Kwa mario utafanikiwa ila kwa hustler sahauAtakayenioa anacho atafua boksa zake na michupi yangu 😹🤣🤣
Namwambia kabisa ukimaliza babe uje nikupoze na tumbua 🤭
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Kwa mario utafanikiwa ila kwa hustler sahauAtakayenioa anacho atafua boksa zake na michupi yangu 😹🤣🤣
Namwambia kabisa ukimaliza babe uje nikupoze na tumbua 🤭
Kwa nini niteme mate chini?( sijaelewa).Tema mate chini. Hata ufanye nini kamwe huwezi kuwatimizia watakayo hawa wapenzi wetu. Natoa mfano, humu JF kila wakati utasikia, mwanaume tafuta pesa. Je Kocha wa Manchester City si mke wake ambaye ameishi naye miaka 30 ametoa sababu ipi ya kudai talaka? Just imagine! Mwanamke kama ni mnoko ni mnoko tu, jinsi ya kuishi naye ni agreement ya division of labour na unahakikisha huo mkataba unadumu miaka yote, ukivunja kipengele kimoja basi wewe kwisha.
Hamna jema nyie Watu, mnatumika kutupa faraja ila mkitukuta na hio faraja mnatupa stressHata mim ningekuhoji au Kuna jambo limetendeka lakukufanya wewe ufue hiyo nguo? Maana sio kazi yako kufua
Hapa hatuishii kusema Mashaallah tu.Ni maisha raha!🙏Wife ana raha sana
Acha mbwembwe.Sugua zitakate!😂Kumbe mambo ya kufua chupi alaah! Anakufulia af siku mkikosana anasema "mwanaume ananitesa yule namvumilia tu nilifua boxa nikakuta vimavi mavi" [emoji3]
...
Kama nitamfulia mke wangu vyupi formula ni moja gusa achia suza anika twende mbele
Maisha ya ndoa ukiyachukulia simple unaishi vizuri sana. Tatizo ukikaza shingo na kujifanya wewe ndio wewe lazima ndoa uione chunguHapa hatuishii kusema Mashaallah tu.Ni maisha raha!🙏
Umeelezwa na JF uwe unatumia neno "MKUU" kila unapomu-address member humu.Hayo majina ya mwanamke au mwanaume au mtoto au mwanafunzi unayatoa wapi?Nani alikueleza mimi ni mwanamke?Halafu jifunze kutoa komenti fupifupi.Kitu kidogo unajieleza utadhani umemuona mkweo?Kuwa na adabu.Marabook!Mwanamke kama unamawazo hayo na bado upo kwenye ndoa, basi huyo mmeo anae jifuria hizo nguo zake mshikilie sana .
Mwanaume rijali siwezi kuingia bafuni kuoga nianze kufua boksa na mke yupo, nitafanya hiyo kazi kama nipo kambini ambapo najua wazi sina wakunijali zaidi ya mm kujijari tena nitafua na nitaivaa hata bado haijakauka, itakaukia mwilini.
Ila eti nipo nyumbani kabisa naingia bafuni kuoga , namaliza nusu saa bafuni kumbe nafua na nguo za ndani , huyo mke si bora aondoke tu sasa.
Man be a Man.
Mimi hata kipindi cha ubarobaro , akinitembelea mwanmke geto asipo fua nguo na kufanya usafi ndani ,ajue ndo mwisho wake huo, sitaki mwanamke anae taka kutawala mwanaume mm.
Mwanamke majukumu yote ya ndani ya nyumba ni yako, iwe kupika , iwe usafi wa nyumba, na mambo yanayo mhusu mmeo kama usafi wa nguo zake nk ni juu yako.
Hakuna cha kusema sijui mme wangu na wewe leo pika sijui nini na nini , hakuna hicho kitu, kuna wanaume wanajifanyaga wanajua kujibebisha eti siku moja moja wanaingia jikoni kupiga , huo ni upuuzi na mwisho wa siku mambo huwa yanawageukia, mwanamke anaakiri zake anazo zijua mwenyewe.
Ukimpa favor ya jambo fulani anaanza kulifanya kuwa ni haki yake.
Utashangaa mwisho wa siku anakupangia zamu ya kupika.
Siku zote mwanamke usimchukulie poa ,wana mambo ya ajabu sana kutokana na kuishi kwa kuendeshwa na hisia zao,mda wowote ana halibu jambo ,ndio maana ukitaka umfaidi mwanmke ishi nae kibishi,usilete mazoea nae ya kipuuzi.Atakufanyia vitu vya kipuuzi sana usipo kuwa makini .
Mwisho: mwanaume hafui nguo,ukianza kufua nguo tambua kabisa tayari wewe umeshaelekezwa kibra.
Nenda kaungane na kataa ndoa mana ndoa huiwezi,ndoa si kwa wanaume dhaifu,ndoa ni kwa wanaume Ngangari tu.
Sahihi.Mimi nikiwa na memsaheeb huwezi kujua mpaka uambiwe au uwe umepitia "the very deeper school of life"!Ni kirafiki zaidi.Nami utani ulivyonijaa basi utadhani nipo na mfanyakazi mwenzangu tu.🙏Maisha ya ndoa ukiyachukulia simple unaishi vizuri sana. Tatizo ukikaza shingo na kujifanya wewe ndio wewe lazima ndoa uione chungu
mkuu kufua nguo za ndani ni jukumu la mke Full stop muulize [@nakwede7] anaelewaAcha mbwembwe.Sugua zitakate!
Sugua suuza hakikisha imetakata!khee? 😳unasema?
Na inapaswa iwe hivyo.Maisha ya ndoa ukiyachukulia simple unaishi vizuri sana. Tatizo ukikaza shingo na kujifanya wewe ndio wewe lazima ndoa uione chungu
Mkuu, kwenye ndoa ukishaona mnaanza kupeana formula na masharti ya kuishi, basi ujue hiyo ndoa ina tatizo. Ndoa inataka muishi kama watoto wadogo. Kwa mfano simu: msiviziane kuchunguza simu zenu na pia msiwekeane masharti kuwa lazima unionyeshe simu yako. Nguo hivyo hivyo na mapishi na hata kutandika kitanda. Kuhusu nguo za ndani hili nalo mnaweza kufuliana bila masharti japo mara nyingi kwa mila za kiafrika mtu anapooga huwa anafua nguo yake ya ndani. Ila msimpe mfanyakazi.Nimetebasamuu halafu nikataka kucheka ila kicheko kikapotea....
Haya mambo banaa, na usishangae kuna walioachana kisa kufua nguo za ndani....
Mke anasema mimi sifui boksa zako unavaa wiki nzima unarudia...
Mume anakasirika kwanini hunijali na mimi nispoona boksa safi navaa ya jana...!!!🤔🤔🤔 (ana mkomoa nani...! Mbupuuu au mkee..!!?). Ukurutu unaanzia hapa..
Kuoa au kuolewa ni zaidi ya kufanya harusi, shurti kwanza uwe umepevuka kiakili/maarifa na uwe na busara za kutosha.
Ukiwa na mihemko, hasira za mkizi na maamuzi yasiyo na kichwa wala miguu, umekwisha.....!!
Jiulize tuu, kutoa/kutolewa mahari ndo sababu ya kubadili mfumo wako wa maisha?
Kama wakati uko mseja ulikuwa unajimudu, kwanini baada ya kuoa/kuolewa uwe mlemavu mwenye viungo vyote? Hii ni hata kina dada, kama ulikuwa unajigharamia kwanini baada ya kuolewa ugharamikiwe...!!
Fanya huduma unayopewa na mwenza kama zawadi/nyongeza isipokuwepo isokuletee masononeko, maumivu au kuona hutendewi haki au kudhulumiwa.
Sikuzote penda maisha ya kujitegemea na si kutegemea flani kwa namna yeyote ile. Atayekupenda kwa dhati atakufata hapo ulipo ukiwa unajimudu na yeye asikufanyie jambo ili umuelekee, afanye bila kutarajia malipo.
Suluhiso la kuondoa hiyo kero tajwa, wekeni bajeti ya luku ya kutosha kwa mwezi, bajeti ya bili ya maji, nunueni mashine ya kufulia, chupi/boksa za kuvaa mwezi mzima bila kurudia.
Siku ya kufua iwe mara moja au 2 kwa wiki mnatumbukiza visinda vyenu humo, vesti, soksi, hendikachifu, brazia, gagulo, skin tite kisha mnaanika kama hamna mashine ya dryer.
Mkishindwa hapo tembeeni wizout. Yaani wewe usivae boksa, nayeye asivae kufuli wala brazia, nawewe usivae vesti wala soksi kukwepa nani afue na pia mtapunguza gharama ya kuzinunua.
NB: Dada wa kazi asifue nguo yeyote ya ndani. Mpeni suruali mashati magauni sketi blauzi basi. Hata hendikachifu asifue.
HYGENE: Usirudie kuvaa nguo ya ndani, vaa nguo ya ndani.mara moja kisha ifue.
Mwenye sikio asikie.
Bibi Kasinde.
Nimekutunuku medani kwa hii comment. Ndoa inatakiwa watu waishi free bila fomula, bila masharti na bila kuviziana. Ukishaona ndoa ambayo ina mambo kama kupekua simu ya mwenzako, masharti ya nani anahistahili kutandika kitanda na kufua nguo za mwenzake nk basi hiyo ndoa ina tatizo.Kwenye ndoa.. Hasa kwa wanaojua maana ya ndoa mambo mengi hayana formula.. Ama formula Ku u ni upendo