Kwanini Kila anayefanikiwa lazima aitwe Mwizi, atoa Kafara, Free mason, Tapeli

Kwanini Kila anayefanikiwa lazima aitwe Mwizi, atoa Kafara, Free mason, Tapeli

Mi mtu Mzima Kidogo ambaye nimeishi miongo kadhaa na kushuhudia uongozi wa awamu zote na nimekaa vijijini na mijini

Kwanini Kila mtaa au kijiji au mji mtu akionekana kupata maendeleo watu ukimbilia

1. Mwizi
2. Katoa Kafara
3. Free mason
4. Tapeli

Kwanini uwa wengi hawasujudu nguvu za kazi wanazofanya watu ?

Unakuta kijana mdogo tu anajitahidi analima kisasa zaidi mazao anayataftia soko na kuweza kuuza kwa gredi ya Juu sana! Ila kwasababu ameuza zaidi ya wengine ataambiwa ni Freemason, au anatumia madawa!

Au mtu anafanya biashara yake, amefanya utafiti wa kutosha, amejitosa kwenye ulimwengu wa biashara kwa mtaji huo mdogo au muda Mwingine mikopo ya mabenki, halali usiku kucha lakin ukisikia akianza kufanikiwa kwenye familia wanaangalia Kama kuza zezeta wanasema katolewa Kafara, au ni Tapeli au Mwizi usiku anatumia bunduki kukaba watu!

Tokea Nimezaliwa nimekua nimezaa nimekuza

Kila Tajiri hata mwenye mafanikio ya kawaida tu vijijini unapoishi, watasema ni mwizi , ni Ana chuma ulete, ametoa Kafara, wakati Wengine wamepata Mali tukiwa tunawaona kwa macho yetu kutokana na juhudi zao,

Je hii ni kutokana na uelewa finyu? Ni wivu au ni ujinga??

Nipe maoni yako, na kabla hujatoa maoni chunguza matajiri watano tu kijijini kwenu alafu jaribu kuvuta kumbukumbu uwa wanapewa sifa zipi?

Britanicca
Hakuna utamaduni wa kufanya kazi kwa bidii Tanzania ndo maana.

Watu hawaoni kwamba kufanya kazi kwa bidii kunalipa.

Kwahiyo wanafuatilia habari za watu kuwa matajiri wakubwa na wanawaza utajiri na Range Rover huku hata mfukoni hana senti.
 
Lakini hizo pesa za ufreemason utapeli pia zipo tusikatae japo sio matajiri wote!

Pia hata ukiwa na pesa za njia hizo zilizotajwa kwenye uzi, inahitaji uendelee kujituma na sio uvivu
Pesa za Freemason hazipo ni uongo.

Jaribu kupitia threads humu utajifunza.

Kuna moja inaitwa “Freemasons inside out”

Freemason ni jamii ya watu siyo wachovu. Na hakuna miujiza zaidi ya wao kusaidiana na wanachaguana. Huwezi ingia tu kama unavyoona matapeli wanaweka namba za simu huko mtaani eti kujiunga freemason.
 
Hata hao freemasons, waganga majini wanataka mtu mwenye nyota yake
Sio nyota yako ya kinyesi hupati pesa ng'oo

Hivyo kama utapeli, ufreemason, majini ni rahisi waende na wao tuwaone.
Hakika Ila sasa wasione kila aliyefanikiwa wakadhani ni wa namna Hiyo
 
Pesa za Freemason hazipo ni uongo.

Jaribu kupitia threads humu utajifunza.

Kuna moja inaitwa “Freemasons inside out”

Freemason ni jamii ya watu siyo wachovu. Na hakuna miujiza zaidi ya wao kusaidiana na wanachaguana. Huwezi ingia tu kama unavyoona matapeli wanaweka namba za simu huko mtaani eti kujiunga freemason.
Exactly and Masonic movement started in 1970’s
 
Mengi wamechangia wenzangu hapo juu na baadhi ya sababu wewe pia britanicca umezianisha hapo.

Kikubwa ambacho nilichojifunza, ambacho najifunza na bado naendelea kujifunza ni suala linalohusiana na KUJITAMBUA.

Kujitambua kuna uhusiano mkubwa sana na mambo mengi na yote ambayo yanatokea na kuyaishi katika maisha yetu.

Ukichunguza na kuangalia kwa kina utaona watoto, vijana na watu wazima hawajui utambulisho wao na ukimuuliza swali wewe ni nani? Atakujibu yeye ni ephen_ au yeye ni min -me na pengine atakujibu yeye ni GENTAMYCINE, Mwifwa, raraa reree n.k .n.k

Twende kwenye mada yetu sasa, ili kuweza kujitambua kwanza tunapaswa kutambua na kufahamu identity zetu halisi, je, mimi ni nani? Sisi ni akina nani? Mimi nimetoka wapi? Mimi nilikuwa wapi? Je, kwanini ninaishi? Kuzaliwa kwangu ni kwa bahati Mbaya? Wajibu wangu ni nini katika maisha yangu? Wajibu wangu ni nini katika ulimwengu huu au dunia hii? Je, nimezaliwa ili niteseke? Nimezaliwa ili nisheherekee maisha?

Hayo ni maswali ambayo ili uweze kujitambua na kufahamu utambulisho wako halisi tunapaswa kuwa na ufahamu wa kina na majibu yake kwa ufasaha..

Sifahamu au pengine sina uhakika( nipo tayari kujifunza na kurekebishwa). Watu wengi sana katika ulimwengu huu wamefungwa na wapo katika gereza kwa kutokujua na kujitambua kuhusiana na wao ni nani? Identity ambazo wamekuwa wakijinasibu au kudhani katika fikra zao zimewafanya washindwe kufahamu kabisa life purpose yao au madhumuni ya maisha yao.

Mafundisho mengi hasa ya baadhi ya dini ambazo ni tumejishikiza au kujifunganisha nazo naongelea dini kongwe zimekuwa ndio gereza au jela kubwa ambazo zimekamata na kufunga ufahamu wa watu wengi sana.( nitajitahidi sana kuepuka kuongelea na kugusa Imani zetu kadiri nitakavyoweza katika Uzi huu).

Mafanikio na safari ya kujitambua inaanza kwa kujiuliza na kujihoji maswali mwenyewe na kujiongelesha wewe na wewe na kuongea wewe na wewe, hapa namaanisha ili niweze kufahamu na kupata maswali naongea na mimi na ninafanya majadiliano na mimi mwenyewe kwanza na mara kwa mara.

Katika safari hii ya kujitambua na kufahamu utambulisho wako ni lazima utoe makorokoro na makorokocho yote uliojaziwa au kupewa na kufundishwa katika fikra zako. Hapa una empty kabisa mind yako na unakuwa mjinga, ndio nimesema unakuwa mjinga ili uweze kuruhusu weledi, hekima na werevu kuingia ili uweze kufikia malengo ya kujitambua! Inaitwa ujinga wa werevu ambao ni bora na una manufaa kuliko werevu wa ujinga. Tunapaswa kuwa wajinga wa werevu ili tuweze kupata wisdom au hekima ambayo itakuwa na msaada mkubwa katika safari yetu.

Sasa basi baada ya wewe unaesoma Uzi huu kukubali kwa muda kuwa mjinga wa werevu tunaweza kuendelea, nikiongelea ujinga nafurahi sana ninapokumbuka maneno ya mama FaizaFoxy ; umekwenda shule kusomea ujinga!

Fikra zetu na mawazo yetu yanapokuwa huru bila kujifungamanisha au kujishikiza na chochote ndipo hapo hekima na werevu wa kujua na kutambua utambulisho wako halisi unaupata kutoka ndani mwako na sio kutoka nje, hapa nasema majibu na ufahamu wa wewe ni nani upo tayari ndani yako ila ukishindwa kujua au kutambua kutokana na kuwa gerezani na kutokuwa huru. Hapa Unajikuta unaishi katika upeo huru na unaishi katika uhuru wa nafsi yako.

Mara nyingi na wengi wetu tumekua tukijitambulisha kutokana na jinsi tulivyo, muonekano wetu, kazi zetu, taaluma zetu, makabila yetu, rangi zetu, dini zetu, vyama vyetu, jinsia zetu n.k. n.k! Hapa ninachoweza kusema tumekuwa tukibeba na kungangania fake identity pasipo kufahamu na kutambua madhara na faida ya utambulisho tunaoungangania. Akili zetu au mind zetu zinatuweka katika mtego mkubwa kutukamata na kutuweka gerezani.

Je, mimi nani hasa? Wewe ni nani hasa? Mimi na wewe tunatofauti gani hasa?

Mimi ni ROHO, wewe ni ROHO, mimi na wewe ni ROHO hatuna tofauti.

Kama sisi ni Roho basi ni wazi kuwa sisi tulikuwepo, tupo na tutaendelea kuwepo na sisi hatuna mipaka tupo kila mahali hatuna ukomo wa kufanya chochote na zaidi tumekamilika na hatuna mapungufu kwa chochote! Sisi kama roho ni wakamilifu.

Sisi kama roho hatuhitaji kuomba sababu tunavyo vyote na tunamiliki vyote, vyote vilivyopo ni vya kwetu na vipo chini yetu katika mamlaka yetu.

Sisi kama roho sio tu tuna mamlaka au tumepewa mamlaka bali sisi ni mamlaka kamili inayojitosheleza na hatuhitaji msaada sababu tumekamilika.

Kumbuka tulipo kuwa watoto tuliweza na tulikuwa na mamlaka ya kumiliki chochote kile ndio maana mtoto utamsikia alisema lile ni gari langu na ile ni nyumba yangu! Umiliki unaanzia kutoka kwenye mawazo yetu na fikra zetu.

Mwisho ila sio kwa umuhimu utajiri ni matokeo ya kujitambua na kutumia nguvu na uwezo tulionao kupata, kufanya, kuishi na kumiliki chochote ukitakacho katika ulimwengu huu. Rasilimali zilizopo ulimwenguni ni zetu kwa pamoja na kwa manufaa yetu sote na sio kwa ajili ya wachache.

Ulimwengu umekamilika unatoa chochote kwa yeyote anayehitaji na yupo na mwenye tayari kupokea.

britanicca mkuu wangu, nashukuru kwa mada chokonozi hii. Natumaini itawasaidia na kuwafungua wengi.

Uzi huu ukafungue macho yako ya ndani na ukawe ufunguo wa yote uyatakayo.
Sijajua kwanini Nimetajwa katika huu Uzi.
 
Africa tutakuita mchawi ila ulaya watasema ni mchapa kazi
 
Mi mtu Mzima Kidogo ambaye nimeishi miongo kadhaa na kushuhudia uongozi wa awamu zote na nimekaa vijijini na mijini

Kwanini Kila mtaa au kijiji au mji mtu akionekana kupata maendeleo watu ukimbilia

1. Mwizi
2. Katoa Kafara
3. Free mason
4. Tapeli

Kwanini uwa wengi hawasujudu nguvu za kazi wanazofanya watu ?

Unakuta kijana mdogo tu anajitahidi analima kisasa zaidi mazao anayataftia soko na kuweza kuuza kwa gredi ya Juu sana! Ila kwasababu ameuza zaidi ya wengine ataambiwa ni Freemason, au anatumia madawa!

Au mtu anafanya biashara yake, amefanya utafiti wa kutosha, amejitosa kwenye ulimwengu wa biashara kwa mtaji huo mdogo au muda Mwingine mikopo ya mabenki, halali usiku kucha lakin ukisikia akianza kufanikiwa kwenye familia wanaangalia Kama kuza zezeta wanasema katolewa Kafara, au ni Tapeli au Mwizi usiku anatumia bunduki kukaba watu!

Tokea Nimezaliwa nimekua nimezaa nimekuza

Kila Tajiri hata mwenye mafanikio ya kawaida tu vijijini unapoishi, watasema ni mwizi , ni Ana chuma ulete, ametoa Kafara, wakati Wengine wamepata Mali tukiwa tunawaona kwa macho yetu kutokana na juhudi zao,

Je hii ni kutokana na uelewa finyu? Ni wivu au ni ujinga??

Nipe maoni yako, na kabla hujatoa maoni chunguza matajiri watano tu kijijini kwenu alafu jaribu kuvuta kumbukumbu uwa wanapewa sifa zipi?

Britanicca
asilimia kubwa ya utajiri si halali
hata akina ronaldo utasikia wamekwepa kodi
 
Sijajua kwanini Nimetajwa katika huu Uzi.
x.jpg
 
Mi mtu Mzima Kidogo ambaye nimeishi miongo kadhaa na kushuhudia uongozi wa awamu zote na nimekaa vijijini na mijini

Kwanini Kila mtaa au kijiji au mji mtu akionekana kupata maendeleo watu ukimbilia

1. Mwizi
2. Katoa Kafara
3. Free mason
4. Tapeli

Kwanini uwa wengi hawasujudu nguvu za kazi wanazofanya watu ?

Unakuta kijana mdogo tu anajitahidi analima kisasa zaidi mazao anayataftia soko na kuweza kuuza kwa gredi ya Juu sana! Ila kwasababu ameuza zaidi ya wengine ataambiwa ni Freemason, au anatumia madawa!

Au mtu anafanya biashara yake, amefanya utafiti wa kutosha, amejitosa kwenye ulimwengu wa biashara kwa mtaji huo mdogo au muda Mwingine mikopo ya mabenki, halali usiku kucha lakin ukisikia akianza kufanikiwa kwenye familia wanaangalia Kama kuza zezeta wanasema katolewa Kafara, au ni Tapeli au Mwizi usiku anatumia bunduki kukaba watu!

Tokea Nimezaliwa nimekua nimezaa nimekuza

Kila Tajiri hata mwenye mafanikio ya kawaida tu vijijini unapoishi, watasema ni mwizi , ni Ana chuma ulete, ametoa Kafara, wakati Wengine wamepata Mali tukiwa tunawaona kwa macho yetu kutokana na juhudi zao,

Je hii ni kutokana na uelewa finyu? Ni wivu au ni ujinga??

Nipe maoni yako, na kabla hujatoa maoni chunguza matajiri watano tu kijijini kwenu alafu jaribu kuvuta kumbukumbu uwa wanapewa sifa zipi?

Britanicca
MKuu kupata Kila mtu anapata utajiri au maisha fulani Kwa juhudi binafsi!

Ishu inakuja baada ya kupata Nini kinakupata!!

Bila kukwepa kodi vizuri au kuwa mjanja mjanja kibongo bongo hutoboi coz mifumo ya kodi imekaa kinyonyaji sana kuliko uhalisia was kipato husika!!
Ndio maana mkwepa Kodi huitwa mwizi!

Matajiri wanajipendenkeza Kwa wanasiasa Ili kukwepa panga la Kodi na kupata favor!!

Lakini kumbuka kupata jiwe la kweli lazima upandishe viwango vya kujitolea binafsi au kivingine,au magendo!huwezi tajirika kihalali kimfumo ni ngumu sana labda uwe na connection!!!

Kama unabisha wewe ni mtu wa mfumo hebu fuatilia ishu ya yule "Rama was kariakoo alijipiga risasi"utajua hujui!

Juhudi bila baraka za Dola na mfumo inakula kwako peupe kabisa Wala sio utani!!
 
Back
Top Bottom