Mbo Mpenza
JF-Expert Member
- Apr 11, 2017
- 445
- 1,114
Kuna baadhi ninavyo kwangu
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Ukiweza jifanyia vitu vidogo vidogo kwako, hutokuja shindwa ishi popote wala na yoyote, iwe kwa ndugu au kwako utaonekana mtu muhimu sana, nakumbuka enzi nakua pale mtaani kwetu (kota) nilivyokuwa muhimu, kurekebisha tv, deki, antenna, simu, sprayers, mabomba, baiskeli nk nilikuwa naonekana mtoto wa mfano kwa kila mtuHapa nyumbani kwa shangazi napoishi hua kazi zote za namna hizo hua nafanya mimi, wao wananishangaa nawezaje kufanya hizo kazi na mimi nawashangaa wanashindwaje kufanya hizo kazi ndogo ndogo.
Nimeona uzi nikaangalia room yangu na sebule ilivojaa nadhani nikinunua vifaa vyote ulivyoweka hapa labda niwe naviweka kitandaniKwa wanaume wenzangu habari za muda huu, naomba niende moja kwa moja kwenye mada husika kama nilivyoitambulisha hapo juu. Ikiwa una familia au unaishi bachelor tafadhali zingatia hili linakihusu.
Nyumbani kwako hakikisha mwanaume hukosi essential tools kadhaa kwa ajili ya kupunguza changamoto ndogo ndogo ukizingatiwa wewe ni mwanaume, familia nzima itakutegemea wewe. Vifaa muhimu kabisa hutakiwi kukosa kwako ni kama ifuatavyo:
1. Tester ya umeme. Hakikisha hiki kifaa hukosi kwako, kitakupunguzia ajali kwako za umeme kwa kutambua wapi kuna leakage ya umeme pia itakusaidia ku repair issue ndogo ndogo zinazohusiana umeme kwako, imagine hata kubadilisha holder ya balbu ya taa chumbani kwako uende kumwita fundi aingie chumbani kwako na mkeo.
2. Nyundo ndogo. Vifaa vingi ndani ya nyumba vimeundwa kwa misumali, sasa hata kugongea msumali ulio loose ushindwe?
3. Screw driver. Wengine wanaiita "bisibisi" siku hizi kuna set hata machinga wanaziuza itakusaidia hata kukaza nati ya kitasa chako cha chumbani
4. Panga. Licha ya kazi nyingine ni silaha pia.
5. Jembe. Kila mtu anajua kazi yake
6. Shoka, sururu, kwanja hii inategemea na mazingira yako
7. Tool box, sio lazima liwe special weza tengeneza la mbao au chuma, hifadhi powertools zako.
8. Drills, siku hizi kuna simple drills zinauzwa madukani tena za kuchaji ambayo una regurate speed unaweza tumia kama drill au hata kama screw driver, bei yake inategemea ila ni tool muhimu sana, imagine chumban kwako sasa hivi ukitaka tundika tv ukutani unafanyaje? Utamwita fundi chumban kwako? Kuitumia ni rahisi sana tena YOUTUBE WANAFUNDISHA.
9. Spana. Hapa si lazima uwe na set nzima angalau hata ile adjustable ambayo inaweza fanya kazi kwenye nati tofauti tofauti.
10. Koleo (pliers) siku hizi zipo zenye kazi hadi 4 ndani ya moja
11. Chepe. Hata kuzoa taka ndani ya nyumba uweze, usishindwe hata chimba shimo la taka
12. Reki. Usiwe kila siku wa kuazima reki ya sh 5000
13. Baiskeli. Hii kwa mazoezi, kama nafasi yako ni ndogo siku hizi zipo unazoweza kuzikunja na kuhifadhi sehemu ndogo.
14. Misumari, akiba ya misumali saizi tofauti tofauti itakusaidia repairs zisizotarajiwa
15. Air pump yoyote hata ya mkono. Kama unamiliki chombo chochote cha usafir kilicho na tire ya kujaza upepo usikose hii kitu, imagine umeamka pikipiki au gar imepungua sana upepo utafanyaje? Ndio wamwita fundi? Jaza upepo ukusogeze kwenye tire services
16. Torch. Kazi ya tochi inajulikana kuna wenzetu hata tochi ya battery hana, dharula haina hodi
17. Mashine ya kunyolea (homecut). Kama una watoto hakikisha una mashine yako, weekend watoto unawanyoa mwenyewe, hii inaongeza mapenz ya baba na watoto.
18. Msumeno, yes kwenye toolbox yako uwe na msumeno mdogo hata ule wa 5000 utakusaidia siku moja
19. Mzani, hata ule simple wa spring unaoishia kilo 5 wa bei ndogo sana, kuna siku utakupunguzia kazi hapo kwako.
20. Toroli, kama unaishi nje ya mji toroli muhimu sana kwa shughuli ndogo ndogo nyumbani, usipende kila kitu kubeba utapata madhara ya mgongo.
21. Extension ya umeme, yes kaa na extension ya ziada ya umeme, kuna siku utahitaji kuliko kwenye wagongea majiran upate fedheha.
Kwa mwingine anaeweza endeleza list, share nasi
Imagine unakuja kwangu unakutana na hivyo vitu vyote alivyoorodhesha mleta mada.Itakuwa wanajiandaa kufungua chuo Cha veta😀
😀😀Imagine unakuja kwangu unakutana na hivyo vitu vyote alivyoorodhesha mleta mada.
Unaweza kujiuliza "hivi huyu jamaa hiki ni chumba cha kuishi au stoo ya fundi makenika?
jembe,nyundo,sururu,chepe, panga, n.kTester, pliers, inakubanaje?
Aaah! kwahiyo huu uzi ni wa wafuga kuku na mafundi?Sawa,basi huu uzi haukuhusu
HIV RAPID TEST hiv zinauzwa ? hiz na bei gan??Box la condom na vipimo vya HIV (rapid test) ni muhimu sana
Hakuna kitu hapo mkuuAcha kukaza hilo fuvu hapo juu ya shingo. Vitu simple lkn unashindwa kuelewa kwa sababu umekaza hilo fuvu.
Sasa si unaona we una fundi seremala kabisa. Hongera bwanaHapa nyumbani kwa shangazi napoishi hua kazi zote za namna hizo hua nafanya mimi, wao wananishangaa nawezaje kufanya hizo kazi na mimi nawashangaa wanashindwaje kufanya hizo kazi ndogo ndogo.
Wadau wamechangia na box la roughrider liwepo, so hadi hilo unabisha?Hakuna kitu hapo mkuu
Let's say vijana hawa wanaosajili laini unamshauri kuwa na msumeno,msumari,toroli vya nini? Namshukuru aliyeconclude kwa kusema huu uzi sio wa wote ni wa wafuga kuku na maseremala kama wewe tu. Ndio ile mnawafanya watu wawe na full equiped work shop ndani unajikuta unawafurahisha majirani maana wana fundi karibu wa kurekebisha samani zao