Kwa wale tuliowahi kwenda kwa waganga wa kienyeji, tukutane hapa

Kwa wale tuliowahi kwenda kwa waganga wa kienyeji, tukutane hapa

Nilienda tena nilivuka border hadi Msumbiji!! Ajali mara nne mfululizo hiyo ya mwisho niliona giza then gari ikajiongeza speed wakati nilikanyaga break!! Nikaona wataniua siku zi zangu.

Nikaenda Msumbiji kuleta jamaa huyo anabinuka binuka nyumbani uchi mchana kweupee lakini watu hawamuoni!!

Tangu siku hiyo heshima imetawala na watoto wapo poa sana na ajali hakuna.
Kuna mijitu kweli ina roho mbaya waweza kuta kuna mtu alikuwa na wivu tu na maendeleo yako akataka akuondoe duniani
 
Kuna mume wa shangazi yangu alikuwaga ni "mtu asiyejulikana" alikuwa akifanya ambush zake huko anakimbilia nyumbani (tulikuwa tunaishi mikoa tofauti) na mi wakati huo bado bwana mdogo tu......nikawa namsindikiza kwa babu saa 7 za ucku tunaenda makaburini tukiwa uchi hata cjui tulikuwa tunaenda kufukia nini, na baada ya siku chache tu msala wake unasahaulika kabisa na anarudi huko anakoishi akiwa mtu huru kabisa, lakini mwaka 2006 alikufa kwa kupigwa mshale wa kifua halafu wananchi wenye hasira kali wakaja kummalizia kwa kipigo kizito......sasa cjui hapo ilikuwaje yule babu alishindwa kumsaidia
 
Mimi naendaga sana, hapa nasubili ombi la

Mshana Jr likubaliwe lile la jukwaa la wachawi
 
Waganga wengi ni waongo balaa
Kuna dada mmoja tulikuwa tunajua anaumwa nini lakini tuliamua kwenda kwa mganga ili tumsikie anasema nini
Mganga akaanza kumwambia umetupiwa jini na mchepuko wa mmeo na ndio linalokutesa
Daah tulicheka balaa baada ya kusikia uwongo wa mganga
 
Msema kweli mpenzi wa mungu.nilishakwenda kwa mganga.kwa ajili ya demu.tulikuwa wapenzi ghafla aka badilika.akawa mgumu kinomaaa.hanipendi tena.niliumia.kuna rafiki yangu yeye ni mganga nikamueleza akasema tulia atarudi.
Tukafanya Mandingo mixer kuoga njia panda usiku.kuchoma sana UDI.kupasua Nazi n.k
Kiukweli demu alianza kubadilika na kuanza kuongea na Mimi.Mara salam n.k.
Siku zikapita tukarudi tena kwenye penzi.ila hatukudumu tuliachana.
Ushauri kama MTU hakupendi ACHANA NAE.MADAWA HUISHA NGUVU.
I like it
 
ilikuwa ni darasa la sita mwanafunzi mwenzetu aliiba box la kalamu lote tena la mwanafunzi aliyekua mtoto wa mwalimu ikapita msako mkali hazikupatikana mwalimu akasema kesho asubh wote tuandike jina la mtu unaemhisi

Basi jioni tukajipanga wanaume kadhaa kama kumi na saba tukashauriana tuende kwa bibi mmoja ni mtaalamu huyu jamaa aliyeiba tutampata fasta

kikundi kikatimia tukatoroka moja kwa moja safari ikaanza tufafika kwa mtaalam na sare zetu za shule tukaingia wote kwa pamoja akaanza kutoa misauti yake akatueleza muna shida tofauti au ni moja mmoja akajibu ni moja

akasema haya mmoja aelezee jamaa akatiririka vya kutosha akasema andikeni majina yenu na ya baba yenu na shule mnayotoka kisha munipe ukishanipa unageuka nakuondoka hadi nyumbani kwako huyo mwizi asubuhi atapiga kelele nakuzirudisha mwenyewe sitawatoza hela nawasaidia tu kama wajukuu zangu tukafanya kama alivyosema

kumbe pale jirani kuna mwalimu wetu yupo karibu na yule bibi jioni akamfuata akampa na yale majina asubuh tupo paredi tukaanza kuitwa jina mmoja baada ya mwingine tukijiangalia ni wale wote tuliokuwa kwenye tukio ohoo kilochofuata siwezi ata elezea ngoja niishie tu hapa

na hapo ndipo nilopotokea kuwachukia hadi leoo
 
Mh mko wengi,haya endeleeni kutupa uzoefu wenu...
 
zamani kuna mtu aliibiwa redio akaenda kwa mganga ambaye ni jirani yetu.mganga akamwambia aje na watu wote anaoishi nao .Baada ya watu wote kufika mganga akawaambia kila mtu anyanyue begi , wakanyanyua mmoja baada ya mwingine ikafika zamu ya mama mzazi wa mteja wake alikua ni mzee, kabla ajanyanyua begi mganga akasema subiri akaenda ndani na begi alivyorudi akamwambia yule mama anyanyue begi,mama wa watu akashindwa mganga akamwambia mteja wake nadhani umemuona aliye kuibia redio,mteja akasema haiwezekani mama yake aibe redio akamwambia mganga afungue bengi, mganga akagoma mteja akafungua begi kwa lazima, ndani ya begi wakakuta matofali ya blocks.Mganga alikula kichapo.

Nilipelekwa na mganga mtoni maeneo ya Msambiazi kwenye zile kona,mganga akaita mamba mtoni akaniambia nimkalie kichwani,wakati akifanya hivyo alikuwa amenishika nisikimbie.
Yaliyotekea ...nilijikuta kibenderani (polisi)nahojiwa kwa kosa la kushambulia na kutaka ku uwa

Waganga wengi ni waongo balaa
Kuna dada mmoja tulikuwa tunajua anaumwa nini lakini tuliamua kwenda kwa mganga ili tumsikie anasema nini
Mganga akaanza kumwambia umetupiwa jini na mchepuko wa mmeo na ndio linalokutesa
Daah tulicheka balaa baada ya kusikia uwongo wa mganga

[emoji38][emoji38][emoji38]uwiii nimecheka
 
Rekebisha maelezo yako sasa kama hujawahi kwanini useme tulio wahi! Sema mliowahi kwenda kwa waganga njooni hapa. Inavyoonesha wewe ni mmoja wao wa kwa hizo imani ila umeamua ujitoe bila kujijua ukakosea kuandika.
Ulishawahi kwenda kwa daktari akakuambia, tuna tatizo gani leo?

Au akakuandikia dawa alafu akakuambia, tutatumia hizi dawa kwa siku tano, tukiona hali haijatengemaa, tutajua kingine cha kufanya.

Yaani Kuna kitu kinaitwa pragmatics na semantics. Ukivijua hivi huwez kutoa maelezo kama hayo kwenye andiko kama hili
 
Back
Top Bottom