Kwanini Kituo cha mafuta 'Rupeez Oil' kimejengwa kwenye hifadhi ya barabara Kimara Stop Over?

Wenyewe kwa wenyewe wazee wa feva
 
Yaleyaleeeeee!!!
Nimeshangaa sana kuona hicho kituo nikahisi kuna mnene ameiweka serikali mfukoni
 
UKIONA HIVYO NI CHA KIONGOZI ndani ya CHAMA DOLA
 
Upo utaratibu unapanga kwa tanroad unawalipa wao.
Hivo vituo vyte unaona vimesimama wameshindwa masharti.
Mfano hai cha SuCa kile. Mmiliki alikua bwana mmoja judge wa zamani kidogo, yeye inaonekana kagoma kupanga maana eneo ni lake long time. Hawezi panga na kufawana mzgo na tanroad. Wapo wa temboni. Wapo ambao wao wameona potelea pote. Wapo walioona wanunue maeneo wajenge nje ya hifadhi mfano ni stopover upande wa pili na kwamsuguri.. rupees hawajawa na presha ya masharti.
 

Inasemekana ni ya kiongozi anayekaimu mambo ya ardhi nchini ndo maana Inajengwa kwa kasi ya 5g na kuna sheli nyingine kwa nyuma yake ndo ilianza ila nashangaaa inasuasua ila huyo wa apo barabarani anakimbia hatari
 
Yule amepanga eneo la Tanroad kwa muda fulani, anawalipa Tanroad hela, siku wakitaka tumia eneo anapewa notice anaondoka bila kudai chochote
Ok kumbe Tanroads wanaweza pangisha eneo la barabara, asante kwa ufafanuzi mkuu. Ila sidhani kama na wale wengine wenye vituo wangekubali kuvifunga na kuacha magofu kama kweli Tanroads wanayo hiyo option unless Tanroads nao wamekula mchongo kuwabagua wengine . Bado inafikirisha
 
Ok kama walipewa hayo masharti wakashindwa hapo ni sawa
 
Tumesitisha vibali vipya vya ujenzi wa sheli.
 
Acha watu wafanye Kazi Ni Upumbavu unajua Ni mafundi wangapi na Mama ntilie wangapi wanapata Maisha happy?
hapa ndipo waafrika huwa tunaonekana ubongo wetu una shida(ni sokwe aliyechangamka tu)
Mtu amehoji inakuwaje eneo la serikali ambalo watu walivunjiwa nyumba zao kutokana na kuwa ndani ya hifadhi ya barabara,leo hii mtu anakuja kujenga kituo cha mafuta eneo hilo,wakati ,vituo vyote vilivyopo mbele ya eneo hilo,vilivunjwa,na vilivyobakia vimefungwa.Mtu anahojo hiyo double standard itnatokea wapi,labda kama kingekuwa ni cha serikali.
 
kama sio mpita njia wa eneo hilo,lazima utasema ni umbeya,lakini tunaopita hapo, tunajua ni kweli,na mimi nilihisi labda ni cha serikali.
Sasa unafikiri kila mtu Jf anakaa Dar. Mwambie aweke vielelezo
 
Tumetoka wamu ya tano, tuko awamu ya nne sasa.
 
Kwa sasa eneo hilo lipo ndani ya himaya ya tanroad, ukitaka kufanya biashara eneo hilo hata wewe unaweza, kiufupi unatakiwa kulipia kwao, pia utalipia na watu wa maegesho ya magari ili wateja wako wasisumbuliwe parking fee.
 
Sasa unafikiri kila mtu Jf anakaa Dar. Mwambie aweke vielelezo
inshu sio kuishi dar,unaweza kuishi dar,lakini ukawa sehemu hiyo hujaiona.Kwani hapa ni mahakamani kila kitu kiwe na kielelezo?!!sio kila habari lazima iwe na picha.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…