Kwanini dhehebu la SDA huwa wanalishambiulia zaidi Kanisa Katoliki na siyo madhehebu mengine?

Kwanini dhehebu la SDA huwa wanalishambiulia zaidi Kanisa Katoliki na siyo madhehebu mengine?

Kaangalie amri kumi za Mungu zilizokwenge Biblia, kisha utakapoona Sabato basi ujue ndio hiyohiyo hakuna amri nyingine ya Sabato zaidi ya Ile iliyoandikwa kwenye amri kumi.

Kutimiza Torati hata wewe ukiifuata unatimiza, unafuata, unaifanya kama ilivyoagiza. Hiyo ndio maana yake.

Kumpendeza Mungu ni kufuata amri na sheria zake na sio vinginevyo. Yesu alichosema ni kuhusu upendo lakini kisheria na Torati upendo unatafsirika katika sheria. Za Mungu.

Sabato ni moja ya amri za Mungu ambazo haya huyo Yesu mnayemfuata aliifuata Kwa adabu na heshima Kwa sababu Mungu aliagiza iwe hivyo.
Fanyeni utafiti wa kutosha. Jiulize why alipoulizwa kuhusu dhambi ya uasherati yetu hakukazia hizo amri kumu badala yake akatoa kanuni kwamba mtu anayemtazama mwanamke na kumtaman amezini moyon mwake? Alipoulizwa ili umpendeze Mungu why hakuanza kuorodhesha hizo amri ba masheria badala yake akataja jambo moja tu yani upendo kwa Mungu na Jirani?

Yesu aliposema hayo kwa kunukuu torati alitaja amri ya msingi kabisa kwa wakristo bila kujali mahali alipo duniani. Mfano kama unampenda Mungu huwez kuzini au kama unampenda jirani(neno pana) huwezi kumsemea uwongo.

Nakuelewesha tena ukianza kuzifuatilia hizo amri kumi bado kulikua na vijiamri vidogo vidogo vingi vinaingia hapo kutia ndani hata vijiamri vya sabato. Ndomana nilimuuliza mwenzako mbona mnangangania sabato ya siku tu na si zingine? Kwa msingi huo unaposema yesu alikuja kutimiza kwa majibu yake ni kama yesu alikuja kuziboresha. Yan hizo amri na sheria zilikua msingi tu na zenye kasoro nyingi. Yesu akaja kuweka kila kitu sawa.

Ndio sababu kila siku unaambiwa moyo wa mtu wa upendo ndio jambo ambalo Mungu anataka na sio masheria ya waisrael ambayo walipewa ili wasijichanganye na mataifa ya kipagani kwa wakati huo.

Sasa tuulizane nyie wasabato ni waisraeli? Mbona kila kitu kilichowahusu hamkifuati mnatenga vingine? Waisraeli walikua na lengo pa kuikumbuka sabato na maandiko yanafunua kwamba ni ili kukumbuka mateso na jinsi Mungu alivyowaokoa wakiwa misri, je nyie mnaifuata sabato kwa lengo gani? mnaifuata sabato ya siku ya Mungu kupumzika au sabato ya siku ya kawaida?
 
Kaangalie amri kumi za Mungu zilizokwenge Biblia, kisha utakapoona Sabato basi ujue ndio hiyohiyo hakuna amri nyingine ya Sabato zaidi ya Ile iliyoandikwa kwenye amri kumi.

Kutimiza Torati hata wewe ukiifuata unatimiza, unafuata, unaifanya kama ilivyoagiza. Hiyo ndio maana yake.

Kumpendeza Mungu ni kufuata amri na sheria zake na sio vinginevyo. Yesu alichosema ni kuhusu upendo lakini kisheria na Torati upendo unatafsirika katika sheria. Za Mungu.

Sabato ni moja ya amri za Mungu ambazo haya huyo Yesu mnayemfuata aliifuata Kwa adabu na heshima Kwa sababu Mungu aliagiza iwe hivyo.
Mwisho hizo amri zote waisrael walipewa kutokana na agano ambalo Mungu alilifanya pamoja nao. Sasa soma Yeremia 31:31,32.... Inaonyesha Mungu anaanzisha agano jipya. Je unadhani hilo la zaman linalohalalisha hizo amri ambazo mnajitutumua kuzifuata bad liko hai? Je hilo agano jipya unalijua ni lipi? Na msingi wa agano jipya ni nani? Then malizia Soma wagalatia 4:8-11 na wakolosai 2:16,17

Nimeamua nikupe hili andiko moja tu ili tumalize mjadala mana nyie ni wabishi sana
 
Nimeona comment nyingi Sana mwisho wa siku WAKATORIKI wakawa wanashambuliana na WASABATO.

Ngojeni niwaambie kitu wote makosani kwa maana mmeiacha Ile neema na kukomaa na siku. Enyi wasabato mnafikiri nini siku ya sabato ndio itakayowaokoa? Vyakula kuviita najisi ndicho kitakachowakoa? Ama je amri kumi za Mungu ndizo zitakao waokoa? Nawaambia kweli la hasha tena hiyo sio Ile kweli. Je hamkusoma katika hiyo hiyo torati kwamba Kuna Ibada siku ya ya kwanza ya juma na ya Saba ya juma? Je! Hamkusoma ya kwamba hata Yesu walimshitaki eti kisa ameivunja sabato? Je hamkusoma hiyo. Basi ipo wapi wapi Sheria? Imefunikwa na kuondolewa na neema ya Kristo. hiyo ni kweli, hatupo tena chini ya torati,, unaona??! ilikua kwa Ajili ya Ile miaka 400. Je hamkusoma kwamba sasa hivi hatupo chini ya Sheria tena, Bali Tupo chini ya neema(zaidi ya Sheria) "mkikaa ndani yangu nami ndani yenu" hiyo ndio neema naam hiyo ni kweli AMEEN. Ludini kwenye biblia enyi wasabato biblia imesema kila kitu kiende kwa uzuri na kwa utaratibu wa Mungu hiyo neema imetokana na Neno la Kristo hiyo ni kweli,unaona?!! Utaratibu wa Mungu ni kwamba MWANAMKE ASIHUBIRI KANISANI HANA RUHUSA YA KUFUNDISHA CHOCHOTE. Je yupo wapi Ellen G white, ni mwanaume? Mpo nje ya mstari wa neema unaona? Je hamkusoma vyakula vyote vimetakaswa kwa neema? Je hamkusoma ya kwamba ya kwamba kwa sababu ya Ile neema mtu asiwahukumu kwa sababu ya chakula, vinywaji wala sabato? Je Imani yenu imetokana na nini basi, bila shaka na lile anguko maana mmevuka nje ya mstari wa neema kutaka kurudi kwenye Sheria. Ludini katika Neno la Mungu sasa. NAWAPENDA SANA.

WAKATORIKI NAO HIVYOHIVYO MIMI SITETEI UKATORIKI WALA USABATO MAANA yote ni madhehebu na madhehebu si ya Mungu kamwe, na hata mitume walinena vibaya juu ya madhehebu.
Enyi WAKATORIKI liludieni Neno la Mungu maana mmeliacha mbali mno tangu katika mtaguso wa Kwanza uliofanyika nikea kumekua na mafundisho mengi kutoka kwa Wana theologia je hamfahamu ya kwamba theology ni za ibirisi eti elimu kuhusu Mungu wapi hiyo ipo hayo ni mawazo ya watu ambao walitumwa na ibirisi Mungu Hana theologia Mungu ana Neno lake Tu! Yaani "BWANA ASEMA HIVI" hiyo ni kweli kwenye bible askofu lazima awe na mke hiyo ni kweli kwa askofu imempasa kua na mke. Mimi na wewe si lazima unaona, pia mwanamke haruhusiwi kufundisha hiyo ni kweli. Enyi wakatoriki kama nasema nje ya neno la Mungu itanibidi hukumu. Basi je mmeipata wapi mwanamke kufundisha kanisani? Mmeipata wapi mwanamke kumpa cheo katika jumuia, kigango,palokia Hadi jimbo? Mmeipata wapi kubatiza ubatizo wa tofauti na wa mitume? Alafu mnajiita WA mitume!! Mmelipata wapi la kumpigia goti mwanadamu mwenzako? Mmelipata wapi la kuwaomba wafu na malaika? Bila shaka ni kwenye theologia Kule nyuma kwenye mitaguso hiyo ni kweli mliyaingiza hayo na kutafuta mistali furani ya bible iwabariki.
ludini kwenye neno enyi watu kama kweli u na chembe ya Mungu moyoni mwako ludini kwenye neno. Msiteee UKATORIKI huu WA sasa WA ulimwengu tetea neno wewe kama wewe simama na Neno la Mungu Tu!
NAWAPENDA ndugu zangu .
 
Ndio hao SDA, muanzilishi wa hilo dhehebu ni demu mmoja wa Kimarekani anaitwa Hellen G White.

Ukijuwa tu muanzilishi wa dhehebu ni demu ndio unaweza kuwapuuza hapohapo.
hata mimi nimezaliwa na demu... Yesu pia kazaliwa na demu
 
...mimi naogopa jehanum kwakwel, pia namwogopa mungu, pia mimi ni mmojawapo...
 
Nitakujibu bila shaka Ila kwa kujirizisha kasome historia ya mtaguso mkuu wa Kwanza uliofanyika tarehe 20 mei 325- tarehe 25 julai 325.

Jibu:kabla ya mtaguso mkuu wa Kwanza uliofanyika tarehe 20 mei 325- tarehe 25 julai 325, huko nikea, lilikua kanisa Lakini baada ya huu mtaguso, kutokana na mambo waliokubaliana likawa dhehebu kwa sababu wameliacha Neno la MUNGU na kufuata kanuni zao wenyewe kama ilivyosema katika Marko 7:13. Na ilibidi itokee hili ili litimie neno la alilosema Mungu kwa ufunuo wa Yohana katika kitabu cha ufunuo wa Yohana sura ya 17.

Hili linathibitisha wazi kua wameliacha Neno la MUNGU na Roho mtakatifu kuondoka kabisa. Angalia Leo mambo yaliyokinyume na bible (askofu kutokuoa, mwanamke kuhubili,utatu mtakatifu,kuwaomba wafu, n.k)
Twende taratibu, huo mtaguso uliinda dhehebu jipya? Alafu Kanisa lenye likawa lipi?
 
Waislamu hawata kuja kuisahau the crusade war,walikoma kujitoa akili,hadi leo wanamuona papa kama Mungu,hata misikitini anaingia bila kuvua viatu[emoji28]
Sasa crusade nani alishinda!?..unamjua Saladin(salahuddin),Zena,mamluks!?..au huko kwenu vigangoni mnafundishana wimbo la pili tu la crusade ambalo wamagharibi walishinda!?..hawakufundishi kuhusu peter the hermit alivyobondwa na jeshi lake kwenye awamu ya kwanza!?..Leo Lebanon Kuna wakiristo 40% ambao ni masalia ya crusaders waliozingirwa bila kushambuliwa na Saladin,jifunze
 
Inasemekana katoriki ni mama wa machukizo ndani ya makanisa mengi, katoriki ndiye alibadilisha siku ya kumuabudu Allah, inafahamika katoriki siyo dini ni serikali inayotumia dini kujikweza na kujiimarisha kwa kuhadaa, katoriki ndiye kasemwa kwenye kitabu cha Ufunuo 17...

Yaani SDA ukimwambia juu ya RC ni sawa na Black tiger mwenye njaa na akamuona mamba mtoni.

SDA na RC hawawezi kukaa kwenye mimbari moja, yaani SDA anaweza kupasua hapo, ni vita kali [emoji1]!.
Katoliki na siyo katoriki
 
Twende taratibu, huo mtaguso uliinda dhehebu jipya? Alafu Kanisa lenye likawa lipi?
Unachanganya mada. Dhehebu NI kanisa lililoanguka. Hivyo baada ya katoliki KUINGIZA mapokeo ya kibinadamu tiyali ni dhehebu hilo.
 
Sasa crusade nani alishinda!?..unamjua Saladin(salahuddin),Zena,mamluks!?..au huko kwenu vigangoni mnafundishana wimbo la pili tu la crusade ambalo wamagharibi walishinda!?..hawakufundishi kuhusu peter the hermit alivyobondwa na jeshi lake kwenye awamu ya kwanza!?..Leo Lebanon Kuna wakiristo 40% ambao ni masalia ya crusaders waliozingirwa bila kushambuliwa na Saladin,jifunze

Itabaki historia kuwa waislamu wa puuzi walitandikwa hawatarudia tena kujitoa akili.
 
Itabaki historia kuwa waislamu wa puuzi walitandikwa hawatarudia tena kujitoa akili.
We unasema waislam,wakati hao crusaders walipofika Jerusalem waliua waislam, wakiristo na wayahudi,kabla ya kuja kubondwa na kufurushwa baadae
 
Kumbe ni dhehebu ambalo alilianzisha Mwanamke.
Mbona wao wanasema ndio dhehebu halisi toka wakati wa Yesu Kristo.
 
Ukitulia na kuisoma Bible ukiwa neutral, utagundua kuwa wasabato wapo sahihi kuliko dhehebu lolote lile duniani,
1: infact ulaji nguruwe ni kharam hata kibiblia,,eti wanadai "kimuingiacho mtu hakimtii unajisi bali kimtokacho"Kiuhalisia ukiisoma aya nzima pale yesu wala hakuwa akizungumzia ulaji wala nini ,alikuwa akizungumzia "maneno mabaya".
2:mamlaka ya papa kwenye biblia biblia,hivyo wapo sahihi kuipinga
3:mapadri-& masista hawajaandikwa popote pale kwenye biblia.
4:kuabudu siku ya kwanza ya juma " jumapili" hakujaandikwa popote pale kwenye biblia
5:katoliki haliongozwi na mwongozo wa biblia bali "amri za kanisa" na "katekisimu"....kwanini mtu aliyesoma biblia asipinge?
WASABATO WANATUMIA BIBLIA KUHOJI, HIVYO WAKATOLIKI HUWA HIYO LIGI WANAIKIMBIA ,HAWAYATAKI MAANDIKO YA BIBLIA AMBAYO PIA MARA MOJAMOJA NA WAO BIBLIA WANAITUMIA..

Mimi siyo msabato,bali muabudu mizimu ya mababu zangu,dini zenu hazinihusu kivile ila huwa nasoma biblia na Quran ili kujua mbivu na mbichi na kupanua ufahamu.
Wachina wanaokula nyoka, vyura, wadudu wao pia ni wazambi?

Toeni ujinga wenu humu.
 
Back
Top Bottom