Kwanini historia ya Zanzibar ya kweli haisomeshwi?

Kwanini historia ya Zanzibar ya kweli haisomeshwi?

Kuna vitu viwili unachanganya. Utumwa na uchaguzi

Utumwa ni uharamaia uliofanywa na Wazungu na Waarabu dhidi ya Waafrika

Huo hauna utetezi wa aina yoyote kwa wanaofikiria vema. Hakuna ushenzi mzuri

Tatizo lako Mohamed, unadhani kulaani Waarabu ni kulaani Uislam.

Hujui tofauti ya vitu hivyo. Uarabu ni asili au unasaba au kabila

Uislam ni imani ya dini ambayo imekuja kupitia kwa Waarabu.

Waliotenda udhalim wa utumwa ni Waarabu ambao wali practice Uislam.

Siyo Uislam uliosababisha biashara ya utumwa. Tofautisha hapo

Hivyo Sultani alitenda kama Mwarabu na kama alitumia Uislam basi ni kwa manufaa yake lakini hilo halikuwa takwa la Uislam kama dini.

Kuhusu chaguzi, matokeo ya chaguzi yanakwazwa na Wazanzibar wenyewe.

Laiti wangekuwa na msimamo mmoja kama Umma, hakuna kitu kingewakwamisha

Nimekuuliza, unajua maana ya ''machotara'' warudi kwao?
Unajua kipili pili cha kichwani na Mkuranga na Morogoro?

Kisa cha Salim Ahmed, kaa kimya Mohamed huko usiende kabisa, wewe elekea Kipumbwi

Hizi siasa za Kitaifa na Kimataifa tafadhali jieupushe nazo, endelea na Kipumbwi

Ni hivi Mpinduzi Daima na Zanzibar ya Sultani yamebaki kuwa makovu makubwa ya siasa za Zanzibar na wala hayapona katika miaka ya karibuni.

Mateso ya kusimama katika milango kusbiri leftover za Biriani walioshuhudia hayo wapo hai
mkuu nguruvi nakukubali unachambua vizuri .
 
Lusungo,
Umewashutumu Waarabu.
Vipi kuhusu Wazungu?

Unayo elimu ya Transatlantic Slave Trade?
lusungo hakuwastumu Waarabu, ameeleza kilichotokea
Wazungu walifanya TansAtlantic trade kwa kutumia Wamishenari

Hilo halihalalishi unyama wa Waarabu hata kidogo.
Katika mijadala kuna maneno si mazuri kuyatumia, lakini biashara ya utumwa haielezeki kwa lugha nyingine zaidi ya Ushenzi. Uwe wa Askofu au Sheikh ni ushenzi tu.

Kwa taarifa yako Mohamed, biashara ya utumwa kupitia bahari ya Hindi ilituathiri sana kuliko TransAtlantic, ni haki tukiijadili kwani wahanga ni ndugu zetu wa Damu si Sultan na nduguze

Huko nyuma ukijadiliana na Wickama umekubali uwepo wa soko la watu na biashara hiyo
Unaposema Sultan mikono yake haina damu ni kuudhalilisha utu

Yaani unataka watu waelewe kuwa kuuawa kwa vipigo ni kubaya zaidi kuliko kuuawa katika utumwa. Mwisho wa siku waliofanya unyama huo hawana afadhali

Si kweli, mikono ya Sultan imetapakaa damu ya watu wa Afrika na hasa Afrika Mashariki
 
Naunga mkono hoja, tena ni afadhali humu jf anafanya kuandika tuu, hivyo there is a room ya kumkosoa anapoleta maurongo humu, lakini anapokaribishwa kwenye redio zao, urongo wake huenea bila room ya critics, wasikilizaji wake wanameza mazima maxima, hivyo nimeishawahi kutoa angalizo hili kumhusu mtu huyuP
Mfano upo katika uzi huu.
Rudi nyuma uangalie ''clip' ya mahaojiano ya TV moja Zanzibar

Yule mtangazaji mwanamke anawaambia Watazamaji amealika mgeni kueleza historia ya mapinduzi ya Zanzibar wakati ''inapata uhuru'' Jan 12 964

Mtangazaji asiyejua Zanzibar ilikuwa huru 1963 na mapinduzi ni 1964, mtu huyo anawezaje kumhoji MS? Kinachobaki ni MS kumwaga sera zake bila kufanyiwa tathmini.

Japa JF, mmh-mh! tutaangalia kila neno na herufi halafu tutasema

Kaingia mitini!
 
Mfano upo katika uzi huu.
Rudi nyuma uangalie ''clip' ya mahaojiano ya TV moja Zanzibar

Yule mtangazaji mwanamke anawaambia Watazamaji amealika mgeni kueleza historia ya mapinduzi ya Zanzibar wakati ''inapata uhuru'' Jan 12 964

Mtangazaji asiyejua Zanzibar ilikuwa huru 1963 na mapinduzi ni 1964, mtu huyo anawezaje kumhoji MS? Kinachobaki ni MS kumwaga sera zake bila kufanyiwa tathmini.

Japa JF, mmh-mh! tutaangalia kila neno na herufi halafu tutasema

Kaingia mitini!
Nguruvi3,
Nimkimbie nani ndugu yangu hapa?
Nipo.

Nimeingia Maktaba na nimekuletea hayo hapo chini:

1575147681225.png

Faraja Sendegea akifanya mahojiano na Mohamed Said​
Ingia hapa kusikiliza kipande cha mahojiano:
http://www.mohammedsaid.com/2016/01/kumbukumbu-ya-mapinduzi-zanzibar-azam.html

''Leo asubuhi nilifanyiwa mahojiano na mtangazaji Faraja Sindegea wa Azam TV kuhusu Mapinduzi ya Zanzibar.

Mtangazaji alifungua kipindi kwa utangulizi kuhusu historia ya mapinduzi na umuhimu wa kuyaenzi mapinduzi.

Nilimtaka radhi kwa kumwambia kuwa itafaa kama tutayazungumza mapinduzi kutoka kumbukumbu ya mashujaa waliopigania uhuru wa Zanzibar lakini michango yao haitambuliwa na nchi yetu.

Nilikwenda moja kwa moja kwenye kumbukumbu za Aman Thani kueleza yale ambayo si wengi wanayafahamu.

Watazamaji nadhani kwa mara ya kwanza waliona picha ya Aman Thani kwenye televiseheni zao na picha ndiyo hiyo hapo juu.

Nilieleza kuwa nimezisoma kumbukumbu za Aman Thani na niligusia umuhimu wa nyaraka zake kwa mwanafunzi yoyote yule anaejifunza historia ya siasa za Afrika hususan historia ya Zanzibar na mapinduzi yaliyokuja kutokea mwaka wa 1964.

Nimesema kuwa kumbukumbu za Aman Thani zinakuja na picha nyingine kabisa ya mapinduzi ambayo si wengi wanaijua.

Nilieleza kuwa ni Aman Thani peke yake katika wafungwa wa siasa wa Zanzibar aliyeweza kueleza kwa kirefu kuhusu Jela za Mateso zilizoundwa baada ya mapinduzi na jinsi alivokabiliana na Mtesaji Mkuu Hassan Mandera.

Niliwaonyesha watazamaji baadhi ya vitabu muhimu vya historia ya Zanzibar pamoja na kitabu, ''Masimulizi ya Sheikh Thabit Kombo Jecha,'' kitabu ambacho nilisema mwandishi Minael- Hosanna O. Mdundo amepotosha mambo mengi.

Mtangazaji Faraja alitaka kujua John Okello ni nani.

Nilimweleza kuwa John Okello hakuwa chochote katika mapinduzi ila alitumiwa kutoa matangazo ya kuwatisha wananchi.

Kwa lugha ya wenye mapinduzi yao ni kuwa, ''Walimvisha blanketi la U-Field Marshall na likamwenea na yeye mwenyewe akaamini khasa kuwa hakika ni ''Field Marshall,''

Hapa kuhusu, ''Blanketi la Okello,'' niliwapeleka watazamaji wangu kwenye rejea ya kitabu cha Dr. Harith Ghassany, ''Kwaheri Ukoloni Kwaheri Uhuru.''

Nilimtaja Abdallah Kassim Hanga kuwa ndiye aliyepanga mapinduzi.

Katika muktadha huu niliwarejesha tena watazamaji kwenya kumbukumbu za Aman Thani aliposema kuwa hayakuwa ''mapinduzi,'' bali mavamizi.

Aman Thani nikaeleza kuwa ametoa changamoto katika picha maarufu ya Okello hapo juu kuwa atokee mtu awaonyeshe Wazanzibari khalis katika picha ile.''

 
lusungo hakuwastumu Waarabu, ameeleza kilichotokea
Wazungu walifanya TansAtlantic trade kwa kutumia Wamishenari

Hilo halihalalishi unyama wa Waarabu hata kidogo.
Katika mijadala kuna maneno si mazuri kuyatumia, lakini biashara ya utumwa haielezeki kwa lugha nyingine zaidi ya Ushenzi. Uwe wa Askofu au Sheikh ni ushenzi tu.

Kwa taarifa yako Mohamed, biashara ya utumwa kupitia bahari ya Hindi ilituathiri sana kuliko TransAtlantic, ni haki tukiijadili kwani wahanga ni ndugu zetu wa Damu si Sultan na nduguze

Huko nyuma ukijadiliana na Wickama umekubali uwepo wa soko la watu na biashara hiyo
Unaposema Sultan mikono yake haina damu ni kuudhalilisha utu

Yaani unataka watu waelewe kuwa kuuawa kwa vipigo ni kubaya zaidi kuliko kuuawa katika utumwa. Mwisho wa siku waliofanya unyama huo hawana afadhali

Si kweli, mikono ya Sultan imetapakaa damu ya watu wa Afrika na hasa Afrika Mashariki
Nguruvi3,
Umeeleza yako nami nimeeleza yangu.

Yako yalitawala kwa miaka lakini nashukuru kuwa nami nimepata fursa ya kueleza yangu katika miaka hii ya karibuni.
 
"Mohamed Said, post: 33635045, member: 12431"]
Nguruvi3,Umeeleza yako nami nimeeleza yangu.
Hapana sijaeleza yangu. Picha za watumwa zimewekwa hapo. Sasa wasomaji wanataka kujua hizo zilikuwa propaganda kama Mohamed Said anavyodai?
Yako yalitawala kwa miaka lakini nashukuru kuwa nami nimepata fursa ya kueleza yangu katika miaka hii ya karibuni.
Sina nilichoandika kuhusu mapinduzi. Haya yako uliyoandika yana upotoshaji uliokithiri tukiyaita Ngano

Ndiyo maana tunakuuliza tena na tena, je, picha za watumwa wakiwa na minyororo ni propaganda? Je, Sultan alikuwa na mikono safi isiyo na damu ya wamatumbi?
 
Pascal Mayalla unakumbuka kuna mahali umesema mzee akibanwa hutumbukiza mambo mengine kuwavuruga watu!!

Ndicho kinachoendelea. Tunaongelea Mapinduzi na utumwa tayari kaingiza Aman Thani na jela za mateso baada na si kabla ya mapinduzi

Hata hivyo tutakwenda naye sambamba tulitendea jukwaa hili haki.

Ni jukwaa lililoachwa bila 'care' kwa muda kiasi kwamba limegeuka eneo la upotoshaji wa makusudi. Tumepiga kambi

Kuna jingine limejitokeza bandiko#125.

Mohamed anadai aliasisi na kupanga mapinduzi ni Abdallah Kassim Hanga.
Naomba hili liwe katika kumbukumbu bila kulinukuu kama lilivyo

Pili, kasema Okello si lolote si chochote latika mapinduzi ya Zanzibar
Nalo tunaomba liwe katika kumbu kumbu

Tatu, MS kadai alikuwa anamfahamu A.K.Hanga na Wazazi wake walikuwa maswahiba
Hili naomba liwekwe katika kumbu kumbu

Nne, kuna picha ya Okello na wenzake.
Mohamed anasema kama kuna Mzanzibar halisi attajwe
a) MS hajatueleza picha hiyo ilipigwa wapi na lini
b) MS akumbuke Okello ameishi katika nchi tatu na kila alipotua lilizuka la kuzuka

Haya tunaomba yawe katika kumbu kumbu kwasababu mjadala unaendelea na tutayatumia

JokaKuu Mag3
 
Biashara Ya Watumwa Ya Afrika Ya Mashariki
Bwana Alpers anahitimisha, “lazima iwe wazi sasa kwamba wengi wa watumwa walikamatwa na wafanya biashara wanyang’anyi wa Kiarabu
Wakiongozwa na Hamad bin Muhammad bin Juma bin Rajab el Murjebi, kwa jina maarufu la
Tippu Tip, or Tippu Tib
Tippu_Tip_(Muhammed_el_Murjebi_also_Hemed_bin_Mohammed).jpg


Madhila waliotufanyia watu hawa, nimeyaeleza napa


p
 
Pascal Mayalla unakumbuka kuna mahali umesema mzee akibanwa hutumbukiza mambo mengine kuwavuruga watu!!

Ndicho kinachoendelea. Tunaongelea Mapinduzi na utumwa tayari kaingiza Aman Thani na jela za mateso baada na si kabla ya mapinduzi

Hata hivyo tutakwenda naye sambamba tulitendea jukwaa hili haki.

Ni jukwaa lililoachwa bila 'care' kwa muda kiasi kwamba limegeuka eneo la upotoshaji wa makusudi. Tumepiga kambi

Kuna jingine limejitokeza bandiko#125.

Mohamed anadai aliasisi na kupanga mapinduzi ni Abdallah Kassim Hanga.
Naomba hili liwe katika kumbukumbu bila kulinukuu kama lilivyo

Pili, kasema Okello si lolote si chochote latika mapinduzi ya Zanzibar
Nalo tunaomba liwe katika kumbu kumbu

Tatu, MS kadai alikuwa anamfahamu A.K.Hanga na Wazazi wake walikuwa maswahiba
Hili naomba liwekwe katika kumbu kumbu

Nne, kuna picha ya Okello na wenzake.
Mohamed anasema kama kuna Mzanzibar halisi attajwe
a) MS hajatueleza picha hiyo ilipigwa wapi na lini
b) MS akumbuke Okello ameishi katika nchi tatu na kila alipotua lilizuka la kuzuka

Haya tunaomba yawe katika kumbu kumbu kwasababu mjadala unaendelea na tutayatumia

JokaKuu Mag3
Mkuu Nguruvi3, Mkuu Maalim Mohammed Said ni very controversial kwenye baadhi ya hoja zake, na kila akileta any controversial issue, ukihoji, kwake ni kama kumpiga chura take, anakumwagia nondo na nyingine ni zenye maurongo ndani yake.

Kwa uzoefu wangu humu, tukijadili issue yoyote ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar, sometimes it gets so emotional, kuna bandiko humu hali ya hewa ilichafuka watu tukatishiwa kifo tukikanyaga tuu Zanzibar hadi mode akalifuta bandiko lile.

Hii ya kumtaja Okello sii lolote sii chochote ni kumdogosha tuu, huyu ndiye alyeyatangaza Mapinduzi ya Zanzibar kwenye redio na ndiye alikuwa Mwenyekiti wa kwanza wa Baraza la Mapinduzi mara baada ya Mapinduzi, hawezi kuwa sii lolote sii chochote.

Ukimsoma vizuri Mkuu Maalim Mohammed Said in between the lines, utagundua the motive behind ya baadhi ya maandiko yake ni ill motives, hata ile historia ya kuwakweza wazee wake, lengo sio tuu kuwataja wakumbukwe bali pia kutaka kumdogosha Mwalimu Nyerere ili aonekane sii lolote sii chochote mbele ya wazee wake.

Ni ama tuendelee kumpiga chura mateke tumuongezee mwendo ama maurongo mengine tuyanyamazie kama hili la Okello sii lolote sii chochote



Kwenye video hiyo inathibitisha Okello ndio alipanga Mapinduzi, Karume hakuwepo Zanzibar, Babu hakuwepo Zanzibar, na Nyerere hakujua ndio kwanza alimuuliza Babu, what happened in Zanzibar?!.

Halafu leo anakuja mtu kusema eti Okello sii lolote sii chochote!.
P
 
"Pascal Mayalla, post: 33635440, member: 17813"]
Mkuu Nguruvi3, Mkuu Maalim Mohammed Said ni very controversial kwenye baadhi ya hoja zake, na kila akileta any controversial issue, ukihoji, kwake ni kama kumpiga chura take, anakumwagia nondo na nyingine ni zenye maurongo ndani yake.
Hoja ya Thani ameileta makusudi kufunika hoja ya Utumwa, Uarabu na ushiriki wa Sultan

Alijaribu kutumia TransAtalantic slave trade kutuondoa katika mstari tukamwambi huko sipo

Akatupeleka Kipumbwi tukamwambia tunakwenda, tukaishia mapinduzi daima na Sultan safi

Hapa kukawa na utata, ni ''double edged sword'' ima kumkubali Sultani na kuwakana Wamatumbi au kuwakubali wamatumbi na kumkana Sultan.

Ni ngumu, makundi hayo yanaunganishwa na kitu kimoja chenye ''interest'' kwake'
Ndio maana hawezi kusema mapinduzi ni halali au ni haramu, anafanya ''insinuation'' tu

Katika kubabisha anatuletea Picha ya Okello bila kutueleza ilipigwa lini, wapi na hao ni akina nani aliokaa nao.

Halafu anataka watu watambue Wazanzibar ''khalisi''

Kwanza hakuna kitu kinaitwa Mzanzibar khalisi tumemuuliza atueleze yupo je, kachikia

Pili kasema aliyepanga mapinduzi ni Abdallah Kassim Hanga.
Kama ndivyo, Hanga ndiye aliye organize watu kutoka Kipumbwi kwenda kumuondoa Sultan

Tatu, anasema anamfahamu Hanga .
Ikiwa ni hivyo, wazee wa Dar walijua mipango ya Hanga kupeleka watu kutoka Kipumbwi.

Nne, anasema Okello si lolote si chochote.
Ikiwa ni hivyo, kwanini alipewa kazi ya kutangaza Mapinduzi?
Je, wahusika akina Hanga walikuwa wapi na waliogopa nini?

Tano, je watu 12 wa mwanzo wa baraza la Mapinduzi walikuwa Wazanzibar ''khalisi'' au la

Watu wanadhani tupo hapa kumpinga MS, la hasha! tunachofanya ni ''ku-critic'' historia jambo la kawaida kabisa katika mijadala. Sasa kukiwa na disjointed story watu wasiseme!

Kama kuna upotoshaji kuna ku''debunk' hoja na ngano, si kumeza mazima

Katika utata na asivyoweza kutetea hoja bado anataka historia ya 'kweli'' ifundishwe
 
Mkuu Nguruvi3, Mkuu Maalim Mohammed Said ni very controversial kwenye baadhi ya hoja zake, na kila akileta any controversial issue, ukihoji, kwake ni kama kumpiga chura take, anakumwagia nondo na nyingine ni zenye maurongo ndani yake.

Kwa uzoefu wangu humu, tukijadili issue yoyote ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar, sometimes it gets so emotional, kuna bandiko humu hali ya hewa ilichafuka watu tukatishiwa kifo tukikanyaga tuu Zanzibar hadi mode akalifuta bandiko lile.

Hii ya kumtaja Okello sii lolote sii chochote ni kumdogosha tuu, huyu ndiye alyeyatangaza Mapinduzi ya Zanzibar kwenye redio na ndiye alikuwa Mwenyekiti wa kwanza wa Baraza la Mapinduzi mara baada ya Mapinduzi, hawezi kuwa sii lolote sii chochote.

Ukimsoma vizuri Mkuu Maalim Mohammed Said in between the lines, utagundua the motive behind ya baadhi ya maandiko yake ni ill motives, hata ile historia ya kuwakweza wazee wake, lengo sio tuu kuwataja wakumbukwe bali pia kutaka kumdogosha Mwalimu Nyerere ili aonekane sii lolote sii chochote mbele ya wazee wake.

Ni ama tuendelee kumpiga chura mateke tumuongezee mwendo ama maurongo mengine tuyanyamazie kama hili la Okello sii lolote sii chochote



Kwenye video hiyo inathibitisha Okello ndio alipanga Mapinduzi, Karume hakuwepo Zanzibar, Babu hakuwepo Zanzibar, na Nyerere hakujua ndio kwanza alimuuliza Babu, what happened in Zanzibar?!.

Halafu leo anakuja mtu kusema eti Okello sii lolote sii chochote!.



P
Paschal,
Kuandika kitabu kusahihisha yaliyokuwa si kweli unachukulia ni kudogosha?

Sasa wale walioandika historia ambayo haikuwa sawa na wao tusemaje?
 
Hoja ya Thani ameileta makusudi kufunika hoja ya Utumwa, Uarabu na ushiriki wa Sultan

Alijaribu kutumia TransAtalantic slave trade kutuondoa katika mstari tukamwambi huko sipo

Akatupeleka Kipumbwi tukamwambia tunakwenda, tukaishia mapinduzi daima na Sultan safi

Hapa kukawa na utata, ni ''double edged sword'' ima kumkubali Sultani na kuwakana Wamatumbi au kuwakubali wamatumbi na kumkana Sultan.

Ni ngumu, makundi hayo yanaunganishwa na kitu kimoja chenye ''interest'' kwake'
Ndio maana hawezi kusema mapinduzi ni halali au ni haramu, anafanya ''insinuation'' tu

Katika kubabisha anatuletea Picha ya Okello bila kutueleza ilipigwa lini, wapi na hao ni akina nani aliokaa nao.

Halafu anataka watu watambue Wazanzibar ''khalisi''

Kwanza hakuna kitu kinaitwa Mzanzibar khalisi tumemuuliza atueleze yupo je, kachikia

Pili kasema aliyepanga mapinduzi ni Abdallah Kassim Hanga.
Kama ndivyo, Hanga ndiye aliye organize watu kutoka Kipumbwi kwenda kumuondoa Sultan

Tatu, anasema anamfahamu Hanga .
Ikiwa ni hivyo, wazee wa Dar walijua mipango ya Hanga kupeleka watu kutoka Kipumbwi.

Nne, anasema Okello si lolote si chochote.
Ikiwa ni hivyo, kwanini alipewa kazi ya kutangaza Mapinduzi?
Je, wahusika akina Hanga walikuwa wapi na waliogopa nini?

Tano, je watu 12 wa mwanzo wa baraza la Mapinduzi walikuwa Wazanzibar ''khalisi'' au la

Watu wanadhani tupo hapa kumpinga MS, la hasha! tunachofanya ni ''ku-critic'' historia jambo la kawaida kabisa katika mijadala. Sasa kukiwa na disjointed story watu wasiseme!

Kama kuna upotoshaji kuna ku''debunk' hoja na ngano, si kumeza mazima

Katika utata na asivyoweza kutetea hoja bado anataka historia ya 'kweli'' ifundishwe
Nguruvi3,
Unasema Waarabu wametesa na kuua Zanzibar na haya yametokea miaka mingi nyuma.

Hakika kuua ni jambo ovu.

Mimi nimekuletea maelezo ya Aman Thani ya miaka ya 1960 juzi tu hapa ya kutesa na kuua.

Hebu hesabu miaka kati ya historia hizi mbili.

Mandera analipiza kisasi cha biashara ya utumwa ya zaidi ya miaka 300 iliyopita?

Kuna nantiki hapo.
 
Pascal Mayalla unakumbuka kuna mahali umesema mzee akibanwa hutumbukiza mambo mengine kuwavuruga watu!!

Ndicho kinachoendelea. Tunaongelea Mapinduzi na utumwa tayari kaingiza Aman Thani na jela za mateso baada na si kabla ya mapinduzi

Hata hivyo tutakwenda naye sambamba tulitendea jukwaa hili haki.

Ni jukwaa lililoachwa bila 'care' kwa muda kiasi kwamba limegeuka eneo la upotoshaji wa makusudi. Tumepiga kambi

Kuna jingine limejitokeza bandiko#125.

Mohamed anadai aliasisi na kupanga mapinduzi ni Abdallah Kassim Hanga.
Naomba hili liwe katika kumbukumbu bila kulinukuu kama lilivyo

Pili, kasema Okello si lolote si chochote latika mapinduzi ya Zanzibar
Nalo tunaomba liwe katika kumbu kumbu

Tatu, MS kadai alikuwa anamfahamu A.K.Hanga na Wazazi wake walikuwa maswahiba
Hili naomba liwekwe katika kumbu kumbu

Nne, kuna picha ya Okello na wenzake.
Mohamed anasema kama kuna Mzanzibar halisi attajwe
a) MS hajatueleza picha hiyo ilipigwa wapi na lini
b) MS akumbuke Okello ameishi katika nchi tatu na kila alipotua lilizuka la kuzuka

Haya tunaomba yawe katika kumbu kumbu kwasababu mjadala unaendelea na tutayatumia

JokaKuu Mag3
Nguruvi 3,
Mjadala wowote ukiugeuza kuwa mahali pa ushabiki unaupunguzia hadhi panakuwa mahali pa kusutana.

Mnakasha ni sehemu ya kushindanisha hoja kwa njia za kistaarabu.
Matati\o ya ushabiki ni kama hay hapo chini:

''Tatu, MS kadai alikuwa anamfahamu A.K.Hanga na Wazazi wake walikuwa maswahiba
Hili naomba liwekwe katika kumbu kumbu.''


Wazanzibari waliokuwa marafiki ya baba yangu ni Jaha Ubwa na Abdulaziz Twala na urafiki wao ni toka enzi za 1950s wakiwa vijana kabisa.

Kassim Hanga alikuwa akija mtaani petu Gogo Street kona na Mchikiichi nje ya nyumba ya Mama Abdul Kiguja.

Kwenye nyumba hii nje wakicheza bao na hapo mimi ndipo nilipokuwa nikimuona Hanga akija tena kwa miguu kuja kucheza bao.

Kilwa Jazz Band walikuwa na club yao kwenye chumba cha pembeni nje katika nyumba hii.

Kulikuwa na picha yao watu watatu wamepiga na walipouliwa baba aliiondoa picha ile ukutani.

Tofauti baina yetu ni kuwa mimi nimeishi ndani ya historia hii.

Rudi nyuma unisome upya.
 
Hoja ya Thani ameileta makusudi kufunika hoja ya Utumwa, Uarabu na ushiriki wa Sultan

Alijaribu kutumia TransAtalantic slave trade kutuondoa katika mstari tukamwambi huko sipo

Akatupeleka Kipumbwi tukamwambia tunakwenda, tukaishia mapinduzi daima na Sultan safi

Hapa kukawa na utata, ni ''double edged sword'' ima kumkubali Sultani na kuwakana Wamatumbi au kuwakubali wamatumbi na kumkana Sultan.

Ni ngumu, makundi hayo yanaunganishwa na kitu kimoja chenye ''interest'' kwake'
Ndio maana hawezi kusema mapinduzi ni halali au ni haramu, anafanya ''insinuation'' tu

Katika kubabisha anatuletea Picha ya Okello bila kutueleza ilipigwa lini, wapi na hao ni akina nani aliokaa nao.

Halafu anataka watu watambue Wazanzibar ''khalisi''

Kwanza hakuna kitu kinaitwa Mzanzibar khalisi tumemuuliza atueleze yupo je, kachikia

Pili kasema aliyepanga mapinduzi ni Abdallah Kassim Hanga.
Kama ndivyo, Hanga ndiye aliye organize watu kutoka Kipumbwi kwenda kumuondoa Sultan

Tatu, anasema anamfahamu Hanga .
Ikiwa ni hivyo, wazee wa Dar walijua mipango ya Hanga kupeleka watu kutoka Kipumbwi.

Nne, anasema Okello si lolote si chochote.
Ikiwa ni hivyo, kwanini alipewa kazi ya kutangaza Mapinduzi?
Je, wahusika akina Hanga walikuwa wapi na waliogopa nini?

Tano, je watu 12 wa mwanzo wa baraza la Mapinduzi walikuwa Wazanzibar ''khalisi'' au la

Watu wanadhani tupo hapa kumpinga MS, la hasha! tunachofanya ni ''ku-critic'' historia jambo la kawaida kabisa katika mijadala. Sasa kukiwa na disjointed story watu wasiseme!

Kama kuna upotoshaji kuna ku''debunk' hoja na ngano, si kumeza mazima

Katika utata na asivyoweza kutetea hoja bado anataka historia ya 'kweli'' ifundishwe
Nguruvi,
Alipofariki Ali Nabwa mimi nilimwandikia taazia ambayo ilichapwa na The East African:http: //www.mohammedsaid.com/.../obituary-weeping-and...Obituary The Weeping and Whipping Pen of Ali Mohamed Nabwa 1936 -2007.

Nakueleza haya tufahamiane vyema.

Makala ilipendwa na Channel Ten waliniomba nishiriki katika kipindi cha tv kuhusu Ali Nabwa.

Ally Saleh Alberto sasa Mheshimiwa Ally Saleh na Mohamed Ghassani walikuwa ndani ya studio za Channel Ten Dar es Salaam mimi wakani- link kwa simu kutoka Tanga.

Kipindi kilikuwa moto kiasi kuwa taarifa zilizonifikia ni kuwa wandaaji wa kipindi walililalamikiwa na kipindi hakikurudiwa.

1575172287318.png

Nikishiriki kipindi Hamza Kassongo Hour kuhusu Ali Nabwa nikiwa Tanga kwenye phone link
kwenye TV kushoto ni Ally Saleh na kulia ni Mohamed Ghassany
 
Mohamed Said tafadhali rejea bandiko#132 kipengele cha Hanga ulicholalamikia
Nilifanya editing nahisi ulinukuu baada tu ya bandiko

Pamoja na hayo umetueleza baba yako aliondoa picha, hivyo kulikuwa na mahusiano makubwa

Ukasema Hanga alikuwa akicheza bao na wazee wako wa Dar.

Hayo tuyaache yasituondoe katika mstari na wala kuingiza mengine kama bandiko# 136 ambalo sijui hata linahusiana vipi na hoja zilizoainishwa hapo awali zinasoburi hoja zako pia

Hoja hizo ni kama ifuatavyo;
1. Picha ya Okello ilipigwa lini, wapi ,na hao aliokaa nao ni akina nani kwa majina

2. Mzanzibar ''khalisi'' ana haiba, wasifu au sifa gani tofauti na mzanzibar mwingine

4. Abdallah Kassim Hanga ndiye alipanga mapinduzi kwa mujibu wako.
Je, ni Hanga ndiye aliyehusika na kupeleka mamluki wa Kimakonde kutoka Kipumbwi

5.Ikiwa Hanga aliandaa mapinduzi, je,wanaosema mapinduzi daima wapo sahihi au wanakosea

6. Ikiwa Hanga ndiye aliye andaa mapinduzi wazee wako wa Dar ambao ni maswahiba wa Hanga katika kucheza bao na maongezi walijua mpango huo?

7. Ikiwa Okello alikuwa si lolote si chochote, dhima ya kutangaza mapinduzi alipewa kwa minajili gani na kwanini akina Hanga hawakwenda kutangaza wao

8. Nani mwenyekiti wa kwanza wa baraza la mapinduzi na wajumbe walikuwa akina nani


Hizi ndizo hoja zilizopo mbele yetu, tukimaliza tutaweza kupata picha halisi ya mapinduzi

Pascal Mayalla Mag3 JokaKuu
 
Atakwambia watu waliletwa kutoka Kipumbwi kufanya mapinduzi.

Hasemi kama tukio hilo limeharamisha mapinduzi, lakini between the lines Mohamed anaamini Zanzibar ilikuwa bora wakati wa Sultan.

Mapinduzi anayaona kama shambulizi dhidi ya Uislam. Hasemi wazi maandiko yake yanasema

Kwa msingi huo mwenzetu yupo njia panda kati ya mambo mawili yanayotofautiana

Hawezi kusema mapinduzi ni haramu, atawaudhi Wamatumbi Waislam
Hawezi kusema mapinduzi ni halali, atawaudhi waathirika ambao ni Waislam

Kwahiyo njia nyepesi ni kutafuta ''grey area'' akijivika wajihi wa Popo

Kwani uongo ? mapinduzi ni vita dhidi ya uislamu na waislamu Zanzibar. Hayo yamo katika kitabu cha Padri Sullivan ,Kanisa Katoliki na sisa za Tanzania Bara
 
Wakiongozwa na Hamad bin Muhammad bin Juma bin Rajab el Murjebi, kwa jina maarufu la
Tippu Tip, or Tippu TibView attachment 1277794

Madhila waliotufanyia watu hawa, nimeyaeleza napa


p

Ulisahau kuandika mnunuzi wa watumwa Mreno na Mfaransa
 
Paschal,
Kuandika kitabu kusahihisha yaliyokuwa si kweli unachukulia ni kudogosha?

Sasa wale walioandika historia ambayo haikuwa sawa na wao tusemaje?
Mkuu Maalim Mohammed Said, bado unaweza kuandika historia ya kusahisha urongo wa historia zilizoandikwa kwa lengo la kuweka bayana mchango wa wazee wako bila kuwakweza unnecessarily na bila kuwadogosha wengine.

Mfano harakati za uhuru wa Tanganyika zimeanzia
AA, TAA na TANU, nikiamua kuzero in kwenye mashujaa viongozi waanzilishi, nitawataja mashujaa watatu tuu, Cecil Matola, Dr. Vedastus Kyaruzi na Mwalimu Julius Kambarage Nyerere!. Nilisema kina Sykes were nothing, I will still be right kwenye muktadha wa Wenyeviti waanzilishi ila nitakuwa nimewagogosha.

Nilisema nayasoma maandishi yako in between the lines na kuiibaini the ill motives behind baadhi ya hoja zako kutaka kumdogosha Mwalimu Nyerere na kuwakweza wazee wako!. Ukatumia urongo kuonyesha Mwalimu Nyerere hakulijua jiji hadi alipotambulishwa na wazee wako in 1950s, Mkuu Nguruvi3 akakuwekea data za ujio wa Mwalimu Nyerere kwenye mkutano Mkuu wa TAA mwaka 1948, ukakimbia.

Unaweza kuandika historia sawia bila kukweza wala kudogosha na bila kuongopa kwa kujazia vionjo vya maurongo.

Sasa kwenye hili la Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar, dunia nzima inaujua mchango wa John Okello, wewe kuibuka na kusema Okello sii lolote sii chochote ni kumdogosha.

Tunakueleza madhila ya babu zetu yaliyowakuta kwenye utumwa wa Waarabu na Sultan wa Zanzibar, wewe unataka tuzungumzie utumwa wa Trans Atlantic Slave Trade ili tuu kuudogosha utumwa wa Indian Ocean Slave Trade.

Historia ya kweli ya Zanzibar inaweza kuandikwa kwa ukweli huku ukiyaenzi Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar na kutumia kibwagizo cha "Mapinduzi Daima" kwa kuyalaani mabaya na maovu ya Sultani wa Zanzibar kuhalalisha Mapinduzi at the same time na bado kuyaenzi mazuri ya Sultani.
P
 
Back
Top Bottom