Kwa mtaji wa Shilingi laki moja hadi laki tisa (100,000 - 900,000) unaweza kufanya biashara gani?

Kwa mtaji wa Shilingi laki moja hadi laki tisa (100,000 - 900,000) unaweza kufanya biashara gani?

Nianzishe Biashara gani ambayo inaweza kunisogeza mbele Kwa mtaji wa laki 2 ?
Pitia nyuzi hzo hakika utapata chochote kitu


 
Skin Jeans za kike tunaenda Tandika na Kariakoo tunanunua kwa Tsh. 3000/= kwa kila PC 1.

Hiyo laki mbili yako unapata hizo skin jeans 50,baada ya hapo unazifanyia modification kwa Tsh1000/= kwa kila skin jeans na laki mbili yako inakuwa imeisha na unakuwa umetumia 4000/= kwa kila jeans

Huku kwetu Mbagala kila jeans unauza Tsh 10000/=,hii ina maana umepata faida ya Tsh 6000/= kwa kila jeans na ili upate faida ya Tsh 20,000/= inabidi uuze PC 4 za skin jeans na lengo lako linakuwa limetimia ila huwa tunauza hadi PC 5-8 kwa siku.

Wengi watadharau ila wengine ndio tuanishi mjini kwa style hizo

Wanangu wa Tudo watakuwa wanaelewa nilichokiandika hapa
Naomba tuwasiliane boss unipe muongozo vizuri
 
Kuna zile baiskeli za mayai zinauzwa laki tatu na 50 ukimuajili kijana kwa siku una uhakika wa kulaza elfu 10
IMG_20220926_160112.jpg
 
Mimi machinga wa kutengeneza wadada kucha na rangi,mtaji wangu ni elfu20,siku mbaya napata15 ikiwa nzuri 20 au 25.
Naunga hoja![emoji106][emoji106]Kupaka rangi na kutengeneza kucha hadi elfu 40 kwa siku unalaza!
 
Mkuu maisha ni rahisi ukiamua kuyafanya yawe rahisi.Faida anayotaka ni faida ya 20,000 ambayo ni sawa na 10%.So anatakiwa tu ajue ni bidhaa agani ambayo anaweza akauza moja na akapata faida ya 10% on the spot.

Sasa kuhusu consistency hapo inategemea na bidii yake ila kwa uzoefu wangu katika biashara najua kwamba inawezekana kuwekeza 200,000 kwa siku na kutengeneza faida ya 20,000.Kama unakataa kwa sababu huna imani au huwezi hapo ni sawa ila haimaanishi kwamba haiwezekani.Inawezekana.

SWALI lake ni JE ni Biashara gani hiyo?JIBU langu ni Biashara ya kuuza TAARIFA.
Usitumie nguvu nyingi kumwelewesha mtu kama huyu, watu kama hawa always huwa wapo kupinga mawazo ya watu wengine! Hawataki watu waujue ukweli ili wajikwamue kiuchumi kiufupi ni wabinafsi! Yaan mtu atumie laki 2 ashindwe kuingiza elfu 20 kwa siku??? Wakat kuna watu ninawajua kwa mtaji wa laki 3 wanatengeneza laki 1+!!
 
Usitumie nguvu nyingi kumwelewesha mtu kama huyu, watu kama hawa always huwa wapo kupinga mawazo ya watu wengine! Hawataki watu waujue ukweli ili wajikwamue kiuchumi kiufupi ni wabinafsi! Yaan mtu atumie laki 2 ashindwe kuingiza elfu 20 kwa siku??? Wakat kuna watu ninawajua kwa mtaji wa laki 3 wanatengeneza laki 1+!!
Natamani kuijua hii biashara!

Japo kiuhalisia haiwezi kuwa biashara halali
 
Wakuu,

Kutokana na wadau kadhaa kuja na mijadala anuai inayoonyesha kuwa wanayo mitaji yenye kuanzia kiasi cha TZS 100,000/= hadi TZS 999,999/=, tumeona ni vema tukawa na mjadala mmoja endelevu ambao utatoa mawazo mbalimbali ya jinsi ya kutoka kimaisha ukiwa na mtaji huo.

Aidha, tunashauri usome maoni mbalimbali ya wadau kuweza kupata kujua wengine wametokaje kwa viwango hivi na unaweza kufikiria namna unayoona inafaa kwako. Tumejitahidi kupangilia posts humu kukurahisishia usomaji kwa ufanisi wako.

Asante

View attachment 1482167

Biashara za kuanzia 100,000 - 200,000


-----

----

----

----

----

----

----



Biashara za mtaji wa kuanzia 300,000-500,000



-----

----

----



Biashara za mtaji wa kuanzia 600,000-900,000



----
Sawa
 
NAOMBA KUULIZA NI BIASHARA GANI INAYOWEZA KUKUA KWA HARAKA KWA MTAJI SH.10000?
Uza mayai ya kuchemsha.
Mtaji tray 8500/=
Mkaa 500.
Chumvi chukua nyumbani.
Jumla 9000/=
Unauza 500*30pcs jumla 15,000/= faida 6000 per tray.

Mchana nenda kwa bakresa ongea nao chukua ice cream pita juan haukosi 25k hadi 30k n ujanja wako wa kujua location za madada au wahitaji.

Ni rahisi ukijikana uwezo wa kutengeneza 30k per day n mkubwa baada ya muda fulan unaachana na utumwa unahamia kivulini.
 
Uza mayai ya kuchemsha.
Mtaji tray 8500/=
Mkaa 500.
Chumvi chukua nyumbani.
Jumla 9000/=
Unauza 500*30pcs jumla 15,000/= faida 6000 per tray.

Mchana nenda kwa bakresa ongea nao chukua ice cream pita juan haukosi 25k hadi 30k n ujanja wako wa kujua location za madada au wahitaji.

Ni rahisi ukijikana uwezo wa kutengeneza 30k per day n mkubwa baada ya muda fulan unaachana na utumwa unahamia kivulini.
Sijui akauzie wapi, nipo kkoo, nawaoneaga huruma wauza mayai. Kiasi kwamba huwa nanunua mengi nikiwakuta wanapita, ila bado, kazi ngumu sana hiyo kumaliza trey.
Vijana wapambane tu.
 
Sijui akauzie wapi, nipo kkoo, nawaoneaga huruma wauza mayai. Kiasi kwamba huwa nanunua mengi nikiwakuta wanapita, ila bado, kazi ngumu sana hiyo kumaliza trey.
Vijana wapambane tu.
Hakuna kazi rahisi ndg yangu,mambo yangekua mepesi kila mtu angekua bilionea akiwa mjanja tena tray mbili siku ya kwanza yanaisha.

Nakufungua macho ukishaona vijana wengi wanazungusha jua kuna soko kubwa na lililotayari,kikubwa usafi,uchangamfu na kuvua aibu.
 
Back
Top Bottom