Kwanini Mwamposa asiende kwenye mahosiptali kuombea wagonjwa na tukaona wanapona?

Kwanini Mwamposa asiende kwenye mahosiptali kuombea wagonjwa na tukaona wanapona?

Kuombea watu ili wapate afya ni agizo la Yesu Kristo kiongozi wa kanisa.
Aya Zipo.
Swala kuombea wagonjwa haliji tu haraka haraka au kwa mapenzi ya muombeaji.

Hamjiulizi tu, ni kwanini hakuna Nabii wala Mtume aliyewahi kwenda Hospitali kuombea Wagonjwa kwenye hivyo vitabu mnavyoviamini ?

Mnaosema hivyo ni kwamba hamyaamini Mambo ya Imani wala Dini.

Hali inayo pelekea kuwatukana watumishi wa Mungu kila kukicha, wawe wanaombea au hawaombei nyie kila siku kazi yenu ni kupinga, Hakuna Mungu, Dini ni utapeli, flani ni mwango Nk.

Watumishi wengi katika hali yoyote ile wanaisaidia jamii fulani kuacha matendo maovu na kuwapa nafuu ya kisaikolojia.

Ki Imani ya Kikristo kuombea hakuji kwa mapenzi ya Muombeaji Bali ruhusa ya Roho Mtakatifu.
Hivi mmejiuliza kuwa.

Je huko Hospitali kuna mazingira ya Uwepo wa Roho Mtakatifu?

Je Roho Mtakatifu amemruhusu Muombeaji akaombee watu Mahospitalini?

Je hao wanaotaka kuombewa wamefanya juhudi yoyote ya kuhitaji maombi toka Imani fulani na wakashindwa hadi wafuatwe walikolazwa?

Kwa Imani ya Kikristo Kiongozi wao Kristo mwenyewe alishawahi kuombea wagonjwa Mahospitalini?

Au Musa au Paulo au Elisha?
Kama sio ni kwanini musiwaulize wao kwanza ?

Kama hao watumishi hawaendi kuombea watu Mahospitalini Nendeni nyie mkawaombee huko Mahospitalini.

Kumbukeni kuwa hata akina Gwajima pamoja na ujinga wao mwingi lakini wamesaidia Maelfu ya watu kutenda wema, na kustawi na Kuokoka.

Hivyo kila mtumishi wa Mungu ana mchango mkubwa kwa jamii husika, hivyo anastahili heshima hata ndogo tu kwa hiyo kazi.

Nyie wapinga Dini na Imani endeleeni tu na Kauli zenu za kupinga Dini inatosha.
Na sio kuanza kusema wapi panahitaji maombezi na wapi hapahitaji.
Kazi ya kuombea wagonjwa sio ya kula chapati na Maharage na kushiba na kuanza kuongea ongea pumba.
1. Roho mtakatifu ni Nini? Na anabidi awe na mazingira gani? Au hapendi harufu ya dawa?
2. Usitumie kigezo Cha hekaya za dini coz kila dini inazo na kila dini inawaponyaji according to Mungu wao so Kuna Mungu wangapi asa...na usiseme Mungu ni mmoja kisa dini mbili unazoziona mtaani kwenu dini zipo kibao na zote watu huhisi kuponywa..
Vitu vingine penda kufikiria achana na hisia za uwoga, ujinga na matumaini
 
1. Roho mtakatifu ni Nini? Na anabidi awe na mazingira gani? Au hapendi harufu ya dawa?
2. Usitumie kigezo Cha hekaya za dini coz kila dini inazo na kila dini inawaponyaji according to Mungu wao so Kuna Mungu wangapi asa...na usiseme Mungu ni mmoja kisa dini mbili unazoziona mtaani kwenu dini zipo kibao na zote watu huhisi kuponywa..
Vitu vingine penda kufikiria achana na hisia za uwoga, ujinga na matumaini
Pana Mungu na miungu u God and goodness.
Mungu ni mmoja The Creator.
Roho Mtakatifu ni uwepo wa Mungu ndani ya mtu ni Ile sauti ikuonyayo kuhusu mabaya,thus mwenye Roho Mtakatifu uogopa kufanya mabaya yaani hofu ya Mungu,kama hauna kwako dhambi ni kawaida tu
 
Danganya hao hao wapumbavu, wote hawa ni matapeli wanao ride kwenye mtaji wa ujinga, mama kauza vijichapati vyake, tapeli hili linaenda na kumfagia huyu mama, tapeli mwingine anayejiita bushiri no 1,amekua fugitive kwa raping cases na ponzi schemes, kama yupo safi why akimbie kesi zake?
Penye ngano magugu hayakosi
 
Pana Mungu na miungu u God and goodness.
Mungu ni mmoja The Creator.
Roho Mtakatifu ni uwepo wa Mungu ndani ya mtu ni Ile sauti ikuonyayo kuhusu mabaya,thus mwenye Roho Mtakatifu uogopa kufanya mabaya yaani hofu ya Mungu,kama hauna kwako dhambi ni kawaida tu
Sawa
 
Kutakuwa na conflict of interest hospitali sio sehemu ya kupona TU pale Bali kuna biashara ya dawa inafanyika pale.
Unaweza pewa dawa ya kupoza Ili kesho uje tena na tena.
Muhimbili kuna kitengo cha utalfiti i.e: tiba asili ambapo atapewa kibali na wodi yake ili awaombe then madaktari wa utafiti wapitie wagonjwa wote upya kuwapima watoe majibu
 
Kwann hao wagonjwa wasiende kwa mwamposa kuponywa hadi wafatwe hospitalini.
Anayetoa na kusmba huduma ni mwamposa au mgongwa?

Hivi baada ya huyo yesu na muhamadi kuna WATUME na MANABII wengine waliozaliwa MBEYA?
Wajinga ndiyo waliwao!!
 
Kama hawataki kuyajua maandiko kwa nini wasiyajue kwa kulipishwa Hela,manabii wapo sawa kuwauzia uponyaji watu
Kwanini manabii wa Afrika/mbeya wasiombee UFISADI,UMASIKINI,UJINGA na MARADHI vinavyowasumbua waafrika vikaondoka?
 
Mimi mwenyewe ni Mkristo lakini vitu vingine lazima tuhoji.
Wewe ni m-kristo wa ukoo gani?
2023_11_22_22.39.37_edit.jpg
 
1. Roho mtakatifu ni Nini? Na anabidi awe na mazingira gani? Au hapendi harufu ya dawa?
2. Usitumie kigezo Cha hekaya za dini coz kila dini inazo na kila dini inawaponyaji according to Mungu wao so Kuna Mungu wangapi asa...na usiseme Mungu ni mmoja kisa dini mbili unazoziona mtaani kwenu dini zipo kibao na zote watu huhisi kuponywa..
Vitu vingine penda kufikiria achana na hisia za uwoga, ujinga na matumaini
Anaye hitaji maombi anaenda mwenyewe kuombewa huko kunako husika.
Benki zinawafuata wateja wake.

Hata watumishi wa Mungu pia wanawafuataga wateja wao pale inapobidi.
Kuna mikutano mingi ya Injiri inaandaliwa siku zote na wanaohitaji mahubiri wanashiriki kikamilifu.

Ukitaka mkopo Benki lazima wewe binafsi uende Benki kukamilisha maombi yako na Kamwe pale kwenye mafundisho Yao huwezi kuletewa pesa

Mambo ya Roho Mtakatifu wanayafahamu wahusika na wanayaamini.

Wanaohitaji maombezi wanayapata na wanaridhika. Hata huko Benki sio kila Mteja anaweza pata pesa.
Ni lazima vigezo vya kupata pesa vitimizwe.

Kuwakashifu watumishi wa Mungu ni kukosa maadili.

Wakashifuji wapo tu hata Yesu Mwenyewe alikashifiwa.

Jambo usilolijua ni kama usiku wa kiza, ni vema kuuliza kuliko kujifanya mjuaji.

Hakuna mtu aliyekuwa na nia ya maombezi akayakosa, na maombi hayalazimishwi.

Nenda sehemu husika, fuata vigezo utapata maombezi sahihi. Haya Mambo ni ya Kiimani na sio ya Kisayansi.

Na hata hiyo sayansi hadi leo imeshindwa kutimiza mahitaji ya Binadamu.

Haspitali zipo na kila siku vifo vinatokea huko Mahospitalini.

Je tuwakashifu Wataalamu wa afya kwa kusababisha vifo?

Ulimwengu una kanuni zake, na bado haujatoa majibu ya ustawi wa Binadamu, zaidi ya kuleta unafuu mchache kwa wachache.

Kama mtu haamini Mambo ya Dini hana sababu ya kusifu au kukebehi Mambo ya Dini.
 
Anayetoa na kusmba huduma ni mwamposa au mgongwa?

Hivi baada ya huyo yesu na muhamadi kuna WATUME na MANABII wengine waliozaliwa MBEYA?
Wajinga ndiyo waliwao!!
Mitume na manabii wapo hadi kesho,elewa kwanza nini maana ya mtume Nini maana ya nabii
 
Back
Top Bottom