sana hasa wakina mama ndio wanampenda mtoto ata akiwa situation gani, wazee wanazinguaga sana. Yalishanikuta
Wewe, huyo jamaa and the like .. ndiyo mnazingua.
Wazazi wametimiza wajibu wao wamekuzaa, kukulea na kukusomesha, umefikisha 25yrs bado unataka wakubebe?
Mbaya zaidi unawaongezea mzigo kuwapa mtoto wako wamlee wakati Sasa ni wakati wao wa kupumzikia na kula pesa zao.
 
Sometime hali ngumu vijana wanazitafutaga wenyewe.

Wala wasitafute huruma, wakomae na matatizo yao yaliyotokana na ujinga pamoja na uzembe wao.

Tena huyo mzee akaze kabisa hadi huyo jamaa atoke hapo.

Ningekuwa mimi ndio huyo mzee, Ningemfurumusha huyo jamaa.
 
Rafiki yako aliyataka hayo. Mtu kaja na hasira zake na anaondoka kwa haraka akiwa na hasira unamsimamisha unamuomba hela ya penseli ya mwanao kweli? Kichwani hayupo vizuri, umri miaka 28
Huyo mzazi wake ana busara sana. Alikubali kusimama na kumsikiliza huyo kijana mfedhuli na kumwambia hela ameiacha wapi. Kijana hana hata aibu kumkimbilia mzazi (at the age of 28yrs) kuomba hela kama mtoto wa chekechea.
 
Dah,Nampa pole mshkaji..Kuzaa na binamu na hata kumuoa sio tatizo kwa watu wengi tu,labda tamaduni za kabila la jamaa yako ndio makosa.
Kwangu Mimi hio sio laana.
Jamaa yako Angekuwa na misuli ya kipato Wala kusingekuwa na tatizo.
Mshauri aondoke nyumbani,akapambane.Akawe hata saidia fundi kwanza,akifanya kwa muda naye anaweza akawa fundi mzuri tu.
Unasema hakumaliza chuo,kwa maana hiyo Hana fani,atafute fani afanye kazi zake,alee mtoto wake.
Mambo ya kung'ang'ania kukaa home tu na huna kipato dharau lazima zitakuwepo tu.
Hata mbwa wenu wataanza kukubwekea!
Saidia fundi anakula 15k-18k per day,jamaa yako akiipata hii anaenda kupanga chumba mbande Cha 20k anafanya Maisha!
Mwambie aache uoga,atajiua Bure!
 
Situation ya kuwa bulled na kunyanyapaliwa na mzazi wengi tumepitia, na wakati mwingine Kwa kutuhumiwa vitu vya kusingiziwa, nakumbuka na mm nilisingiziwa kupitan na binamu yangu ambae tulikuwa karibu sana..Solution ni kunyanyuka na kwenda kusaka maisha mbali, hiyo misamaha wataombana baada ya muda hasira zikitulia na mhanga akiwa tayari ameshajitegemea kimaisha.
 
Unaendaje kusaka maisha hauna kianzio mjomba? Halafu huyo hakutuhumiwa bali alikiri mwenyewe hata akazaa na huyo binamu yake.
Ni kweli na ni sahihi utekelezaji ufanyike hasira zikitulia - Kwani hasira hasara
 
Kabisa mkuu akiondoka akaenda kujitafuta hata mzee hasira inapungua maana amuoni badae anakuja kuomba msamaha tu.
 
Vijana nao watuelewe wazazi wao....sio unaona tuna mood mbaya unaanza kituongelesha kwani kulikuwa na ulazima gani kuongea nae muda huo kama wewe tu mgeni ulihisi mzee kaingia kwa makasiriko,angemlia ganzi tu
 
Unaendaje kusaka maisha hauna kianzio mjomba? Halafu huyo hakutuhumiwa bali alikiri mwenyewe hata akazaa na huyo binamu yake.
Ni kweli na ni sahihi utekelezaji ufanyike hasira zikitulia - Kwani hasira hasara
Hapo mtaani akiona fundi ujenzi akaanze kuomba kazi ya saidia.
Atazoeleka na mafundi ataanza kupata pesa kidogo ya kuanzia maisha.
Aende hata kijiwe Cha madalali akaanze kazi ya udalali wa nyumba , magari, Viwanja na mashamba.
Tatizo vyeti vyetu vya shule wengi wanawapa aibu ya kufanya kazi flani.
 
Vijana wajifunze kuchakarika na kujitafutia maisha.
Unyoronyoro wa kuogopa kupambana na maisha , unadharulika na hata wazazi wako.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…