Pre GE2025 Kwa Mujibu wa Tundu Lissu, Majimbo Mapya hutengezwa kutoa fursa kwa watu fulani fulani nao wapate majimbo. Kama ni kweli basi tuna safari ndefu

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Nzega iligawanywa ili Kigwa na Bashe wasiuane.
Bashe aliwabana mbavu maana alikuwa anakubalika na wananchi ila wenye nchi kwa kipindi kile walikuwa wanamtaka Kigwa na ndio maana pamoja na kushika namba 3 akachukuliwa plus kumpiga zengwe Bashe sio raia. Next uchaguzi watu wakaona isiwe tabu tukagawe majimbo
 
Duuh
 
Hii ingekuwa poa kabisa na uzuri kila mbunge anahesabiwa kama diwani kwenye baraza la madiwani hivyo issue zote za halmashauri anashiriki kikamilifu ambapo maamuzi yote yanaachwa kwa DED Kwa ajili ya utekelezaji.

Kwa maana hiyo yale yote nje ya uwezo wa halmashauri mbunge ndo alitakiwa ayabebe ayapeleke bungeni kupata support kwa serikali kuu lakini ajabu unakuta wilaya moja majimbo mawili
 
May be
 
Changamoto ya wanasiasa huwa gharama za kuendesha nchi haziwahusu lakini pia kulinganisha maendeleo nyakati za sasa na miaka ya nyuma. Unakuta mwanasiasa huyo huyo anahubiri kwamba nchi imepiga hatua na inafikika kwa urahisi kila pembe ya nchi ukilinganisha na miaka ya nyuma alafu baadae unasikia wanataka kugawa majimbo au wilaya au mikoa ili waweze kuwafikia wananchi kiurahisi huku report zao zikisheheni sifa kibao za urahisi wa kufikia wananchi kuimarishwa
 
Hahaha.....umeona hizo janja janja zao?
 
Ndo umejua leo mkuu baada ya TAL kusema? Mbona sisiem hiyo tabia walianza zamani.

Hata Magufuli alimegewa na Mkapa Jimbo la Chato kutoka Biharamulo baada ya kuona mwamba kila uchaguzi anachezea za uso kutoka kwa Phares Kabuye.
 
Sahihi kabisa Tena hata yangepunguzwa tu. Ni sahihi pia sababu ni kweli kero nyingi zinaibuliwa na wananchi zaidi kuliko wawakilishi wenyewe
 

Tubadiliahe Katiba ya nchi ili Wabunge watokane na mikoa, kila Mkoa utoe Wabunge wa kuchaguliwa wapatao wawili au wanne, yaani Wabunge Wanaume Wawili na Wabunge Wanawake pia wawe wawili. Kusiwepo na Wabunge wa Viti Maalumu wa kuteuliwa Kutokea Majimboni au wa kuteuliwa kutoka kwenye Uwakilishi wa Majimbo au Mikoa.

Rais wa nchi apewe nafasi zake Kumi tu (10) za kuteua Wabunge wa Kuteuliwa, pasiwepo na idadi nyingine zaidi ya Wabunge wa kuteuliwa zaidi ya hao Kumi wa kuteuliwa na Rais wa nchi.
 
Hili limeelezwa na kupangwa vyema kwenye Katiba ya Jaji Mstaafu Warioba
 
Ndo umejua leo mkuu baada ya TAL kusema? Mbona sisiem hiyo tabia walianza zamani.

Hata Magufuli alimegewa na Mkapa Jimbo la Chato kutoka Biharamulo baada ya kuona mwamba kila uchaguzi anachezea za uso kutoka kwa Phares Kabuye.
Phares Kabuye alikuwa wa Moto sana.
 
Mbinu hiyo ipo muda mrefu tu.... Nakumbuka awamu ya nne kipindi cha pili cha Kikwete kuna kituo kilifunguliwa kinyemela kikatumika kama kituo fulani hivi maalumu kwa VIPs.
Kalumanzira huko shamba anakotoka huwa anaaswa kabisa kuwa makini afikapo mjini. Hizo ndizo zao CCM yenye wenyewe. 🤔
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…