Kwanini Baba wa Taifa Mwalimu J.K. Nyerere hakunyanyua kalamu kuandika maisha yake?

Shetani / Ibilisi kazini katika muendelezo wa kumchafua Mwalimu
Mzizi...
Ningeandika kitabu kwa nia ya kumchafua Mwalimu kitabu changu ningekiua mapema sana kisingeendelea kuwa hai hadi leo.

Kitabu cha Historia ya TANU kilichoandikwa na Chuo Cha CCM Kivukoni kwa kuwa kiliandikwa kwa nia ya kufuta historia ya kweli kimekufa hakisikiki wala hakionekani popote pale.

Ikiwa unaona nimeandika kitu chochote ambacho si kweli ila ni kumchafua Mwalimu kiweke hapa wasomaji wote washuhudie ukweli wako.

Nami ningependa kukuuliza swali.
Ulikuwa unaijua historia ya Abdul Sykes na Julius Nyerere?

Huoni kama kwa mimi kuiandika historia hii tumeiongeza elimu katika historia ya Mwalimu binafsi na historia ya TANU na harakati za kupigania uhuru?

Hujaipenda historia hii?
Je, ungependa tubakie na historia ya Kivukoni peke yake?

 
We mzee uache ujinga wakati mwingine, kwani wewe unaijiua historia ya Mwl Nyerere na baba yangu?

Walishawahi kuwa pamoja kabla ya uhuru na wakasaidiana mengi tu, tunaoijua wachache tu...lkn haitusumbui!
Mwl Nyerere alishafanya kazi na watu wengi tu na wengine walikuwa muhimu sana.

Any way twende kwenye point yangu, shetani yuko hivi...akija kwa mtu hajitambulishi kuwa yeye ni yule shetani mlaaniwa, anajifanya mwema na mleta habari njema. Mahala pengine alileta na dini, watu wakawa tayari kuuakuitetea dini hiyo kumbe wanamtetea shetani!
 
Eti usingekuwa hai hadi sasa!..
Ona ulivyojaa hila wewe mzee mwovu, hapo unawafundisha "ndugu zako" kuwa Nyerere aliua na anaendelea kuua wanao mkosoa.

Mbona wewe na ndugu zako mnamwita laana Mwl na hamfi?

Kufa utakufa tu siku moja siku yako itakapofika wala sio kwa kumkosoa Mwl
 
Aliacha historia ijiandike, maana alifanya mengi. Ila hawa wanaofosi kutuandikia story za maisha yao zilizorembwa, wanatuchanganya tu
 

Historia ya Tanganyika na kwa makusudi nataka nianze na hii kwa kuwa mimeitafiti na kuandika kitabu ambacho naamini sote tunakifahamu.

Umuhimu wa historia hii unasimama kwenye historia ya kudai uhuru chini ya TANU.

Chuo Cha CCM Kivukoni kilichapa kitabu cha historia ya TANU mwaka wa 1981.

Kitabu hiki kilichapwa baada ya Abubakar Ulotu kuandika historia ya TANU kutoka mswada ulioanza kuandikwa na Abdul Sykes na Dr. Wilbard Kleruu labda mwaka wa 1962.

Uandishi wa kitabu hiki uliingia katika matatizo na Abdul Sykes akajitoa kazi ikakamilishwa na Dr. Kleruu peke yake.

Tatizo katika utafiti huu lilikuwa kwanza nafasi ya baba yake Abdul, Mzee Kleist Sykes katika uasisi wa African Association mwaka wa 1929.

Tatizo jingine likawa nafasi ya Abdul Sykes katika TAA baada ya kifo cha baba yake mwaka wa 1949.

Halafu pakawa na tatizo la Julius Nyerere.
Nini mchango wake katika kuunda TANU?

Abdul alipojitoa katika uandishi wa historia hii ikawa kwa uamuzi ule umetoa fursa kwa waliobakia kuandika historia waliyoitaka wao.

Abdul Sykes akafutwa kwenye historia ya TANU na uhuru wa Tanganyika.

Mswada huu haukuchapwa na ukawa Maktaba ya TANU Mtaa wa Lumumba na hivi ndivyo ulivyoangukia mikononi kwa Abubakar Ulotu na yeye akachapa kitabu kwa jina lake.

Historia iliyoandikwa na Chuo Cha CCM Kivukoni haina tofauti na ile "aliyoandika," Abubakar Ulotu.

Miaka ikapita.

Mwaka wa 1998 mimi nikachapa kitabu cha maisha ya Abdul Sykes kitabu kilichoeleza historia ya TANU na harakati za kudai uhuru.

Kitabu hiki kilipindua historia ya TANU juu chini.

Kitabu kilimleta Abdul Sykes na Hamza Mwapachu kama chanzo cha kuundwa kwa TANU na harakati za uhuru.

Kadhalika kitabu katika hili kitabu kikamleta Chief David Kidaha Makwaia katika juhudi za kutafuta kiongozi wa kuongoza harakati za kudai uhuru.

Kuna watu hawakuridhika na kitabu hiki hasa kwa kuwa kilionyesha mchango mkubwa wa Waislam katika kupigania uhuru wa Tanganyika.

Watu hawa wakataka kiandikwe kitabu kuonyesha mchango wa Julius Nyerere katika kuunda TANU.

Kitabu hiki kipo sokoni hivi sasa.

Swali la kujiuliza ni hili.

Je kuna mapya ndani ya kitabu hiki ambayo yanabadilisha yaliyomo kwenye historia ya TANU iliyokwisha andikwa?

Tutegemee nini katika historia hii mpya inayotayarishwa hivi sasa?

Picha hiyo hapo chini ilipigwa siku TANU wanamsindikiza Julius Nyerere uwanja wa ndege safari ya kwanza UNO 1955.

 
Asichotaka kukubali huyu Mjahdina ni kuwa wazee wake walianzisha harakatti za Uhuru ,wakawa hawana Vision namna ya kusonga mbele!
Wakampata kijana smart ,wakaona wampe kijiti,Julius akaichuakua TAA na kuipeleka juu kileleni!
Tatizo Liko wapi,inakuuma Nini!
Mbona Nyerere na Historia inawatambua wale wote nchi mzima!
Hii kuimba Sykes ,mara Dosa ...kunaboa !
Historia inabeba Tanganyika na Wala Si mzizima!
 
Makulaga,
Kipi kinakughadhibisha kufikia kutoa matusi?
Kwani kuwa ''Mujahid,'' hakuruhusiwi?

Mbona tunao walokole nchini petu wengi tu?

Kuwa wazee wangu hawakuwa na ''vision,'' hii si kweli kwani wameunda African Association 1929 na Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika 1933.

Vyama vyote hivi vimepigania uhuru wa Tanganyika.

Hafla ya kumuaga Nyerere safari ya kwanza UNO 1955 ilifanyika katika jengo la Al Jamiatul Islamiyya.

Iko barua ya 1933 Mzee bin Sudi President wa AA akimwandikia Kleist Sykes kukumbusha umuhimu wa kuitoa Tanganyika katika mikono ya wakoloni.

Soma kitabu hiki: ''Modern Tanzanians,'' (1973) kimehaririwa na John Illife utakuta mengi usiyoyajua.

Ikiwa uko ''bored,'' na kalamu yangu dawa ni kutonisoma siyo kunitukana.
Lakini kuna wengi wanapendezewa na ninayoandika na wananisoma kila uchao.

Hujalazimishwa kuingia ukurusa huu.

 
Huyu mzee ni tapeli, kawashika sana akili ndugu zake waliozoea kugeuziwa uongo kuwa ukweli!
 
Kila mtu Aandike historia katika nchi hii nani Atasoma sasa!
 
Kila mtu Aandike historia katika nchi hii nani Atasoma sasa!
Kiok...
Haijawa kila mtu kuandika.

Historia ya uhuru wa Tanganyika imeandikwa na Judith Listowel (1965), John Iliffe (1968), Kimambo na Temu (1969), Abubakar Ulotu (1971), Chuo Cha CCM Kivukoni (1981), Mohamed Said (1998) na Shivji, Saida Othman na Ngwazi Kamata (2020).

Hawa hawajawa kila mtu kwani ni wachache sana.

Wasomaji wa vitabu ni maelfu ya watu.
 
Nyerere alikuwa mtu smart sana tofauti na yule hayati wa Chato ambae alikuwa ana mienendo yenye kuutia dosari udaktari wake
 
Huyu mzee ni tapeli, kawashika sana akili ndugu zake waliozoea kugeuziwa uongo kuwa ukweli!
Mzizi...
Kuwa mimi ni mwizi labda ni hasira ndizo zimekuzidi sasa huwezi tena kupima kauli zako unatokwa na matusi bila kujijua.

Mimi niko JF kwa miaka mingi sana na wengi wananifahamu.
Tulia akili zirejee mahali pake utanifahamu vyema.

Angalia picha hiyo hapo chini.
Naamini unamfahamu Bwana Mkubwa huyu.

Alikuja nyumbani kwangu kunikabidhi zawadi ya simu Infinix Note 10 na cheti nilichotunukiwa na JF kwa uandishi wa makala za historia.

 
Stories/myths zilizozaliwa, kukua na kukomaa ndizo zimeibua na kuangusha mataifa, falme na empires. Watawala wengi wanafahamu hilo ndio maana wanapatwa na hofu na kufanya kila njia kunyamazisha sauti za mawazo tofauti hata kama ni ndogo sana.
Nilijua tangu mwanzo ulikuwa unazunguka tu lakini nia yako ipo katika sentensi ya mwisho.

Mwl Nyerere kamwe hawezi kuhofia Mambo madogo madogo,Huyu ni jabali wa siasa za Afrika hawezi kuhofia wenyeji wa Tandamti na Msikiti wa Manyema.
 
Bi Kidawa utafanya uchafuzi tu hapa, hembu kaa kimya wenye busara wazungumze.
Nafsi ilikuwa inamsuta, sio muda. Kama alikuwa na muda wa kutafsiri ngano za Shakespeare asingeweza kuandika ukweli kuhusu yeye mwenyewe?
 
Alishirikiana na nani kuuondoa mfumo wa vyama vingi kwenye hii nchi mwaka 1967?
 
Sasa ilikuaje Mwalimu akawazidi wote aliowakuta mjini na waliomtangulia akawa nyota wa mchezo kitaifa na kimataifa!
Kubalini tu yule alikuwa mjanja kuwazidi wengi hadi watoto wa mjini.
 
Maelezo yako ni ngumi ya uzito wa heavyweight haswa ila hapo uliposema Mwalimu hakutaka kuweka na ilikuwa sahihi kutoweka mambo yote kwenye maandishi mezani ndipo umeharibu. Ni bora yote yangewekwa katika historia huru na ya wazi tu, yasingetugawa bali yangemulika mwanga mkubwa katika historia yetu.
US historia ya utumwa, ubaguzi na vita vya wenyewe kwa wenyewe imewekwa wazi hadi kwenye shule za msingi na imesaidia kusahihisha na kuliimarisha sana taifa hilo.
 
Sasa ilikuaje Mwalimu akawazidi wote aliowakuta mjini na waliomtangulia akawa nyota wa mchezo kitaifa na kimataifa!
Kubalini tu yule alikuwa mjanja kuwazidi wengi hadi watoto wa mjini.
Yoda,
Mwalimu hakuwa nyota peke yake ukiwa unakusudia kuwa mtu aliyeweza kuongoza harakati za kudai uhuru.

Wewe umemfahamu Mwalimu kwa sifa hiyo kwa kuwa hapakutolewa nafasi ya kueleza historia ya kweli ya harakati za kudai uhuru wa Tanganyika.

Ikawa kama vile ni mwiko kwa mtu kueleza historia nyingine yeyote ila hii ya Nyerere ya kuwa ni yeye pekee hakuna mwingine.

Wala halikuwa suala la kuwazidi wote.

TAA ilikuwa na watu hodari sana mfano wa Dr. Wilbard Mwnjisi, Dr. Michael Lugazia, Dr. Vedasto Kyaruzi aliyekuwa President wa TAA hata kabla ya Nyerere 1950.

Nafasi ya rais wa TAA kisha kuundwa TANU nafasi hii Abdul Sykes alimkusudia Chief David Kidaha Makwaia wa Siha.

Kisa hiki nimekieleza mara nyingi sana hapa barzani.

Hamza Mwapachu yeye aliona Nyerere anafaa zaidi kwa nafasi hiyo kuliko Chief Kidaha na tangiapo Chief Kidaha hakuonyesha nia ya kuitaka nafasi ile.

Mwapachu alitoa sababu zake za kumtaka Nyerere ashike nafasi ile.

Ni kisa kirefu kina mambo mengi lakini ikutoshe kuwa hata uchaguzi ulipofanyika mwaka wa 1953 kutafuta rais wa TAA kati ya Abdul Sykes na Nyerere, Mwalimu alishinda kwa kura chache na hivyo ile ''inner circle,'' kamati ya ndani ya TAA ilikubaliana Nyerere lazima ashinde uchaguzi ule TANU iundwe mwaka unaofuatia 1954 na Nyerere aongoze mapambano ya kudai uhuru wa Tanganyika.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…