Kwanini mitume na manabii huishiwa upako baada ya muda? Je, hizi pako zao ni za kweli au za mchongo?

Kwanini mitume na manabii huishiwa upako baada ya muda? Je, hizi pako zao ni za kweli au za mchongo?

Kakobe alikua anaombea vilema wanapona lakin siyo vilema unao waona mtaani vilema wote huwa ni wageni wanakuja nae
🤣🤣😂😂Anakuja Nao Yeye Mwenyewe
Haendi MtaAni Kuwaombea Anajua Ataaibika
 
Jambo wadau?​

Naingia kwenye mada moja kwa moja pasipo kuwachosha na maneno mengi. Kwa muda mrefu sasa nimekuwa nikifuatilia upako wa manabii na mitume jinsi wanavyoanza huduma zao kwa pako za hali ya juu sana lakini baada ya muda zile pako huanza kufifia taratibu na kuisha kabisa. Nabaki najiuliza maswali kadhaa yasiyokuwa na majibu:
  1. Kwanini pako za hawa manabii zinapanda na kushuka ghafla kiasi hiki?
  2. Je, hizi pako ni za kweli au ni za mchongo?
  3. Kama ni za kweli kwanini zinaisha na kama ni za mchongo kwanini zikiisha wasirudi tena kuchukua nyingine kule wanakozitoa?
Yaani najiuliza maswali mengi bila majibu. Ndipo nikaamua kuanzisha huu uzi kwa kuwa humu JF kuna wabobevu wa masuala ya theology akina Mshana Jr wanaweza kutusaidia kujibu baadhi ya maswali haya.

Hebu jaribu kufikiria nguvu za upako alizokuwa nazo Askofu Kakobe enzi zile anafungua kanisa lake la Full Gospel Bible Fellowship (FGBF) halafu ulinganishe na hali aliyo nayo sasa hivi utagundua kuna kitu hakiko sawa. Si huyu tu bali walikuwepo Mitume na Manabii wengi hapa nchini wakiwemo Mzee wa Upako, Mch Antony Lusekelo ukiangalia jinsi alivyokuwa akikusanya mtiti na mabasi yake kila kona ya nchi halafu leo ukienda kule kanisani kwake unakuta mabasi yote yamepaki unabaki unashangaa. Hapa lazima kuna tatizo sio bure.

Ukitoka kwa hawa wawili njoo kwa Mtume Mwingira na Mtume Gwajima ujiulize zile nguvu walizokuwa nazo zamani zilipotelea wapi hadi sasa wamebaki na waumini wa kuungaunga. Tatizo ni nini hasa?

Manabii na mitume waliovuma siku za nyuma na kupotea kimuujiza ni wengi lakini nimetoa mifano ya hawa wachache kama msingi wa kujenga hoja yangu. Sasa hivi Mtume Mwamposa ndiye yupo juu lakini naye atakuja kuporomoka baada ya muda mfupi.

Njooni wajuzi wote tujadiliane hili jambo mpaka tupate jawabu la pamoja.

Nawasilisha.​

Nguvu zao ni za muda tu. Wanatoa kafara.
 
Hata nyakati hizo walikuwa wanakuja na kupita wao sio Mungu kwamba wadumu milele
Alikuwepo Eliya akaja Elisha na kuendelea

Anaongelea kuwa wapo hai lakini hawana nguvu Tena. Eliya na Elisha walipokezana.
 
Gwajima sio mtume, na bado yupoyupo sana, Mwingira anamiliki shekeli za kutosha, makanisa kila Kona, benki, mashamba, kimsingi ana mihela, Kakobe serikali ilimtapeli mabilioni yake halafu wakampelekea mamluki wampindue!!! wa upako umesema magari yamesimama yote duh, hii sijui

Yeye anazungumzia nguvu wewe unaongelea pesa. Pesa wanazo je nguvu za mwanzo bado zipo?
 
HAKUNA MTUME MJINI NI UONGO.
HAWAJUI MAANA YA MTUME.
MTUME HANA KANISA KAZI YAKE NI KUANZISHA KANISA NA KUMWACHIA MCHUNGAJI NA MWALIMU.

Mtume ni mfyeka pori yaani mpeleka dini/imani pasipokuwa na imani.
Yaani kuwaendea watu ambao hawajafikiwa na imani au ambao bado hawajapokea imani.

Rejea Mtume Paulo
 
Ndio maana nimeuliza hili jambo kwa kutoa mifano halisi. Hivi inakuwaje hawa manabii wanapoteza nguvu zao za upako baada ya muda? Ni wapi wanapokosea?

Wale hawana upako bali Wana nguvu za kafara. Zinakaa kwenye chumvi, maji, sahani, Pete nk. Sasa unaweza kuamua kuendelea kutoa kafara hata ukipata nguvu au Mara moja. Wengi huwa wanachagua Mara moja tu, so nguvu zikiisha wanabaki Kama walivyo na usanii wao.

Zile nguvu zina fanya kazi tatu.

1. Kazi ya kwanza ya hizo nguvu ni kutupia watu matatizo na magonjwa mbalimbali, na zile nguvu kuwaelekeza kwa nabii alipo.

2. Kazi ya pili ni uwezo wa uganguzi, kuona hizo shida za watu waliotupiwa matatizo na kuwapa suluhisho.

3. Kazi ya tatu ni uwezo wa kutoa au kuponya hayo matatizo ndio ambazo nguvu hizo hizo zimeweka. Ndio maana uponyaji wao upo selective , Kuna mambo ambayo hawawezi kuponya hata wafanyeje.
 
Kwa maoni yangu naona Kila kitu au kila kiumbe kinaendeshwa na muda na kamwe hatuwezi kupingana na muda.

Sio kwa manabii na mitume tu hata mashekh, wanasiasa, wanamichezo even wafanyakazi wa kawaida pia wanamuda wakistaaf imeisha hiyo.

Ingawa kukaa sana kwenye masikio ya watu inategemea na nidhamu ya muhusika mfano huyu mwamposa ananidham sana na wito wake na atakaa muda kabla ya kuchuja.

Itoshe kusema kila jambo na wati wake.

Tofautisha mambo ya mwilini na rohoni. Unalinganisha mchezaji mpira na nabii?. Tukubali manabii tulio nao ni mchongo hakuna jingine.
 
HAKUNA MTUME MJINI NI UONGO.
HAWAJUI MAANA YA MTUME.
MTUME HANA KANISA KAZI YAKE NI KUANZISHA KANISA NA KUMWACHIA MCHUNGAJI NA MWALIMU.

Mtume ni mfyeka pori yaani mpeleka dini/imani pasipokuwa na imani.
Yaani kuwaendea watu ambao hawajafikiwa na imani au ambao bado hawajapokea imani.

Very true. Mfano mzuri mtume Paulo, alifungua kazi hadi uarabuni.
 
Yale masharti ni magumu ni lazima utakosea tu, ukikosa upunguza upako
 
Kakobe alikua anaombea vilema wanapona lakin siyo vilema unao waona mtaani vilema wote huwa ni wageni wanakuja nae
Du! Huyu alikuwa balaa aisee! Kumbe vilema wote walikuwa wa mchongo? 😀 😀 😀 😀
Ata huyu anaevuma Sana akienda mkoa fulani wanaopona pale wote kutoka wilaya za huo mkoa akienda Kijijini wanaopona ni wamjini
 
Jambo wadau?​

Naingia kwenye mada moja kwa moja pasipo kuwachosha na maneno mengi. Kwa muda mrefu sasa nimekuwa nikifuatilia upako wa manabii na mitume jinsi wanavyoanza huduma zao kwa pako za hali ya juu sana lakini baada ya muda zile pako huanza kufifia taratibu na kuisha kabisa. Nabaki najiuliza maswali kadhaa yasiyokuwa na majibu:


  1. Nawasilisha.​


  1. Nikujibu swali lako kwa mambo makuu mawili:-

    Mosi, Kulikuwa na maagano ambayo yalikuwa yameunganishwa na falme na mamlaka za giza kila huduma ya atendaye kwa haki kuishia njiani japo alianzia vizuri.Nitakuwekea baadhi ya mistari ila ipo mingi kwenye kitabu:-

    •Daniel 7:21
    “Nikatazama, na pembe iyo hiyo ilifanya vita na watakatifu, ikawashinda;”

    •Ufunuo 13:7
    “Tena akapewa kufanya vita na watakatifu na kuwashinda, akapewa uwezo juu ya kila kabila na jamaa na lugha na taifa.”


    Hivyo kanisa lilikuwa linaweza kuanza vizuri ila huduma yake huishia njiani kupitia kuiba ile huduma kupitia maagano mabaya kuunganishwa nayo kiongozi wake kupitia zinaa na mambo mbalimbali.


    Pili, Manabii na mitume wengi wa sasa ni wa uongo ivyo huduma zao haidumu sababu ya majira ya muumba wa vyote, wote na yote tuliyonayo sasa.
 
Ndio maana hakuna kanisa la Paulo.
Kazi yake ilikuwa kuhubiri na kufungua kanisa na kuweka mzee wa kanisa...leo tunawaita wachungaji
Mtume Paul alifanya Kazi ya uinjilisti zaidi kuliko Kazi ya utume
 
Ndio maana nimeuliza hili jambo kwa kutoa mifano halisi. Hivi inakuwaje hawa manabii wanapoteza nguvu zao za upako baada ya muda? Ni wapi wanapokosea?
Wakishapata pesa SAsa upako tena wa nini tena.
 
Hivi yesu ,aliacha watu wakifate kitabu cha Injili au Biblia maana kila mtume ana kitabu chake yaani zaburi ya Daud ,Torati ya Musa na kila mtume ni Nabii lakini si kila Nabii ni Mtume Sasa wanaofata ya Biblia wanamfata Mtume yupi ?
 
Adamu akapita, Ibrahimu alipita, Isaka akapita, Yakobo akapita, Musa akapita, Yoshua akasepa n.k

Isaya na Yeremia wakaeleza habari za Yesu nao walipita hata wasimuone.

Akaja kristo Yesu akauawa, huyu ndio tumaini akasema hivi:

1. Mathayo 5:20
Maana nawaambia ya kwamba, Haki yenu isipozidi hiyo haki ya waandishi na Mafarisayo, hamtaingia kamwe katika ufalme wa mbinguni.

2. Mathayo 7:12
Basi yo yote myatakayo mtendewe na watu, nanyi watendeeni vivyo hivyo; maana hiyo ndiyo torati na manabii.

Usiwashangae hao kupita bali ndivyo dunia ilivyo
 
Mzee wa upako aliamia kuwa mlevi, mwingira kazaa na mke wa mzungu, gwaji boy kakutwa na kahaba, kakobe kaficha fedha kwenye majaba pia kawakataa wadhamini wa kanisa kwama hawana chao kanisa la kwake. Kesi kasinda mahakamani kwa kanisa ni mali yake. Mwamposa waumini wake walikanyagana na kuangamia yeye kabeba fuko la hela kapanda ndege kia kukimbiza hela dar. Suguye kanisa limefungwa na serikali halina usajili. Mwamposa kajenga hotel kubwa Mbeya shida iko wapi kapiga hela kwa wajinga kawauzia mafuta, maji ya chumvi nk. Geodavie wake za watu wanamkoma. Mwamini Yesu peke yake usiabudu wapiga hela, hao ni binadamu kama wewe. Mungu ni wawote na anamsikia kila anayemwamini na sio kupitia kwa binadamu mwenzako. Mathayo 4:10
Ndipo Yesu alipomwambia, Nenda zako, Shetani; kwa maana imeandikwa, Msujudie Bwana Mungu wako, umwabudu yeye peke yake.
Mnakubaki wake zenu wanakuwa wajinga. Wanakwendabkupikia, kufulia na kuwa hawara wa hao knaowaita "manabii na mitume". Mungu alishaonya kabla. Mathayo 24:24
Kwa maana watatokea makristo wa uongo, na manabii wa uongo, nao watatoa ishara kubwa na maajabu; wapate kuwapoteza, kama yamkini, hata walio wateule.

Mathayo 24:25
Tazama, nimekwisha kuwaonya mbele.

Manabii wanahitajika kwa ajili ya nini ambacho hakijaandikws kwenye biblia. Nabii anatabiri mpira wa Yanga na Simba. Nabii wanatabiri kwamba umelogwa kama waganga wa kienyeji. Ama kweli watu wamepungukiwa na maarifa ya kiimani. Isaya 5:13
Kwa sababu hiyo watu wangu wamechukuliwa mateka, kwa kukosa kuwa na maarifa; na watu wao wenye cheo wana njaa, na wengi wao waona kiu sana.
Watu wamekataa maarifa ya Mungu shetani kupitia kwa mawakala wake amewapiga upofu na hawaoni. Wana kiu na njaa ya maarifa ya Mungu na wasipojitambua watapotea milele.
 
Back
Top Bottom