Kwanini Iran imezipita Ethiopia na Liberia?

Unaokoteza habari alafu unazileta humu bila aibu serious?
 
Nilikuwa namaanisha ndio mwaasisi wa intelligence team ya hashashin sio intelligence branch.πŸ™†β€β™‚οΈπŸ™†β€β™‚οΈ
Niwe mkweli, hata hapo bado umeniacha "mataa". Sijaelewa maana ya hiyo "terminology". Msaada, tafadhali.
 
Nilikuwa namaanisha ndio mwaasisi wa intelligence team ya hashashin( assasin) sio intelligence branch. The order of assasin ukimtafuta hassan i sabah utaelewa vizuri mkuu .πŸ™†β€β™‚οΈπŸ™†β€β™‚οΈ
Sawa mkuu. Ngoja nipekue mtandaoni nione nitakachokipata.
 
Ngozi nyeusi haziwezi demokrasia na zikishika udikiteta ndio kabisa Nchi inakuwa jehanam
 
Hakuna nchi ya Afrika iliyowahi kuwa huru.
Tuna uhuru wa bendera. Hawa viongozi wetu ni mawakala wa mabwana zao whites.
Ni km jela Nyapara anavyocontrol wafungwa ili kumsaidia Askari Magereza.
 
Samahani sana ndugu yangu kwa kukukosea.

Naomba nikae nisome vizuri hii comment yako kisha niweke comment yangu vizuri.

Lakini wewe umeanza kuongelea karne 5 BCE. Mimi nimeongelea 4000BCE kumbuka miaka ilikuwa inasomeka kwa reduction before CE.

Vilevile hujaiomgelea kabisa Ethiopia kuiweka chungu kimoja na Iran.

Ngoja nimalizie kazi kisha niandike maelezo kwa undani.
 
Mimi nimekuelewa vizuri ndugu yangu, nadhani ambapo tumepishana ni mwaka 4000BC na 5BCE. Kipindi cha 4000BCE (The Bronze Age) jamii ndogo-ndogo ambazo zilikuwepo kwenye miji kama Elam, Anshan na Susa kwenye eneo la Mesapotamia. Mambo ambayo nadhani hatukuyaweka sawa mwanzoni mwa mjadala ni haya yafuatayo:

Mosi, wamedi & waajemi (Indo-Aryan) walihamia Mesapotamia mwaka 1000BCE na kubadilisha siasa za ukanda ule na kufanya dola kubwa la Kimedi ambalo makao yake makuu yalikuwa pale Ecbatana. Wamedi walishirikiana na madola jirani kama Elamu ambalo lilikuja kumezwa na Babeli baada ya kuanguka kwa Ashuru. Kiufupi, ndani ya dola la Wamedi, Waajemi (Wafursi) walikuwa hawana sauti kubwa mpaka kipindi cha Koreshi mwaka 552 BCE ambapo alimpindua babu yake Mfalme Astyages na kufanikiwa kuunganisha dola la Umedi, Uajemi, Elamu na Babeli chini ya mwamvuli wa Medo-Persian Empire/ The Achaemenid Empire.

Ukisoma kuhusu The Persian Revolt utaona kabisa kwamba Waajemi walitawaliwa na Wamedi ambao walipinga kabisa dola lao kuwa chini ya Waajemi. Hata Mfalme Astyages alipoota ndoto kwamba binti yake Mandane atazaa mtoto na Muajemi Cambyses I alitoa amri mtoto auwawe, lakini bahati nzuri wakina Mithridates wakaokoa uhai wa Koreshi na kumlea hadi ukubwani.

Pili, kuhusu swala zima la Waajemi kuwa na akili hilo wala sipingani nalo. Historia inathibitisha hili, japo hatuwezi kukataa kabisa sababu za kijiografia ambazo ziliwafanya wao wafanikiwe zaidi kuliko madola mengine kama Seljuks na Ethiopia. Ukitengwa au ukijitenga mbali na dunia siyo rahisi kupata maendeleo, ndicho kiliyakuta madola kama Kushi. Hata Uchina ya Ming Dynasty ilianguka baada ya kuamua kujitenga na dunia ilhali Zheng He ndiye alifika pwani ya Afrika Mashariki miaka 90 kabla ya Vasco Da Gamma.​
 
Nashukuru kwa maelezo yako. Lakini nataka nikupatie clarification kidogo ili tuweze kwenda kwa pamoja.
Tunapoongelea BC and BCE ni kitu kile kile kama CE na AD
BC = Before Christ
BCE = Before the Common Era
CE = Common Era
AD = Anno Domini
Zote hizo zinahusika na kuhesabu miaka. Na uhesabuji wa miaka unaanzia katika kipindi cha kuzaliwa kwa Yesu (CE and AD) zinaongelea jambo lile lile. Lakini kwa sasa wanatumia zaidi CE badala ya AD.
BC na BCE ni jambo lile lile lakini unaanza kuhesabu wakati Yesu alipozaliwa kwa kurudi nyuma. Nikisema 4000BCE ni sawa kabisa na kusema 4000BC. Yaani hesabu miaka 4000 kurudi nyuma baada ya kuzaliwa Yesu.

Sasa ndugu yangu ukisema 5BC huoni ni miaka mitano tu kabla ya kuzaliwa yesu?
TURUDI KWENYE MADA SASA
Wamedi
Hawa watu walianza kutawala maeneo ya ambayo kwa sasa ni Iran, Azerbaijan, Armenia, Georgia na upande wa Mashariki ni Afghanistan na Pakistan. Kutokana na historia inaelezwa kwamba ilianzishwa 675 BC.

Waajemi
Hawa wameanza kujulikana kwa jina hili miaka ya 9th century BCE.
MIMI NAONGELEA NINI SASA?
Ethiopia haina historia ndefu kama ya Iran, kwahiyo siyo sahihi sana kuifananisha Iran na Ethiopia kwa mujibu wa Historia.
Pili niliongeza kuwa Iran civilization haijaanza wakati wa Wamedi. La hasha nimesema kwamba hawa wameanza civilization miaka mingi mno yaani 4000BCE.
Anshan
Hapa niliongelea old civilization ambayo wanahistoria waliweza kuchimba na kuona evidences za civilization. Kwa kutumia carbon 14 waliweza kugundua kuwa archeological kuwa civilization hiyo ni date back 4000 BCE to 1000 BCE


Hii ramani ni kuonesha tu location ya Anshan Civilization.

Kwa sasa naomba niishie hapa kwanza. Nitaweza kuweka taarifa kama kuna maswali zaidi
 
Sidhani kama bara lina tatizo. Afrika Kusini na Misri zipo barani Afrika, lakini angalia zilipo Kiuchumi, ni mbali sana ukizilinganish na nchi nyingi za Afrika.

Africa kusini makaburu bdo wako mkuu nchi inawazungu wakutosha ila na misri wale jamaa ni waarabu ila cjui walifikaje huku [emoji23][emoji23]
 
Haiti achana nao hao ni mizimu inayotembea
Yaani kila nyumba lazima ukute misanamu
Sokoni bidhaa nyingi na wauzaji wengi sana wanauza bidhaa za ushirikina tu hata magari yao yote wameweka voodoo
Wanaamini uchawi sana kuliko dini
Liberia?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…