Kwanini Iran imezipita Ethiopia na Liberia?

Kwanini Iran imezipita Ethiopia na Liberia?

Iran wanawekeza sana kwenye science na wanavumbua vitu vingi sana
Wanasayansi wao wanasakwa usiku na mchana na wengine kuuwawa na maadui ila wamo tu

Na hivi karibuni kuna mwana sayansi kavumbua gari inayotembea kwa maji yes maji ya kunywa


View attachment 2739135
Unaokoteza habari alafu unazileta humu bila aibu serious?
 
Nilikuwa namaanisha ndio mwaasisi wa intelligence team ya hashashin sio intelligence branch.🙆‍♂️🙆‍♂️
Niwe mkweli, hata hapo bado umeniacha "mataa". Sijaelewa maana ya hiyo "terminology". Msaada, tafadhali.
 
Nilikuwa namaanisha ndio mwaasisi wa intelligence team ya hashashin( assasin) sio intelligence branch. The order of assasin ukimtafuta hassan i sabah utaelewa vizuri mkuu .🙆‍♂️🙆‍♂️
Sawa mkuu. Ngoja nipekue mtandaoni nione nitakachokipata.
 
Zote, hasa Ethiopia na Iran, ni nchi kongwe. Zimekuwepo tokea kipindi Biblia inaandikwa.

Nchi zote tatu hazikuwahi kutawaliwa na Wazungu.

Lakini Iran imezipita zote kwa mambo mengi.

Kwa ubabe, imo! Inatunishiana misuli na mataifa makubwa kama Israel na Marekani.

Kama ni nguvu ya kiuchumi, imo.
Nguvu ya kijeshi, imo.

Kisayansi, imo. Hivi Sasa ipo katika harakati za kutengeneza mabomu ya nyuklia.

Ingawa inadaiwa kutokuwa na Demokrasia, lakini ni wazi kuwa imepiga hatua kubwa sana kiuchumi na Kisayansi kuzidi Ethiopia na Liberia.

Nini kimewakwamisha ndugu zetu, Ethiopia na Liberia?
Ngozi nyeusi haziwezi demokrasia na zikishika udikiteta ndio kabisa Nchi inakuwa jehanam
 
Zote, hasa Ethiopia na Iran, ni nchi kongwe. Zimekuwepo tokea kipindi Biblia inaandikwa.

Nchi zote tatu hazikuwahi kutawaliwa na Wazungu.

Lakini Iran imezipita zote kwa mambo mengi.

Kwa ubabe, imo! Inatunishiana misuli na mataifa makubwa kama Israel na Marekani.

Kama ni nguvu ya kiuchumi, imo.
Nguvu ya kijeshi, imo.

Kisayansi, imo. Hivi Sasa ipo katika harakati za kutengeneza mabomu ya nyuklia.

Ingawa inadaiwa kutokuwa na Demokrasia, lakini ni wazi kuwa imepiga hatua kubwa sana kiuchumi na Kisayansi kuzidi Ethiopia na Liberia.

Nini kimewakwamisha ndugu zetu, Ethiopia na Liberia?
Hakuna nchi ya Afrika iliyowahi kuwa huru.
Tuna uhuru wa bendera. Hawa viongozi wetu ni mawakala wa mabwana zao whites.
Ni km jela Nyapara anavyocontrol wafungwa ili kumsaidia Askari Magereza.
 
Jinsi ulivyojibu hoja inaonesha wewe ni mtu wa namna gani. Usomi unataka hoja ijibiwe kwa hoja, kuuliza maswali ya kidadisi na kukubali kujifunza mambo mapya kila siku (Socratic Method of Learning). Kunishambulia mimi binafsi kwamba natumia ChatGpt kumenishangaza mno, hasa kwa mtu ambaye binafsi nilimuona msomi. Mimi nimesoma historia zamani kipindi ambacho hata hizi teknolojia hazikuwepo. Unaponiambia natumia ChatGpt ambayo hata sijui kuitumia, naona unanitukana tu. Binafsi siwezi kukurushia vijembe kwasababu naamini sifahamu kila kitu, mbali na kwamba nimesomea historia na falsafa za kale kwa muda mrefu tu. Ila nitakisema kile nachokifahamu, ukitaka kwenda kufanya utafiti itapendeza, ukiendelea kuamini kwamba unafahamu kila kitu, basi hewala pia. Turidi hojani:

Mosi, mbali na kuwepo vyanzo vya kihistoria ambavy vimegundulika miaka ya hivi karibuni, vyanzo vikubwa vya historia ya kale ni waandishi wa Kigiriki na Kilatini, mfano Herodotus, Strabo, Polybius, Xenophon na Josephus. Taarifa za msingi za dola la madola ya kiajemi ambazo hata wasomi wakubwa duniani wanazitegemea ziliandikwa na Herodotus kwenye kitabu chake cha The Histories. Unapoendelea kubishana na vyanzo ambavyo hata hao wasomi unaowataja wanavitumia unanipa ukakasi sana. Hizi hapa ni kurasa chache za kitabu cha Herodotus kinachozungumzia vita baina ya Uajemi na Ethiopia:

View attachment 2739581

Hapa anaendelea kuelezea jinsi waajemi walivyoshindwa vita dhidi ya Waethiopia:

View attachment 2739583

Pili, unavyozungumzia Archaeological Evidence kuleta uthibitisho wa dola la Umedi & Uajemi, hata mimi binafsi nakushangaa. Hakuna anayepinga uwepo wa dola la Umedi & Uajemi, miaka ya 5th BCE. Ambacho nakushangaa ni kitendo cha wewe kushindwa kukubali kwamba eneo ambalo madola ya Uajemi yamekuwepo ni barabara ya dunia (International Pathway) ambayo baadaye ilikuja kuwa The Silk-Road, iliyounganisha dunia (The Known World) kwa miaka zaidi ya 3000. Hata waajemi wenyewe kiasili ni watu waliohamia kutoka The Indus Valley baada ya kipindi cha Bronze Age kuanguka. Eneo lile liliunganisha dunia biashara ya dunia kutoka Ulaya, Afrika, Arabia na Mashariki ya Mbali.

Hata tunaposoma The Islamic Golden Age, kipindi ambacho The Abbasid Caliphate waliiletea dunia mapinduzi makubwa kwenye sayansi, teknolojia na falsafa, moja ya chanzo kikubwa ni uwepo wa dola hili kwenye sehemu ya barabara ya dunia. Wasomi wa kiislamu walijifunza mambo mengi kutoka Rumi, Uajemi na India ambayo wewe na mimi leo hii tunayasoma. Leo hii msomi yoyote akitoa hoja kwamba Marekani limekuwa taifa kubwa bila msaada wa kijiografia nitamshangaa mno. Kama umesoma vizuri historia, naamini utakuwa unafahamu kuhusu, The Bubonic Plague, tauni ambayo iliua mamilioni ya watu barani Asia na Ulaya.

Ugonjwa ule ulianzia Uchina lakini ulifika kwa haraka mno Ulaya kwasababu ya barabara ya kimataifa (International Pathway/ The Silk Road/Steppe Road) ambayo iliunganisha mabara zaidi ya matatu kibiashara. Huwezi kupinga Geography kwenye maendeleo ya taifa lolote lile kubwa, hence the word GEOPOLITICS. Msomi Tim Marshall kwenye kitabu chake maarufu kiitwacho, PRISONERS OF GEOGRAPHY: TEN MAPS THAT TELL YOU EVERYTHING YOU NEED TO KNOW ABOUT GLOBAL POLITICS, anasema hivi:

View attachment 2739634

Jiografia huathiri mno ustawi wa madola makubwa, kiufupi hata maendeleo ya sayansi na teknolojia hayaletwi na akili za watu peke yake, bali muingiliano wa kiutamaduni ambao hushawishiwa mno na jiografia. Mataifa ya Uajemi yemedumu kwa muda mrefu kwasababu jiografia iliwasaidia kukua kiutamaduni, kiuchumi, kijeshi na kiteknolojia. Mbinu za kijeshi alizotumia Koreshi alijifunza kwa The Scythians, mbinu za mahesabu za kiajemi zilitokea India. Mbona haya yanafahamika vizuri tu.

Tatu, leo umenifanya nichangamke na kupitia madaftari yangu ya notsi ambazo niliziandika nikiwa chuoni nafanya tafiti kuhusu madola ya Kiajemi miaka mingi sana iliyopita. Binafsi hatukuwa na GOOGLE wala ChatGpt, ilikuwa ni kwenda maktaba kuinamisha mgongo mpaka usikuwa wa manane. Wengi wenu mngesoma kwenye mazingira ambayo tumesoma sisi, ya vitabu bila kompyuta mngetia akili. Zamani watu walikuwa hawafaulu wengi kwasababu hakukuwa na dezo, unajua historia, unajua historia, hujui historia unabaki kuwa mjinga mpaka mwisho. Hapa nilikuwa nachukua notsi kwenye mada iitwayo "Why Were the Iranian Empires So Successful" . Mwalimu wa kizungu alikuwa anasoma IMRA (Dictation) sisi tunaandaa notsi zetu fupi (Summary), hakuna ChatGpt wala GOOGLE Hebu angalia:

View attachment 2739637

View attachment 2739638
View attachment 2739641
View attachment 2739643
View attachment 2739648

Baada ya hapa, tulifundishwa kuhus CYRUS THE GREAT- RISE OF THE ACHAEMENID EMPIRE, na baadaye tukafanya mitihani kibao, pamoja na majadiliano. Hivyo naposema nakifahamu kitu wala sijisifii au kutaka mnione nafahamu, ila nasema ili tujifunze:
View attachment 2739657

Hii hapa PHILIP'S ATLAS OF WORLD HISTORY, nimeisomea miaka mingi nyuma nikiwa HIGH-SCHOOL mwaka wa mwisho, mpaka leo ninayo na nimewatunzia watoto wangu wanaendelea kuitumia. Kuna kipindi nilikuwa nimekariri karibia michoro yote na picha za hii Atlas.
View attachment 2739667View attachment 2739668

NB: Mkuu Venus wewe ni watu ambao nawaheshimu sana humu ndani, japo sikufahamu. Uliposema mimi ni ChatGpt a.k.a Roboti, I was really flattered. Watu kunihisi mimi ni kompyuta au kikundi cha watu inaonesha kwamba I Have Mastered My Craft, All Praise To The Most High. Hakuna ChatGpt wala Google ni nidhamu ya kupenda kusoma na uzeoefu wa kazi yangu ambayo naipenda mno na nimeifanya kwa miaka mingi sana.

Uwe na siku njema mkuu Venus Star, you have my Deepest Respect!
Samahani sana ndugu yangu kwa kukukosea.

Naomba nikae nisome vizuri hii comment yako kisha niweke comment yangu vizuri.

Lakini wewe umeanza kuongelea karne 5 BCE. Mimi nimeongelea 4000BCE kumbuka miaka ilikuwa inasomeka kwa reduction before CE.

Vilevile hujaiomgelea kabisa Ethiopia kuiweka chungu kimoja na Iran.

Ngoja nimalizie kazi kisha niandike maelezo kwa undani.
 
Samahani sana ndugu yangu kwa kukukosea.

Naomba nikae nisome vizuri hii comment yako kisha niweke comment yangu vizuri.

Lakini wewe umeanza kuongelea karne 5 BCE. Mimi nimeongelea 4000BCE kumbuka miaka ilikuwa inasomeka kwa reduction before CE.

Vilevile hujaiomgelea kabisa Ethiopia kuiweka chungu kimoja na Iran.

Ngoja nimalizie kazi kisha niandike maelezo kwa undani.
Mimi nimekuelewa vizuri ndugu yangu, nadhani ambapo tumepishana ni mwaka 4000BC na 5BCE. Kipindi cha 4000BCE (The Bronze Age) jamii ndogo-ndogo ambazo zilikuwepo kwenye miji kama Elam, Anshan na Susa kwenye eneo la Mesapotamia. Mambo ambayo nadhani hatukuyaweka sawa mwanzoni mwa mjadala ni haya yafuatayo:

Mosi, wamedi & waajemi (Indo-Aryan) walihamia Mesapotamia mwaka 1000BCE na kubadilisha siasa za ukanda ule na kufanya dola kubwa la Kimedi ambalo makao yake makuu yalikuwa pale Ecbatana. Wamedi walishirikiana na madola jirani kama Elamu ambalo lilikuja kumezwa na Babeli baada ya kuanguka kwa Ashuru. Kiufupi, ndani ya dola la Wamedi, Waajemi (Wafursi) walikuwa hawana sauti kubwa mpaka kipindi cha Koreshi mwaka 552 BCE ambapo alimpindua babu yake Mfalme Astyages na kufanikiwa kuunganisha dola la Umedi, Uajemi, Elamu na Babeli chini ya mwamvuli wa Medo-Persian Empire/ The Achaemenid Empire.

Ukisoma kuhusu The Persian Revolt utaona kabisa kwamba Waajemi walitawaliwa na Wamedi ambao walipinga kabisa dola lao kuwa chini ya Waajemi. Hata Mfalme Astyages alipoota ndoto kwamba binti yake Mandane atazaa mtoto na Muajemi Cambyses I alitoa amri mtoto auwawe, lakini bahati nzuri wakina Mithridates wakaokoa uhai wa Koreshi na kumlea hadi ukubwani.

Pili, kuhusu swala zima la Waajemi kuwa na akili hilo wala sipingani nalo. Historia inathibitisha hili, japo hatuwezi kukataa kabisa sababu za kijiografia ambazo ziliwafanya wao wafanikiwe zaidi kuliko madola mengine kama Seljuks na Ethiopia. Ukitengwa au ukijitenga mbali na dunia siyo rahisi kupata maendeleo, ndicho kiliyakuta madola kama Kushi. Hata Uchina ya Ming Dynasty ilianguka baada ya kuamua kujitenga na dunia ilhali Zheng He ndiye alifika pwani ya Afrika Mashariki miaka 90 kabla ya Vasco Da Gamma.​
 
Mimi nimekuelewa vizuri ndugu yangu, nadhani ambapo tumepishana ni mwaka 4000BC na 5BCE. Kipindi cha 4000BCE (The Bronze Age) jamii ndogo-ndogo ambazo zilikuwepo kwenye miji kama Elam, Anshan na Susa kwenye eneo la Mesapotamia. Mambo ambayo nadhani hatukuyaweka sawa mwanzoni mwa mjadala ni haya yafuatayo:

Mosi, wamedi & waajemi (Indo-Aryan) walihamia Mesapotamia mwaka 1000BCE na kubadilisha siasa za ukanda ule na kufanya dola kubwa la Kimedi ambalo makao yake makuu yalikuwa pale Ecbatana. Wamedi walishirikiana na madola jirani kama Elamu ambalo lilikuja kumezwa na Babeli baada ya kuanguka kwa Ashuru. Kiufupi, ndani ya dola la Wamedi, Waajemi (Wafursi) walikuwa hawana sauti kubwa mpaka kipindi cha Koreshi mwaka 552 BCE ambapo alimpindua babu yake Mfalme Astyages na kufanikiwa kuunganisha dola la Umedi, Uajemi, Elamu na Babeli chini ya mwamvuli wa Medo-Persian Empire/ The Achaemenid Empire.

Ukisoma kuhusu The Persian Revolt utaona kabisa kwamba Waajemi walitawaliwa na Wamedi ambao walipinga kabisa dola lao kuwa chini ya Waajemi. Hata Mfalme Astyages alipoota ndoto kwamba binti yake Mandane atazaa mtoto na Muajemi Cambyses I alitoa amri mtoto auwawe, lakini bahati nzuri wakina Mithridates wakaokoa uhai wa Koreshi na kumlea hadi ukubwani.

Pili, kuhusu swala zima la Waajemi kuwa na akili hilo wala sipingani nalo. Historia inathibitisha hili, japo hatuwezi kukataa kabisa sababu za kijiografia ambazo ziliwafanya wao wafanikiwe zaidi kuliko madola mengine kama Seljuks na Ethiopia. Ukitengwa au ukijitenga mbali na dunia siyo rahisi kupata maendeleo, ndicho kiliyakuta madola kama Kushi. Hata Uchina ya Ming Dynasty ilianguka baada ya kuamua kujitenga na dunia ilhali Zheng He ndiye alifika pwani ya Afrika Mashariki miaka 90 kabla ya Vasco Da Gamma.​
Nashukuru kwa maelezo yako. Lakini nataka nikupatie clarification kidogo ili tuweze kwenda kwa pamoja.
Tunapoongelea BC and BCE ni kitu kile kile kama CE na AD
BC = Before Christ
BCE = Before the Common Era
CE = Common Era
AD = Anno Domini
Zote hizo zinahusika na kuhesabu miaka. Na uhesabuji wa miaka unaanzia katika kipindi cha kuzaliwa kwa Yesu (CE and AD) zinaongelea jambo lile lile. Lakini kwa sasa wanatumia zaidi CE badala ya AD.
BC na BCE ni jambo lile lile lakini unaanza kuhesabu wakati Yesu alipozaliwa kwa kurudi nyuma. Nikisema 4000BCE ni sawa kabisa na kusema 4000BC. Yaani hesabu miaka 4000 kurudi nyuma baada ya kuzaliwa Yesu.
1693926257613.png

Sasa ndugu yangu ukisema 5BC huoni ni miaka mitano tu kabla ya kuzaliwa yesu?
TURUDI KWENYE MADA SASA
Wamedi
Hawa watu walianza kutawala maeneo ya ambayo kwa sasa ni Iran, Azerbaijan, Armenia, Georgia na upande wa Mashariki ni Afghanistan na Pakistan. Kutokana na historia inaelezwa kwamba ilianzishwa 675 BC.
1693926301540.png

Waajemi
Hawa wameanza kujulikana kwa jina hili miaka ya 9th century BCE.
MIMI NAONGELEA NINI SASA?
Ethiopia haina historia ndefu kama ya Iran, kwahiyo siyo sahihi sana kuifananisha Iran na Ethiopia kwa mujibu wa Historia.
Pili niliongeza kuwa Iran civilization haijaanza wakati wa Wamedi. La hasha nimesema kwamba hawa wameanza civilization miaka mingi mno yaani 4000BCE.
Anshan
Hapa niliongelea old civilization ambayo wanahistoria waliweza kuchimba na kuona evidences za civilization. Kwa kutumia carbon 14 waliweza kugundua kuwa archeological kuwa civilization hiyo ni date back 4000 BCE to 1000 BCE

1693927803357.png

Hii ramani ni kuonesha tu location ya Anshan Civilization.

Kwa sasa naomba niishie hapa kwanza. Nitaweza kuweka taarifa kama kuna maswali zaidi
 
Sidhani kama bara lina tatizo. Afrika Kusini na Misri zipo barani Afrika, lakini angalia zilipo Kiuchumi, ni mbali sana ukizilinganish na nchi nyingi za Afrika.

Africa kusini makaburu bdo wako mkuu nchi inawazungu wakutosha ila na misri wale jamaa ni waarabu ila cjui walifikaje huku [emoji23][emoji23]
 
Haiti achana nao hao ni mizimu inayotembea
Yaani kila nyumba lazima ukute misanamu
Sokoni bidhaa nyingi na wauzaji wengi sana wanauza bidhaa za ushirikina tu hata magari yao yote wameweka voodoo
Wanaamini uchawi sana kuliko dini
Liberia?
 
Back
Top Bottom