Kwa nilichomjibu huyu dada nahisi ataghairi kwa muda kuomba wanaume hela

Kwa nilichomjibu huyu dada nahisi ataghairi kwa muda kuomba wanaume hela

Wiki iliopita nilikutana na dada njiani hapa mtaani kwetu, nikamuomba namba akanipa, baadaye nikamwambia atafute siku tuonane kwenye mgahawa/restaurant for a lunch date, tufahamiane zaidi, akakubali. Heee, nimechukua namba yake leo, kesho yake kama kawaida yao si akaniomba elfu 20!

Nikamwambia abadilishe staili ya kukataa wanaume, kupiga mzinga/kuomba hela chap imepitwa na wakati. Nikamwambia napenda kusaidia watu, mimi sio mchoyo, ila sitapeliwi kijinga.

Nikamwambia kama alikuwa hanitaki angeniambia live na ningemwelewa, pia nikamwambia kuwa sinunuagi uchi wa mwanamke!

Hakujibu, mpaka leo nasubiri anijibu, hajanijibu, sijui ameishiwa sms!
Kwa hiyo hapo ndiyo ulimkomoa kwa kula chakula bila kunawa?Elewa swali.
 
Inawezekana alitaka kukuudhi mawasiliano yafe kwahiyo umeingia moja Kwa moja kwenye plan yake...

Next time kama amekuvutia kweli muulize hela ya nini...
Akisema ya saloon mwambie mbona ndogo?itamtosha?halafu mtumie mara 2 au 3 ya alioomba...
Mwisho wa siku wanakuitwa bwege ukiwa unawatumia tumia Hela kirahisi rahisi.

Hizi mbinu hazina mwenyewe na pia inategemea umekutana na mwanamke wa aina Gani.!?

Wako ambao kwa hio approach Yako ndio wanafall zaidi inakuwa kama chambo kumpata tena na tena

Ila Kuna wale makonki anakula Hela zako na hupati kitu hupati hata busu unakuwa unafanya kazi ya kanisa[emoji1]usawa huu.

Solution ni Kila mtu afanye kile moyo utapata amani na faraja
 
Duh,kwa staili hii mtu wa kuoa unampataje,alafu mnasema eti kuolewa ni bahati
Mwanamke wa hivi naye anaolewa[emoji23][emoji23][emoji23], basi ajichumiaye janga........ Utamalizia. Hata niwe stable kiuchumi kiasi gani, nipo kwenye miaka yangu ya late 20s pesa yangu yote niyakujenga maisha yangu kwanza ili nitulie kwa amani nguvu ikianza kupungua. Sasa mke chuma ulete atanirudisha nyuma mno tena mno maana anajiwazia yeye na sio familia na maendeleo. Kuchagua mke sio kazi rahisi!
 
263B357D-4E98-4870-B058-DDBFA2CCBC48.jpeg
 
Hivi vidada vinaomba sana Hela na ukiwazingatia ukawapa basi vinaona wameshakukamata akili vinaanza kukusumbua.

Nyie vidada sisi tunawapa Hela mkituomba ni kwa Sababu zipo ndani ya uwezo.
Swala sio kuwa na hela, kuna siku nilikuwa na laki 9 mdada aliniomba elfu 10, nkamnyima sababu ya mazingira aliyoombea..

Asingeniomba hela angekula hata tshs elf 50,000 yangu Zacht
 
Back
Top Bottom