Kwa wale waliozaliwa na waliowahi kuishi Tabora, tukumbushane vituko vya Mboka

Kwa wale waliozaliwa na waliowahi kuishi Tabora, tukumbushane vituko vya Mboka

mnamktmbuka Papa wemba? alikuwa na gari limeandikwa "mokili ya nzambe"mitaa ya chekilaini ya kiloleni mbele ya town skul.
 
uyui mkuu alikuwa mr diaz au bab d.Ulikuwa fm wani gani?
 
Dah napakumbuka saana Tabora!maana ajira yangu ya kwanza nilianzia pale mwaka 2006
 
uyui mkuu alikuwa kasonta,,baadae katanga then mama shani to now
 
[emoji23][emoji23][emoji23]nzega ndio om mkuu nimesoma nyasa one ,
Hahahaaaa Nyasa Mapangon ndugu, unazkumbuka zile habar za Pango jimunye!!! Mi jiran yako pale shule ya Kitongo
 
Km ulikua unakaa Cheyo,Kitete,Gongoni, Kanyenye miaka ile ya 90 lazima Utakua ulisikia habari zao!

Kulikua na Dr pale Kitete Hospital alikua Maarufu Dr Kobello! Hujapata sikia Hilo jina?

Dr Dassy
Dr Mgumia
Dr Gobbo
 
Habari za familia ya dr. Kobelo inasikitisha sana, tulikaa nao mtaa mmoja kota za boma road (tridep), mtoto mkubwa alikuwa akiitwa Tobby wa pili Steve, mdogo sikumbuki jina lake.
Toby na Steve walisoma na wadogo zangu, walikuwa na akili sana hawa watoto, niliondoka kwenda chuo, mzee naye akahamishwa, baada ya chuo post yangu ya kwanza ya kazi ikawa Tabora, makazi yangu yakawa bachu ground, kumuulizia Toby nikaambiwa yupo mahabusu kwa kesi ya mauaji kama sikosei, wakati huo dr. Kobelo ana dispensary yake bachu karibu na mgahawa wa mikendo.
dr. akawa kashikwa masikio na barmaid wa Georgies bar, dr. alikuwa cha pombe sana. akirudi nyumbani anatembeza kichapo kwa mkewe, inasemekana watoto uzalendo uliwashinda wakaamua kumdunda mpaka kumvunja mguu, Steve naye akaingia mahabusu kwa kesi hiyo.
Nilihama tbr, baada miaka kadhaa nikarudi na kukuta Toby katoka lakini tayari ni chizi, niliumia sana! kuna siku alinikuta nipo ziro bar, kaja na fuko lake la makopo, pamoja na uchizi wake lkn alinikumbuka tukaongea vizuri tu
Mama yao alikufa kwa ajari ya kugongwa na pikipiki maeneo ya chuo cha ualimu.
Mdogo wao Edward Kobelo ni classmate wangu na ni deskmate pale Cheyo "A" Primary. He was a friend indeed ilikuwa kila inapofika muda wa mapumziko tunaenda kupiga chai ya maziwa na mikate kwa mama yao wa kizungu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nimecheza basket ball na hao akina Major na akina Bakari Chaima!

Kumbe Major ni marehemu?

Ntuzu,
Umecheza basket na kina Marehemu major ?
ulikuwa unatumia jina gani?
umesoma shule gani ?
umecheza uwanja gani ?
Ulishawahi kucheza kwenye umissetta ?
uzuri wa wacheza basketball kipindi hicho, sote tulikuwa tunajuana vizuri kabisa.
mimi pia ni zao la Uyui Sec.
 
Hao wote ulio wataja ni wadogo zangu kama Meko ni mdogo wangu wa mbali sana. Huyo Marehemu Byera mwenyewe ni mdogo wangu. Mimi ni miongoni wa wanafunzi wa kwanza kabisa kuanzisha A Level. Na kwa taarifa yako tu Uyui Sec nimesoma miaka sita kuanzia form I mpaka VI. Pia nilikuwa HP kuanzia O level mpaka A Level.
Kwa maelezo haya nadhani utakubali naijua Uyui Sekondari. Pia Primary School nimesoma Tabora pia. Si mbali sana na Uyui.
Huyo Kalovya kama sikosei alikuwa anakaa nyuma ya Kazima Sekondari. Nimesoma na Dada yake mkubwa kabisa akiitwa Kulwa Kalovya.
 
Ntuzu,
Umecheza basket na kina Marehemu major ?
ulikuwa unatumia jina gani?
umesoma shule gani ?
umecheza uwanja gani ?
Ulishawahi kucheza kwenye umissetta ?
uzuri wa wacheza basketball kipindi hicho, sote tulikuwa tunajuana vizuri kabisa.
mimi pia ni zao la Uyui Sec.
Alikuwa shabiki labda
 
Mbona umepaniki... tulia kidogo basi,
kuwa mkubwa sio tatizo,maana kwa kipindi hicho tu kuwa High level inatosha kuonyesha kuwa ulikuwa mkubwa tu,Ila hapa tunakumbushana tu utamu wa Tabora hususani kwa watu tuliokuwa hatujuani .
Haujakosea, akina kalovya ndipo walipokuwa wanakaa, na ni kweli HK alikuwa ana dada zake na kaka yao mkubwa( majina nimesahau).Nilichogundua ni kuwa, ulikuwa shabiki wa Basketball lakini haukucheza.nimekuwekea picha ya miaka hiyo uangalie na kutambua wachezaji( Wengi wao wametajwa kwenye uzi huu.Ukizungumzia High level, walikuwepo akina Salehe Kimenya na wengineo.Hakuna sehemu nimeleta ubishi, rudia post yangu.naamini sote tulikuwa watoto wa "DUGU" PATEL, R.I.P, chini ya mkuu msaidizi Mwl.Mkatakona R.I.P na walimu kama , Mr Mbosori R.I.P, Mr Machibwa,Mr Mrisho (Mtaalam wa Hesabu),Mwalimu mmoja wa Biology, alikuwa na jina gumu tukampa nickname Agama Agama nk hawa wote walikuwa baadhi ya walimu wa O level.
 
😀
unajua uzi wa zamani ndio mtamu hasa.
nimeuchokonoa kwakuwa kama miezi kadhaa iliyopita, mwenzetu mmoja alifariki, tulikuwa nae kwenye basket Uyui,
aliitwa Benedictor Jacob ( R.I.P) natamani kuwajua wengine na wengine.Michezo ilitufanya tukawa marafiki bila kujali unasoma wapi, unafanyakazi wapi, unaishi wapi nk.
 
Back
Top Bottom