Kwa mshahara wa Tsh. 765,000/= nikizama benki naweza kopesheka kiasi gani?

Kwa mshahara wa Tsh. 765,000/= nikizama benki naweza kopesheka kiasi gani?

Biashara ni rahisi kwenye karatasi na sio field haupo mwenyewe.
Ukiloose kwenye businesses ndo utajua ujui.
Bora upoteze pesa kwenye ngono haumi kuliko kupoteza kwenye project utaumia maisha Yako yote.
Bora ukope utie kwenye ardhi Haina hasara unacheza na time TU mkopo ukiisha na ardhi imepanda thamani unapata faida mara mbili.
Biashara sio ngumu sema kutokua na taarifa sahihi nini ufanye ndio mtihani wa kwanza pili usimamizi tatu pesa ya riba ndio maana wanaopata pesa ambazo sio za riba kufanikiwa kwa muda mrefu ni rahisi kidogo na utegemezi huku una marejesho vyote hivyo vinachangia kudumaza maendeleo...
 
Kuna watu wanarudi na pesa kila siku, siku za mapumziko kama hizi wanachukio mishindo inawapita.

Angalia property zao utapata majibu kama ni kweli wanasubili pesa kila mwezi?
Ndio maana siamini kama kuna mtanzania anaeweza kukaa kusubiria mwisho wa mwezi ndio apate pesa za kujikimu....
Mm naona kama waajiriwa wanatudanganya.
Hata benki hatendi kukopa tunakopeshana wenyewe huku mashimoni na kwenye vilinge vya biashara......hadi milioni 100 kurudi chini...ukizingua kulipa.....everybody know the consequence.
 
wanasema mkopo ni chanzo. cha umasikini nilitegemea wamshauri mjuba alternative ili ajiendeleze vizur kifedha
Mbona wameshauri sana tu akina Upepo Wa Pesa, Mzee Wa Kupambania na Bongo Dili kwa kumpatia Mleta mada faida na hasara, soma katikati ya jumbe zao utaelewa.

Sent from my CPH2387 using JamiiForums mobile app
 
To be successful one has to fail several times... Unapoanguka kwenye biashara, kuna somo unalipata, ambalo litakufanya usirudie kosa. Ndiyo maana kama huna uzoefu na biashara don't start big, anza mdogo mdogo ili upate uzoefu. Huwezi anza biashara ya bodaboda kwa kuchukua mkopo na kununua bodaboda 4 kwa mpigo, ilhali huna hata uzoefu wa kusimamia bodaboda moja. Ukweli mwingine ni kwamba siyo kila mtu ana uwezo wa kufanya biashara. So kama ukiona biashara huwezi waweza kopa na kujenga hata fremu chache ukakodisha au kununua shamba ukawa unalima au kukodisha.
Waterbender are you there?

Sent from my CPH2387 using JamiiForums mobile app
 
Mimi nina mshahara kama huyo jamaa ninaishi,niko kwangu,nina nyumba mbili, Sijawahi kulala njaa, mwaka huu january napeleka mtoto wangu English medium school,karo 2M,mwaka jana ndani ya miezi miwili nimekamilisha nyumba ya 13M.


Take home yangu ni 270K


Acha kuogopesha watu, jamaa kama anajiweza akope
Kuna nyumba kweli YA milion 13??? Au ni Banda..sidhani kama Kuna nyumba YA Bei hiyo tuwe serious
 
Ukitaka kutembea na 1 out of three CRDB utakopa 22m watakata bima, processing fee. Kodi utabaki na 19.5m halafu ukae kwa kutulia ulambwe 389000 Kilamwezi kwa miaka 8 JUMLA ULIPE 37m
Hapo ndipo nilipotoka speed 120 kuambiwa mkopo wa M 28 nikatwe 550, 000/= kwa miaka 7 = 46, 200, 000/= ilihali nilipaswa kupewa 26, 800, 000/= kwa upuuzi huo huo wa processing fee na bima.

Sent from my CPH2387 using JamiiForums mobile app
 
Biashara sio ngumu sema kutokua na taarifa sahihi nini ufanye ndio mtihani wa kwanza pili usimamizi tatu pesa ya riba ndio maana wanaopata pesa ambazo sio za riba kufanikiwa kwa muda mrefu ni rahisi kidogo na utegemezi huku una marejesho vyote hivyo vinachangia kudumaza maendeleo...
Mmmh....[emoji848] Au basi...[emoji2960]

Sent from my CPH2387 using JamiiForums mobile app
 
Mimi nina mshahara kama huyo jamaa ninaishi,niko kwangu,nina nyumba mbili, Sijawahi kulala njaa, mwaka huu january napeleka mtoto wangu English medium school,karo 2M,mwaka jana ndani ya miezi miwili nimekamilisha nyumba ya 13M.


Take home yangu ni 270K


Acha kuogopesha watu, jamaa kama anajiweza akope
Usimdanganye mwenzio. Sababu yake kuu ya kukopa ni NJAA, kasema mwenyewe.
Anataka akope mkopo wa juu zaidi kuweza kukopeshwa kwa sababu ana njaa.

Mtumishi unatakiwa ukope ukiwa na biashara au mradi wako ambao umefanya kwa hela za kudunduliza au hela ya kupata kwenye chanzo kingine ila sio mkopo wa riba. Ufanye kwa muda hata zaidi ya mwaka, uanze kupata faida na hasara uzoee hicho kitu, ukue uache kutumia hadithi na simulizi badala yake utumie uhalisia na uzoefu.
Baada ya hapo ukope ili kuendeleza na kukuza hiyo shughuli. Tena napo haukopi mkopo wa kiasi cha juu kabisa kinachowezekana.

Anza kufuga mbuzi au nguruwe, anza kununua mazao kwenye msimu, anzisha biashara ya miche ya miti na matunda, anzisha duka la spare parts au nguo au viatu au vyombo vya ndani, etc. Fanya kwa muda fulani mpaka uwe na uzoefu kisha ndio ukope benki kuanzia kiasi kidogo na unapanda taratibu.
Miaka kadhaa baadae utakuwa na uwezo wa kukopa hata 70M bila wasiwasi. Sio unapigwa njaa unakopa kujimaliza ili ununue sabufa na pikipiki used ya Sanya, na TV ya Aborder ukutani, hela inayobaki ukarabati nyumba.

mkarimani feki dunia sio mama yako, miaka minne ijayo hakuna atakayekuhurumia leo hii ukikopa kisa una njaa.
 
Hapo ndipo nilipotoka speed 120 kuambiwa mkopo wa M 28 nikatwe 550, 000/= kwa miaka 7 = 46, 200, 000/= ilihali nilipaswa kupewa 26, 800, 000/= kwa upuuzi huo huo wa processing fee na bima.

Sent from my CPH2387 using JamiiForums mobile app
chukua tu boss, mimi sikukopa miaka mitano nilikuwa nakataaa kama wewe kuna mwamba akakopa akajenga(kiwanja alikuwa nacho) mimi ambae nilikuwa sitaki kulambwa miaka mitano ikaisha bado nimepanga hapo nimenunua kiwanja tu, mwamba kamaliza mkopo mwezi huohuo akanyonya akachukua ndinga kali hapo ndo akili ikanisogea nikaenda kunyonya nikajenga saivi nakaa kwenye nyumba kali ila sina hela natembelea moja ya tatu.

nilijidai vimiradi uchwara nimepoteza tu mida, niliona nikope tu nijenge baada ya kupata mtoto wa pili familia imekuwa na hizi mambo za kupanga. wewe unaweza kukimbia hayo makato sababu huna majukumu mengi ila ukiwa na majukumu mengi wala hutajali kwenda benki kujitia kitanzi halafu unakaza shingo mpaka mkopo unaisha.
 
Back
Top Bottom