Kwanini maeneo ya jeshi kama Lugalo na External kumejengwa bar na frame nyingi sana?

Kwanini maeneo ya jeshi kama Lugalo na External kumejengwa bar na frame nyingi sana?

Mkuu Commando huwa naona beret zao ni maroon hao wenye beret nyeusi ni special forces wa Navy, halafu kwenye kamandi tano za jeshi hakuna Commando hawa wanaweza kuwa kwenye kamandi yoyote ile ni kama ma MP ambao wao beret zao ni nyekundu, pia umesahau kamandi ya Makao Makuu ambao nao beret na uniform zao zinafanana rangi na kamandi ya Land (Infantry)
Ukiangalia beret za Commandos wa Navy zina ufanano na beret za Commandos wa Infantry. Sijajuwa kwanini?
 

Mkuu kwamba hata hawa wenye vyeo vikubwa vikubwa na wamepiga beret nyekundu na damu ya mzee ni MP's? (ukiacha hao wadada wawili)...

Nilikuwa najua MP's huwa hawafikii cheo cha kuvaa kwenye mabega nyota moja na kuendelea...

1703274358-PANGAWE.jpeg
 
Wakuu ikipita barabara ya external kwenda maji chumvi unapita eneo la jeshi, limejaa bar na frame.

Hali iko hivyo ukipita Lugalo, kumefunguliwa frames nyingi sana kwenye eneo la jeshi.

Swali, je, jeshi letu limeona uwekezaji pekee wanaweza kufanya kwenye maeneo yao ni kufungua bar na frame tu?

Jeshi letu lina maeneo potential sana, mazuri ambayo wangeweza kualika wawekezaji wakubwa wa kujenga shopping centres ama malls, recreational centers, na uwekezaji mkubwa kuliko huu wa bar na frame.

Je jeshi letu limekosa washauri wazuri wa uwekezaji wa ndani ama hata wa nje hadi kuwekeza kwenye bar na frame?
Mwanajeshi ni chakula cha risasi, hana sababu ya kuweka mshahara benki.
 
Tabata imeamia sana maji chumvi na
Hapo mwisho najua umeishi eneo hilo,nini kinaendelea hapo?
hapa kati kuingia bima. Ndio maana watu binafsi wameamua kuwekeza eneo hilo. Kama ujenzi uliofanyika makoka
 
Wamewekeza kwenye sekta nyingi nyingi tu mpaka usafi, afya, ujenzi ulinzi nk kupitia kitengo chao cha SUMA JKT
Fremu hizo pia zimejengwa Kigamboni ferry
Wanastahili pongezi kwa mafanikio haya na kuongeza ajira kwa vijana na wataalamu wetu

Sent using Jamii Forums mobile app
uchumi wa fremu kaka mkubwa ndio wa kustahili pongezi? hiyo ni taasisi kubwa hiyo ilipaswa kuleta mageuzi kwenye macroeconomics.
 
Wakuu ikipita barabara ya external kwenda maji chumvi unapita eneo la jeshi, limejaa bar na frame.

Hali iko hivyo ukipita Lugalo, kumefunguliwa frames nyingi sana kwenye eneo la jeshi.

Swali, je, jeshi letu limeona uwekezaji pekee wanaweza kufanya kwenye maeneo yao ni kufungua bar na frame tu?

Jeshi letu lina maeneo potential sana, mazuri ambayo wangeweza kualika wawekezaji wakubwa wa kujenga shopping centres ama malls, recreational centers, na uwekezaji mkubwa kuliko huu wa bar na frame.

Je jeshi letu limekosa washauri wazuri wa uwekezaji wa ndani ama hata wa nje hadi kuwekeza kwenye bar na frame?
kuanza kutumia maeneo ya jeshi kama maeneo ya biashara na maeneo ya kustaarehe kujitafutia vipato hovyo vya kodi ni umasikini mkubwa kwa jeshi

what a shame

yaani jesho limegeuka kampuni ya real estate kujitafutia vijihela.?

aibu sana kwa serikali na jeshi
 
Hivi Suma JKT ipo chini ya JWTZ au JKT?

Suma ipo chini ya JKT
Kumbuka JKT ni Taasisi imekamilika chini ya Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa.

Hata hivyo muingiliano wa JKT na JWTZ ni mkubwa kifupi ni mtu na mdogo wake wa tumbo moja. Ranks ni zile zile isipokuwa JKT ni junior institution hata top management yake haitakiwi kuizidi JWTZ

Najua kwa uchache tu
 
Ukiangalia beret za Commandos wa Navy zina ufanano na beret za Commandos wa Infantry. Sijajuwa kwanini?
Nafikiri hao wenye beret nyeusi watakuwa ni other special forces kwenye kamandi nyinginezo, lakini special forces wenyewe wale commando wenye insignia ya bawa, beret zao ni za maroon na wengi wao wako kule 92 KJ Ngerengere Air Force Base
 
Nafikiri hao wenye beret nyeusi watakuwa ni other special forces kwenye kamandi nyinginezo, lakini special forces wenyewe wale commando wenye insignia ya bawa, beret zao ni za maroon na wengi wao wako kule 92 KJ Ngerengere Air Force Base

beret nyeusi ni vikosi vya Mizinga
 
Jeshi linatakiwa liondoke maeneo ya mjini yabaki kujengwa majengo ya kiraia. Kama upo umuhimu, basi mjini yabaki maeneo machache na madogo tu kwa ajili yao. Nashangaa jiji kama Dar wamejaza mi-kambi mi-kukubwa ya jeshi. Ya kazi gani?
Tuseme tu ukweli rain ndo tumewafuata jeshi.baada ya population ya watu kuwa kubwa. Wakati jeshi wanachukua hayo maeneo dar.hakuna aliyejua kungekuja kuwa hivi.
 
Jeshi linatakiwa liondoke maeneo ya mjini yabaki kujengwa majengo ya kiraia. Kama upo umuhimu, basi mjini yabaki maeneo machache na madogo tu kwa ajili yao. Nashangaa jiji kama Dar wamejaza mi-kambi mi-kukubwa ya jeshi. Ya kazi gani?
Nadhan ni ngumu Sana
Miaka ya 90 kuna eneo kubwa Sanaa la jeshi ukimaliza tu viwanda vya bakhresa(vikindu) hii ilikuwa mkoa wa peanut by then...ila SASA ni dar na watu wamejazana balaa...hivyo huko unasema nje ya mji after few years kutakuwa katikat ya mji tena
 
Duuh mjomba kwamba hadi leo humfahamu CDF wa jeshi la nchi yako nani, hajamuongelea Makonda amemuongelea Jacob Mkunda ambaye ni CDF wa JWTZ, halafu yeye kaandika kaka wewe hiyo baba sijui umeitoa wapi
Mkuu wapi mimi nimemwongelea Makonda?
 
Kwa kweli inashangaza sana

Eneo la jeshi sabasaba imegeuka kuwa parking ya malori

Eneo la jeshi Mbagala Zakiem limegeuka kuwa parking za Gali na kwandani kule Kuna Bar kibao

Alafu serikali inajenga hospital ya Zakiem katika kaeneo kadogo wakati maeneo ya serikali yapo watu wameweka Bar wanalewa tu
 
Yes, Viettel (Halotel Tanzania) inamilikiwa na Wizara ya Ulinzi ya Vietnam lakini mwanzo wake haikuanzishwa na serikali yao au jeshi lao bali ilirithishwa tu kwa wizara ya ulinzi...

Tambua pia uwekezaji wa kwenye sekta ya mawasiliano si sawa na kujenga fremu na bar...
Duuuh ndo najua hili.

Viettel, hili neno lilisoma badala ya halotel kwa week nzima, hadi nilichachawa, line angu imekuajee? Niliogopaa.

Kumbe ndo wenye mtandao wao, ahsante kwa somo.
 
Duuuh ndo najua hili.

Viettel, hili neno lilisoma badala ya halotel kwa week nzima, hadi nilichachawa, line angu imekuajee? Niliogopaa.

Kumbe ndo wenye mtandao wao, ahsante kwa somo.

😄😄😄

Pole sana, Viettel ni group na Halotel Tanzania ni subsidiary (jina jingine wanatumia kama Viettel Tanzania PLC) ambao wamepewa leseni na TCRA kufanya biashara TZ...
 
Back
Top Bottom