Kwanini nashauriwa nioe?

Kwanini nashauriwa nioe?

Mmmh mbona mm nna 28 na sioni tatzo au mimi ndy tatzo [emoji1787][emoji1787]
 
Habari wana Jf,

Hapa ninapoishi ni mimi pekee ambae sina mke na nilishawahi kuleta uzi hapa ➡️ Thread 'Ninapoishi ni mimi pekee ambae sijaoa' Ninapoishi ni mimi pekee ambae sijaoa

Sasa imekuwa kawaida mwenye nyumba kunitania kila siku kwamba nioe (mwenye nyumba wangu ni mtani wangu kikabila). Maneno haya yamekuwa yakirudia kila wakti jambo ambalo linaanza kunifanya nione au ni kweli sasa napaswa kuoa.

Tuachane na hilo kuna mpangaji mwenzangu leo kanikuta nafanya zangu viusafi akanimbia "Kaka inabidi uoe sasa" huku anacheka (kiumri jamaa kanizidi na anaishi na pisi yake, jamaa ni dokta na pisi yake ni nurse). Me nikamjibu tu kwamba asijali siku akipatikana mwanamke sahihi kwa muda sahihi nitaoa.

Wazazi wangu hawajawahi kuniambia chochote kuhusu kuoa tena, mama ndio huniambia nitulize kiherere cha kuharakia me bado m-little.

Sasa maswali ninayojiuliza kichwani "Hivi ni kigezo kipi cha kuoa? Je, ni kwamba nina vigezo vyote vinavyoonekana ila mimi ndo nafeli au? Au je, ni kwamba ki-Africa kijana ukishakuwa na uwezo wa kukidhi mahitaji yako muhimu unapaswa kuoa?

Au umri wangu ni mkubwa vya kutosha (naelekea 23 sasa)? Au ni kwasababu ya wanavyoniona najifanyia zile shughuli zangu kama kupika, kufua na kujioshea vivyombo vyangu? Au wanahofia nitatafuna pisi zao?

Ebu wakuu nishaurini hapa, hawa watu wakirudia tena haya maneno niwajibuje? Au kama ni kweli ni muda wa kufaa kuoa niambieni? Ila kiukweli kabisa najiona bado nauhitaji huu wepesi hadi baada ya kama 5 years + hivi maana nikiwa hivi naona inanifanya niwe mwepesi ku-risk maisha popote nitakapo.

Tiririka chochote chenye tija kunijenga.
Kuoa ni muda utakaokuwa tayari.
Kuna rafiki yangu mmoja ana miaka 22 na ameoa.
Kwa kuwa ndilo hitaji lake.
 
Miaka 23 wanakupigia yowe? Mkuu utakua wewe ni chibonge..
Miaka 23 baaado sana.
Embu endelea kucheza na wenzio kwanza, muda ukifika hautahitaji kushauriwa, wewe mwenyewe utaenda kuoa kama kondoo.
Hawa wa kataa ndoa wasikutishe, wao ni mabalozi wa mkono bao.
Muda bado
[emoji23][emoji23][emoji23]
 
Kuoa ni muda utakaokuwa tayari.
Kuna rafiki yangu mmoja ana miaka 22 na ameoa.
Kwa kuwa ndilo hitaji lake.
Me niliwahi sana nilishaishi na mwanamke since nikiwa 18yrs tukaachana nikiwa 21yrs ndo maana hata hawa watu hunishauri nioe kwa kuwa walishaniona nikiishi na mwanamke before
 
Mkuu ni hatari wanachokushauri kwa dunia ya sasa
1677491500428.jpg
 
Enzi zile nyumba za kupanga Ni vyumba sita ndani na vingine uani, choo na bafu uani, nilipanga nyumba moja mjini Dar. Chumba changu kilikua Cha ndani, wapangaji wenzangu wote wameoa Ila Mimi tu.
Kila nikitembelewa na pisi langu la kirangi, limeenda juu halafu Lina mzigo makalioni, wake za wapangaji wenzangu wote wanatoka vyumbani wanakaa kwenye korido. Kama atalala ujue kumi na moja na nusu asubuhi tayari wanawake wako nje bombani na wengine wanafagia nje.
Kumbe walikua wanataka nichukue mmoja wao.
Ikawaje mkuu , ulipita nae mmoja?
 
Back
Top Bottom