Kwanini Nchi nyingi zenye asili ya Uislam zinakumbwa na Vita sana?

Kwanini Nchi nyingi zenye asili ya Uislam zinakumbwa na Vita sana?

Nchi nyingi zenye mlengo wa uislamu au majimbo mengi ya nchi yenye mlengo wa uislamu uwa ni kitovu cha ugaidi na maeneo hayo usifika kwa kuzalisha makundi mengi ya Kigaidi.

Sisemi tu kwa sababu nasema bali nasema kwa sababu zipo nadharia nyingi zinazoonesha kuwa ni kweli maeneo hayo ukumbwa na matukio ya kigaidi ama Vita.

Hata Tanzania miaka kadhaa ya nyuma kulikuwa na tetesi za matukio ya kigaidi maeneo ya Kibiti na jirani na maeneo hayo ambayo kwa wingi ukaliwa na watu wa Dini ya uislamu kitendo kilichopelekea Jeshi la Tanzania kuwekeza nguvu huko Kibiti na kutokomeza ugaidi huo ambao ulikuwa umeanza kumea katika maeneo hayo ya pwani ya Tanzania. Hata kijana mmoja wa kitanzania mwenye mlengo wa Dini ya kiislamu aliwahi kukamatwa Kenya akitumikia kikundi cha kigaidi cha Al-Shabab.

Ukiachilia mbali hayo, Duniani ukitamka neno ugaidi alafu ukasema tutajie dini yenye kuhusishwa na ugaidi moja kwa moja hata mtoto atakutajia Uislamu. Na hii ni kwa sababu Watu wote wanaokamatwa katika matukio hayo basi ujinasibu kama wanapigania Dini ama maslahi yao ya kidini. Ukiachilia mbali kupigania Dini au Maslahi ya Kidini. Nchi hizo hizo au maeneo hayo hayo yamekuwa yakikumbwa na Mapinduzi ya kijeshi na watu hao wakitaka kusimika dola la kiislamu.

Alikadharika maeneo hayo uwa yanakumbwa na vurugu za kivita za mara kwa mara.

Hapa Afrika ukitoa Congo DRC tu ambayo haina waislamu wengi, nchi nyingi zilizobaki zenye vita za mara kwa mara maeneo hayo yenye vita ukaliwa na waislamu kwa idadi kubwa.

Ukanda wote wa Sahel, yani kusini mwa mpaka wa jangwa la Sahara, nchi kama Sudan, Niger, Mali, Burkinafaso, Chad na nyinginezo na nchi zinazokumbwa na vikundi vya kigaidi mara kwa mara. Na ni nchi zenye uislamu mwingi na kama unavyoona zinapakana na nchi za waarabu wa kiafrika ambazo kwa asilimia 90 raia wa nchi hizo ni waislamu.
View attachment 2943395
Nigeria pia ni miongoni mwa nchi inayokumbwa na matukio ya kigaidi sana hususani Maeneo ya kaskazini ya nchi hiyo ambayo ukaliwa na waislamu wengi. Nchini Nigeria wakristo wengi wanapatikana Kusini katika majiji kama Lagos, na Abuja, na waislamu wengi upatikana maeneo ya Kaskazini mwa nchi ambayo mara nyingi majimbo ya Maeneo hayo uongozwa kwa Sheria za kiislamu, pia nadhani juzi kati katika mfungo wa ramadhani watu wa maeneo hayo walikamatwa kwa kutokufunga Mfungo wa Ramadhani na waliadhibiwa. Maeneo hayo hayo ndio kituo cha Kundi la Boko Haram na vikundi vingine vya namna hiyo.

Tukiama barani Afrika tukaamia bara la Asia ukanda ya Middle East (Mashariki ya Kati) ambapo ndiko uislamu umeanzia huko ndiko kuna vikundi vingi vya kigaidi, na karibia kila nchi ina vikundi vyake. Nadhani wengi mnavifahamu vikundi kama Hamas kilichoishambulia Israel na kuteka na kuua watu katika tamasha la mziki, na kupeleka vita ambayo imeigharimu ardhi ya Palestina ukanda wa Gaza. Vilevile haikupita miezi mingi kuna kikundi kutoka Yemen nacho kinaitwa Hauthi kikaanza kulipa mashambulizi kwa kupiga meli zinazopita ukanda wa bahari ya sham bila kujali kuwa anaepigwa ni raia wa nchi gani.

Ukiachilia mzozo huo wa Israel na maadui zake, hakuna asiyejua kundi la kigaidi lenye mlengo wa kiislamu lililotikisa Dunia kwa matukio ya kutisha kwa kuchinja, kupiga risasi au kujitoa Mhanga. Hii ya kujitoa mhanga ikapelekea Waislamu hasa waliojifunika mwili mzima kuogopwa sana kuhisi labda wamebeba mabomu ya kujitoa mhanga. Chini ya Osama Bin Laden, kundi hili liliisumbua Dunia hasa Marekani kwa kuipa Jeraha lisilosahaulika la Septemba 11.

Kwa kifupi huko Middle East (Mashariki ya Kati) kuna vikundi vingi sana vya kigaidi, vingine vinakuwaga vimelala tu, vinakuwa (Inactive) lakini viko tayari kwa mashambulizi. Na vikundi hivi ndivyo vinafanya Dola za kiislamu zinaendelea kusimama na sheria kali za kiislamu zifatwe, mfano moja wapo ni Kundi la Taliban kutokea pale Afghanistan ambalo baada ya kushika dola tu likaweka sheria kali za kiislamu ikiwemo wanafunzi kusoma madarasa kwa kuzingatia jinsia mpaka chuo kikuu yani mtoto wa kike na wakiume kila mtu darasa lake.

Kundi jingine la Kigaidi ni kundi la ISIS yani Islamic State. Kundi hili juzi kati limekiri kupiga Tukio pale Russia kwa kumimina Risasi katika Mall moja pale Moscow kwenye tamasha la mziki na kuua watu zaidi ya 150 na kuchoma jengo kwa vilipuzi. Lakini Rais wa Russia Vladimir Putin hajawaacha salama, kawadaka watu kadhaa ambao wanahusika na tukio hilo ambao wengi wao wanasema wamekodiwa kutokea nchi ya Uturuki ambayo ni yenye mlengo wa kiislamu.

Kwa ufupi makundi haya ni mengi sana na yana uhusiano wa moja kwa moja, kwa sababu mengi yanakuwa na link au uhusiano.

Kwani ndugu zetu waislamu mnapokuwa mnafundishwa Dini uwa mnapewa maelezo gani yanayowatia baadhi yenu mioyo ya kikatili, kutaka kumwaga Damu?
Natamani sana kujibu kwa Lugha rahisi ,ila changamoto kubwa ni kuwa Upo Ignorant kwenye Dini ya Uislamu....Ila Nitajibu kiurahisi ili ieleweke kama Ifuatavyo.....Uislamu haufundishi kumwaga Damu Aidha kwa vita ,au yale mambo yaliyofanyika ya kigaidi kama yaliyofanywa na kina Osama Bin Laden,au vikundi mbalimbali vya kigaidi ikiwemo ISIS ,Hamas Israel,Al Shabab na vyenginevyo ambavyo wengi huviusisha na Mwenendo wa Uislamu...Osama Bin Laden, na Makundi mengine ya kigaidi ,ni magaidi kama Magaidi wengine ambao wanafanya Ugaidi wao wakijificha nyuma ya pazia la Uislamu ,Mara nyingi Makundi haya ya kigaidi na Magaidi hawa wanafanya mauaji na kusababisha kadhia mbalimbali ikiwemo kulipua Majengo, wakisingizia Wanafanya hivyo kwasababu ni "Jihad"....Maana ya Jihadi ni kupigania Dini ya mwenyezimungu ,Jihadi kubwa katika Uislamu ,ni Jihadi ya Nafsi ,ambayo hii ni Jihadi mtu anayoifanya kwa ajili ya kuzuia nafsi yake isitende matendo maovu, kama kuiba, kuzini ,Kuua nk....Jihadi ndogo ni Jihadi ya kivita ambayo ikilazimika na kukiwa hakuna njia ya kuepusha mmoja anapambania dini yake kwa njia ya Kutumia nguvu(Vitani) pindi inapobidi mfano Vita vingi vilivyopiganwa waislamu walichokozwa na waliwekwa to the point of no return ni aidha wapigane au Dini yao iuliwe moja kwa moja na wapoteze kila kitu ikiwemo Uhai wao(Vita vyote ukisoma "Historia ya Uislamu " utaelewa na sababu zake")...Aina hii ya jihadi ni vita ya uso kwa uso ,jeshi na jeshi, sio kulipua majengo,sio kukamata watu na kuchinja ,sio kujilipua kwenye ndege,sio kulipua magorofa lahasha......Hayo ni matendo ya watu ambao ni magaidi ,na gaidi anaweza kuwa Muislamu au dini nyengine, na akifanya hivyo au wakifanya hivyo ,hata kama wote ni waislamu haimaanishi kuwa Uislamu unafundisha Ugaidi....Tuendelee ,Katika hiyo Jihadi ya Vita ,kuna sheria zipo wakati wa kupigana na baada ya kupigana miongoni mwa sheria ni Kukatazwa Kuharibu au kukata miti au njia yoyote ya kuharibu mazingira,Wanawake hawaruhusiwi Kuuliwa au kufanyiwa uhalifu wowote ,Na pindi adui atakapojisalimisha ,harushusiwi kuuliwa ....Hizo ni baadhi ya Sheria zilizopo katika vita ya Jihadi....Kwa Muhtasari huo ningependa kuhitimisha kukufungua ,kukuambia kuwa Hao Magaidi ambao ni waislam au pengine sio waislam ila wanajificha nyuma ya Mgongo wa Uislamu(Mfano hawa ISIS ni Organization inasemekana inakuwa run by American Government ,it's a propaganda, yeah lakini there must be something in it)..Kwakuhitimisha Hao magaidi mnaowaita waislamu ,though huenda ni waislam ,matendo yao wanafanya kwa Matakwa yao wenyewe ,ila Uislam haufundishi kumwaga Damu wengi wanasingizia ,"JIHADI" ,Lakini baada ya kukuelezea kwa Ufupi maana ya Jihad Utajua kuwa wako Ignorant ,hawajaelewa au wameelewa Ila Ni wanafanya Makusudi wakijificha nyuma ya Kivuli cha Uislamu.Wanafanya Hivyo na wataendelea kufanya hivyo because wanakitu cha kusingizia na Kujustify Ukatili wao ,wakidai wanafanya wachofanya In the Name of Allah and Jihad..."Na watawaaminisha Watu kama wewe kuwa Islam Teaches evil na Muslims are proud killing and bombing innocents, (Hata Atheists hawawezi fanya hiki kitu)"
UKITAKA KUULEWA UISLAMU NI LAZIMA USOME NA NDIO UJUDGE ,UISLAMU HAUFUNDISHWI KWA KUJUDGE CHARACTERS ZA WATU LAHASHA ,UTALETA WRONG CONCLUSIONS...."Kasome FIQH ya Usilamu ,au sheria Katika Dini ya Uislamu au Kasome Historia ya Uislamu".......Islam means Peace ..Maadui wanapambana kuvuruga hii Peace...By the way ISLAM is the Fastest growing religion in the world currently Despite hivyo vitu vyote Ulivyongea ,Vinavyotokea na Vilivyotokea...UKITAKA KUELEWA ZAIDI PLEASE UKASOME USIANGALIE MATUKIO YANAYOTOKEA NCHI ZA KIISLAMU..
 

Attachments

  • Screenshot_20240322-155914_X.jpg
    Screenshot_20240322-155914_X.jpg
    465.4 KB · Views: 3
  • Screenshot_20240322-155914_X.jpg
    Screenshot_20240322-155914_X.jpg
    465.4 KB · Views: 3
Yesu: aliyeniona Mimi, amemwona Mungu. (Yohana 14:5-9).


Unaweza kufafanua maana ya maandiko haya?

^Tumfanye mtu katika mfanano Wetu, katika sura Yetu^ (Mwanzo 1:26).

^Bwana Mungu akasema: Basi, huyu mtu amekuwa kama mmoja Wetu...^ (Mwanzo 2:22).

Hicho kiwakilishi cha nafsi ya kwanza wingi (^wetu^ na ^yetu^) humaanisha nini?

Unaelewaje? Kwa sababu Mungu ndiye anazungumza hapo.

Soma pia:

Yohana 1:1-4 Neno (Kristu) alikuwa Mungu kabla hajaja duniani na kufanyika mwanadamu.

Wakolosai 1:16, 17 Ndiye Muumbaji wa vyote, mbinguni & duniani.


"mfano wetu" pekee na inamaanisha tu kujua Mema na mabaya katika Biblia (Luka 2:52: MUNGU alisamehe dhambi za Yesu na alikuwa "mfadhili" pamoja naye).

Hii inafanya "sura yetu (au mfano)" na "mfano wetu" kurejelea na kumaanisha kitu kimoja.

Katika sehemu inayofuata hapa chini, tutaona ulinganisho kati ya mali ya miili yetu ya kibinadamu na ya MUNGU Mwenyezi na kuona jinsi ambavyo haiwezekani kwa miili yetu ya kimwili kufanana na ya MUNGU Mwenyezi, kwa vile viungo vyetu vya kimwili (mapafu, mioyo, uume, matako, sivyo? ini, figo n.k.. vyote vilitengenezwa na kubuniwa ili kutusaidia kuishi hapa duniani).

Lakini kwanza, acheni kwanza tuangalie baadhi ya mifano mingi ya usemi wa sitiari ulio katika Biblia ili msomaji aweze kufahamu na kuelewa jinsi mambo nyakati fulani yanavyoandikwa katika Biblia, na maana yake hasa.

Jaribu la mfano la MUNGU Mwenyezi:

Luka 11

2 Akawaambia, “Mnaposali, semeni: ‘Baba, jina lako litukuzwe, Ufalme wako uje.

3 Utupe kila siku mkate wetu wa kila siku.

4 Utusamehe dhambi zetu, kwa maana sisi pia tunamsamehe kila mtu anayetukosea. Wala usitutie majaribuni.' "
5 Kisha akawaambia, Tuseme mmoja wenu ana rafiki, akamwendea usiku wa manane na kumwambia, Rafiki, nikopeshe mikate mitatu;

Lakini, MUNGU MWENYE NGUVU HAJARIBU:

Yakobo 1
13Mtu akijaribiwa asiseme, Mungu ananijaribu. Kwa maana Mungu hawezi kujaribiwa na uovu, wala yeye hamjaribu mtu ye yote;

14lakini kila mmoja hujaribiwa anapovutwa na kudanganywa na tamaa yake mwenyewe.

15Kisha tamaa ikiisha kuchukua mimba huzaa dhambi; na dhambi ikiisha kukomaa huzaa mauti.

Luka 11:2-5 na Yakobo 1:13-15 hapo juu, zinathibitisha wazi kwamba MUNGU Mwenyezi haruhusu shetani atujaribu, si sisi tu bali pia Manabii wake.



Mkono wa MUNGU Mwenyezi:

1 Samweli 5

9 Lakini baada ya kuuhamisha, mkono wa BWANA ukawa juu ya mji ule, na kuutia hofu kuu. Aliwatesa watu wa jiji, vijana kwa wazee, kwa mlipuko wa uvimbe.

10 Basi wakalipeleka sanduku la Mungu Ekroni. Sanduku la Mungu lilipoingia Ekroni, watu wa Ekroni walipiga kelele, “Wamelileta sanduku la mungu wa Israeli karibu nasi ili kutuua sisi na watu wetu.

11 Basi wakawaita wakuu wote wa Wafilisti, wakasema, Liondoeni sanduku la mungu wa Israeli, lirudi mahali pake, la sivyo litatuua sisi na watu wetu. Kwa maana kifo kilikuwa kimeujaza mji hofu; Mkono wa Mungu ulikuwa mzito sana juu yake.

Mistari hiyo ni wazi haizungumzii juu ya Mkono wa kimwili wa MUNGU Mwenyezi, Mkono na Vidole.
 
Kanuni ni rahisi sana;-

Uislam:-ujamaa

Ukristo:-ubepari

Sisi tulioamua kuwa huru tupo mixed!!
Nchi nyingi za kiislamu ziko chini ya Ubepari... Nyingine ni mixed economy za Ubepari na Miongozo ya Dini kama Iran na Iraq ambazo dini ndio inaongoza
Here are the Arab nations typically recognized as having capitalist economies:

1. Saudi Arabia
2. United Arab Emirates
3. Qatar
4. Kuwait
5. Bahrain
6. Oman
7. Jordan
8. Lebanon
9. Egypt
10. Tunisia
11. Morocco
12. Algeria
13. Sudan
14. Palestine (West Bank and Gaza Strip)
15. Mauritania
16. Yemen


These countries have market-oriented economies where private ownership of property and the means of production predominates, with varying levels of government regulation and involvement in economic activities.
 
"mfano wetu" pekee na inamaanisha tu kujua Mema na mabaya katika Biblia (Luka 2:52: MUNGU alisamehe dhambi za Yesu na alikuwa "mfadhili" pamoja naye).

Hii inafanya "sura yetu (au mfano)" na "mfano wetu" kurejelea na kumaanisha kitu kimoja.

Katika sehemu inayofuata hapa chini, tutaona ulinganisho kati ya mali ya miili yetu ya kibinadamu na ya MUNGU Mwenyezi na kuona jinsi ambavyo haiwezekani kwa miili yetu ya kimwili kufanana na ya MUNGU Mwenyezi, kwa vile viungo vyetu vya kimwili (mapafu, mioyo, uume, matako, sivyo? ini, figo n.k.. vyote vilitengenezwa na kubuniwa ili kutusaidia kuishi hapa duniani).

Lakini kwanza, acheni kwanza tuangalie baadhi ya mifano mingi ya usemi wa sitiari ulio katika Biblia ili msomaji aweze kufahamu na kuelewa jinsi mambo nyakati fulani yanavyoandikwa katika Biblia, na maana yake hasa.

Jaribu la mfano la MUNGU Mwenyezi:

Luka 11

2 Akawaambia, “Mnaposali, semeni: ‘Baba, jina lako litukuzwe, Ufalme wako uje.

3 Utupe kila siku mkate wetu wa kila siku.

4 Utusamehe dhambi zetu, kwa maana sisi pia tunamsamehe kila mtu anayetukosea. Wala usitutie majaribuni.' "
5 Kisha akawaambia, Tuseme mmoja wenu ana rafiki, akamwendea usiku wa manane na kumwambia, Rafiki, nikopeshe mikate mitatu;

Lakini, MUNGU MWENYE NGUVU HAJARIBU:

Yakobo 1
13Mtu akijaribiwa asiseme, Mungu ananijaribu. Kwa maana Mungu hawezi kujaribiwa na uovu, wala yeye hamjaribu mtu ye yote;

14lakini kila mmoja hujaribiwa anapovutwa na kudanganywa na tamaa yake mwenyewe.

15Kisha tamaa ikiisha kuchukua mimba huzaa dhambi; na dhambi ikiisha kukomaa huzaa mauti.

Luka 11:2-5 na Yakobo 1:13-15 hapo juu, zinathibitisha wazi kwamba MUNGU Mwenyezi haruhusu shetani atujaribu, si sisi tu bali pia Manabii wake.



Mkono wa MUNGU Mwenyezi:

1 Samweli 5

9 Lakini baada ya kuuhamisha, mkono wa BWANA ukawa juu ya mji ule, na kuutia hofu kuu. Aliwatesa watu wa jiji, vijana kwa wazee, kwa mlipuko wa uvimbe.

10 Basi wakalipeleka sanduku la Mungu Ekroni. Sanduku la Mungu lilipoingia Ekroni, watu wa Ekroni walipiga kelele, “Wamelileta sanduku la mungu wa Israeli karibu nasi ili kutuua sisi na watu wetu.

11 Basi wakawaita wakuu wote wa Wafilisti, wakasema, Liondoeni sanduku la mungu wa Israeli, lirudi mahali pake, la sivyo litatuua sisi na watu wetu. Kwa maana kifo kilikuwa kimeujaza mji hofu; Mkono wa Mungu ulikuwa mzito sana juu yake.

Mistari hiyo ni wazi haizungumzii juu ya Mkono wa kimwili wa MUNGU Mwenyezi, Mkono na Vidole.
42f6ba9d06e483bd0c1027b0b12c919b.jpg
 
Ni rahisi sana kumtawala mtu mweusi nani aliyoanzisha neno gaidi au terrosrism na akatunga hadi na sheria zake na kutaka nchi zote duniani zitumie sheria hiyo?
Unajua kwamba mandela nae aliitwa gaidi na hao hao waliokufundisha hilo neno?
Kwa akili yako wale wazungu au marekani kwa nini anaweka base kwenye nchi za kiarabu kama hana maslahi mapana na kuamua nani awe raisi na nani asiwe raisi ?

Marekani na israel wanatafuta nini syria hadi leo?
Kulikuwa na sababu gani ya westerners kutaka kumtoa gadafi madarakani na kumuua ?
Kulikuwa na sababu gani za marekani na washirika wao kumtoa na kumuua saddam hussein ?
Tatizo la africa ni elimu bado tunakaririshwa hatuwezi kufikiri
Jana lile tukio la russia, skynews wakasema ni isis kwenye comments wazungu wote wakakataa wakasema isis of cia, ila mswahili wa mbagala ukishasmbiwa tu na cnn ni isis tayari unaanza kuja kubwabwaja humu bila ya hata kufikiria
Mimi sizungumzii mzungu au Israel... Nimezungumzia kwa nini Magaidi wengi wanahusishwa na Uislamu na si Uhindi au Ubudha au Ukristo
 
  • Thanks
Reactions: 511
Mimi sizungumzii mzungu au Israel... Nimezungumzia kwa nini Magaidi wengi wanahusishwa na Uislamu na si Uhindi au Ubudha au Ukristo
Ongezea pia kwaajili ya kulaaniwa wengi wao ndiyo maana wametupwa kuishi jagwani.
 
Yesu: aliyeniona Mimi, amemwona Mungu. (Yohana 14:5-9).


Unaweza kufafanua maana ya maandiko haya?

^Tumfanye mtu katika mfanano Wetu, katika sura Yetu^ (Mwanzo 1:26).

^Bwana Mungu akasema: Basi, huyu mtu amekuwa kama mmoja Wetu...^ (Mwanzo 2:22).

Hicho kiwakilishi cha nafsi ya kwanza wingi (^wetu^ na ^yetu^) humaanisha nini?

Unaelewaje? Kwa sababu Mungu ndiye anazungumza hapo.

Soma pia:

Yohana 1:1-4 Neno (Kristu) alikuwa Mungu kabla hajaja duniani na kufanyika mwanadamu.

Wakolosai 1:16, 17 Ndiye Muumbaji wa vyote, mbinguni & duniani.

‘ushahidi’ wa uungu wa Yesu ulionukuliwa sana ni Yohana 1:1 na 14, “Hapo mwanzo kulikuwako Neno, naye Neno alikuwako kwa Mungu, na Neno alikuwa Mungu… Naye Neno alifanyika mwili, akakaa kwetu; nasi tukauona utukufu wake, utukufu kama wa Mwana pekee atokaye kwa Baba; amejaa neema na kweli.”

Hata hivyo, maelezo haya hayakutolewa na Yesu Kristo, wala hayakuhusishwa naye na mtunzi wa Injili kwa mujibu wa Yohana.

Hivyo, mistari hii haiundi ushahidi wa uungu wa Yesu, hasa hasa kuzingatia shaka inayoshikiliwa na wasomi wa Kikristo juu ya Injili ya Nne. Wasomi wa Biblia waliotunga Injili tano:

“Picha mbili zilizochorwa na Yohana na muhtasari wa injili (yaani Injili ya Mathayo, Marko na Luka) zote mbili haziwezi kuwa ubainifu wa kihistoria.

Neno lilohusishwa na Yesu katika Injili ya Nne limeundwa na wainjilisti kwa sehemu kubwa, na linaakisi mwendelezo wa lugha ya jamii ya Wakristo wa Kiyohana.

Neno la Kigiriki lilotumiwa na mtunzi wa Injili ya Nne asiyejulikana kwa “neno” ni logos.

Kwa kufanya hivyo, huyo mtunzi anamtambulisha Yesu kwa logos la wanafalsa wapagani wa Kigiriki, neno ambalo lilikuwa na lengo takatifu na thabiti lililojitokeza ulimwenguni, huyo mtunzi akalipangilia neno hilo na kulipa mfumo na maana.

Wazo la logos katika fikra za Kigiriki huenda linarejea nyuma, kwa uchache hadi kwa mwanafalsafa wa karne ya sita BC, Heracleitus, aliyependekeza kuwa, kulikuwa na logos ulimwenguni anayetenda kwa mwanadamu kulingana na nguvu ya hoja.

Baadaye, Stoics analitambulisha logos kuwa ni tendo, mantiki, na kanuni ya kiroho inayosambaa katika ukweli wote.

Mwanafalsafa wa Kiyahudi anayeongea Kigiriki, Judaeus Philo wa Alexandria (15 BC -45 CE), amefundisha kuwa logos alikuwa ni mpatanishi baina ya Mungu na ulimwengu, kwa kuwa na sifa mbili za uwakala wa Mungu na ulimwengu, na kuwa na sifa mbili za uwakala wa viumbe na wakala wa ambaye kupitia kwake akili ya mwanadamu inaweza kumfahamu Mungu.

Maandiko ya Philo yalihifadhiwa na kutunzwa na kanisa, na kueneza ufunuo kwa mafundisho ya kistaarabu ya tiolojia ya kifalsafa ya Kikristo. Aliacha mafundisho ya fikra za Kipilato wakichukulia logos (Neno) na kuliita “mtoto wa kwanza wa kuzaliwa na Mungu.”

Utambulisho wa Yesu kwa logos, uliendelezwa katika kanisa la kwanza ikiwa ni tokeo la majaribio yaliyofanywa na wanatiolojia wa kwanza wa Kikristo pamoja na watetezi kuielezea imani ya Kikristo kwa istilahi ambayo ingekuwa wazi kwa ulimwengu wa Wayunani.

Zaidi ya hayo, ilikuwa ni kuwavutia wasikilizaji wao na mtazamo wao kuwa Ukristo ulikuwa unashinda, au mrithi wa wale wote waliokuwa wanafalsafa bora wa kipagani.

Kwa hiyo, katika kazi zao za utetezi na ubishani, Mapadri wa Kikristo wa kwanza wameeleza kuwa Yesu alikuwa ni logos aliyekuwepo hapo kabla.

Neno la Kigiriki lililotumika kwa maana ya ‘Mungu’ katika hiyo ibara ni “na Neno lilikuwa kwa Mungu,” lipo katika mtindo wa “definite form- yaani mtindo uliowazi, au unaofahamika” batheos, Linalomaanisha “Huyo Mungu, au Mungu maalum”.

Hata hivyo, katika ibara ya pili “na Neno alikuwa Mungu”, neno la Kigiriki lililotumika kwa maana ya ‘Mungu’ katika ibara lipo katika mtindo wa “indefinite form- yaani mtindo usiowazi, au usiofahamika” tontheos, Linalomaanisha ‘mungu yoyote, yaani mungu asiyejulikana, au mungu yoyote asiye maalumu’.

Kwa hiyo, Yohana 1:1, kwa uwazi zaidi ilipaswa itafsiriwe, “Hapo Mwanzo kulikuwa na Neno, na hilo Neno lilikuwa kwa Mungu, na hilo Neno lilikuwa mungu mwingine.” Kwa hiyo, kama hilo neno lilikuwa mungu mwingine kwa ufahamu wa kifasihi, itamaanisha kuwa kulikuwa na miungu miwili na sio mmoja.

Hata hivyo, katika lugha ya Kibiblia, neno ‘mungu – asiyefahamika’ linatumika kwa maana ya istiari ili kuashiria nguvu. Kwa mfano, Paulo alimtaja shetani kuwa ni ‘mungu – asiyefahamika’ katika 2 Wakorintho 4:4, "ambao ndani yao mungu wa dunia hii amepofusha fikira zao wasioamini, isiwazukie nuru ya injili ya utukufu wake Kristo aliye sura yake Mungu."

Pia, Musa alitajwa kama ni ‘mungu – asiyefahamika’ katika Kutoka 7:1, "BWANA akamwambia Musa, Angalia, nimekufanya wewe kuwa Mungu kwa Farao; na huyo ndugu yako Haruna atakuwa nabii wako.
 
Pili,Hoja ya jihadi ni kutetea maslahi yako ikiwa hayajafikiwa na hasa kuhusu imani ukiona kuna mambo ya jihadi ujue ni mambo ya ndani ya nchi kuwa wananchi wamezuiwa kusali au dini imekejeliwa hapo jihadi ndiyo itafanyika ila siyo baina ya nchi na nchi.
Ukifanya Jihad na kuua watu basi hiyo ndio Ugaidi
 
Shia hawawez kuudhalilisha uislamu kwa kuwatukana, kubeza na kudharau maswahaba. Pia hawawez kumtukana mke wa kipenzi chetu eti kahaba. Lazima pachimbike maamaee

Wewe unaingia kwa id nyingi unafikiri hatukuoni , unaingia kuvuruga tu na kubadilisha hoja
 
Mimi sizungumzii mzungu au Israel... Nimezungumzia kwa nini Magaidi wengi wanahusishwa na Uislamu na si Uhindi au Ubudha au Ukristo
Kwa sababu aliyeanzisha huo mfumo wa kutengeneza vikundi alivianzisha vingi huko nchi za kiarabu kugawa watu ili kuingiza malengo yake ikiwemo kuweka viongozi anayewataka yeye na kuweza kutumia na kucontrol rasilimali zao hiyo haihitaji elimu kubwa kugundua na hadi leo anavifinance yeye.
Huoni ajabu jana baada ya mlipuko tu isis kajitokeza faster kama yeye ndio kafanya na wahusika wamekamatwa border ya ukraine,na marekani anasisitiza hao ni isis, ni rahisi kwa wajinga huku africa kuwadanganya ila mrusi picha lote analijua na ameshaanza kudeal nao
 
Wewe unaingia kwa id nyingi unafikiri hatukuoni , unaingia kuvuruga tu na kubadilisha hoja
Waislam tukicheza na kukaa kimya tutakosa janah na firdaus siku ya qymah. Haiwezekani Iran na shia wawadhalilishe na kuwatukana maswahaba. Haiwezekani hawa makafir Iran na Shia wamuite mke wa kipenzi chetu Kahaba. Halafu ummah wa uislamu umekaa kimya tu. La hasha sojood inatakikana kwa sana
 
Ukifanya Jihad na kuua watu basi hiyo ndio Ugaidi
kulingana na tafsiri yako,,,,,kwani bible inasemaje kuusu kuuwa?katiba hazitoi pia haki ya kuuwa ikiwa imethibitishwa na mahakama?

hao NATO hawauwi watu kwa maslahi ya nchi yao?iweje muislamu akitaka kuikomboa dini na imani yake aonekane ni gaidi?
 
Waislam tukicheza na kukaa kimya tutakosa janah na firdaus siku ya qymah. Haiwezekani Iran na shia wawadhalilishe na kuwatukana maswahaba. Haiwezekani hawa makafir Iran na Shia wamuite mke wa kipenzi chetu Kahaba. Halafu ummah wa uislamu umekaa kimya tu. La hasha sojood inatakikana kwa sana

KAFIRI WEWE MBONA HWISHII KUKERA WATU UNATAKA KUVURUGA UZI`` umechanganyikiwa
 
Waislam tukicheza na kukaa kimya tutakosa janah na firdaus siku ya qymah. Haiwezekani Iran na shia wawadhalilishe na kuwatukana maswahaba. Haiwezekani hawa makafir Iran na Shia wamuite mke wa kipenzi chetu Kahaba. Halafu ummah wa uislamu umekaa kimya tu. La hasha sojood inatakikana kwa sana
hujielewi
 
Vietnam
Russia
Ukraine
Drc
Hizo zote nchi za kiislam
Vietnam, Russia, Ukrein sio nchi zenye kukumbwa na Ugaidi wa mara kwa mara... Japo Urusi juzi kavamiwa na Magaidi ambao abajiita ISIS yani Islamic State
 
Kama ningekuwa mkristo wallah kwakufuata hoja zenye akili ningesilimu chap

Katika biblia kuna mambo yanajichanganya sana kwakweli,,, ndio maana viongozi wao hawatakagi maswali.

Namshukuru Allah kwa hii neema ya uislamu.
 
Back
Top Bottom