Kwa mtaji wa Shilingi laki moja hadi laki tisa (100,000 - 900,000) unaweza kufanya biashara gani?

Kwa mtaji wa Shilingi laki moja hadi laki tisa (100,000 - 900,000) unaweza kufanya biashara gani?

Mkuu tunaomba utuwekee mtiririko wa chanjo na tiba za magonjwa ili wote tujifunze.
*MAGONJWA YA KUKU NA TIBA ZAKE*

UTANGULIZI
Kuku kama wanyama wengine hushambuliwa
na magonjwa mbalimbali ambayo mengine
yanatibika kwa dawa na mengine hayana tiba
bali kuku hupewa chanjo maalumu ambayo
huzuia magonjwa hayo.Leo nitawaeleza baadhi
ya magonjwa ambayo hushambulia kuku mara
kwa mara na ambayo ni chanzo cha
kuwakatisha tamaa wafugaji wa kuku.
A.) MAGONJWA YANAYOHITAJI CHANJO
1> GUMBORO
Ugonjwa huu husababishwa na virusi.
DALILI ZA UGONJWA
-Kuku kuzubaa na kulundikana, pamoja na
kusinzia
-Kuku kuharisha
-Kuwa na vifo vingi kwa kuku
TIBA
Ugonjwa huu hauna tiba,,Kuku wakipewa Dawa
za oxytetracycline hupunguza vifo.
KINGA
wakinge kuku wapo kwa kuwapa chanjo ya
gumboro (Gumboro vaccine)
2> MAHEPE (Marecks)
Ugonjwa huu husababishwa na virusi
DALILI
-Kuku hupata ulemavu na vifo vya mara kwa
mara.
TIBA
Ugonjwa huu hauna tiba
KINGA
Chanjo hutolewa kwa vifaranga wenye umri wa
siku moja,vifaranga hupewa chanjo ya mahepe
(Marecks vaccine)
3>NDUI YA KUKU (Fowl Pox)
Ugonjwa huu husababishwa na virusi.
DALILI
-Kuku hupatwa na vidonda kichwani.
-Kuku hupata uvimbe mweupe kwenye
mdomo na kushindwa kula.
TIBA
Ugonjwa huu hauna tiba.
KINGA
Chanja kuku wako wa siku 60-90 kwa chanjo ya
Ndui ya kuku (Fowl pox vaccine).
4>MDONDO (New castle)
Ugonjwa huu husababishwa na virusi
DALILI
-Ugonjwa huu hutokea kwa ghafla na kuenea
kwa haraka
-Vifo vya kuku huwa vingi
-kuku hupumua kwa shida
-Kuku hupooza na kulemaa miguu
-Kuku hupinda shingo yake
-Kuku hupunguza kutaga mayai
-kuku huarisha
-Kuku Kuzunguka zunguka na kutembea
kinyume nyume.
TIBA
Hauna tiba
KINGA
Chanja vifaranga wako na kuku wako kwa
chanjo ya Mdondo (New Castlef vaccine) na
urudie chanjo hii kila baada ya miezi mitatu.
B.)MAGONJWA YANAYOTIBIKA KWA DAWA
1>KUHARA DAMU (coccidiosis)(Koksidiosisi
Ugonjwa huu husababishwa na virusi.
DALILI
-Kuku huzubaa na kujikunyata
-Kuku kuharisha LinkedI chenye damu au
kinyesi cha kahawi
-Kuku hudhoofika,manyoya huvurugika na
kulegea mabawa na kuonekana kama wawevaa
koti
-Kuku hupungukiwa homa ya kula
-Vifo huwa vingi kwa vifaranga
TIBA
Wape kuku wako dawa kama Esb 3, Amprolium,
au Basulfa.
KINGA
Zingatia usafi wa banda la kuku na usiruhusu
unyevuunyevu katika banda la kuku,
2>HOMA YA MATUMBO(Fowl typhoid)
Husababishwa na bakteria
DALILI
-Kuku hupata homa kali
-Kuku huarisha kinyesi cha kijani au njano
-Vifo huwa vingi hasa kwa vifaranga wenye
wiki 1-2
-Kuku huzubaa,kuvimba viungo vya
miguu,kuchechemea,kukosa hamu ya kula
-Kuku wanaotaga hupunguza utagaji,hutaga
mayai yenye ganda laini na hupata vifo vya
ghafla

TIBA
Dawa za oxytetracycline kama
Furamax,Typhoprim hutibu ugonjwa huu.
KINGA
Hakikisha usafi wa banda na vyombo vya
chakula na maji kwa kuku.
Tenganisha kuku wagonjwa na wazima
C)MINYOO
Hushambulia kuku wote wakubwa na vifaranga
DALILI
-Kuku hukonda
-Kuku huarisha
-Kuku hukohoa
-Kuku hupunguza utagaji
-Kuku hudumaa katika ukuaji/hawakui vizuri
-Kuku hupungua uzito
TIBA
Tumia dawa za minyoo kama piperazine
KINGA
Wapewe dawa za minyoo mara kwa mara kila
baada ya miezi mitatu
D)VIROBOTO/CHAWA/UTITIRI
Hushambulia sana vifaranga na hutokea vifo
kwa wingi kwa vifaranga Kwa kuku wakubwa
tatizo halionekani kwa sana lakini nao
huathiriwa sana.
DALILI
-Kuku kutochangamka
-Ukuaji mdogo wa kuku
-Kuku kutotaga na kuhatamia vizuri kutokana
na kusumbuliwa na chawa,utitiri au viroboto
-Viroboto huonekana kuganda machoni
wakinyonya damu
TIBA
Tumia dawa za unga kama sevin dust
5% ,Malathion ,akheri powder kwa kuku wote na
mabanda yao.
KINGA
Boresha usafi wa mabanda ya kuku.
E)UKOSEFU WA VITAMINI A
huathiri sana kuku wadogo.


*DALILI*
-Kuku huvimba macho na kutoa uchafu mzito
kama sabuni ya kipande iliyolowana.
-Mara nyingi ugonjwa hujitokeza baada ya
kipindi kirefu cha kiangazi
TIBA
wape kuku wote dawa za vitamini za kuku
zinazouzwa dukani.


KINGA
Wape kuku wako mchicha na majani mabichi
mara kwa mara.

ZINGATIO
Fuata ushauri wa matumizi sahihi kwa kila
dawa pindi ununuapo katika duka la dawa..
 
mkuu the farmer umesomeka vizuri sana, sasa nina swali langu dogo tu kuhusu chanjo ili kuzuia magonjwa, je kuku wanapatiwa chanjo za magojwa yote hayo tofauti tofauti? au kuna chanjo moja tu inayozuia magonjwa yote?
 
mkuu the farmer umesomeka vizuri sana, sasa nina swali langu dogo tu kuhusu chanjo ili kuzuia magonjwa, je kuku wanapatiwa chanjo za magojwa yote hayo tofauti tofauti? au kuna chanjo moja tu inayozuia magonjwa yote?
chanjo zipo nyingi kama za
1.kideri
2.mdondo
3.gumboro n.k
pia zinatolewa kwa muda tofauti..nilizotoa hapo juu ni tiba ila chanjo utazipata muda si mwingi mkuu
 
mkuu the farmer umesomeka vizuri sana, sasa nina swali langu dogo tu kuhusu chanjo ili kuzuia magonjwa, je kuku wanapatiwa chanjo za magojwa yote hayo tofauti tofauti? au kuna chanjo moja tu inayozuia magonjwa yote?
*ZIFAHAMU TARATIBU NA RATIBA ZA UCHANJAJI WA KUKU KUANZIA VIFARANGA NA KUKU WAKUBWA.*
*TARATIBU NA RATIBA ZA UCHANJAJI*

Wakati wa kutayarisha mpango wa kuchanja kuku kwa ajili ya kinga dhidi ya magonjwa, kuna vipengele vikuu sita Ambavyo unatakiwa uvifahamu na kuvizingatia. Vipengele hivyo ni kama ifuatavyo:
1. Vifaranga vinavyoanguliwa kwa pamoja:
Iwapo una kundi zaidi ya moja la vifaranga wanaoanguliwa,
Weka utaratibu wa chanjo ambao utapunguza uwezekano wa magonjwa kuenea shambani. Hivyo basi,
Hakikisha vifaranga na kuku wote wanapata chanjo kwa pamoja.
2. Umri wa kuchanja kuku:
Kwa kuku ambao wanatarajiwa kutaga mayai au kuwa kuku wazazi, chanjo
nyingi hutolewa si zaidi ya mwezi mmoja kabla ya kuku kuanza kutaga. Pia kuna baadhi ya chanjo ambazo haziruhusiwi kwa kuku wadogo. (Angalia Ratiba).
3. Magonjwa muhimu katika eneo husika:
Ni muhimu sana kuelewa magonjwa ya kuku yaliyopo katika eneo lako kabla ya kuandaa programu ya uchanjaji, hasa kwa yale magonjwa ambayo chanjo zenye
Vimelea hai hutumika. Hivyo basi, sio busara kuanza kutumia chanjo za aina hii katika maeneo ambayo
Ugonjwa huo haujawahi kuripotiwa.
4. Hali ya kiafya ya kuku watakaochanjwa:
Usiwape chanjo kuku ambao wanaonyesha dalili za kuathirika kwa mfumo wa hewa au wanaonyesha kuwa na minyoo au wadudu wengine. Kwa kuku walio na dalili hizi chanjo zinaweza kuleta madhara na zisifanye kazi.
5. Aina ya kuku watakaochanjwa:
Kuku wanaofugwa kwa ajili ya nyama wanahitaji kinga ya muda mfupi, hivyo basi chanjo moja inaweza kutosha kabla ya kufikia umri wa kuuzwa. Lakini kuku wa mayai na kuku wazazi wanahitaji programu ya chanjo ambayo itawakinga na magonjwa kwa kipindi chote wanapokua na kutaga. (Zingatia Ratiba).
6. Historia ya Magonjwa katika shamba:
Kabla ya kuandaa mpango wa chanjo, lazima ufahamu ni
*Magonjwa gani yaliyoenea katika shamba.*
a) Kama unataka kuingiza kuku wapya kutoka mahali ambako ugonjwa umeshawahi kutokea,
kuku hao wachanjwe wiki 3 kabla ya kuwaingiza shambani
b) Iwapo utatumia chanjo yenye vimelea hai, hakikisha kwamba magonjwa hayo yameshawahi
kutokea katika shamba husika. Usitumie chanjo hizi katika shamba ambalo ugonjwa huo
haujawahi kutokea au kutambuliwa.
c) Wasiliana na mashamba jirani kufahamu iwapo wanatumia chanjo zenye vimelea hai. Toa taarifa
kwa mamlaka za mifugo iwapo unapanga kutumia chanjo hizo katika eneo lako. Pata ushauri wa daktari.

*TARATIBU ZA UCHANJAJI*
Mambo muhimu ya kuzingatia:
•Hakikisha unazingatia kwa makini masharti ya mtengenezaji wa chanjo: jinsi ya kuhifadhi, kutayarisha na njia inayotumika kumchanja kuku. Wakati wote zingatia masharti ya mtengenezaji kuhusu uhifadhi wa
chanjo ili isipoteze nguvu.
• Fuata ushauri wa daktari wa mifugo unapoandaa programu ya chanjo.

• Watoa chanjo wapatiwe mafunzo ya jinsi ya kutayarisha na kutoa chanjo
• Chagua aina ya chanjo kulingana na umri na hali ya kiafya ya kuku.
• Fanya usafi wa mara kwa mara katika mabanda ili kupunguza wingi wa vimelea kwenye mazingira.
• Tumia maji ambayo hayajawekwa dawa au kemikali kwa ajili ya kuchanganyia chanjo, k.m. maji ya kisima, mvua, n.k. Maji ya kuchanganyia chanjo yawe na ubaridi, yasiwe moto.
• Changanya chanjo kabla ya kutumia na iwekwe mbali na kuku.


• Pata ushauri wa daktari wa mifugo kabla ya kuchanja kuku wagonjwa au wale ambao hawako katika
muonekano mzuri
• Siku ya chanjo, usiwape kuku maji kwa masaa 3 – 4 ili waweze kunywa maji yaliyowekwa chanjo kwa
haraka.
• Zoezi la uchanjaji lifanyike haraka ili kupunguza usumbufu kwa kuku.
• Tenganisha kuku waliochanjwa na wale ambao hawajachanjwa.
• Baada ya kuchanjwa, kuku wawekwe kwenye banda linalopitisha hewa vizuri
• Baada ya kila zoezi la kuchanja, wafanyakazi wabadilishe mavazi, viatu/buti zisafishwe na kuwekwa dawa, na vifaa vilivyotumika viwekwe dawa ya kuua vimelea.

• Fuata utaratibu uliowekwa wa kuharibu/kusafisha vifaa vilivyotumika kuchanja
• Weka kumbukumbu za uchanjaji vizuri
Mambo ambayo hutakiwi kuyafanya unapochanja
• Kumwaga chanjo ovyo na kuchafua mikono au nguo
• Kuchanganya chanjo za aina mbili au zaidi, isipokuwa pale tu mtengenezaji wa chanjo atakavyoagiza
hivyo, au kwa ushauri wa daktari wa mifugo.

• Kutumia chanjo iliyopita muda wake
• Kutumia chanjo iliyobaki ili itumike kwa kazi ya siku nyingine
• Kuchanja kuku ambao wamepatiwa dawa aina ya antibiotiki.
• Kuchanja zaidi ya chanjo moja kwa wakati, iwapo haikuagizwa hivyo.


*CHANJO ZINAZO PENDEKEZWA*
Aina ya Chanjo
Umri wa Kuchanja Kuku
Muda kati ya kutoa chanjo
Njia inayotumika kuchanja kuku
Lasota – kwa ajili ya Mdondo/Kideri
Kifaranga wa Siku 3
Rudia baada ya siku 21, baada ya hapo kila baada ya miezi 3

Maji safi yasiyowekwa dawa
Chanjo inayohimili joto - I-2 kwa ajili ya Mdondo/Kideri
Kifaranga wa Siku moja
Rudia baada ya kila miezi 4 kwa kuku wa mayai na wazazi
Tone la chanjo kwenye jicho kwa kila kuku
Hipraviar-B1 - kwa ajili ya
Mdondo/Kideri na Ugonjwa wa Mapafu (Infectious Bronchitis)
Kifaranga wa Siku moja
Rudia baada ya siku 21, baada ya hapo kila baada ya miezi 3

Maji safi yasiyowekwa dawa
VIR-114 – kwa ajili ya Gumboro
Siku 10 au 14
Inaweza kurudiwa Siku ya 17 kwa
wale waliochanjwa wakiwa na Siku
10; na Siku ya 28 kwa wale waliochanjwa wakiwa na Siku 14
Maji safi yasiyowekwa dawa.

Avipro – kwa ajili ya Ndui ya Kuku
Wiki 7 hadi 14
Chanjo moja Chanja katikati ya ngozi
kwa kutumia utando wa ngozi kwenye bawa
Chanjo ya Mareksi
Kifaranga wa Siku moja
Chanjo moja
 
Madini ya humu ni balaa hivi mtu anaweza akakuuzia kuku wa mayai mjini hapa dsm au wanapatikana sehemu gani?
 
Kama una laki tatu uza na hiyo smartphone jumlisha then utajua mtaji wako halisi mana unakuta kijana ana genge but anamiliki cm ya laki tatu!
Ukishafanya hivyo angalia biashara yenye mzunguko wa haraka mana kwa mtaji mdogo ukifanya biashara ya mda mrefu sana utakula mtaji buree.
 
*MAGONJWA YA KUKU NA TIBA ZAKE*

UTANGULIZI
Kuku kama wanyama wengine hushambuliwa
na magonjwa mbalimbali ambayo mengine
yanatibika kwa dawa na mengine hayana tiba
bali kuku hupewa chanjo maalumu ambayo
huzuia magonjwa hayo.Leo nitawaeleza baadhi
ya magonjwa ambayo hushambulia kuku mara
kwa mara na ambayo ni chanzo cha
kuwakatisha tamaa wafugaji wa kuku.
A.) MAGONJWA YANAYOHITAJI CHANJO
1> GUMBORO
Ugonjwa huu husababishwa na virusi.
DALILI ZA UGONJWA
-Kuku kuzubaa na kulundikana, pamoja na
kusinzia
-Kuku kuharisha
-Kuwa na vifo vingi kwa kuku
TIBA
Ugonjwa huu hauna tiba,,Kuku wakipewa Dawa
za oxytetracycline hupunguza vifo.
KINGA
wakinge kuku wapo kwa kuwapa chanjo ya
gumboro (Gumboro vaccine)
2> MAHEPE (Marecks)
Ugonjwa huu husababishwa na virusi
DALILI
-Kuku hupata ulemavu na vifo vya mara kwa
mara.
TIBA
Ugonjwa huu hauna tiba
KINGA
Chanjo hutolewa kwa vifaranga wenye umri wa
siku moja,vifaranga hupewa chanjo ya mahepe
(Marecks vaccine)
3>NDUI YA KUKU (Fowl Pox)
Ugonjwa huu husababishwa na virusi.
DALILI
-Kuku hupatwa na vidonda kichwani.
-Kuku hupata uvimbe mweupe kwenye
mdomo na kushindwa kula.
TIBA
Ugonjwa huu hauna tiba.
KINGA
Chanja kuku wako wa siku 60-90 kwa chanjo ya
Ndui ya kuku (Fowl pox vaccine).
4>MDONDO (New castle)
Ugonjwa huu husababishwa na virusi
DALILI
-Ugonjwa huu hutokea kwa ghafla na kuenea
kwa haraka
-Vifo vya kuku huwa vingi
-kuku hupumua kwa shida
-Kuku hupooza na kulemaa miguu
-Kuku hupinda shingo yake
-Kuku hupunguza kutaga mayai
-kuku huarisha
-Kuku Kuzunguka zunguka na kutembea
kinyume nyume.
TIBA
Hauna tiba
KINGA
Chanja vifaranga wako na kuku wako kwa
chanjo ya Mdondo (New Castlef vaccine) na
urudie chanjo hii kila baada ya miezi mitatu.
B.)MAGONJWA YANAYOTIBIKA KWA DAWA
1>KUHARA DAMU (coccidiosis)(Koksidiosisi
Ugonjwa huu husababishwa na virusi.
DALILI
-Kuku huzubaa na kujikunyata
-Kuku kuharisha LinkedI chenye damu au
kinyesi cha kahawi
-Kuku hudhoofika,manyoya huvurugika na
kulegea mabawa na kuonekana kama wawevaa
koti
-Kuku hupungukiwa homa ya kula
-Vifo huwa vingi kwa vifaranga
TIBA
Wape kuku wako dawa kama Esb 3, Amprolium,
au Basulfa.
KINGA
Zingatia usafi wa banda la kuku na usiruhusu
unyevuunyevu katika banda la kuku,
2>HOMA YA MATUMBO(Fowl typhoid)
Husababishwa na bakteria
DALILI
-Kuku hupata homa kali
-Kuku huarisha kinyesi cha kijani au njano
-Vifo huwa vingi hasa kwa vifaranga wenye
wiki 1-2
-Kuku huzubaa,kuvimba viungo vya
miguu,kuchechemea,kukosa hamu ya kula
-Kuku wanaotaga hupunguza utagaji,hutaga
mayai yenye ganda laini na hupata vifo vya
ghafla

TIBA
Dawa za oxytetracycline kama
Furamax,Typhoprim hutibu ugonjwa huu.
KINGA
Hakikisha usafi wa banda na vyombo vya
chakula na maji kwa kuku.
Tenganisha kuku wagonjwa na wazima
C)MINYOO
Hushambulia kuku wote wakubwa na vifaranga
DALILI
-Kuku hukonda
-Kuku huarisha
-Kuku hukohoa
-Kuku hupunguza utagaji
-Kuku hudumaa katika ukuaji/hawakui vizuri
-Kuku hupungua uzito
TIBA
Tumia dawa za minyoo kama piperazine
KINGA
Wapewe dawa za minyoo mara kwa mara kila
baada ya miezi mitatu
D)VIROBOTO/CHAWA/UTITIRI
Hushambulia sana vifaranga na hutokea vifo
kwa wingi kwa vifaranga Kwa kuku wakubwa
tatizo halionekani kwa sana lakini nao
huathiriwa sana.
DALILI
-Kuku kutochangamka
-Ukuaji mdogo wa kuku
-Kuku kutotaga na kuhatamia vizuri kutokana
na kusumbuliwa na chawa,utitiri au viroboto
-Viroboto huonekana kuganda machoni
wakinyonya damu
TIBA
Tumia dawa za unga kama sevin dust
5% ,Malathion ,akheri powder kwa kuku wote na
mabanda yao.
KINGA
Boresha usafi wa mabanda ya kuku.
E)UKOSEFU WA VITAMINI A
huathiri sana kuku wadogo.


*DALILI*
-Kuku huvimba macho na kutoa uchafu mzito
kama sabuni ya kipande iliyolowana.
-Mara nyingi ugonjwa hujitokeza baada ya
kipindi kirefu cha kiangazi
TIBA
wape kuku wote dawa za vitamini za kuku
zinazouzwa dukani.


KINGA
Wape kuku wako mchicha na majani mabichi
mara kwa mara.

ZINGATIO
Fuata ushauri wa matumizi sahihi kwa kila
dawa pindi ununuapo katika duka la dawa..
Asante mkuu, nimekuelewa sana.
 
Back
Top Bottom