Kwanini asilimia 98 ya watanzania wanaojua Kingereza wanaongea Broken!! Tumerogwa au

Kwanini asilimia 98 ya watanzania wanaojua Kingereza wanaongea Broken!! Tumerogwa au

Kwa mazingira ya TZ Kiswahili lazima tu utaongea. Kwa hiyo mkazo uwekwe kwenye Kiingereza. Kiswahili kiwe somo tu. Medium of instruction kwa masomo yote yaliyobaki iwe Kiingereza. Ndivyo ilivyo Kenya, Uganda, Malawi... Wao wanaongea lugha zao na Kiingereza kwa ufasaha. Sisi tumeweka mkazo kwenye Kiswahili ambacho hata usipoenda shule utazungumza tu.
Hili ni tatizo la mitaala yetu Wala sio tatizo la wazungumzaji.

Tumechanganyikiwa , msingi tunasoma kwa kiswahili Kisha Sekondari Kiingereza.

Breakthrough (sijui kiswahili chake) ya lugha ni kati ya umri wa 1-10.

Na tuliowengi Kiingereza ni lugha yetu ya tatu. Na hili haliathriri uzungumzaji wetu tu. Linaenda mbali na kuathiri hata confidence yetu.

Tuamue moja, kutumia kiswahili au Kiingereza ngazi zote.
 
Tatizo letu tunasoma masomo ya Kiingereza kwa Kiswahili. Mwl wa Physics anafafanua kwa Kiswahili. Chuo Ma lecturer wengi Sasa nao wanaandaa PPT kwa Kiingereza lakini wanasoma na kufundisha kwa Kiswahili, hapo Kama nchi hatuwezi kufika. Imagine Profesa Kama mama Yetu wa Kasulu mjini anaongea Kiingereza chenye ugoko vile, vipi ndugu zangu waliopo maji uko na vidiploma vyao?
 
Kama mimi huku,nikiwa namsikiliza mtu akinisemesha namwelewa vizuri sana na kichwani nakuwa najua kabisa namna ya kumjibu ila sasa nikianza kufungua mdomo yote sijui ni yanakimbia au nisemeje maana hiyo broken yake ni ya kiwango cha lami,ila at least tunakielewa vibaya kama kinazungumzwa halafu hujui kinachosemwa.

Inavunja sana moyo but siyo lugha yetu so hatuna cha kupoteza (kujifariji tu)
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Nadhani badala ya kujikita kushadadia lugha tusiyoielewa (miaka zaidi ya 60 sasa tangu Uhuru), hebu tukuze lugha yetu ya Kiswahili. China, Urusi, nchi za Kiarabu na hata Ulaya wanajivunia lugha zao.
Mambo ya kukuza lugha ni ushamba, lugha huwa inakuwa yenyewe kwa sababu ya uhitaji na umuhimu wake katika muingiliano wa watu. Tunachotakiwa ni kuamua lugha moja ya kufundishia kuanzia darasa la kwanza hadi chuo kikuu.
 
Kuna shida Gani, Sasa hivi suala la kuongea Kingereza limezidi kuwa kubwa kadiri siku zinavyozidi kusogea, Sasa hivi yani watanzania wengi Wana elimu ya form four au six , Ila wengi hawajui Kingereza, na hao wachache wanaojitahidi au tumasema wanakijua asilimia kubwa zaidi ya 98 ukiwasikiliza wanaongea Broken English japo anaeleweka lakini broken c sana mfano waziri wa elimu Prof. ndalichako, hata lisu ana kizungu kizuri lakini anachapia akiongea muda mrefu, mama Samia anaupiga mwingi kwasababu anasoma, katika kusoma ni rahisi kuliko free style.
Wakenya wanafanyaje, na hizi aibu zetu tunaziweka wapi, sababu hata Mwalimu wa lugha Dr.Lwaitama anachapia Kingereza. Wanaosoma shule za English Medium ni wachache mno 0.0x , wengi ni mashule ya serikali ambapo hata walimu hawajui Kingereza, SoMo la English linafundishwa kwa kiswahili , yaani wanafundishwa Cha kujibia mtihani.

Ukienda You tube , Mtanzania akaongea Kingereza atapata comments mbaya sana, Kuna wakati Hadi wanasema lisu anawahUtubia mabeberu c watanzania.

Angalau Mkapa alikuwa anakipiga chenyewe
Hata baadhi ya waingereza huongea kiingereza kibovu.
 
KIKUBWA PUMZI BURE.
Kuna mchina,mjapan,mrusi n.k
Hyo NI lugha ya watu Kama unavyoona kimakonde,kimatumbi,kichaga n.k
 
Kama mimi huku,nikiwa namsikiliza mtu akinisemesha namwelewa vizuri sana na kichwani nakuwa najua kabisa namna ya kumjibu ila sasa nikianza kufungua mdomo yote sijui ni yanakimbia au nisemeje maana hiyo broken yake ni ya kiwango cha lami,ila at least tunakielewa vibaya kama kinazungumzwa halafu hujui kinachosemwa.

Inavunja sana moyo but siyo lugha yetu so hatuna cha kupoteza (kujifariji tu)
Ni kweli.mimi siwezi kuongea kiingereza.ila mtu hawezi kuniteta kiingereza nikashindwa kumuelewa.
 
Midahalo ya Kiingereza hakuna kabisa amashuleni. Sisi wakati tunasome kuanzia shule ya msingi hadi sekondari kulikuwa debate sessions kila wiki, ambapo watu wanajipanga makundi mawili na kuepwa topici ya kubishana kwa kiingereza. Ilikuwa inasaidia sana uwezo wa kujenga hoja kwa kiingereza. lakini sasa watu wengi hupanga hoja zao kwa kiswahili halafu ndipo waziongee kwa kuzitafsiri kiingereza. Inatakiwa hoja ipangwe moja kwa moja kwa kiingereza. Kwa Mfano paper hii ya "Dr." Biteko unaona kuwa mawazo yake yalipangwa kwa kiswahili, na alipoamishia mawazo yake katika kiingereza akaandika broken tupu. Na huyo ni Dokta yaani Ph.D. holder.

1639887125261.png
 
Midahalo ya Kiingereza hakuna kabisa amashuleni. Sisi wakati tunasome kuanzia shule ya msingi hadi sekondari kulikuwa debate sessions kila wiki, ambapo watu wanajipanga makundi mawili na kuepwa topici ya kubishana kwa kiingereza. Ilikuwa inasaidia sana uwezo wa kujenga hoja kwa kiingereza. lakini sasa watu wengi hupanga hoja zao kwa kiswahili halafu ndipo waziongee kwa kuzitafsiri kiingereza. Inatakiwa hoja ipangwe moja kwa moja kwa kiingereza. Kwa Mfano paper hii ya "Dr." Biteko unaona kuwa mawazo yake yalipangwa kwa kiswahili, na alipoamishia mawazo yake katika kiingereza akaandika broken tupu. Na huyo ni Dokta yaani Ph.D. holder.

View attachment 2049315
Samahani, unaweza kukorect Ili nasi tujifunze kitu Mana wengine tunaweza Ina Kama amepatia
 
Shule ya msingi masomo 5 yote kiswahili moja tu ndo kingereza, secondary masomo 9-12 yote kingereza 1 tu ndo kiswahili elimu ya Tz inacheza sarakasi za hatari sana mtu unamaliza had form4 lakin hujui unasoma ili uwe nani, na hata ukitaka kuwa nani utakuja kufanya kazi ambayo hukuiwaza, wengi wanafanya kazi ambazo ni nje ya ndoto zao
 
Kuna shida Gani, Sasa hivi suala la kuongea Kingereza limezidi kuwa kubwa kadiri siku zinavyozidi kusogea, Sasa hivi yani watanzania wengi Wana elimu ya form four au six , Ila wengi hawajui Kingereza, na hao wachache wanaojitahidi au tumasema wanakijua asilimia kubwa zaidi ya 98 ukiwasikiliza wanaongea Broken English japo anaeleweka lakini broken si sana mfano waziri wa elimu Prof. Ndalichako, hata Lissu ana kizungu kizuri lakini anachapia akiongea muda mrefu, mama Samia anaupiga mwingi kwasababu anasoma, katika kusoma ni rahisi kuliko free style.

Wakenya wanafanyaje, na hizi aibu zetu tunaziweka wapi, sababu hata Mwalimu wa lugha Dr. Lwaitama anachapia Kingereza.

Wanaosoma shule za English Medium ni wachache mno 0.0x , wengi ni mashule ya Serikali ambapo hata walimu hawajui Kingereza, Somo la English linafundishwa kwa kiswahili , yaani wanafundishwa cha kujibia mtihani.

Ukienda You tube , Mtanzania akaongea Kingereza atapata comments mbaya sana, Kuna wakati Hadi wanasema Lissu anawahutubia mabeberu siyo watanzania.

Angalau Mkapa alikuwa anakipiga chenyewe
Iwapo wanaongea broken ni dhahiri hawajui kiingereza
 
Inawezekana kabisa. Tukiweka mjadala wa kitaifa jibu litaptikana.

Suala la Lugha linatuvuta nyuma saana.
Mkuu kama mambo mepesi hatujafanikiwa, unadhani hili ndilo tutafanikiwa? Kama hafi ujenzi wa madarasa ni shida hadi kumaliza tu ufisadi bandarini tumeshindwa walau hata ukapungua mizigo ikatoka kwa wakati, hili la kukuza lugha ndo tutaweza?
 
Kuna shida Gani, Sasa hivi suala la kuongea Kingereza limezidi kuwa kubwa kadiri siku zinavyozidi kusogea, Sasa hivi yani watanzania wengi Wana elimu ya form four au six , Ila wengi hawajui Kingereza, na hao wachache wanaojitahidi au tumasema wanakijua asilimia kubwa zaidi ya 98 ukiwasikiliza wanaongea Broken English japo anaeleweka lakini broken si sana mfano waziri wa elimu Prof. Ndalichako, hata Lissu ana kizungu kizuri lakini anachapia akiongea muda mrefu, mama Samia anaupiga mwingi kwasababu anasoma, katika kusoma ni rahisi kuliko free style.

Wakenya wanafanyaje, na hizi aibu zetu tunaziweka wapi, sababu hata Mwalimu wa lugha Dr. Lwaitama anachapia Kingereza.

Wanaosoma shule za English Medium ni wachache mno 0.0x , wengi ni mashule ya Serikali ambapo hata walimu hawajui Kingereza, Somo la English linafundishwa kwa kiswahili , yaani wanafundishwa cha kujibia mtihani.

Ukienda You tube , Mtanzania akaongea Kingereza atapata comments mbaya sana, Kuna wakati Hadi wanasema Lissu anawahutubia mabeberu siyo watanzania.

Angalau Mkapa alikuwa anakipiga chenyewe
Nyie ndo mnasababisha broken isiishe,
Mna critique issue ndogo kwenye maongezi na mnaongeza uoga wa kuongea,
Watu wanakosea Kiswahili na hamuoni shida Ila mtu akikosea kingereza kwenye public speaking inakuwa nogwa.
Acheni hizo
 
Back
Top Bottom