Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Hapa nimeinukia uyui sec 1997,njooni
Hahahaaaa Nyasa Mapangon ndugu, unazkumbuka zile habar za Pango jimunye!!! Mi jiran yako pale shule ya Kitongo[emoji23][emoji23][emoji23]nzega ndio om mkuu nimesoma nyasa one ,
Km ulikua unakaa Cheyo,Kitete,Gongoni, Kanyenye miaka ile ya 90 lazima Utakua ulisikia habari zao!
Kulikua na Dr pale Kitete Hospital alikua Maarufu Dr Kobello! Hujapata sikia Hilo jina?
Adam Gosho alikuwa anatutembeza mji mzima tunaimba wimbo wa "adam! gosho! Ninja!...acha kulia lia ninja kiboko yao!Kitambo sana,hivi Adam Gosho Ninja yuko wapi sasa hivi!?
Mdogo wao Edward Kobelo ni classmate wangu na ni deskmate pale Cheyo "A" Primary. He was a friend indeed ilikuwa kila inapofika muda wa mapumziko tunaenda kupiga chai ya maziwa na mikate kwa mama yao wa kizungu.Habari za familia ya dr. Kobelo inasikitisha sana, tulikaa nao mtaa mmoja kota za boma road (tridep), mtoto mkubwa alikuwa akiitwa Tobby wa pili Steve, mdogo sikumbuki jina lake.
Toby na Steve walisoma na wadogo zangu, walikuwa na akili sana hawa watoto, niliondoka kwenda chuo, mzee naye akahamishwa, baada ya chuo post yangu ya kwanza ya kazi ikawa Tabora, makazi yangu yakawa bachu ground, kumuulizia Toby nikaambiwa yupo mahabusu kwa kesi ya mauaji kama sikosei, wakati huo dr. Kobelo ana dispensary yake bachu karibu na mgahawa wa mikendo.
dr. akawa kashikwa masikio na barmaid wa Georgies bar, dr. alikuwa cha pombe sana. akirudi nyumbani anatembeza kichapo kwa mkewe, inasemekana watoto uzalendo uliwashinda wakaamua kumdunda mpaka kumvunja mguu, Steve naye akaingia mahabusu kwa kesi hiyo.
Nilihama tbr, baada miaka kadhaa nikarudi na kukuta Toby katoka lakini tayari ni chizi, niliumia sana! kuna siku alinikuta nipo ziro bar, kaja na fuko lake la makopo, pamoja na uchizi wake lkn alinikumbuka tukaongea vizuri tu
Mama yao alikufa kwa ajari ya kugongwa na pikipiki maeneo ya chuo cha ualimu.
Nimecheza basket ball na hao akina Major na akina Bakari Chaima!
Kumbe Major ni marehemu?
Huyo Kalovya kama sikosei alikuwa anakaa nyuma ya Kazima Sekondari. Nimesoma na Dada yake mkubwa kabisa akiitwa Kulwa Kalovya.Hao wote ulio wataja ni wadogo zangu kama Meko ni mdogo wangu wa mbali sana. Huyo Marehemu Byera mwenyewe ni mdogo wangu. Mimi ni miongoni wa wanafunzi wa kwanza kabisa kuanzisha A Level. Na kwa taarifa yako tu Uyui Sec nimesoma miaka sita kuanzia form I mpaka VI. Pia nilikuwa HP kuanzia O level mpaka A Level.
Kwa maelezo haya nadhani utakubali naijua Uyui Sekondari. Pia Primary School nimesoma Tabora pia. Si mbali sana na Uyui.
Alikuwa shabiki labdaNtuzu,
Umecheza basket na kina Marehemu major ?
ulikuwa unatumia jina gani?
umesoma shule gani ?
umecheza uwanja gani ?
Ulishawahi kucheza kwenye umissetta ?
uzuri wa wacheza basketball kipindi hicho, sote tulikuwa tunajuana vizuri kabisa.
mimi pia ni zao la Uyui Sec.
hahaha!Alikuwa shabiki labda
Mimi apa au..?