Kwanini Mungu na Shetani wasimalize tofauti zao?

Kwanini Mungu na Shetani wasimalize tofauti zao?

Nani kakuambia emotioms hazithibitishiki?

Role ya Amygdala ni nini

Na nani kakuambia emotions haziko physical?

Na finally ni nai kakuambia hivyo havithibotishiki mpaka utumie kama mlango wa kuingizia habari zako za uzushi (roho&nafsi) kuwa vipo?
Nipe uthibitisho wa kuwepo hisia in their own form.
 
Hutapata jibu kwa kuwa ni "vitu vya kufikirika" hakuna uhalisia. Mf. Ukishindwa kupata jibu unakuwa na wazo la Mungu akilini, hivyo unamuumba Mungu ndani ya ibongo wako. Basi binadamu ndio waliomuumba Mungu.
 
Mkuu omba na tafuta sana usije kuingia kuzimu na hatimaye motoni. Ile sehemu huwezi hata kuwish your worst enemy aende. Ni sehemu ya mateso sana na hata hutapata nafasi ya kuangalia nani yupo jirani kwasababu ya maumivu na mateso. Mungu aturehemu ili tuurithi uzima wa milele.
Mpenda Amani na Mpenda wote alitengeneza sehemu ya Mateso ? Au hii kaitengeneza Shetani ? Na kama ni Shetani kaitengeneza kwahio yeye haitamsumbua ? Na kama Ni Mungu huoni this goes against mercy ? Yaani alitenga kabisa huku nitawaonyesha wale ambao hawakunifuata ?
 
Hicho chombo kinaweza kung'amua exact thing ambacho mtu anawaza au kinaonesha tu kwamba huu ubongo unayo mawazo.

Kama hakiwezi kuelezea exact thoughts basi kinapima dalili tu.
Ndio inawezekana kupitia FMRI

Na hata isingekuwa haiwezekani, isingethibitisha madai yako batili kuwa ni kweli
 
Mpenda Amani na Mpenda wote alitengeneza sehemu ya Mateso ? Au hii kaitengeneza Shetani ? Na kama ni Shetani kaitengeneza kwahio yeye haitamsumbua ? Na kama Ni Mungu huoni this goes against mercy ? Yaani alitenga kabisa huku nitawaonyesha wale ambao hawakunifuata ?
Hiyo iliwekwa na Mungu kwa ajili ya kumuadhibu shetani alipoasi. Kwenye spiritual world kila action ina consequences. Sheria ya uhai na mauti zipo pamoja ila kuna conditions zinazofanya sheria hizo zifanye kazi.

Mmea ukishikamana na ardhi yenye maji utaendelea kuwa hai ila ukitengana na ardhi basi wala Mungu hahitaji kuuua, unakufa automatically kama consequence ya kuacha ardhi.
 
Hili suala tulijadili kwa Logic!

Iwapo tunaambiwa kusamehe mara sabini mara saba, inakuwaje hawa wasimalize tofauti zao sababu naona hivi vita vyao sisi nyasi tunaumia.

Okay unaweza kusema kwamba Shetani hajarepent (kuomba msamaha) ndio maana hajapewa msamaha, lakini je inamaanisha Mungu anapenda kuombwa ombwa na kunyenyekewa kiasi kwamba hatoi msamaha mpaka aombwe.

Na je, Hadithi za Mwana Mpotevu, Je inamaanisha siku Shetani akirudi na kupiga magoti atasamehewa ? Au kuna Muda wa kuomba msamaha ukipita ndio basi.

Au baada ya kukaa Motoni kwa karne kadhaa huenda ukapita msamaha kama wa wafungwa na kila mtu akawa huru na sio hawa tu ambao walijinyima bata huku duniani?

NB: Kama kuna anayeweza kunielewesha haya logically kwa kanuni za imani yake naomba tujadili (na sio kutumia kanuni za multiplication kwenye paraghraph moja na ya Pili kutumia kanuni za Addition) yaani inconsistency!
Duh
 
Ndio inawezekana kupitia FMRI

Na hata isingekuwa haiwezekani, isingethibitisha madai yako batili kuwa ni kweli
Chombo chako unachokiamini sana kimekuangusha maana kinapima dalili za uwepo wa mawazo na sio mawazo yenyewe.

Kubali sasa uwepo wa reality beyond the physical world halafu umpokee Yesu akusamehe dhambi na kukupa uzima wa milele. Haya uyafanye kwa imani.
 
Huwa najiuliza kama wazungu wasingeleta dini waafrika tungemuuaje Mungu yupo au hayupo
 
Huwa najiuliza kama wazungu wasingeleta dini waafrika tungemuuaje Mungu yupo au hayupo
Wafrika walikuwa wanamwabu Mungu kama kawaida tatizo lao hawakuweka mafundi yake pamoja.

Amri kumi zote zilikuwepo na zilifuatwa kama kawaida na mababu zetu.

Ndio maana kulikuwa na Majina ya Mungu kwenye lugha ya kienyeji kabla ya kuja kwa wazungu.

Neno Kilima-njaro maana yake mlima wa Mungu.
 
Mkuu chanzo cha uhai ni nini?
Kwa nini swali hili ni muhimu katika mjadala wa kuwapo Mungu?

Naweza kukuambia kwamba chanzo cha uhai si huyo Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote. Kwa sababu ingekuwa hivyo, hao viumbe wake anaowapenda wasingekufa kikatili kama wanavyokufa sasa.

Naweza kuwa sijui chanzo cha uhai ni nini, lakini nikajua si Mungu.

Naweza kujua square root ya 2 si 10, bila kujua square root ya 2 ni nini.

Naweza kujua mtu mwenye miaka 30 leo hawezi kuwa na mama mzazi mwenye miezi 6 leo, bila ya kumjua mama mzazi wa huyo mtu.

Sasa, mimi nakwambia huyu mtu ana miaka 30 leo, hawezi kuwa na mama mzazi mwenye miezi 6 tu leo, it is against the laws of logic.

Wewe unaniuliza, sasa kama mama yake si huyu mwenye miezi 6, mama yake ni nani?

Mimi sihitaji kumjua mama yake huyu mtu mwenye miaka 30 ni nani ili kujua kwamba huyu wa miezi 6 hawezi kuwa mama mzazi wa mtu mwenye miaka 30.
 
Wafrika walikuwa wanamwabu Mungu kama kawaida tatizo lao hawakuweka mafundi yake pamoja.

Amri kumi zote zilikuwepo na zilifuatwa kama kawaida na mababu zetu.

Ndio maana kulikuwa na Majina ya Mungu kwenye lugha ya kienyeji kabla ya kuja kwa wazungu.

Neno Kilima-njaro maana yake mlima wa Mungu.
Mungu yupi huyo unaemsemea
Zamani watu waliwatambikia mababu zao waliokwisha fariki zamani
 
Chombo chako unachokiamini sana kimekuangusha maana kinapima dalili za uwepo wa mawazo na sio mawazo yenyewe.

Kubali sasa uwepo wa reality beyond the physical world halafu umpokee Yesu akusamehe dhambi na kukupa uzima wa milele. Haya uyafanye kwa imani.
Kwahio uwepo wa reality beyond physical world kama upo kwanini tusikubali chochote kile cha kufikirika ? Kwanini tusikubali mizimu ya mababu zetu au Krishna wa wahindi na tumuamini messiah wa wayahudi ?

Why is any of this superior than the other..., ukizingatia option unayonipa kwamba nikifanya mazuri huku kinachonisubiri ni maisha ya kuimba na kusifia to infinity ?!! Huoni kwa mie nisiyependa kuimba kwamba huenda alternative Imani ya Wasabato kwamba nitalala milele bila kufufuka is a better option ?
 
Chombo chako unachokiamini sana kimekuangusha maana kinapima dalili za uwepo wa mawazo na sio mawazo yenyewe.

Kubali sasa uwepo wa reality beyond the physical world halafu umpokee Yesu akusamehe dhambi na kukupa uzima wa milele. Haya uyafanye kwa imani.
Usi flip hoja yangu. Hakuna sehemu nimeandika habari za dalili

Hayo ni maneno yako binafsi na wala hayahusiani na majibu yangu
 
Ibilisi mara baada ya kuasi amri ya Mungu .Aligoma kumsujudia Adam ,kumpa heshima yake kuwa ana elimu kumzidi yeye. Akasema kuwa yeye ni bora kuliko Adam kwakuwa ameumbwa kwa moto na Adam ameumbwa kwa udongo.

Hakuomba msamaha badala yake alikuwa na ombi lake tofauti, Alimuomba Mungu amjaalie umri ulio mrefu, apate kuishi mpaka mwisho wa ulimwengu huu. Mungu alimkubalia ombi lake na akawa ni miongoni mwa waliopewa uhai mrefu. Hili ndilo ombi lake na alifanya hivyo ikiwa ni kiburi,chuki na husda dhidi ya Adam na uzao wake. Alijua akipewa umri mrefu basi atahakikisha anaingia motoni pamoja na uzao wote wa Adam.

Suala la kuomba msamaha halipo ndani ya nafsi ya ibilisi na halitakuwepo mpaka dunia hii inatamatika

Ibilisi alijuaje kuwa Ulimwengu ulioumbwa na Mungu Una mwisho?
Kumbuka tukio hilo linatokea Adamu alikuwa hajaasi, na Eva bado hajaumbwa
Unaweza kufafanua hapo
 
Siyo kufuru.
Kwa sisi wenye mwili tunaona kama kifo ni adhabu.
Kiuhalisia kifo ni mabadiliko tu ya binadamu kutoka stage moja kwenda nyingine.
Kama Mungu anaamuru ufe ki uhalisia ni jambo jema kabisa.

Aliyekuleta anakupeleka katika dalaja lingine ambolo ni bola zaidi.

Mfano. Mtoto anapozaliwa analia sana hataki kuja diniani kwa kulizoea tumbo la mama yake na kuona ndio sehemu sahihi yakuishi.

Akisha zaliwa baada ya muda anaona kumbe kule tumboni kulikuwa hakuna maana. Maisha mazuri ni haya ya sasa ya kula samaki na maziwa.

Ndivyo kilivyo kifo, ni kizuri sana mimi nitakapo karibia kufa nitawaambia waliobaki "Sitaki mtu anililie" nitaandaa bajeti ya Kusheherekea Kifo changu na Bia zitakuwepo.

Najua naenda sehemu nzuri zaidi ya hapa nilipo.
Na je anapanga pia jinsi ya kukuondoa ? Kwamba huyu afe akiwa tumboni baada ya mama kuhangahika miezi tisa ? (Na sio kwamba mama alikuwa mpiga tungi na kufanya mambo ya kuhatarisha mimba) !!!
 
Biblia imesema hapo mwanzo Mungu aliumba mbingu na nchi. Dunia iliumbwa pamoja na ulimwengu billions of years ago. Zile siku unazoona kwenye kitabu cha mwanzo zinahesabiwa baada ya tukio la dunia kuwa ukiwa na utupu.

Na kwenye theolojia inaelezeka kwamba tukio la ukiwa tena utupu lilikuja baada ya shetani kumwasi Mungu. Ukisoma kitabu cha Ezekiel sura ya 28 unaona shetani kabla hajaasi alikuwa na ofisi hapa duniani. Alipoasi ndio Mungu aliharibu dunia pamoja na ofisi aliyokuwa anaitumia hapa duniani.

Sasa baada ya kipindi fulani ndio Mungu akarudi kuanza kuweka new life kwenye dunia hii na hapo ndio zile siku za kitabu cha mwanzo zinatajwa.
And this was pre-arranged yaani alijua yote haya yatatokea au alikuwa taken by surprise hence hajui kila kitu ?
 
Back
Top Bottom