Kwanini benki hakuna vyoo/maliwato kwa ajili ya wateja?

Kuna bank fulani choo kipo tena kinaonekana. Nilipokiona nikaingia nikamaliza mambo yangu nilipotoka mfanyakazi wa benki ananiambia hicho choo sio cha wateja ni cha wafanyakazi.

Nikamwambia nimeona alama ya choo tu sijaona katazo wateja tusitumie.

Siku yoyote nikizidiwa naingia humo.
 
Na wenyewe waache sasa kuwakalisha foleni wateja wao kwa masaa kibao, huku madirisha ya kutolea huduma yakiwa hayana wahudumu.
 
Yaani utoke utokako uje chooni upange mipango ya wizi!
Kwhy wewe uliyekuwa unakunya ulikuwa unapanga kuiibia bbenk?
Huna akili kabisa 😂
 
Vyoo vipo ila unamuomba afwande ndo uingie maana ni maalumu kwa stafu wa benki, hatahivyo vipo nje haviungani (vipo mbali) na majengo ya kutolea huduma za kifedha nadhani ni kwajili ya usalama...

Ukiuliza (ukitaka) vyoo vya umma benki eti kisa ni sehemu ya huduma kwa jamii basi utatakiwa kujiuliza pia vyoo vya umma mahakamani, shuleni, polisi, halmashauri, na kadhalika maana namo ni sehemu za huduma kwa jamii
 
Benki ni kwenda kuweka hela na sio makimba.
 
Wanatoa huduma za kifedha. Wamelenga kwa hicho wanachofanya.

Hii ni sawa na kuuliza kwana wanaotoa huduma ya CHOO CHA KULIPIA hawatoi mikopo wala kupokea amana.

Kinachokupeleka benk ni huduma ya fedha na sio choo yako. Ikikubana tafuta choo.

Mwisho mtauliza kwanini hawatoi chakula kwani wateja wanakaa zaidi ya saa 1.😂😂
 
Sababu za kiusalama
 
Sehemu zote ulizozitaja zina vyoo vya umma.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…