Kwanini gharama za kutuma pesa kutoka Akaunti ya benki kwenda mtandao ya simu ni kubwa sana?

Kwanini gharama za kutuma pesa kutoka Akaunti ya benki kwenda mtandao ya simu ni kubwa sana?

Simbanking hasara sana kwa wateja wa banks, ila ni faida kubwa kwa mabenki. Serikali inatakiwa itoe masharti kwa gharama rasmi za fedha za Simbanking..!!

Banks nyingi zinawanyonya sana wateja wao kwa Simbanking, hasa CRDB, NMB… Ingetakiwa Simbanking gharama zake ziwe ndogo kuliko hata gharama za kwenda bank kutoa fedha au iwe sawa na gharama za ATM au chini..!!

Mimi nailaumu Serikali kwa hili, hasa wizara ya fedha, ingethibiti hili, gharama za Simbanking ni kubwa sana bila sbb yoyote
 
Huduma nilizoacha kutumia
1. Kutoa fedha zilizoko kwenye account ya bank kwa wakala
2. Kutumia apps mbali mbali za fedha kwenye simu
3. Kutuma ama kutoa fedha kwenye account ya bank kwa njia ya simu

Waweza ona imerahisha huduma bali ni garama sanaa
 
Hili suala limekaaje kitaalamu, mfano benki kama NMB ukitaka kutuma pesa kwa mtu kutoka kwenye Akaunti ya benki kwenda kwa namba yake ya simu Cha mtema Kuni utakiona. Je hii ni sawa wakuu? Kwanza gharama za makato hazionekani kabla ya kutuma pesa, ila utakutana nazo tu ukishatuma tayari. Hii si sawa benki kama taasisi muhimu za kiuchumi zijaribu kuwa wawazi katika mchakato mzima wa utumiaji wa huduma zao kwa njia ya simu.
Una compare na nini? Kubwa zaidi ya nini ? Ngapi ulitaka iwe ndio uone fair ?
 
Hili suala limekaaje kitaalamu, mfano benki kama NMB ukitaka kutuma pesa kwa mtu kutoka kwenye Akaunti ya benki kwenda kwa namba yake ya simu Cha mtema Kuni utakiona. Je hii ni sawa wakuu? Kwanza gharama za makato hazionekani kabla ya kutuma pesa, ila utakutana nazo tu ukishatuma tayari. Hii si sawa benki kama taasisi muhimu za kiuchumi zijaribu kuwa wawazi katika mchakato mzima wa utumiaji wa huduma zao kwa njia ya simu.
weka takwimu uzi unoge!
 
TAFUTENI FEDHA MAZEE na mtumie muda wenu vizuri kwenye mambo yenye tija na ya maana, hivi mmejaribu kutafakari kuhusu muda na usumbufu ulipo wakati unahangaika kukaa kwenye foleni kufanya miamala ukiwa benki?
 
Back
Top Bottom