Kwahili la Mabasi kusafiri Usiku, nampongeza Mbunge Tulia Ackson

Kwahili la Mabasi kusafiri Usiku, nampongeza Mbunge Tulia Ackson

Pia wanaotoka vijijini wanateseka sana, inabidi alale mjini ili kesho yake aweze kuwahi saa 12 Kwenda mikoani, wakati angeweza kuondoka kwake mchana jioni akapata Basi Kwenda mikoani
Bihashara ni muda. Uwezi kujifanyia bihashara Kwa kusikiliza ushauri wa masikini
 
Kipindi Fast jet anakwenda Mwanza kwa bei bwerere abiria wa mabus kiasi fulani walipungua, tumeruhusu ATCL amemonopolize soko na kuufanya usafiri wa ndege ni anasa kwa mabei ya nauli ya ajabu..
Idea nzuri sana sana
 
Hatari zipo nyingi

Ilishawahi kutokea saa sita usiku dereva akasinzia kwenye usukani gari iliacha njia
Mungu saidia ilikuwa tambarare
Nakubaliana na wewe.Nilikuwa nashangaa magari yanazuisa moro ikifika saa 6 usiku kwa yanayoenda Dar nikabaki najiuliza Dar Moro kuna hatari gani?
 
Mkuu kuna kitu ki1 kitafanyika.
Magari yataruhusiwa then kitaibuka kikundi cha utekaji kitaleta madhara kadhaa then sisi tutalalmikia safari za usiku.....mamlaka zitasitisha ma tutazipongeza sana.
Matukio yanaweza kuwa kweli au ya kutengenezwa
 
Wewe kichwa maji unataka kampuni za kenya zifanye biashara na midege yao mibovu?
Kipindi Fast jet anakwenda Mwanza kwa bei bwerere abiria wa mabus kiasi fulani walipungua, tumeruhusu ATCL amemonopolize soko na kuufanya usafiri wa ndege ni anasa kwa mabei ya nauli ya ajabu..
 
Mbona mna maswali ya kipimbi sanaa? Hivi mnajua miaka ya 90 mabasi yalikuwa yakisafiri usiku? Ngorika, Lang'ata kutoka Arusha kuja Dar, tena barabara ilikuwa mbaya maeneo mengine. Pale Mbwewe tulikuwa kunapiga sana vyuku... Iringa, Mbeya kulikuwa na Zainabu bus, Scandinavia etc... Songea kulikuwa na Kiswere nk.. Yote yalikuwa yakipiga ruti za usiku. Sasa tunaenda mbele au tunarudi nyuma?? Hatuwezi kuingia uchumi wa juu ikiwa watu hawawezi kufanya kazi usiku, eti hakuna kusafiri usiku na asubuhi Bus zinapangiwa wote waanze saa 12 wakimbizane njia nzima, haya mambo ya kiwaki sana aisee daaah.
Kabisa zamani barabara mbaya sana lakini magari yalikuwa safari za usiku. Mimi nadhani turudi kwenye zilezile sababu walizotoa kuzuia safari za usiku na tuziangalie je bado zina mashiko? kama hakuna basi kuwe na uhuru watu kupanga safari zao kwa mujibu wa matakwa yao na chagua la abiria. Nakumbuka wakati ule kulitokea ajali usiku basi wakaamka asubuhi marufuku kutembea usiku lakini kwani ajali ngapi zimetokea baada ya hapo, nyingi tu. Baya zaidi unasema mwisho saa 5 usiku sasa kuna tofauti gani saa moja usiku mpaka saa 5 na kuanzia saa 5 mpaka asubuhi? Mimi nadhani tuache mambo ya kucopy na kupaste mambo yamebadilika uchumi uko speed tuache biashara zifanywe kwa matakwa ya walaji wako watapenda usiku na wako watapenda mchana. Hili ni kama lile la kuzuia mirungi wakati haina shida yoyote ni starehe kama starehe zingine, unaacha pombe za kienyeji unazuia mirungi😛
 
Hili ni kama lile la kuzuia mirungi wakati haina shida yoyote ni starehe kama starehe zingine, unaacha pombe za kienyeji unazuia mirungi😛
Umeongea kwa uchungu saaaaaàana sana, I can feel it Brother
 
Mimi kwa Safari za usiku labda kwa sharti moja kubwa Tuu wanaondesha mabasi usiku lazima umri wao uwe kuazia miaka50 kwenda Juu ili Dreva awe na nidhamu kubwa usiku
Mkiwapatia awa madreva vijana kumbukeni hili ni muhimu sana
 
Safari za usiku zilikuwepo katika nchi yetu Tanzania.Nakumbuka miaka ya 1986 tulisafiri sana kutoka Dodoma KWENDA Dsm.Tuliondoka saa mbili usiku Dodoma na kufika Dsm saa kumi na mbili asub.Safari hizo zilizuiliwa Mwaka 1992 na wazir mkuu wa Wakati huo Dr John Samuel Malechela baada ya ajali mbaya ya basi ,ambalo silikumbuki na kuwaua watu wengi sana.Sababu ya ajali ilielezwa kuwa ni kutokana na dereva kushindwa kuona vizuri.Kwa upande wangu mm nafikiri mheshimiwa spika wa Bunge kabla hajashauri kuhusu hizo safari angeangalia emprical review .Yaan nn kilisababisha zikazuiliwa.Je hizo sababu bado zipo?Je ajali tu za mchana zimepungua?Mm naona sababu za ajali za usiku kwa Sasa ni nyingi sana kuliko Mwaka huo 1992.Kwa Sasa Kuna malori yanayofeli breki mengi sana barabarani.Tutegemea vifo vingi vya Watanzania.Kama mchana tu malori yanafeli breki,usiku ndio vifo vitakuwa vingi sana.

Kulikuwa na miundo mbinu kama ya sasa? Na je mchana hakuna ajali?
 
Mimi kwa Safari za usiku labda kwa sharti moja kubwa Tuu wanaondesha mabasi usiku lazima umri wao uwe kuazia miaka50 kwenda Juu ili Dreva awe na nidhamu kubwa usiku
Mkiwapatia awa madreva vijana kumbukeni hili ni muhimu sana
Miaka hio NDIO wanasinzia sasa Kwa taarifa Yako
 
Miaka hio NDIO wanasinzia sasa Kwa taarifa Yako
Acheni kufananisha miaka hiyo sasa kwa sasa vyombo vya usafiri vipi vingi sana
Malori ni mengi sana pengine karibu mara 1000 na yaliyokuwepo miaka ya 1990

Nasisitiza tuacheni Siasa kwenye hili lazima tuwe na mikakati muhimu

Mchana tuu basi linagongana na Lori uso kwa uso acheni hayo mambo
 
Matajiri wa Mabasi Yenye kujiekewa hawatapeleka mabasi yao usiku
 
Serikali iweke speed radar kwenye maeneo hatarishi, ukivuka unakutana na cheti chako. Uzuri speed radar za siku hizi hupiga picha pia. Hii itasababisha madereva na wenye vyombo kuwa makini
 
Nimapanda IT zaidi ya mara 10 ila sijaona hizo mbio ambazo watu husema.

Ajari saa zingine ni bahati mbaya
 
Nyie watoto! Mna nini? nchi yetu bado ni pori kwa asilimia 80 na maskini kunuka....sasa mkipata ajali huko porini tuta shindwa kuwa fikia kwa haraka mtakufa wengi nyau nyie!!.....

hayaa hata km tuta amua weka ambulances za dharula hela hizo hazipo!...Hospitali hazitoshelezi mahitaji ya huduma hizo kwanza hazina dawa, wataalamu hakuna woote wamekimbilia njei!

hata zikiwepo ambulances haya maskini nyie mna hela za kuwalipa hao wahudumu?? hapo bado hamjatekwa na maharamia wanyarwanda, wasomali njaa kali!

Hizo hotel zinazo wahudumia usiku zinahitaji ulinzi pia~ usalama barabarani usiku anahitaji ulinzi pia na over time zao! Risk allowance wanataka! askari gani atakaa porini huko bila usalama wake?

Hayaa!! tumewaambia kateni Bima za afya Bima za ajali hamtaki, mnaona sie wezi, sujui lkn mnataka kusafiri usiku ili mfe?? na nyoote mnao shabikia mkiumia mnapiga kelele km mitoto yatima

sie serikali hatutaki kuona mizoga yenu km mnataka kufa nendeni Somalia!! au tumbukieni baharini muwe chakula cha samaki baaasi...tumechoka sasa Mama weye chapa kazi hawa niachie mie!!........

Lazima sasa tuwaburuze tunavyoona ni sawa kenge nyie sababu uhuru una wazidi kimo sasa......kuumbe jiwe alikuwa sahihi!
 
Back
Top Bottom