Kwanini kila ikifika Mwaka mmoja kabla ya Uchaguzi Lazima kutokee Mikwaruzano Ya Kisiasa CHADEMA Ya FAM Hii ndo SIRI ILIYOJIFICHA

Kwanini kila ikifika Mwaka mmoja kabla ya Uchaguzi Lazima kutokee Mikwaruzano Ya Kisiasa CHADEMA Ya FAM Hii ndo SIRI ILIYOJIFICHA

DR Mambo Jambo

JF-Expert Member
Joined
May 10, 2012
Posts
11,622
Reaction score
26,005
Kiistoria, kila unapobaki mwaka mmoja au miwili kuelekea uchaguzi mkuu wa rais na wabunge nchini, ndani ya chadema kunaibuka minyukano.

Hii ilikuwa kweli mwaka 2008 na 2009, kuelekea uchaguzi mkuu wa 2010

Na Ikawa kweli 2013 na 2014, kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka 2015

Na sasa ni kweli pia mwaka huu ukiwa umebaki mwaka mmoja tu kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka 2025, tunaona minyukano

Mwaka 2008 Aliyekuwa makamu mwenyekiti wa Chadema taifa, na mbunge wa Tarime, marehemu Chacha wangwe anatoa waraka fulani kwenda kwa wanachama wote ndani ya chama chao.

Ndani ya waraka ule, Wangwe anaeleza nia yake ya kugombea uenyekiti wa Chama hicho huku akianisha sababu...

Sababu ya kwanza ya Wangwe ni kuhusu matumizi mabaya ya ruzuku.

Ifahamike kuwa kipindi hicho chama hicho kilikuwa kikipokea ruzuku ya milioni 66 kwa mwezi

Wangwe akaeleza matumizi ya ruzuku ile hayakuwa na uwazi wala baraka za vikao vya chama.

Na Kuwa Mbowe aliwaambia wajumbe wenzake kuwa, kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka 2005, alikikopesha chama hicho kiasi cha dola za Marekani 181,949 (sawa na mil 218 wakati ule)

Kuwa hadi mwaka 2008, chama kilishamlipa Mbowe milioni 175
Lakini Wangwe akatia mashaka kwenye hili..

Wangwe alihoji akaunti ipi ya chama iliingiziwa pesa hizo?

Kwa hundi ipi? Tarehe gani?

Na Kwa vikao vipi vya chama vilivyotathmini na kuupitisha mkopo ule?

Wangwe akahoji mbona wao huingia gharama majimboni mwao na hawajakidai chama?

Ukiachana na hoja hii, Wangwe alitoa sababu nyingine zilizomsukuma kugombea uenyekiti

Upendeleo kwenye uteuzi wa wabunge wa viti maalumu na ajira za watumishi wa chama, na uongozi wa kibabe.

Baada ya waraka huu, Wangwe akashukiwa kama tai na kamati kuu ya Chadema

Wangwe aliishia kuvuliwa cheo na uanachama wa chama chake kwa tuhuma kuwa anatumiwa na mfumo kuiba siri za chama na kuzivujisha.

Siku chache baadae, Wangwe akafa kwa ajali mbaya maeneo ya Pandamili akitokea Dodoma kwenda Dar Es Salaam

Huku dereva wake Deus Mallya akinusurika..

Huo ukawa ndio mwisho wa ndoto ya Wangwe kuukwaa uenyekiti Chadema.

Mwaka 2009, aliyekuwa mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Zuber Kabwe naye akatangaza kutamani "kiti cha enzi"

Ikafata minyukano ndani kwa ndani ambayo ilitulizwa

Ukafanyika uchaguzi mkuu mwaka 2010

Baada ya uchaguzi wa 2010, mambo hayakuwa tena sawa baina na Mwenyekiti Mbowe na Naibu katibu mkuu wa chama hicho (bara) ndugu Zitto Kabwe

Zitto akashutumiwa kuwa ni mtu wa mfumo

Gazeti moja likaandika jinsi Zitto alivyokuwa akiwasiliana sana na afisa usalama taifa Jack Zoka.

Ilidaiwa kuwa wakati wote wa kipindi cha uchaguzi mkuu 2010, Zitto alikuwa akiwasiliana mara nyingi sana na aliyekuwa naibu Mkurugenzi wa Usalama wa taifa Bw. Jack Zoka

Akatuhumiwa kuwa mawasiliano yale yalikuwa ni ya kukiuza chama chake wakati wa uchaguzi..

Zitto aliendelea kuwa kimya bila kujibu tuhuma zozote alizorushuwa.

Nachelea kusema alikuwa kimya huku nyuma ya pazia akiratibu mipango kabambe

Haya yalikuja kuthibitika mwaka 2012 baada ya wanachama vijana wa chama hicho kuanza kuvuana nguo hadharani.

Kwa mujibu wa Ben Saanane Ben Saanane
aliyekuwa msaidizi wa Mbowe, alieleza juu ya kuanzishwa kisiri kwa kundi la PM 7 ndani ya chama hicho

Kundi hili ambalo mwanzoni lilijiita Patriotic Movement liliundwa na watu 7

Tuwajue kwa uchache wao!
  1. Juliana Shonza,makamu mwenyekiti BAVICHA
  2. Habib Mchange
  3. Mtela Mwampamba(Jiwe alimtumbua kisa Jokate)
  4. Festo Sanga (Mbunge wa sasa Njombe)
  5. Exaud Mamuya
  6. Gwakisa Burton
  7. Ben Saanane

Mwenyekiti wa kundi hili alikuwa Juliana Shonza huku makamu akiwa ni Habib Mchange..

Kwa mujibu tena wa Ben Saanane, malengo ya kikundi hiki yakahama kutoka kwenye kuwajengea vijana uwezo kisiasa hadi kugeuka kuwa Pindua Mbowe 7

Kuwa wafadhili wao walikuwa ni David Kafulila, Mwigulu Nchemba, Deo Filikunjombe na Hussein Bashe

Bila kujua Ben Saanane ni pandikizi

20241222_091944.jpg


Ben Saanane anadai kundi hili lilikuwa likifanya vikao kwa baraka za Zitto Kabwe na Kitila Mkumbo na wakaamua kujiita majina ya uficho wawasilianapo
  • Shonza akajiita Benazir
  • Mchange akajiita Mdude
  • Mwampamba akajiita Kony
  • Sanga akajiita Tuntemeke
  • Zitto akajiita Prezzo

INAENDELEA HAPA

 
Kiistoria, kila unapobaki mwaka mmoja au miwili kuelekea uchaguzi mkuu wa rais na wabunge nchini, ndani ya chadema kunaibuka minyukano.

Hii ilikuwa kweli mwaka 2008 na 2009, kuelekea uchaguzi mkuu wa 2010

Na Ikawa kweli 2013 na 2014, kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka 2015

Na sasa ni kweli pia mwaka huu ukiwa umebaki mwaka mmoja tu kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka 2025, tunaona minyukano

Mwaka 2008 Aliyekuwa makamu mwenyekiti wa Chadema taifa, na mbunge wa Tarime, marehemu Chacha wangwe anatoa waraka fulani kwenda kwa wanachama wote ndani ya chama chao.

Ndani ya waraka ule, Wangwe anaeleza nia yake ya kugombea uenyekiti wa Chama hicho huku akianisha sababu...

Sababu ya kwanza ya Wangwe ni kuhusu matumizi mabaya ya ruzuku.

Ifahamike kuwa kipindi hicho chama hicho kilikuwa kikipokea ruzuku ya milioni 66 kwa mwezi

Wangwe akaeleza matumizi ya ruzuku ile hayakuwa na uwazi wala baraka za vikao vya chama.

Na Kuwa Mbowe aliwaambia wajumbe wenzake kuwa, kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka 2005, alikikopesha chama hicho kiasi cha dola za Marekani 181,949 (sawa na mil 218 wakati ule)

Kuwa hadi mwaka 2008, chama kilishamlipa Mbowe milioni 175
Lakini Wangwe akatia mashaka kwenye hili..

Wangwe alihoji akaunti ipi ya chama iliingiziwa pesa hizo?

Kwa hundi ipi? Tarehe gani?

Na Kwa vikao vipi vya chama vilivyotathmini na kuupitisha mkopo ule?

Wangwe akahoji mbona wao huingia gharama majimboni mwao na hawajakidai chama?

Ukiachana na hoja hii, Wangwe alitoa sababu nyingine zilizomsukuma kugombea uenyekiti

Upendeleo kwenye uteuzi wa wabunge wa viti maalumu na ajira za watumishi wa chama, na uongozi wa kibabe.

Baada ya waraka huu, Wangwe akashukiwa kama tai na kamati kuu ya Chadema

Wangwe aliishia kuvuliwa cheo na uanachama wa chama chake kwa tuhuma kuwa anatumiwa na mfumo kuiba siri za chama na kuzivujisha.

Siku chache baadae, Wangwe akafa kwa ajali mbaya maeneo ya Pandamili akitokea Dodoma kwenda Dar Es Salaam

Huku dereva wake Deus Mallya akinusurika..

Huo ukawa ndio mwisho wa ndoto ya Wangwe kuukwaa uenyekiti Chadema.

Mwaka 2009, aliyekuwa mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Zuber Kabwe naye akatangaza kutamani "kiti cha enzi"

Ikafata minyukano ndani kwa ndani ambayo ilitulizwa

Ukafanyika uchaguzi mkuu mwaka 2010

Baada ya uchaguzi wa 2010, mambo hayakuwa tena sawa baina na Mwenyekiti Mbowe na Naibu katibu mkuu wa chama hicho (bara) ndugu Zitto Kabwe

Zitto akashutumiwa kuwa ni mtu wa mfumo

Gazeti moja likaandika jinsi Zitto alivyokuwa akiwasiliana sana na afisa usalama taifa Jack Zoka.

Ilidaiwa kuwa wakati wote wa kipindi cha uchaguzi mkuu 2010, Zitto alikuwa akiwasiliana mara nyingi sana na aliyekuwa naibu Mkurugenzi wa Usalama wa taifa Bw. Jack Zoka

Akatuhumiwa kuwa mawasiliano yale yalikuwa ni ya kukiuza chama chake wakati wa uchaguzi..

Zitto aliendelea kuwa kimya bila kujibu tuhuma zozote alizorushuwa.

Nachelea kusema alikuwa kimya huku nyuma ya pazia akiratibu mipango kabambe

Haya yalikuja kuthibitika mwaka 2012 baada ya wanachama vijana wa chama hicho kuanza kuvuana nguo hadharani.

Kwa mujibu wa Ben Saanane Ben Saanane
aliyekuwa msaidizi wa Mbowe, alieleza juu ya kuanzishwa kisiri kwa kundi la PM 7 ndani ya chama hicho

Kundi hili ambalo mwanzoni lilijiita Patriotic Movement liliundwa na watu 7

Tuwajue kwa uchache wao!
  1. Juliana Shonza,makamu mwenyekiti BAVICHA
  2. Habib Mchange
  3. Mtela Mwampamba(Jiwe alimtumbua kisa Jokate)
  4. Festo Sanga (Mbunge wa sasa Njombe)
  5. Exaud Mamuya
  6. Gwakisa Burton
  7. Ben Saanane

Mwenyekiti wa kundi hili alikuwa Juliana Shonza huku makamu akiwa ni Habib Mchange..

Kwa mujibu tena wa Ben Saanane, malengo ya kikundi hiki yakahama kutoka kwenye kuwajengea vijana uwezo kisiasa hadi kugeuka kuwa Pindua Mbowe 7

Kuwa wafadhili wao walikuwa ni David Kafulila, Mwigulu Nchemba, Deo Filikunjombe na Hussein Bashe

Bila kujua Ben Saanane ni pandikizi

View attachment 3182204

Ben Saanane anadai kundi hili lilikuwa likifanya vikao kwa baraka za Zitto Kabwe na Kitila Mkumbo na wakaamua kujiita majina ya uficho wawasilianapo
  • Shonza akajiita Benazir
  • Mchange akajiita Mdude
  • Mwampamba akajiita Kony
  • Sanga akajiita Tuntemeke
  • Zitto akajiita Prezzo

INAENDELEA...


Tunakusubiri uchambuzi umekaa vizuri .
 
Ben Saanane akawa akiripoti kila mkakati wa kundi hili kwa Mwenyekiti Mbowe

Kutokana na hili, kundi hili likafanya kikao Pacific Hotel maeneo ya Manzese na ikatolewa hoja waende kwa mganga kula viapo vya uaminifu.

Mambo yakatibuka ilipoingia hoja ya sumu.

Ilidaiwa kuwa, kwenye moja ya kikao kilichofanyikia Lunch time Hotel maeneo ya External, Ben Saanane akiwa amelewa huku akitoa bahasha ili atoe pesa alipe bili, akaangusha kifuko chenye unga mwekundu kutoka kwenye bahasha hiyo.

Kuwa Mwampamba aliokota kifuko hicho na kumuuliza Saanane kile ni nini?

Saanane akajibu ni ugoro tu anaotumia

Mwampamba akagoma kumrudishia Saanane kifuko kile na akaondoka haraka pale kikaoni

Kesho yake asubuhi, Ben akaenda Temeke kwa Mwampamba kumuomba kifuko kile

Kwa jinsi walivyozidi kuvuana nguo vijana hawa ikadaiwa kuwa Ben Saanane aliungama kuwa kifuko kile kilikuwa na sumu aliyotumwa kumuwekea Zitto endapo angetokea kikaoni.

Kwa mujibu wa Shonza ni kuwa Zitto alisafiri kwenda Marekani hivyo kushindwa kufika kwenye kikao kile.

Wakati haya yanaendelea, likasambaa chapisho moja mtandaoni likielezea mienendo ya kiamala aliyokuwa akipokea Zitto na kisha kuwatumia vijana wa PM 7

Haya yote yanaweza kuelezewa na kisa kifuatacho katika zile harakati za vijana "kuanikana"

Ilikuwa hivi👇
20241222_092353.jpg

20241222_092356.jpg

Tangu mwaka 2008 mwenendo wa kisiasa wa Zitto Zuber Kabwe ulianza kutiliwa shaka na wanachama wa CHADEMA ndani na nje ya chama.

Hili lilipelekea kuibuka maneno ya chini kwa chini kuwa anakisaliti chama.

Hali hiyo ililazimu timu ya kijasusi ya chama hicho kuanza kufuatilia nyendo zake kwa ukaribu zaidi usiku na mchana ili kujiridhisha pasipo kuacha chembe ya mashaka.

Bila kusita timu ya ujasusi ilianza kazi rasmi ya ujasusi dhidi ya nyendo zote za Zitto Zuberi Kabwe
Scope ya uchunguzi ikawa ni:

1. Kumfuatilia yeye binafsi nyendo zake.
2. Kufuatilia mawasiliano yake ya simu.
3. Kufuatilia mawasiliano yake ya barua pepe.
4. Kufuatilia pato lake nje ya kazi zake halali za kibunge.

Yafuatayo, ndiyo yalidaiwa kuwa majibu yaliyopatikana..

Mnamo Jumatatu ya tarehe 16/6/2008 saa 09:46 asubuhi, Mh Zitto Kabwe kupitia simu yake ya kiganjani namba +255754787550 alipokea simu kutoka kwa Ramadhani Ighondu mwenye namba +255717760473 ambaye alikuwa ni afisa Usalama wa Taifa anayefanya kazi ikulu.

20241222_092933.jpg

20241222_092935.jpg


Rama alijitambulisha kuwa yeye ni Usalama wa Taifa na ametumwa na mkuu wake wa kazi.

Maelezo ya msingi katika simu hii ilikuwa ni bwana Rama kuomba miadi ya kuonana kutokana na agizo la mkuu wake wa kazi.

Siku sita baadae yaani Jumatatu ya tarehe 23/6/2008 saa 07:52 asubuhi, Zitto alipigiwa tena simu na Rama akimkumbusha maongezi waliyofanya siku 6 zilizopita na kumuomba siku hiyo jioni waonane.

Taarifa inadai ingawa Zitto alionekana kusita kidogo lakini baadae alikubali.

20241222_093059.jpg

Wakakubaliana wakutane Sea Cliff Hotel.

Ilipofika jioni ya siku hiyo Zitto akiwa na marafiki zake wawili Omar Lyasa na Abdalah Said walifika Sea Cliff Hotel wakaketi na kuagiza vinywaji.

Baada ya kama dakika kumi hivi, Zitto alipokea simu ikimuelekeza alipo bwana Rama

Zitto akawaambia marafiki zake wamsubiri kidogo, akaondoka kuelekea alikoelekezwa

Kuna Mengi yako Nyuma ya Pazia ila Mbowe Anaweza Kuwa Muhusika wa Mambo mengi sirini..

Lissu kachukua fomu kugombea uenyekiti Chadema huku Mbowe naye akidai "kulazimishwa" kugombea

Huu ni mtiririko wa simulizi Hatari sana

unajua hata Lema alivyopora laptop kikaoni yenye waraka Mzito.?
Kuna Vingi Vitaonekana mwaka Huu Unaokuja baada ya Lissu Kushindwa Mambo yatakuwa Wazi tusubiri
 
Jana niliandika Uzi, nikitaka LISSU asikae kimya, Kwa kuhofia kupasuka chama, chama kilishapasuka,

Yeye amlipue FAM tu Kwa SHAHIDI na Hoja

 
Wanasiasa wote ni wezi na wachumia tumbo

Familia zao ndio kipaumbele

Leo hakuna anayejua mtoto wa soka,Ben saanane wanakula nini

Vijana wanatumika kama makarai ,ndio maana kina mdee na kundi lake waligoma kuachia ubunge maana wanajuana wote ni walafi, ile ilikuwa wote tukose,
 
Vidagaa vinatiliwa shaka kuwa ni watu wa mfumo, halafu papa lenyewe la mfumo linaendelea kudunda na kutafuna fedha za chama bila wenzake kujua.

Duniani ukiwa mjanja plus hela mfukoni kwako. Unaweza kufanya lolote ikiwepo kutengeneza mazingira ya kuabudiwa kama anavyoabudiwa mwenyekiti na chawa wake.
 
Ipitishwe sheria.kuwa mshahara wa raisi uwe m2.wabunge laki5(bila posho).
Utaona wote watageukia biashara na kilimo.....hakuna ambaye hapiganii masrai yake na familia yake kwanza,wanaona ugumu ulivyo kwenye kujiajiri na ajira kulivyo kugumu.
 
Back
Top Bottom