Kwa wanaoamini hakuna Mungu, njooni hapa

Kwa wanaoamini hakuna Mungu, njooni hapa

Kwa kawaida kwa akili ya binadamu kila kitu kikiwepo sehemu ni juhudi za watu barabara zikichongwa watu wamepambana internet simu roboti nk Lakini hili la sisi kuwepo duniani amuamini kwa kuna juhudi ama mambo yamefanyika na hii dunia kuwepo hivi unavutia kiasi uoni hata kasoro si juhudi ama kweli natwanga maji kwenye kinu😭
Wewe huelewi kuwa hiyo hoja yako ni hoja ya kuonesha Mungu hayupo.

Yani ukichoandika, kwa ntu mwenye kufikiri kwa kina, ni hoja ya kukataa uwepo wa Nungu.

Ila wewe hujajua tu, kwa sababu hufikiri kwa kina.

Kimsingi umeweka hoja kwamba order cannot come out of disorder, vitu haviwezi kuwepo tu vimejioanga, lazima kuwepo na aliyevipanga, na aliyevipanga lazima awe na order au intelligence ya zaidi.

Sasa, unalazimisha Mungu awepo na awe ndiyo huyo akiyepanga (hata kama hoja hii ina non sequitur fallacy kutoka kwako, nitaiendekeza tu kwa sasa).

Tuseme Mungu yupo, na ndiye kaumba haya tunayoyaona.

Bado, kwa kufuata kanuni yako ya order au ibtelligence haiwezi juwapo tu, ni kazima iwe imeumbwa na order au ibtelligence ya juu zaidi, utakuwa umejipa hoja kwamba Mungu naye hawezi juwapo, itabidi awe ameumbwa na Mungu wake.

Na Mungu wake hawezi kuwapo, naye lazima kaumbwa na Mungu wake.

Ad infinitum, ad nauseam.

Hapo utaona msururu usioisha wa miungu wanaoumbwa na miungu wao.

Hapo hakuna Mungu muumba vyote.

Hoja yako inaonesha Mungu hayupo.

Of course unaweza kusema Mungu yeye hajaumbwa.

Which is special pleading logical fallacy.

Na hii special pleading logical fallacy inaharibu hoja nzima kuwa order haiwezi kuwapo bila kuumbwa.

Naandika lakini sina hakika kama unaweza kufuatilia mantiki ya ninachoandika.
 
OK.

Mimi nawaza kimantiki. Logically.

Ukweli una tabia ya kuwa logically consistent.

Kwa mfano. Kuanzia na Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na uoendo wote. Ukisema kuna Mungu, mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote, Mungu huyo kuumba ulimwengu ambao unaweza kuwa na mabaya mengi, mauaji, magonjwa, majanga ya kiasili, uonevu, ni logically inconsistent.

Ni contradiction.

Hii logical inconsistency inaleta contradiction, hii contradiction inaonesha Mungu huyu hayupo, ni stories za watu tu.

Kwa nini Mungu mwenye uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote aumbe ulimwengu huu unaoweza kuwa na mabaya wakati alikuwa na uwezo wote wa kuumba ulimwengu huu uwe hauruhusu baya lolote?

Kama huelewi hoja za kimantiki kama logical consistency, contradiction, the problem of evil, unaweza kupata tabu kuelewa nilichoandika.

Kama unaelewa haya ni mambo yaliyo wazi kabisa.

Kwa hivyo, ukitaka nikubali uwepo wa Mungu, angalau weka maelezo ya uwepo wa huyo Mungu ambayo yapo logically consistent na hayana contradiction.

Siyo unanipa stories za Mungu za kuungwaungwa ambazo ukizipima kimantiki unaona kabisa hazina logical consistency.
Ila ninavyojua ni kuwa Mungu amempa Kila mtu uhuru wa kufanya anachotaka yaani wewe ndio utaamua ufanye anachotaka yeye au ufanye unachotaka wewe ila mwisho wa siku mkifunga mahesabu hakutakuwa na kulaumiana kwa sababu yote uliyafanya kwa dhamiri yako mwenyewe.Magonjwa pia yapo sababu ni binadamu,muda mwingine Magonjwa yanasabishwa na wanadamu pia Bila magonjwa duniani tungeishi milele sababu hakuna ambae angekufa
 
Yaani huyu akili zake ukweli mimi sijasoma lakini nakuona nakuzidi uelewa pakubwa sana, mungu kaumba watu, na kwa mantiki yako ulitaka aumbe watu waliokuwa perfect wasio na kasoro hata kidogo si ndio, ndo unazo zitaja uzuri ubaya n.k, katuumbia sifa zote izo na kutuwekea uwelewa mpana wa kufahamu juu ya yale tutendayo anae fanya uzuri anajua kwamba huu uzuri na huu ubaya na uwezo wote wakuzuia anao, uoni kama sifa za mungu ni kubwa sana, na kubwa tuko dunia kama mtihani ambao tunapaswa tufanye vizuri kwa juhudi ili uko ahera hivyo vitu perfect unavyo vitaka vipo umeelewe?
Kwa nini Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote kaumba ulimwengu huu unaoweza kuwa na mabaya wakati aliweza kuuumba ulimwengu huu uwe hauwezi kuwa na mabaya?
 
Ila ninavyojua ni kuwa Mungu amempa Kila mtu uhuru wa kufanya anachotaka yaani wewe ndio utaamua ufanye anachotaka yeye au ufanye unachotaka wewe ila mwisho wa siku mkifunga mahesabu hakutakuwa na kulaumiana kwa sababu yote uliyafanya kwa dhamiri yako mwenyewe.Magonjwa pia yapo sababu ni binadamu,muda mwingine Magonjwa yanasabishwa na wanadamu pia Bila magonjwa duniani tungeishi milele sababu hakuna ambae angekufa
Kwanza Mungu hakumpa kila mtu uhuru wa kufanya anachotaka.

Hatunanuhuru wa kufanya tunachotaka.

Wewe huna uhuru wa kurudi mwaka 1982.

Kwa hiyo hizo habari za Mungu katupa uhuru wa kufanya tunachotaka si kweli.

Mtu aliyekufa mwaka 1982 hana uhuru wa kujiunga na JF leo tuongee naye.

Swali la msingi ni hili.

Kwa nini Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote kaumba ulimwengu huu unaoweza kuwa na mabaya wakati aliweza kuuumba ulimwengu huu uwe hauwezi kuwa na mabaya?
 
I mean sawa you don't believe about God then what do you say about superstition.Tumeona mambo yakichawi hapa Tanzania mtu anazikwa anakuja kuonekana baada ya miaka kumi na alizikwa na ndugu zake walikuwepo,watu wanatengeneza radi huko mtwara,watu wanatibu mifupa bila kuishika ila kwa kupaka dawa mikononi na kunuia
 
Ukishakufa hayo mambo ya kusomewa au kutosomewa ni sherehe ya waliobaki, aliyekufa hata hajui nini kinaendelea by all scientific evidence.

Mimi kwetu wanajua siamini uwapo wa Mungu. Huwa nawanunulia vitabu vya kuonesha Mungu hayupo nawapa zawadi.

Mkuu,

Ukisali na ukapata kitu fulani utajuaje umekipata kwa sababu Mungu yupo kasikia sala zako na kakupa hicho kitu na si kwa sababu yoyote ile nyingine?

Na vipi kuhusu mara zote unazosali kutaka kitu halafu hupati, hilo nalo linathibitisha Mungu hayupo?

Ukiombewa shida ikaondoka, unajuaje imeondoka kwa sababu ya Mungu kasikia na kaiondoa, na si kwa sababu nyingine yoyote?

Na vipi kuhusu siku zote unapoombewa na shida haiondoki, hilo linathibitisha Mungu hayupo?

Unaelewa kitendo cha kusali na kuomba chochote kwa Mungu kinathibitisha Mungu hayupo?

Mungu muweza yote, mjuzi wa yote na mwenye upendo wote angekuwepo, angejua utakachohitaji kabla wewe hujakijua, na angekupa kabla wewe hujakiomba, na kama hakikufai asingekupa hata tamaa ya kukitaka.

Ukijiona una uhitaji mpaka ukafikia hatua ya kumuomba Mungu akupe kitu, huo uhitaji ni uthibitisho kwamba Mungu hayupo.

Angekuwapo, usingekuwa na uhitaji kabisa. Angekupa unachohitaji kabla hujajua unakihitaji.
Kwani wewe ukimuamini yupo kuna nini ..?
 
Sitaki kuamini, nataka kujua ukweli.

Kuamini unaweza kuamini hata uongo, mimi sitaki uongo, nataka kujua ukweli.
Kwanini unaamini Mungu hayupo leta udhibitisho ?!! Kwasababu ushahidi kuwa yupo umejaa Kuna mimea ...wanyama tofauti Kuna kila kitu
 
Mungu ni mungu mimi ni mimi, ingekuwa mungu ndani yangu nisinge kubali kufaa
Muumba alisema majira ikifika ataishi katikati yetu na majira yake ndo hii kwa mujibu wa

Ufunuo 21:3
Nikasikia sauti kubwa kutoka katika kile kiti cha enzi ikisema, Tazama, maskani ya Mungu ni pamoja na wanadamu, naye atafanya maskani yake pamoja nao, nao watakuwa watu wake. Naye Mungu mwenyewe atakuwa pamoja nao.

Isaya 57:15
Maana yeye aliye juu, aliyetukuka, akaaye milele; ambaye jina lake ni Mtakatifu; asema hivi; Nakaa mimi mahali palipoinuka, palipo patakatifu; tena pamoja na yeye aliye na roho iliyotubu na kunyenyekea, ili kuzifufua roho za wanyenyekevu, na kuifufua mioyo yao waliotubu.

Zekaria 14:9
Naye Bwana atakuwa Mfalme juu ya nchi yote; siku hiyo Bwana atakuwa mmoja, na jina lake moja.
 
Kwani binadamu alitoa wapi akili adi akajua monosaccharides... disaccharides
Kwamba Ukifika mwisho wa Kufikiri Basi lazima Useme kuwa Lazima kuna sehemu binadamu alitoa Akili au Sio??
Uwepo wa Akili wa Binadamu unachangiwa na Neurones nyingi na Cells Nyingi za Utambuzi alizonazo kwenye Ubongo ambazo Hutengeneza mawimbi makali ya Umeme kwa ajili ya Kutafuta Suluhisho
 
Kwamba Ukifika mwisho wa Kufikiri Basi lazima Useme kuwa Lazima kuna sehemu binadamu alitoa Akili au Sio??
Uwepo wa Akili wa Binadamu unachangiwa na Neurones nyingi na Cells Nyingi za Utambuzi alizonazo kwenye Ubongo ambazo Hutengeneza mawimbi makali ya Umeme kwa ajili ya Kutafuta Suluhisho
Kwamba izo sell umeziunda wewe
 
Kwanini unaamini Mungu hayupo leta udhibitisho ?!! Kwasababu ushahidi kuwa yupo umejaa Kuna mimea ...wanyama tofauti Kuna kila kitu
Unfahamu Kama Kuna mimea Ambayo miaka 1000 iliyopita au 2000 iliyopita haikuwepo na Kuna wanyama ambao hawakuwepo Miaka 2000 iliyopita ila sasa wapo??

Unafahamu kuwa Ng'ombe waliopo sahizi ni zao la Asili ya Ngombe mwitu waliokuwa wanaitwa Aurochs..
Ambao kwa sasa wamekuwa extinct..
Vipi hawa Ngombe wa sahizi mumgu aliwaumba??
Vipi kuhusu mimea Ambayo Zamani haikuwepo??

So kuihusisha Mimea na Wanyama kama Mifano nafikiri sio sawa Mtu wa Miaka 2000 iliyopita akija akakuta wanyama Tulionao na Mimea Tulionao atashangaa sana
 
Ukweli upi?
Ukweli ulio na logical consistency.

Usio na contradiction.

Dhana ya sasa ya kuwepo Mungu, hususan kuanzia na Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote ina contradiction, haina logical consistency.

Contradiction moja kubwa ni The Problem of Evil, ambayo nimeielezea hapo juu.

Contradiction hii haijapatiwa ufumbuzi mpaka leo. Inaonesha huyo Mungu hayupo ndiyo maana contradiction hii haijapatiwa ufumbuzi.

Ila, katika uzi huu, kufanya mazungumzo ya kifalsafa ya logical consistency, contradiction, the problem of evil, etc, na watu wengi, ni kazi ngumu.

Kwa sababu watu wengi hawaelewi au hawajali haya mambo.

Watu wengi hapa hawaelewi hata The Problem of Evil ni nini.

Wangeelewa, nisingekuwa na kazi kubwa sana ya kujieleza.
 
Kwamba Ukifika mwisho wa Kufikiri Basi lazima Useme kuwa Lazima kuna sehemu binadamu alitoa Akili au Sio??
Uwepo wa Akili wa Binadamu unachangiwa na Neurones nyingi na Cells Nyingi za Utambuzi alizonazo kwenye Ubongo ambazo Hutengeneza mawimbi makali ya Umeme kwa ajili ya Kutafuta Suluhis

Unfahamu Kama Kuna mimea Ambayo miaka 1000 iliyopita au 2000 iliyopita haikuwepo na Kuna wanyama ambao hawakuwepo Miaka 2000 iliyopita ila sasa wapo??

Unafahamu kuwa Ng'ombe waliopo sahizi ni zao la Asili ya Ngombe mwitu waliokuwa wanaitwa Aurochs..
Ambao kwa sasa wamekuwa extinct..
Vipi hawa Ngombe wa sahizi mumgu aliwaumba??
Vipi kuhusu mimea Ambayo Zamani haikuwepo??

So kuihusisha Mimea na Wanyama kama Mifano nafikiri sio sawa Mtu wa Miaka 2000 iliyopita akija akakuta wanyama Tulionao na Mimea Tulionao atashangaa sana
Sasa kama hoja Yako inasema Mungu hayupo basi unaamini recaination ipo
 
Kwanini unaamini Mungu hayupo leta udhibitisho ?!! Kwasababu ushahidi kuwa yupo umejaa Kuna mimea ...wanyama tofauti Kuna kila kitu
Anayesema Mungu yupo ndiye mwenye mzigo wa kuthibitisha Mungu yupo.

Mimea na wanyama vinathibitishaje Mungu yupo?
 
Kwamba Ukifika mwisho wa Kufikiri Basi lazima Useme kuwa Lazima kuna sehemu binadamu alitoa Akili au Sio??
Uwepo wa Akili wa Binadamu unachangiwa na Neurones nyingi na Cells Nyingi za Utambuzi alizonazo kwenye Ubongo ambazo Hutengeneza mawimbi makali ya Umeme kwa ajili ya Kutafuta Suluhisho

Ina maana Hata Cell Theory Huijui???
Na bado unaleta Discussion ya Uumbaji??
Kila uumbaji au upatikani wa kitu una mizizi yake, kama ilivyo simu ya kwanza kutengeneza, gari, na vitu vengine utaniambia sayansi kibao sababu wewe ni daktari nazungumza sababu ya vitu vyote kuwepo hizi sio nadharia zenu za binadamu wa kwanza alikuwa nyani
 
Back
Top Bottom