Kwanini China nchi ya kidikteta ina maendeleo makubwa kuliko Kenya na Zambia?

Kwanini China nchi ya kidikteta ina maendeleo makubwa kuliko Kenya na Zambia?

Demokrasia inategemea kwa kiasi kikubwa factors 3 zifuatazo hili iweze kuleta positive impacts

1). Historia na asili ya watu wa jamii husika, kwa watu ambao wamezoea kutawaliwa kwa mtindo wa kifalme, mfano kama waarabu leo hii ukiwapelekea demokrasia hawawezi kuwa katika chain ile ile ya maendeleo, lazima watayumba.

2). Ufahamu/elimu na ethics, hili hiyo demokrasia yako iwe applicable kwa urahisi ni lazima watu wawe na ufahamu wa kutosha na pia vile vile watakaochaguliwa wawe na Nia ya dhati, Sasa kwa afrika hapa ni raia wangapi wanaojua demokrasia ni kitu gani? Na viongozi wangapi waadilifu tulionao?

3).Uchumi wa jamii husika, demokrasia Ina thrive kwenye jamii ambayo tayari wameshafika level Fulani hivi ya kiuchumi, yaani hawana Tena njaa, Sasa hapa kwetu kwanzia wapiga kura tu wenyewe Wana njaa kama nini wanajua kabisa kiongozi Fulani ni fisadi lakini wakihongwa hela ya chumvi tu wanaenda kumpigia kura huyo huyo.. Sasa hapo maendeleo yataletwa na hiyo demokrasia saa ngapi??

Kimsingi Demokrasia sio main indicator ya utawala Bora, na neno utawala Bora likoo too subjective.

Nachoona Wewe Bado umekalili terminologies za Civics ya Form Two na umekuwa nazo mpaka leo hii, hujataka kabisa hata ku-unlearn hili kupata uhalisia na undani wa hicho ulichofundishwa huko shuleni.
Sawa
 
Mkuu, nataka kuzamia China nipe mbinu.
Nenda Guangzhou kachukue mzigo wa kuja kuuza.

Nb: Sio rahisi kuzamia China tena kwa raia wa kiafrika ambao ambao hamna nchi iliyopakana na China kidogo wakorea huwa wanazamia japo nao wakinaswa wanarudishwa kwao.
 
Wachina hawajawahi kugundua miaka mingi kwamba demokrasia sio kichocheo cha maendeleo, China haijawahi kufikiria hata suala la demokrasia. Kwa miaka 2000 mpaka mwaka 1912 China ilikuwa inatawaliwa na Emperors, baada ya utawala wa emperors kuanguka ikaanza kutawaliwa kama jamuhuri chini ya mtawala wa kijeshi, mwaka 1959 Wakomunisti ndipo wakauipindua utawala uliokuwepo baada ya vita vya muda mrefu.

Pamoja na kutokuwa nchi ya kidemokrasia baada ya Mao China imekuwa ikibadilisha viongozi mara kwa mara na katiba yao waliweka ukomo wa miaka 10 japo ni chini ya chama kimoja. Maendeleo makubwa China iliyopata na kuweka msingi wa sasa wa uchumi ni wakati wa Deng Xiaoping. Huyu Xi amekuta uchumi wa China tayari unafanya vizuri sana akajijengea umaarufu halafu juu ya ule udikteta wa kichama akijitengenezea cult of personality. Viongozi waliomtangulia walikitanguliza mbele zaidi chama ndio maana hawakuwa maarufu kama yeye ila sio kwamba eti yeye ana miujiza kuliko wengine waliomtangulia.
Asante kwa kuweka marekebisho, kwa hiyo tunakubaliana kwamba hiyo demokrasia haiwezi kuwa main driving factor ya maendeleo tukitumia hii hii ya reference ya China?

Na pia kama Xi Hana maajabu ni nini kilimfanya mpaka wabunge wa chini karibu wote 2000 wakampigia kura ya ndio siku walivyokuwa wanaondo ukomo wa muhura na kumtaka awe raisi wa kudumu? Kwanini jambo kama Hilo wasingelifanya kwa mtu Kam Dieng Xioaping ambaye ndio anaaminika alikuwa genius kuliko hata watangulizi wake na alirekebisha makosa mengi yalioachwa na Mao na kisha kuja na mipango yake ambayo ndio imeifanya China kuwa hivi tunavyoiona leo?
 
China walipata bahati ya kumpata mzee mmoja anaitwa Deng Xiaoping. Huyo ndio chanzo HALISI cha mafanikio ya China. Hayo mengine ni mengineyo. Bila huyo mzee, China ingekuwa nchi maskini kama nchi zingine.


Kamgugo Deng Xiaoping
Huyo mzee ndio alisuka kila kitu China wanamuita the Architect of modern China. Marais Baada yake walifuata njia yake, alifuata Jiang Zemin akaboresha kisha akafuaya Hu Jintao na sasa hivi Xi Jinping.
Deng Xiaoping namfahamu japo bila hata Deng kuna watu wengi tu China wangeboresha mawazo ya Mao na kuleta mabadiliko.

Bila foundation ya Mao naye Deng asingeweza kufanikiwa katika mambo mengi sana.
 
Wachina wengi wanakimbilia kuishi na kuwa wakazi Marekani lakini ni nadra kukuta Mmarekani anaenda kuweka makazi ya kudumu China. Raia wengi wa Iran, Urusi, Uarabuni na Africa wanakimbilia Marekani na Ulaya.
Hii peke yake haitoshi kuwa sababu kwamba eti demokrasia ni Bora kuliko mifumo mingine ya kiutawala.

Hata Mimi ninaweza nikakwambia raia wa Qatar wanaishi maisha matamu sana kuliko wamarekani na hawajui hata hiyo demokrasia inafananaje.
 
Miaka ya 1950s mpaka 1970s mzee Mao alikuja na campaign maalimu ya GLF(Great Leap Forward) ambayo ililenga kuitrasnform China kutoka kwenye agrian economy na kuipeleka kwenye uchumi wa viwanda, campaign ambayo iligharimu mamilioni ya maisha wa wachina, watu walikufa sana na njaa na Mao alipata wapingaji wengi sana. Lakin wapingaji hao hawakuwa na nguvu sababu hapakuwepo na demokrasia ya kimagharibi.
GLF ilileta majanga China ni moja ya historia mbaya ya chama cha kikomunisti huwa hawapendi kuizungumzia sana
 
Asante kwa kuweka marekebisho, kwa hiyo tunakubaliana kwamba hiyo demokrasia haiwezi kuwa main driving factor ya maendeleo tukitumia hii hii ya reference ya China?

Na pia kama Xi Hana maajabu ni nini kilimfanya mpaka wabunge wa chini karibu wote 2000 wakampigia kura ya ndio siku walivyokuwa wanaondo ukomo wa muhura na kumtaka awe raisi wa kudumu? Kwanini jambo kama Hilo wasingelifanya kwa mtu Kam Dieng Xioaping ambaye ndio anaaminika alikuwa genius kuliko hata watangulizi wake na alirekebisha makosa mengi yalioachwa na Mao na kisha kuja na mipango yake ambayo ndio imeifanya China kuwa hivi tunavyoiona leo?
 
Kwa kipindi chote hicho hawakuendekeza siasa za kidemokrasia uchwara, ilikuwa ni mwendo wa KUPIGA kazi tu, muda wa kupigana majungu na kukosoana kukosoana kiholela mara sijui purukushani za uchaguzi haukuwepo, waliamini katika maono ya Mao Zedong na baadae kupokelewa kijiti na Dieng Xiaoping. Mpaka leo hii wamefika hapo waliopo ni vision na uwajibikaji na Wala sio siasa za demokrasia.
Upingwaji ulikuwepo hawa wakina Deng walikuwa na faction yao ilikuwa labelled capitalist roaders walishughulikiwa haswa
 
Nenda Guangzhou kachukue mzigo wa kuja kuuza.

Nb: Sio rahisi kuzamia China tena kwa raia wa kiafrika ambao ambao hamna nchi iliyopakana na China kidogo wakorea huwa wanazamia japo nao wakinaswa wanarudishwa kwao.

Sitaki kufanya uchuuzi. Kila mtu anachukua mizigo China kuja kuuza TZ in an already saturated market kwa watu wenye vipato finyu. GSM hadi mtu wa kawaida wote wanauza nguo toka China kweli! Me nataka nizamie huko niishi zangu freely kama mtu akizamia nchi za Magharibi bongo nirudi kuzikwa tu.
 
Kwa ufupi tu China waliligundua hili miaka mingi sana kuwa demokrasia sio kichocheo halisi Cha maendeleo hususani kwa taifa ambalo Bado linajitafuta.

Miaka ya 1950s mpaka 1970s mzee Mao alikuja na campaign maalimu ya GLF(Great Leap Forward) ambayo ililenga kuitrasnform China kutoka kwenye agrian economy na kuipeleka kwenye uchumi wa viwanda, campaign ambayo iligharimu mamilioni ya maisha wa wachina, watu walikufa sana na njaa na Mao alipata wapingaji wengi sana. Lakin wapingaji hao hawakuwa na nguvu sababu hapakuwepo na demokrasia ya kimagharibi.

Kwa kipindi chote hicho hawakuendekeza siasa za kidemokrasia uchwara, ilikuwa ni mwendo wa KUPIGA kazi tu, muda wa kupigana majungu na kukosoana kukosoana kiholela mara sijui purukushani za uchaguzi haukuwepo, waliamini katika maono ya Mao Zedong na baadae kupokelewa kijiti na Dieng Xiaoping. Mpaka leo hii wamefika hapo waliopo ni vision na uwajibikaji na Wala sio siasa za demokrasia.

Wachina hawaamini Kwenye utawala wa kubadilisha badilisha viongozi kuwa eti ndio chachu ya kupata maendeleo kwa haraka, wao wanaamini kwenye utawala Bora unaozingatia katiba ambayo inaweza ikamuwajibisha mtu yoyote pale anapoikiuka.

Na ndio maana leo hii wameamua kumfanya Xi Jinping kuwa raisi wa kudumu, sababu Wanaamini katika maono yake na pia hawana wasi wowote kuhusu yeye maana katiba yao ni Bora na ipo kwa ajili ya kulinda maslahi ya China.
China wana age limit na term limit kwenye positions mbalimbali suala kubadilishana madaraka wanalo.

Xi Jinping sio raisi wa kudumu walichofanya ni kuondoa term limits jambo la kawaida mataifa mengi wanafanya.
 
Asante kwa kuweka marekebisho, kwa hiyo tunakubaliana kwamba hiyo demokrasia haiwezi kuwa main driving factor ya maendeleo tukitumia hii hii ya reference ya China?

Na pia kama Xi Hana maajabu ni nini kilimfanya mpaka wabunge wa chini karibu wote 2000 wakampigia kura ya ndio siku walivyokuwa wanaondo ukomo wa muhura na kumtaka awe raisi wa kudumu? Kwanini jambo kama Hilo wasingelifanya kwa mtu Kam Dieng Xioaping ambaye ndio anaaminika alikuwa genius kuliko hata watangulizi wake na alirekebisha makosa mengi yalioachwa na Mao na kisha kuja na mipango yake ambayo ndio imeifanya China kuwa hivi tunavyoiona leo?
Deng Xiaoping hakuwa na nafasi yoyote kubwa ila alikuwa na nguvu ambayo Xi hana na sina hakika kama atakuwa nayo maana Deng hakuwa katibu wa chama cha kikomunisti wala Rais wa China
 
Upingwaji ulikuwepo hawa wakina Deng walikuwa na faction yao ilikuwa labelled capitalist roaders walishughulikiwa haswa
Kwa jinsi GLF ilivyoleta athari wapingaji hawakukosekana, lakini je walikuwa na impact yenye uzito kiasi gani? maana Mao haku retreat hata pale alipoona mamilioni kwa malioni ya watu wakipoteza maisha sababu ya njaa na kukosa makazi.....
 
Deng Xiaoping hakuwa na nafasi yoyote kubwa ila alikuwa na nguvu ambayo Xi hana na sina hakika kama atakuwa nayo maana Deng hakuwa katibu wa chama cha kikomunisti wala Rais wa China
Kwa mtindo wao wa uongozi wa China nafasi aliyokuwa nayo Dieng Xioaping (Paramount leader) ni sawa na raisi tu, kwani baada ya kuondoka kwa Mao yeye ndio alikuwa mbeba maono.

Naona mnanchukulia poa sana Xi ila wachina wanajua ni kwanini wameona yeye ndio anawafaa kuwaongoza kwa maisha yake yote hasa kwenye hizi nyakati ngumu ambapo Kuna battle kubwa sana ya kiuchumi kati yao na Marekani
 
Na pia kama Xi Hana maajabu ni nini kilimfanya mpaka wabunge wa chini karibu wote 2000 wakampigia kura ya ndio siku walivyokuwa wanaondo ukomo wa muhura na kumtaka awe raisi wa kudumu? Kwanini jambo kama Hilo wasingelifanya kwa mtu Kam Dieng Xioaping ambaye ndio anaaminika alikuwa genius kuliko hata watangulizi wake na alirekebisha makosa mengi yalioachwa na Mao na kisha kuja na mipango yake ambayo ndio imeifanya China kuwa hivi tunavyoiona leo?
Udikteta ndio uliofanya Xi abadilishe katiba kwa kupata kura za wajumbe wote wa mkutano mkuu/congress(bunge). Mbunge katika bunge la Marekani anaweza kumtukana hata Biden na asifanywe chochote , Elon Musk anamtukana Biden na chama chake Marekani mara nyingi bila kufanywa chochote. Hakuna Mbunge anaweza kumpinga Xi China bila mkakati mpana na wa muda mrefu. Jack Ma aliyekuwa bilionea namba 1 China alijaribu kukosoa kwa mbali tu CCP wakomunisti wakamchukua wakamficha kwa muda aliporudi akawa anaimba Xi anaupiga mwingi na utajiri wake wakautikisa sasa hivi amepoa na kunywea kabisa.

Deng Xioaping hakubadilisha kwa sababu hakutaka na wakati huo kulikuwa na watu watata sana katika siasa za China kuliko walivyo leo hii. Hata Deng kuyapata madaraka ya China na kuwa mtawala kamili ilikuwa mtiti sio wa kitoto na palichimbika haswa ndani ya chama cha CCP hadi kuwazidi wengine.
 
Kwa mtindo wao wa uongozi wa China nafasi aliyokuwa nayo Dieng Xioaping (Paramount leader) ni sawa na raisi tu, kwani baada ya kuondoka kwa Mao yeye ndio alikuwa mbeba maono.

Naona mnanchukulia poa sana Xi ila wachina wanajua ni kwanini wameona yeye ndio anawafaa kuwaongoza kwa maisha yake yote hasa kwenye hizi nyakati ngumu ambapo Kuna battle kubwa sana ya kiuchumi kati yao na Marekani
Hakujawahi kuwa na battle kubwa ya uchumi kati ya China na Marekani kama ilivyokuwa enzi za Cultural Revolution na Cold war.
 
Kwa jinsi GLF ilivyoleta athari wapingaji hawakukosekana, lakini je walikuwa na impact yenye uzito kiasi gani? maana Mao haku retreat hata pale alipoona mamilioni kwa malioni ya watu wakipoteza maisha sababu ya njaa na kukosa makazi.....
Impacts ilikuwepo Deng alipewa jukumu la kufanya policy reforms baada ya GLF kuleta madhara
 
Back
Top Bottom