Kwa mshahara wa Tsh. 765,000/= nikizama benki naweza kopesheka kiasi gani?

Kwa mshahara wa Tsh. 765,000/= nikizama benki naweza kopesheka kiasi gani?

Usimdanganye mwenzio. Sababu yake kuu ya kukopa ni NJAA, kasema mwenyewe.
Anataka akope mkopo wa juu zaidi kuweza kukopeshwa kwa sababu ana njaa.

Mtumishi unatakiwa ukope ukiwa na biashara au mradi wako ambao umefanya kwa hela za kudunduliza au hela ya kupata kwenye chanzo kingine ila sio mkopo wa riba. Ufanye kwa muda hata zaidi ya mwaka, uanze kupata faida na hasara uzoee hicho kitu, ukue uache kutumia hadithi na simulizi badala yake utumie uhalisia na uzoefu.
Baada ya hapo ukope ili kuendeleza na kukuza hiyo shughuli. Tena napo haukopi mkopo wa kiasi cha juu kabisa kinachowezekana.

Anza kufuga mbuzi au nguruwe, anza kununua mazao kwenye msimu, anzisha biashara ya miche ya miti na matunda, anzisha duka la spare parts au nguo au viatu au vyombo vya ndani, etc. Fanya kwa muda fulani mpaka uwe na uzoefu kisha ndio ukope benki kuanzia kiasi kidogo na unapanda taratibu.
Miaka kadhaa baadae utakuwa na uwezo wa kukopa hata 70M bila wasiwasi. Sio unapigwa njaa unakopa kujimaliza ili ununue sabufa na pikipiki used ya Sanya, na TV ya Aborder ukutani, hela inayobaki ukarabati nyumba.

mkarimani feki dunia sio mama yako, miaka minne ijayo hakuna atakayekuhurumia leo hii ukikopa kisa una njaa.
daah umeponda ila umenipa fact
 
chukua tu boss, mimi sikukopa miaka mitano nilikuwa nakataaa kama wewe kuna mwamba akakopa akajenga(kiwanja alikuwa nacho) mimi ambae nilikuwa sitaki kulambwa miaka mitano ikaisha bado nimepanga hapo nimenunua kiwanja tu, mwamba kamaliza mkopo mwezi huohuo akanyonya akachukua ndinga kali hapo ndo akili ikanisogea nikaenda kunyonya nikajenga saivi nakaa kwenye nyumba kali ila sina hela natembelea moja ya tatu.

nilijidai vimiradi uchwara nimepoteza tu mida, niliona nikope tu nijenge baada ya kupata mtoto wa pili familia imekuwa na hizi mambo za kupanga. wewe unaweza kukimbia hayo makato sababu huna majukumu mengi ila ukiwa na majukumu mengi wala hutajali kwenda benki kujitia kitanzi halafu unakaza shingo mpaka mkopo unaisha.
ushauri mzuri mkuu
 
Mimi nina mshahara kama huyo jamaa ninaishi,niko kwangu,nina nyumba mbili, Sijawahi kulala njaa, mwaka huu january napeleka mtoto wangu English medium school,karo 2M,mwaka jana ndani ya miezi miwili nimekamilisha nyumba ya 13M.


Take home yangu ni 270K


Acha kuogopesha watu, jamaa kama anajiweza akope
Inaonekana iyo business unayofanya inakulipa.
 
Usikope kununua sofa na TV wala kujenga kama una idea ya biashara ndio ukope na utakachopata kwenye biashara kidogo kidogo ndio uanze kujenga maana mnapenda kujenga hata kama uwezo wa kujenga hauna baadae unaipeleka nyumba Bank kukopa huku mtaji ukiwa hauna...unapotaka kukopa inatakiwa ufanye feasibility study ya kutosha ukiona majibu sio sawa achana na mkopo mpaka utakapopata wazo zuri la biashara na hiyo biashara ufanye mwenyewe kwa usimamizi wako sio sijui mtoto wa Mjomba utaishia kumkata kichwa tuu wakati biashara ndio zilivyo...
Haya muelekeze time management ili aweze kubalansi kazi yake na kuisimamia biashara anayoiwaza.

Pili umkumbushe biashara haianzishwi kwa pesa ya mkopo.

Tatu mwambie ili isimame hiyo biashara inahitaji muda na mtaji.
Kimoja kikikosekana itaanguka.

Tano mpe kabisa takwimu za biashara mpya zinazoanzishwa, ni asilimia 5 tu ndio zinadumu.

Hapo hujaangalia kama zinazalisha faida au lah!

La sita na mwisho hatujajua kazi ya anayofanya

La saba je ana elimu ya fedha, kama Hana mwambie aangalie ambacho ni rahisi kukimanage.
 
15million had 21

[emoji91][emoji2781][emoji3][emoji2]
Kopa kistaarabu
Screenshot_2024-01-01-20-51-00-599_com.financial.calculator.jpg
 
Nenda Bayport mkuu,ili uone rsha ya mkopo.
Kwa maana umekuja kututambia huku kuwa unamshahara.
Kawashirikishe ndugu zako Kwanza mkuu.
Ila baadae usije Anza kutulilia humu na kuwatupia lawama Serikali.
 
Mnaomshauri akope 25M
Mwambieni pia atalipa 47,318,177.1(47M),
Mwambieni katika hio 25M cash atakayopata ni 22.5M.
Mwambieni atakatwa 438,131.27 kila mwezi kwa miaka 9.
Mwambieni jumla ya riba atakayolipa ni
22,318,177.1.
Mwambie katika 47M atakayolipa,
Yeye atachukua 22.2M na 24.5M anawaachia Bank.
Mwambieni ni sawa kutoa 226,851 kila mwezi kwa miaka 9 kulipa riba tuu.
Mwambie hio pesa Akiamua kujitunzia mwenyewe angetumia miaka 4 kuipata, huku ⅓ ikibaki pale pale.

Akili Kukichwa.
 
Mnaomshauri akope 25M
Mwambieni pia atalipa 47,318,177.1(47M),
Mwambieni katika hio 25M cash atakayopata ni 22.5M.
Mwambieni atakatwa 438,131.27 kila mwezi kwa miaka 9.
Mwambieni jumla ya riba atakayolipa ni
22,318,177.1.
Mwambie katika 47M atakayolipa,
Yeye atachukua 22.2M na 24.5M anawaachia Bank.
Mwambieni ni sawa kutoa 226,851 kila mwezi kwa miaka 9 kulipa riba tuu.
Mwambie hio pesa Akiamua kujitunzia mwenyewe angetumia miaka 4 kuipata, huku ⅓ ikibaki pale pale.

Akili Kukichwa.
Fact
 
Usikope kununua sofa na TV wala kujenga kama una idea ya biashara ndio ukope na utakachopata kwenye biashara kidogo kidogo ndio uanze kujenga maana mnapenda kujenga hata kama uwezo wa kujenga hauna baadae unaipeleka nyumba Bank kukopa huku mtaji ukiwa hauna...unapotaka kukopa inatakiwa ufanye feasibility study ya kutosha ukiona majibu sio sawa achana na mkopo mpaka utakapopata wazo zuri la biashara na hiyo biashara ufanye mwenyewe kwa usimamizi wako sio sijui mtoto wa Mjomba utaishia kumkata kichwa tuu wakati biashara ndio zilivyo...
Asikope kwasababu ana idea ya biashara .....hapa ndipo watu wengi wanapofeli katika mikopo.Kopa ili kuikuza au kuitanua biashara ambayo tayari unaendelea kuifanya, inakulipa vizuri na una uwezo wa kuzikabili changamoto zake.

Unakopa ili kuongeza uzalishaji au uingizaji wa bidhaa sokoni. Usikope ili kuanzisha biashara utakuja kukutwa na kitu kizito hutoamini.

Mfano labda ulikuwa unaingiza mzigo mchache unauzika kwa wakati na bado kuna demand kubwa ya uhitaji wa bidhaa yako kwa wateja. Hapa unaweza kukopa ili uwe na uwezo wa kuingiza mzigo mkubwa zaidi ili uongeze faida pia.

Ukifanya hivyo fasta utaweza kuulipa mkopo na utaona manufaa ya mkopo. Mwisho kabisa nakushauri uepukane na mikopo yenye Riba.

Kumbuka RIBA sio faida. Riba ni laana . Wengi wamefeli katika biashara kutokana na kujihusisha na mikopo yenye riba.
 
Mimi nina mshahara kama huyo jamaa ninaishi,niko kwangu,nina nyumba mbili, Sijawahi kulala njaa, mwaka huu january napeleka mtoto wangu English medium school,karo 2M,mwaka jana ndani ya miezi miwili nimekamilisha nyumba ya 13M.


Take home yangu ni 270K


Acha kuogopesha watu, jamaa kama anajiweza akope
Ukitaka kufanya jambo lako sasa hivi, usiulize ushauri mitandaoni. Humu kuna watu wa kila aina, wengine humu watakwambia mshahara wa million 1 ni mdogo sana hautoshi kitu kumbe hata kazi hana.

Tafuta ushauri sehemu sahihi na kwa watu sahihi.
 
Back
Top Bottom