Kwanini Mungu na Shetani wasimalize tofauti zao?

Kwanini Mungu na Shetani wasimalize tofauti zao?

Hawawezi kumaliza tofauti zao, kwa sababu hawapo kiuhalisia, ni wahusika wa hadithi ya kutungwa tu.

Kwa hivyo, kama unataka wamalize tofauti zao kama wahusika wa hadithi ya kutungwa, ni suala la kuandika hadithi ambayo Mungu na Sjetani wanapatana tu.

Hata wewe unaweza kuandika hiyo hadithi.
Ndio hapo sasa hata kama hii ni hadithi hata hadithi zina logic..., hata Game of Thrones ambayo ni make believe na unajua ni uongo na kuna dragons na White Walkers wanaoweza kuona future ilikuwa inakwenda poa na logically kwa sheria walizojiwekea mpaka pale mwisho hiki kiumbe kinachoweza kuona future na kila kitu kuweza kuuliwa kwa urahisi which means they could not see the future...

Which means the writers were making things as they go along thus insulting our intelligence (tulikubaliana kwa kuwekeana assumptions sasa hizo assumptions zinapobadilika for their convinience sio poa)
 
Hawawezi kumaliza tofauti zao, kwa sababu hawapo kiuhalisia, ni wahusika wa hadithi ya kutungwa tu.

Kwa hivyo, kama unataka wamalize tofauti zao kama wahusika wa hadithi ya kutungwa, ni suala la kuandika hadithi ambayo Mungu na Sjetani wanapatana tu.

Hata wewe unaweza kuandika hiyo hadithi.
Mkuu chanzo cha uhai ni nini?
 
Nadhani watu wa wakati ule walikuwa na imani kupitiliza kiasi kwamba hata mungu alikuwa akijiamini kuwa myu fulani hawezi ingia ktk mtego wa shetani.

Embu linganisha na dunia ya sasa nani avumilie hayo mambo? Jambo dogo tu mtu ashaenda kwa mganga kuuliza /aangaliziwe nini kinaendelea😅
Nadhani na wengine walipitisha dhambi zao kwa mgongo wa Mungu..., just imagine kama mtu unaweza kufanya kitu eti Mungu / Mizimu imekwambia si una-get away with murder...

Vilevile tusisahau huyu Mungu wa Wa-Israel au Waarabu na sisi tulikuwa nao wetu kama vile wahindi walikuwa nao wao na wapagani walikuwa na Miungu yao...
 
😂😂😂 Wewe hata sayansi huifuatilii. Ulimwengu unaendelea na creation infinitely ndio maana jamaa bado hawajafanikiwa kuuona mwisho wa ulimwengu. Mungu yupo busy na project zake nyingine nyingi.
Na hayo mambo ya kiyama yanakujaje kama Kuna project zinaendelea?
 
Mtume Muhammadi keshamaliza huo uhasama.

Kwa kufanikiwa kumsilimisha Shetani na kwa sasa Shetani ni Muislamu safi kabisa.

Kwa sasa Allah na Shetani ni marafiki wa kupika na kupakua.
Na wote kwa pamoja wanamswalia mtume na kumtakia rehema.

Kumbukeni Allah aliumba Mtu, Majini na Ibirisi Shetani na viumbe vyote ili vimuabudu.

Tunamshukuru sana m'bora wa mitume kwa kufanikisha hili swala.
Sasa hio Memo mbona haijapatikana huku kitaa, kwahio tunaweza kusema Binadamu naturally are Bad (Human Beings are Not Good People) Huku ni survival of the fittest / meanest.... kwahio popote pale ni mwendo wa mwenye nguvu kumuumiza mwenye udhaifu na kutengeneza Katiba ya kuhakikisha analamba asali mpaka tamati
 
Nyinyi wa dunia ya tatu, mkifa mnapelekwa kufukiwa na mnasema na mnaingiza imani zenu kama sababu yakufa....

Dunia ya kwanza, ukifa, ni kisheria uthibitishwe umekufaje kisayansi...hata kama ni melala nyumbani kwako, hamuendi kuzika mpaka wajue huyo mtu amekufa kwa sababu gani...
Na sayansi haidanganyi.....
Unakula mifuta imeziba matundu ya moyo, umepata shinikizo la damu au stroke usiku umelala, pia wanafanya autopsy/post mortem kuhakikisha hivyo, imetoka hiyo...
Au....
Umepata ajali na kupoteza damu nyingi au organ kama moyo, mapafu au ubongo umevurugwa, wanafanya autopsy/post mortem kuhakikisha hivyo imetoka hiyo...

Mtu anapata Arrythmia ya moyo na anakuwa katika hali ya nusu kufa na kama hamna namna ya kumukoa, ni anakufa tu baada ya muda mchache, lakini kwenye huduma bora, unarudishwa kuendelea na joto ya jiwe, mpaka kuna watu wanaweka signature inaitwa DO NOT RESUSCITATE ya kuwa akifikia hiyo hali asirudishwe duniani kuendelea na msoto...

Na ukisikia amekufa kwa natural causes, pia kuna sababu ya moyo umesimama kupiga, ubongo umeumaliza mwendo....yaani kila kufa kuna sababu yake kisayansi zaidi kuliko hizi stori za kiroho....
Umeandika sana japo sijaona sehemu umeeleza nini hasa ni chanzo cha life force ndani ya mwanadamu.
 
😂😂😂 Wewe hata sayansi huifuatilii. Ulimwengu unaendelea na creation infinitely ndio maana jamaa bado hawajafanikiwa kuuona mwisho wa ulimwengu. Mungu yupo busy na project zake nyingine nyingi.
Hao jamaa ni kina nani ? Wewe sio hao jamaa, Sayansi haina mtu hata wewe kesho ukitwambia kwamba dunia ni kama bakuli ukaja na vivid evidences ambazo kweli zitakubaliana na known facts tutakubaliana na wewe na kusema we have been wrong all along (sio kubadilisha facts tuonekane we were right all along)

Mwisho wa living thing ni kifo chake mwisho wa hii solar system ambayo na sisi dunia tupo kama isipotokea kitu kingine chochote ni pale nguvu za jua (energy) Hydrogen itakapoisha, the all system will collapse na hii can be elaborated scientifically na sio kuamka tu na kusema I have seen the light...
 
Haijalishi upo dini gani, ukisikia habari za Kristo lazima moyo wako uguswe.
Kwahio in your statement kuna watu hawajasikia hizi habari ? Shetani hakumjua huyu Kristo ?
 
Kwahio huyu Mungu Mpenda wote na Msamehe Makosa ambaye ni superior bila weaknesses zozote aliweka hii technicality ya kutokusamehe baadhi ya makosa?

Na huku kitaa hio spirit realm ambayo ni perfect inapatikana wapi ? Kwahio huenda na wewe mtenda mema ukishafika mbinguni baada ya miaka kadhaa ukaamua kujitia ujuaje huenda uka-end up na kina Shetani ? Yaani the Struggle Continues ? (My way or the Highway)!!!!
iyo realm ipo hapo hapo ulipo its just other side of the coin
 
Nimesoma kitabu kitabu kinaitwa enoch book 1-3 acha kabisa

Kuna dubwana humo linaitwa phoenix shetani anapita nalo mbali kabisa na lingine linaitwa behemoth na leviathan...ila hilo phoenix balaa aisee, someni hizo attachment..hiyo mistari nilipiga mm..ila someni page nzima aisee nimejifunza mengi sana..

Ukitaka hv vitabu njoo inbobo..maana ukikisoma vibaya inakula kwako.
Screenshot_20221021-143254_Gallery.jpg
View attachment 2393711
 
Kuwa mkristo ni bahati. Inaitwa bahati ya kupata habari njema ya ulimwengu.
Hakuna imani inayo tangaza Amani na Upendo kwa jirani yako hapa duniani zaidi ya Ukristo.

Mathayo 22:36 Mwalimu, katika torati ni amri ipi iliyo kuu?

37 Akamwambia, Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa akili zako zote.
38 Hii ndiyo amri iliyo kuu, tena ni ya kwanza.
39 Na ya pili yafanana nayo, nayo ni hii, Mpende jirani yako kama nafsi yako.
40 Katika amri hizi mbili hutegemea torati yote na manabii.

Ukristo ndio imani pekee duniani inayosema.

Mathayo 18:21 Kisha Petro akamwendea akamwambia, Bwana, ndugu yangu anikose mara ngapi nami nimsamehe? Hata mara saba?

22 Yesu akamwambia, Sikuambii hata mara saba, bali hata saba mara sabini.

Na inasisitiza

Mathayo 5:43 Mmesikia kwamba imenenwa, Umpende jirani yako, na, Umchukie adui yako;

44 lakini mimi nawaambia, Wapendeni adui zenu, waombeeni wanaowaudhi,

45 ili mpate kuwa wana wa Baba yenu aliye mbinguni; maana yeye huwaangazia jua lake waovu na wema, huwanyeshea mvua wenye haki na wasio haki.

46 Maana mkiwapenda wanaowapenda ninyi mwapata thawabu gani? Hata watoza ushuru, je! Nao hawafanyi yayo hayo?

Imani ya Kikristo ndio pekee inayofundisha haya mafundisho bora sana na yenye manufaa kwa kila mtu.

Na hayapatikani kabisa kwenye imani nyingine.

Waislamu ukimdhihaki Muhamaadi hakuna msamaha ni wa kuchinjwa tu.

Ukiiba unakatwa mikono hakuna msamaha.

Ukizini ni kuchinjwa
Ukiwa shoga ni kuchinjwa

Usipo vaa hijabu ni kuchinjwa.
Ni afadhari hata Dini ya Shetani, yaani Rusiferian religion.

Katika Satanic religion ukifanya hayo mambo unapendwa sana na unapewa na zawadi.

Nadhani mnaona na kusikia.
Dini yako haikufundishi kutokuhumu ?

Kwahio unataka kuniambia watenda mema wote watakwenda motoni sababu hawana tag ya ukristo ?..., Unasema ukristo unasema mpende jirani yako lakini huenda nikienda kuomba mke nikanyimwa sababu tu sina tag kama hao wenye tag zao...

Jamii yoyote inayojiona sisi ni bora kuliko wao haijengi bali inabomoa na kwa ustawi wa nchi na sisi walipa tozo bora niwe na wapagani wapenda wenzao wote kuliko sijui wanaojiona watakatifu lakini in actual sense ni wabaguzi (na wajiona superior)
 
Kwamfano kwenye dhehebu langu la catholic, kwenye Sala ya ekaristi, padre Kuna sehemu anasema .....Mungu mwenyezi uliye asili ya mema yote...,
Lakini ukifikiria vizuri utagundua Mungu ni asili ya maovu yote pia.
Ninachojiuliza endapo Mungu na shetani wakiamua kumaliza msala wao, sisi huku duniani tutazipata hizo habari kwa njia Gani?
NB
Ukiamua kuamini shetani yupo ukubali kupunguza baadhi ya sifa za Mungu, kama mwenyezi, upendo etc
 
Kilichozaliwa kwa roho tupu hakifi, shetani ni roho hafi, hiyo ndio kanuni ya Mungu. Ndio maana shetani atateseka milele hatapotea baada ya mateso ya jehanam. Kwahiyo binadam ana mwili na roho, makosa yake yanafanyika katika mwili kwa ushawishi wa roho. Binadam hafanyi makosa katika roho bali mwili ambayo ufanya roho yake ife kidunia pia. Shetani amefanya makosa hakiwa katika ukamilifu wa roho hawezi samehewa milele, sababu amekosa kwa makusudi akiwa katika utukufu (amekufuru). Tofauti na binadamu akiwa hajui na udhaifu mwingi amekosea katika mwili. Yesu alisema ukikufuru roho takatifu husamehewi, maana Mungu wetu na shetani ni roho kamilifu.
Kwahio wewe mwili ukikosa utasemahewa na kwenda peponi ambapo huenda utakosa tena hence kutupwa moto wa milele ?

Yaani the struggle continues to infinity ?
 
Back
Top Bottom