Kwahili la Mabasi kusafiri Usiku, nampongeza Mbunge Tulia Ackson

Kwahili la Mabasi kusafiri Usiku, nampongeza Mbunge Tulia Ackson

Nchi za kimaskini ni matatizo sana,usafiri wa kwenda sehemu yoyote unatakiwa kuwepo muda wowote na sio kupangiana wakati.
Inatakiwa kama Upo Dar na unasafari ya mwanza-uondoke hata sa 5 Mchana.
 
Mbona mna maswali ya kipimbi sanaa? Hivi mnajua miaka ya 90 mabasi yalikuwa yakisafiri usiku? Ngorika, Lang'ata kutoka Arusha kuja Dar, tena barabara ilikuwa mbaya maeneo mengine. Pale Mbwewe tulikuwa kunapiga sana vyuku... Iringa, Mbeya kulikuwa na Zainabu bus, Scandinavia etc... Songea kulikuwa na Kiswere nk.. Yote yalikuwa yakipiga ruti za usiku. Sasa tunaenda mbele au tunarudi nyuma?? Hatuwezi kuingia uchumi wa juu ikiwa watu hawawezi kufanya kazi usiku, eti hakuna kusafiri usiku na asubuhi Bus zinapangiwa wote waanze saa 12 wakimbizane njia nzima, haya mambo ya kiwaki sana aisee daaah.
Sawa mkuu
 
Tujiandae na kulia sana
Ajali nyingi mchana Usiku itakuwaje
Wakati wa kuwekewa mawe barabarani/Kitonga ni nyakati za Usiku
Watakaoteseka ni wamama wazee na watoto
Hii nchi inazidi kurudi nyuma…
 
Wakati serikali ya Mwinyi inapiga marufuku mabasi ya abiria kutembea usiku nilikuwa Bado mdogo ila naikumba ile ajali ilikuwa mbaya sana kama sijakosea lile Bus lilichanika ubavuni abiria wakawa wanamwagika kama Michele

Changamoto za safari za usiku
1) Barabara zetu hazina taa hivyo dereva anategemea ta za Gali tu

2) Barabara zetu ni nyembamba sana

3) Maloli yanayo haribika barabarani huwa hayatolewi na kuwekwa katika road reserve kama nchi nyingine hapa kwetu Loli linakaa hata siku 3 barabarani

4) Kuna ukungu pia ni chanzo kikubwa sana Cha ajali kwa Magali yanayosafiri usiku

5) Mabusi ya siku hizi Yana speed sana madereva lazima watashawishika kutembea kwa speed kubwa

6) kwa Sasa barabara ya Dar to Dom ipo bize sana na ajali nyingi zitatokea hapo
 
Wakati serikali ya Mwinyi inapiga marufuku mabasi ya abiria kutembea usiku nilikuwa Bado mdogo ila naikumba ile ajali ilikuwa mbaya sana kama sijakosea lile Bus lilichanika ubavuni abiria wakawa wanamwagika kama Michele

Changamoto za safari za usiku
1) Barabara zetu hazina taa hivyo dereva anategemea ta za Gali tu

2) Barabara zetu ni nyembamba sana

3) Maloli yanayo haribika barabarani huwa hayatolewi na kuwekwa katika road reserve kama nchi nyingine hapa kwetu Loli linakaa hata siku 3 barabarani

4) Kuna ukungu pia ni chanzo kikubwa sana Cha ajali kwa Magali yanayosafiri usiku

5) Mabusi ya siku hizi Yana speed sana madereva lazima watashawishika kutembea kwa speed kubwa

6) kwa Sasa barabara ya Dar to Dom ipo bize sana na ajali nyingi zitatokea hapo
Mbona Kuna coaster za Dar to Singida -Mwanza?! Zinasafiri usiku
 
Tujiandae na kulia sana
Ajali nyingi mchana Usiku itakuwaje
Wakati wa kuwekewa mawe barabarani/Kitonga ni nyakati za Usiku
Watakaoteseka ni wamama wazee na watoto
Hii nchi inazidi kurudi nyuma…
Seems huna taarifa sahihi, Mabasi kadogo na Malori yanatembea
 
Sa tatu watu wanaenda mbeya mwanza..wasubir tu pakuche wapande sauli
Inaendelea....

Muda huu ninapoandika hili ni 21:45 ukienda pale Mbezi Kituo Cha Daladala au pale Ubungo Kimara Kuna abiria wengi sana, hawa wanakwenda Mbeya, Dodoma, Mwanza na kwingine, huu ni mfano tu lakini situation kama hio utaikuta Dodoma CBE, Singida pale Nje, Makambako, Mbeya, Moro, Mombo-Tanga, na kwingine.....

Hawa wote wana-risk maisha Yao, kwanini tusiukubali ukweli kuwa route za usiku haziepukiki? Tuhalalishe hizi safari tupunguze ajali za magari ya IT na zile za magazeti, mfano, ndani ya miezi 36 MAGARI ya magazeti yameondoka na maisha ya watu wasiopungua Kumi, coaster za Usiku zimeondoka na maisha mengi the same to IT na Malori. Tukihalalisha tutapunguza tatizo
 
Usalama wa barabarani iwepo mda wote, 24 hours. Kuna madereva wengine kutumia hii kama nafasi ya kumaliza dashboard ya basi. (120km/h). Matokeo:
Overspeeding.
Ajali
Drinking & Driving.
Trafgic wawepo mda wote na huduma zingenevyo ziwepo huko njiani. Mfano, sehemu za chakula, usalama wa abiria na mali zake. Ofisi za makamouni ya mabasi kuwa wazi, stendi iwe operational mda wote kutokana na mabasi kufika mda tofauti.
Pia, madereva wapate mda wakutosha kupumzika.

All in all, tusonge mbele!!
Upo nchi gani toka 2018 bus zote zina vts speed ni 85,kph
 
Juzi kati nilikuwa natoka maeneo ya kusini nilikuwa ktk speed ya 140KM/H Kuna busi lilinipita na likapotea kabisa machoni kwangu Ina maana yule Jamaa alikuwa katika 160KM/H au 170KM/H

Anyway usiku Kuna changamoto nyingi kama vile Maloli kuharibika njiani , wembamba wa barabara zetu na ukungu mida ya sa 10, 11 hadi sa 12
 
Kwa muda mrefu nilitaka kuandika hili la Sababu za "kitoto" za kuzuia magari yasisafiri usiku, hatimae Mbunge Tulia ameliona Hilo, tusubiri mamlaka zitekeleze. Mimi ni mdau wa safari za usiku sana, kwahio Wacha niwape experience....
1. Zile Coaster za Arusha zinazuiliwa pale Mkata wa saa Tano, matokeo yake, mkifika pale mnachangishana gari inaongeza wese mnazungukia Handeni, hii ni hatari.
2. Pale pale Mkata Kuna uchochoro, kwahio Dereva anazima Taa mnapita kwenye huo uchochoro kwenye makazi ya Watu, risk inazidi kuongezeka. Unajiuliza, hivi barabara ya Dar to Arusha Ina hatari Gani Hadi hizi gari zizuiliwe kama sio kutengeneza mazingira ya Rushwa tu?
3. Coaster za Dar to Mbeyaz wakifika Moro waliweka Picha ya Marehemu kuwa wanasafirisha msiba...tunajua kilichotokea, laiti ingekua ni route Hali.
4. Hivi kuna umuhimu Gani wa mabasi yote kuanza kufukuzana Pale stand kuu saa 12 asubuhi? Mfano, basi linalokwenda Kigoma, Kasulu, Musoma, n.k kwanini wasiondoke saa tatu asubuhi? Au saa Nne? Ili wasilale? Maana madereva ni wawili wawili, sasa watakimbizana kutwa nzima then watalala Kaliua saa nne usiku Hadi saa 12 asubuhi
5. Hivi kwanini Mabasi ya Bukoba, Ngara, Burundi, nk walazimishwe kulala Kahama na sio Nyakanazi? Siku hizi eneo lote liko salama.
6. Kwanini Mamlaka husika wasiruhu mabasi ambayo madereva wake na mabasi Yao yanatambulika kuliko hii ya kukata Kibali Cha Coaster Kila baada ya muda? Hatuna uhakika wa zile Coaster Wala madereva wake....

Inaendelea..
Safari za usiku zilikuwepo katika nchi yetu Tanzania.Nakumbuka miaka ya 1986 tulisafiri sana kutoka Dodoma KWENDA Dsm.Tuliondoka saa mbili usiku Dodoma na kufika Dsm saa kumi na mbili asub.Safari hizo zilizuiliwa Mwaka 1992 na wazir mkuu wa Wakati huo Dr John Samuel Malechela baada ya ajali mbaya ya basi ,ambalo silikumbuki na kuwaua watu wengi sana.Sababu ya ajali ilielezwa kuwa ni kutokana na dereva kushindwa kuona vizuri.Kwa upande wangu mm nafikiri mheshimiwa spika wa Bunge kabla hajashauri kuhusu hizo safari angeangalia emprical review .Yaan nn kilisababisha zikazuiliwa.Je hizo sababu bado zipo?Je ajali tu za mchana zimepungua?Mm naona sababu za ajali za usiku kwa Sasa ni nyingi sana kuliko Mwaka huo 1992.Kwa Sasa Kuna malori yanayofeli breki mengi sana barabarani.Tutegemea vifo vingi vya Watanzania.Kama mchana tu malori yanafeli breki,usiku ndio vifo vitakuwa vingi sana.
 
Back
Top Bottom