Kwahili la Mabasi kusafiri Usiku, nampongeza Mbunge Tulia Ackson

Kwahili la Mabasi kusafiri Usiku, nampongeza Mbunge Tulia Ackson

Kuna siku nilisafiri usiku kutoka mwanza kuelekea kishapu shinyanga aiseeh ile barabara ni nyembamba alafu malori yanawasha full na bado yanatanua kilichonisaidia ni zile sport lights nilifunga kwenye gari vinginevyo.......
 
Safari za usiku zilikuwepo katika nchi yetu Tanzania.Nakumbuka miaka ya 1986 tulisafiri sana kutoka Dodoma KWENDA Dsm.Tuliondoka saa mbili usiku Dodoma na kufika Dsm saa kumi na mbili asub.Safari hizo zilizuiliwa Mwaka 1992 na wazir mkuu wa Wakati huo Dr John Samuel Malechela baada ya ajali mbaya ya basi ,ambalo silikumbuki na kuwaua watu wengi sana.Sababu ya ajali ilielezwa kuwa ni kutokana na dereva kushindwa kuona vizuri.Kwa upande wangu mm nafikiri mheshimiwa spika wa Bunge kabla hajashauri kuhusu hizo safari angeangalia emprical review .Yaan nn kilisababisha zikazuiliwa.Je hizo sababu bado zipo?Je ajali tu za mchana zimepungua?Mm naona sababu za ajali za usiku kwa Sasa ni nyingi sana kuliko Mwaka huo 1992.Kwa Sasa Kuna malori yanayofeli breki mengi sana barabarani.Tutegemea vifo vingi vya Watanzania.Kama mchana tu malori yanafeli breki,usiku ndio vifo vitakuwa vingi sana.
Umesema vyema sana ila Kwa sasa 2022 na 1992 utakubaliana na Mimi kuwa Hali ni tofauti, sababu kubwa haikua barabara tu ila ni Ulinzi na usalama kutokana na mapori makubwa ila Kwa sasa, kwa mfano Kahama to Nyakanazi ya 1992 sio Kahama to Nyakanazi ya 2022, Eneo kubwa limejengwa na Eneo lote ni lami , sasa Kuna sababu Gani magari ya Bukoba kwa mfano, yalazimishwe kulala Kahama na sio Nyakanazi? Huu ni mfano.,..
Pia uhitaji wa abiria kusafiri Usiku umekua mkubwa sana, je tuwaache waendelee kudandia Malori na magari ambayo sio official kubebea abiria au tu-officialize?

Kumbuka, Kwa sasa, mabasi yapo yanayofika Dar asubuhi au Usiku wa manane kama Yale ya Kutoka Kigoma, Kasulu, Bukoba, Karagwe na Katavi, au Yale ya Mbeya to Mwanza, wanafika alfajiri, point Yangu ni kwamba hizi route ziruhusiwe, hazina madhara kama hayo makubwa kiasi hicho kikubwa madereva wawepo wawili kama wale wa Songea to Mwanza ambao hufika siku inayofuata......
 
Mwaka jana mwezi wa tatu, tarehe pendwa, 17.07.2021 nilipata bahati ya kusafiri kwenda Mafinga na basi la Majinja lililoanza safari ya kuelekea Mbeya saa 11 jioni pale Mbezi Magufuli. Hata ile breaking news niliipatia ndani ya basi.

Kipindi kile mabasi ya New Force na Majinja yalisafiri usiku kwa wiki moja kisha yakapigwa marufuku.

Tunataka safari za usiku zirudishwe kama miaka ya zamani
Ewaaaaaaa Majinja alikua anaanzia Lindi nadhani, Dar then Mbeya pia alikuepo Rungwe na Osaka au Chakito kama sijakosea, akaja Dar Express au Kilimanjaro wote hawa wamezuiliwa ila coaster zinaruhusiwa...sasa hizi ni akili au matope?!
 
Root ya usiku imekaa Poa…Japo kuna changamoto kwenye barabara zetu haziruhusu root hyo ifanyike kwa fasaha.

Changamoto nyengine ni mabasi na madereva.
Hakuna shida kwenye barabara, ni kuongeza tu madereva
 
Mbona mna maswali ya kipimbi sanaa? Hivi mnajua miaka ya 90 mabasi yalikuwa yakisafiri usiku? Ngorika, Lang'ata kutoka Arusha kuja Dar, tena barabara ilikuwa mbaya maeneo mengine. Pale Mbwewe tulikuwa kunapiga sana vyuku... Iringa, Mbeya kulikuwa na Zainabu bus, Scandinavia etc... Songea kulikuwa na Kiswere nk.. Yote yalikuwa yakipiga ruti za usiku. Sasa tunaenda mbele au tunarudi nyuma?? Hatuwezi kuingia uchumi wa juu ikiwa watu hawawezi kufanya kazi usiku, eti hakuna kusafiri usiku na asubuhi Bus zinapangiwa wote waanze saa 12 wakimbizane njia nzima, haya mambo ya kiwaki sana aisee daaah.
You nailed it Bro
 
Uchumi utachangamka saa 24.
Vituo vya mafuta watauza saa 24,wausau chakula watauza saa24.wenye mabasi watasafirisha abiria mara 2 zaidi.

Uchumi utakuwa angalau mara 2,mchana na usiku ni kuendelea kulijenga taifa.

Miji itasafishwa mchana na usiku.
Ajira itaongezeka mara 2, wenye viwanda watafanya kazi usiku na mchana.
 
Uchumi utachangamka saa 24.
Vituo vya mafuta watauza saa 24,wausau chakula watauza saa24.wenye mabasi watasafirisha abiria mara 2 zaidi.

Uchumi utakuwa angalau mara 2,mchana na usiku ni kuendelea kulijenga taifa.

Miji itasafishwa mchana na usiku.
Ajira itaongezeka mara 2, wenye viwanda watafanya kazi usiku na mchana.
Yes, hakika umeeleza vyema?
 
Ewaaaaaaa Majinja alikua anaanzia Lindi nadhani, Dar then Mbeya pia alikuepo Rungwe na Osaka au Chakito kama sijakosea, akaja Dar Express au Kilimanjaro wote hawa wamezuiliwa ila coaster zinaruhusiwa...sasa hizi ni akili au matope?!
Akili za polisi utaziweza? Sasa zikutane na za wanaccm wenye uchu wa madaraka na kupenda sifa wasizonazo wala wasizozistahilu, hapo unategemea nini?
 
Kwa muda mrefu nilitaka kuandika hili la Sababu za "kitoto" za kuzuia magari yasisafiri usiku, hatimae Mbunge Tulia ameliona Hilo, tusubiri mamlaka zitekeleze. Mimi ni mdau wa safari za usiku sana, kwahio Wacha niwape experience....
1. Zile Coaster za Arusha zinazuiliwa pale Mkata wa saa Tano, matokeo yake, mkifika pale mnachangishana gari inaongeza wese mnazungukia Handeni, hii ni hatari.
2. Pale pale Mkata Kuna uchochoro, kwahio Dereva anazima Taa mnapita kwenye huo uchochoro kwenye makazi ya Watu, risk inazidi kuongezeka. Unajiuliza, hivi barabara ya Dar to Arusha Ina hatari Gani Hadi hizi gari zizuiliwe kama sio kutengeneza mazingira ya Rushwa tu?
3. Coaster za Dar to Mbeyaz wakifika Moro waliweka Picha ya Marehemu kuwa wanasafirisha msiba...tunajua kilichotokea, laiti ingekua ni route Hali.
4. Hivi kuna umuhimu Gani wa mabasi yote kuanza kufukuzana Pale stand kuu saa 12 asubuhi? Mfano, basi linalokwenda Kigoma, Kasulu, Musoma, n.k kwanini wasiondoke saa tatu asubuhi? Au saa Nne? Ili wasilale? Maana madereva ni wawili wawili, sasa watakimbizana kutwa nzima then watalala Kaliua saa nne usiku Hadi saa 12 asubuhi
5. Hivi kwanini Mabasi ya Bukoba, Ngara, Burundi, nk walazimishwe kulala Kahama na sio Nyakanazi? Siku hizi eneo lote liko salama.
6. Kwanini Mamlaka husika wasiruhu mabasi ambayo madereva wake na mabasi Yao yanatambulika kuliko hii ya kukata Kibali Cha Coaster Kila baada ya muda? Hatuna uhakika wa zile Coaster Wala madereva wake....

Inaendelea..

Usafiri wa ndege ni bora sana sababu kubwa ni kuwa hauna vizingiti vya wapumbavu wote.
 
Nauli za ndege ziwe rafiki, serikali iruhusu ushindani wa ndege kwa mashirika mengi ya ndege kuja kuoperate Tanzania.

Treni ya Mwendokasi Dar-Dom-Mwanza/kigoma iharakishwe, reli ya kusini kuelekea Mbeya to Tunduma iboreshwe.

haya yote yakifanyiwa kazi idadi ya wasafiri kwenye mabus itapungua na wengi watakayoyatumia watakuwa hawana haraka hivyo maspeed na mambo ya hovyo barabarani yataondoka.

Usafiri wa barabara Km1000 na zaidi ni ujinga sana na ni risk sana na mpaka sasa unachukua sana roho za watu.
 
Kipindi Fast jet anakwenda Mwanza kwa bei bwerere abiria wa mabus kiasi fulani walipungua, tumeruhusu ATCL amemonopolize soko na kuufanya usafiri wa ndege ni anasa kwa mabei ya nauli ya ajabu..
 
Back
Top Bottom