Kwani mkiachana lazima muwe maadui?

Kwani mkiachana lazima muwe maadui?

Nafikiri umeongea kwasababu ya ubinafsi zaidi..yan unampaka nafuta kwa mgongo wa chupa

Hapana, hujaelewa maandishi niliyoandika....

Binafsi sipendi ugomvi kugombana kukwaruzana hata kubwatukiana sipendi....
Nimekukera niite niambie Kasinde umezingua na umenikera na umeniboa...
Nami ukizingua nakuita nakwambia kistaarabu umeharibu na nimechukia....

Napenda amani, hata kama nimechukia napenda kumaliza tofauti kwa amani, kisa cha alubati kimenifikirisha namna dunia ingekuwa wanaume wangeishi namna hiyo....

Kikubwa amani ya moyo, ikifika mahala mwanamke/mwanaume amekusaliti kama huwezi kukubali basi utulie uvumilie uwe bwegez uishi kibishi.

Ama laah unaanza upya unaendelea na maisha yako vile unapenda/unataka.

Simsifii mtu, nimeukubali utashi alioutumia, kuna mambo mengine hayahitaji nguvu, akili tuu mtu wangu.
 
View attachment 2627724

Muigizaji Vin Diesel aliachana na mpenzi wake wa miaka mitatu, lakini walipoachana, hakumtoa nje ya nyumba yake, aliogopa kwamba angeishi maisha ya chini, hivyo alimuachia nyumba yao na yeye akaenda kupanga nyumba nyingine.
Sio hivyo tu, aliendelea kulipia bili zote kwaajili yake na binti yao na alikataa kabisa chombo chochote cha habari kuingilia au kuchapisha chochote kuhusu kutengana kwao. Baada ya miaka 6 huyo ex wake alipata ajali na alihitaji kuongezewa damu. Vin Diesel aliwahi haraka hospitalini kwenda kumuongezea damu na alipopona wakarudiana!

𝗖𝗛𝗔 𝗞𝗨𝗝𝗜𝗙𝗨𝗡𝗭𝗔: Nadhani tunatakiwa kuishi pamoja kwa upendo na unyenyekevu Ila ikitokea tumetengana basi isiwe vita, upendo na heshima ubaki kati yetu bila kujali kitakachotokea!
Shetani, mbwa, chatu, cobra hawanaga urafiki wa damu hawq viumbe, haipogo nikipiga chini ndio basi imeisha hio
 
Hapana, hujaelewa maandishi niliyoandika....

Binafsi sipendi ugomzi kugombana kukwaruzana hata kubwatukiana sipendi....
Nimekukera nite niambie Kasinde umezingua na umenikera na umeniboa...
Nami ukizingua nakuita nakwambia kistaarabu umeharibu na nimechukia....

Napenda amani, hata kama nimechukia napenda kumaliza tofauti kwa amani, his cha alubati kimenifikirisha namna dunia ingekuwa wanaume wangeishi namna hiyo....

Kikubwa amani ya moyo, ikifika mahala mwanamke/mwanaume amekusaliti kama huwezi kukubali basi utulie uvumilie uwe bregenz uishi kibishi.

Ama laah unaanza upya unaendelea na maisha yako vile unapenda/unataka.

Simsifii mti, nimeukubali utashi alioutumia, kuna mambo mengine hayahitaji nguvi, akili tuu mtuwangu.
Wachache sana sana watu wa hivi, wakiwepo wanakuwa wamepata mentorship kubwa ama wazazi, Bibi , babu, na wachungaji, Mashehe, na experience.
 
Mimi pia mke wangu alihamishiwa Dodoma kikazi, akawa analiwa na bosi wa wizara! Nikagundua tukaachana,

Lakini nyumbani nilipobaki na watoto chumba cha wageni ndio kilikuwa chake akija kusalimia watoto.

Akapata kesi kikazi mimi nilimchomoa kwenye msala kupitia kwa mjomba wangu aliye na nafasi kwenye vyombo vya sheria.

Sikukuu ya pasaka alikuja nyumbani tukafurahi kama hakuna jambo baya kati yetu.
Watoto wanaona sawa tu hawajui kinachoendelea.

Hatulali pamoja na hatushiriki ngono,ni marafiki sana,akiwa ana shida najiotoa kusaidia,hivyo hivyo nikiwa na shida namcheki.

Tunataniana pia ikibidi.

Pamoja na yaliyotokea bado ndiye mwanamke bora kabisa kuwahi kuwa naye , namuheshimu na kumpenda pia.
Inawezekana sana kama jogoo hapandi mtungi. Ila kwahili linaloendelea kwenu ni swala la muda tu mtapigana miti na kurudiana.
 
Na wapo wa kurithi ni genetic kabisa anakuwa kama baba, mama, Bibi, babu hawa hadi raha hawahitaji training

Sanaa, mimi ni inborn mtu wa amani....
Kwenye ugomvi hunipati, hunishawishi, hunichonganishi...

Akili yangu tangu mdogo ilikuwa inawaza namna ya kuepa kugombezwa, kugomba, kupigwa, kupigana, kugombeza, kupiga etc.

Smiling Always 😊.
 
Ni huruka yao,akipata mahusiano nje au akiona alichokifata hakioni lazima vituko vifate Ni kupata akili ya kuishi nao vinginevyo watoto Ndo wanapata shida badae.Ndoa Ni tatizo kubwa kwa nchi zetu za Afrika.Wengi wnawakomoa Sana wanaume baada ya hamsini kwa hamsini kuwa fashion na Ndo inasababisha haya yote.
 
wenzetu hao mahusiano na ndoa ni suala binafsi tofauti na huku ni suala la ukoo. Ikitokea mmehitilafiana ktk ndoa si ajabu ndugu ndiyo wakawa wa kwanza kuchochea muachane. Ndugu wa mume watataka uachane na mkeo/mpenzi wako na ndugu wa mke watataka mali ziuzwe haraka mgawane. Kati yenu wawili mmoja lazima atawasikiliza ndugu na chuki itaanzia hapo.
Kwani ni kosa ndugu kuhusika. Kwa nini uliwahadithia ndugu kama haiwahusu?
 
Mimi pia mke wangu alihamishiwa Dodoma kikazi, akawa analiwa na bosi wa wizara! Nikagundua tukaachana,

Lakini nyumbani nilipobaki na watoto chumba cha wageni ndio kilikuwa chake akija kusalimia watoto.

Akapata kesi kikazi mimi nilimchomoa kwenye msala kupitia kwa mjomba wangu aliye na nafasi kwenye vyombo vya sheria.

Sikukuu ya pasaka alikuja nyumbani tukafurahi kama hakuna jambo baya kati yetu.
Watoto wanaona sawa tu hawajui kinachoendelea.

Hatulali pamoja na hatushiriki ngono,ni marafiki sana,akiwa ana shida najiotoa kusaidia,hivyo hivyo nikiwa na shida namcheki.

Tunataniana pia ikibidi.

Pamoja na yaliyotokea bado ndiye mwanamke bora kabisa kuwahi kuwa naye , namuheshimu na kumpenda pia.
Mnayafanya hayo kuwa kuwa mmoja wenu hajaoa au kuolewa, subiri vita ya tatu ya dunia inakuijia muda si mrefu ndo utajua mnaishi kama marafiki au mnaishi kinafiki, huwajui wanawake vizuri wewe!
 
Big up kwa Le mutuz
Yule big sitoacha kumpa maua yake

Hayo mambo yakienda kisheria utakuwa mtumwa wa mke ila kibongo bado japo ndipo tunaelekea

X sijawahi achana nae kushari kipolo lazima tu kipashwe
 
Kwani ni kosa ndugu kuhusika. Kwa nini uliwahadithia ndugu kama haiwahusu?
na kwa nini uwahadhithie ndugu masuala yako na mkeo, na kama utawahadithia kwa nini usiweke mpaka wasikuingilie wakapitiliza? Kwa sababu unapaswa kujua kuwa huyo mnayeachana naye kama mmeshakuwa na watoto, lazima maisha yenu yote utawasiliana naye kwa njia moja au nyingine na si ajabu mkizeeka watoto wanaweza wakawakusanya kuwatunza. baba ukakaa kwa mtoto mmoja mama kwa mwingine.

Na hata hatma ya watoto baada ya kuachana haitakuwa juu ya ndugu zenu, itakuwa juu yenu ninyi wawili. Ni lazima ujue kufunga milango ndugu wasiwavuruge zaidi.
 
Inategemea mmeachana vipi kuna namna mkiachana hamuwezi rudiana abadan kuna wanawake wana dharau sana.
 
wenzetu hao mahusiano na ndoa ni suala binafsi tofauti na huku ni suala la ukoo. Ikitokea mmehitilafiana ktk ndoa si ajabu ndugu ndiyo wakawa wa kwanza kuchochea muachane. Ndugu wa mume watataka uachane na mkeo/mpenzi wako na ndugu wa mke watataka mali ziuzwe haraka mgawane. Kati yenu wawili mmoja lazima atawasikiliza ndugu na chuki itaanzia hapo.
🤣🤣🤣🤣🤣
 
Historia....! Unakuta mtu pamoja na baya lake moja mbili au tatu...Ana mazuri mengi pia,dunia tutapita tu kwahiyo mambo mengine unachukulia poa tu maisha yanakwenda.
Very bold.
Kuna mtu anakutendea baya moja na linakuudhi au kukuweka chini, lakini deep inside ana mengi mazuri alikufanyia na kukuweka high up there . Ni bora kyangalua mengi mazuri kuliko baya moja no matter how huge is .
You win some loose some game na duniani tunakaa muda mfupi sana.
 
Back
Top Bottom