Songola
New Member
- May 20, 2022
- 4
- 1
Kila mbuzi anakula kulingana na urefu wa kamba yake........!Chadema wamesimama imara na misimamao Yao imewafanya waitwe ikulu Kwa heshima na siyo kwenda tu: lakini pamoja na nguvu waliyonayo kwanini wanavifanya vyama vingine kama siyo wapinzani? Akina Lipumba na Zito hata Mbatia wamepotelea Wapi kwenye ramani ya siasa?
Lakini pia kuitwa kwao ikulu kimkakati Toka Lisu akutane na Mhe. RAIS mbona kama kunawafanya akina Mdee waonekana kama wanadhalilika? Vyama vingine vitajikwamua vipi mikononi mwa CCM kama Chadema itaamua kusimana yenyewe kama inavyofanya Sasa?