Kwanini ndugu zetu wazaramu wanawapa watoto majina fikirishi?

Kwanini ndugu zetu wazaramu wanawapa watoto majina fikirishi?

Kuna siku nilisoma story ya jamaa kubakwa mahabusu Hadi kufa...alikuwa anaitwa Hasara Omary..
Kila siku nilikuwa najiuliza kama jina lilichangia kumpa matatizo
Japo bado ni myth lakini si vyema kumpa mtoto majina ya aina hiyo. Sijawahi sikia mtu anaitawa ibilisi au yuda iskarioti
 
Kuna makabila mengi majina yao yana maana fikirishi . Kuna mtu tafsiri ya jina lake ni mwanjaaa/njaa (nyanzala/ mayala), mtembezi ( nyamisi) cha pombe, chausiku/usiku(nyangeta) shida (makoye), nk
wenye majina yenye maana nzuri angalau ni wanyakyusa na waha
Tafiti zifanyike kama kuna uhusiano wa jina la mtoto na maisha anayokabili
 
Tafiti zifanyike kama kuna uhusiano wa jina la mtoto na maisha anayokabili
Hakuna haja ya utafiti. Yaani jina ndio kila kitu. Labda tu kuwe na utaratibu wa mtoto kuchagua jina analotaka baada ya kufikisha umri fulani.

Kwasababu tupo wengi tusiopenda majina tuliyopewa na wazazi wetu na ndio maana tunajipa majina mbadala (nickname). Kuna watu majina yao yamebeba tafsiri halisi ya maisha yao na ndivyo walivyo
 
Hakuna haja ya utafiti. Yaani jina ndio kila kitu. Labda tu kuwe na utaratibu wa mtoto kuchagua jina analotaka baada ya kufikisha umri fulani.

Kwasababu tupo wengi tusiopenda majina tuliyopewa na wazazi wetu na ndio maana tunajipa majina mbadala (nickname). Kuna watu majina yao yamebeba tafsiri halisi ya maisha yao na ndivyo walivyo
Tafiti zitajibu maswali mengi na kutoa shuhuda zinazo thibitishwa na numbers, bado kuna haja ya kufanya tafiti
 
Amani iwe nanyi

Wakati tunakua, bado Dar es Salaam ilikua na wazaramu wengi na nilibahatika kusoma na watu wenye majina kama SIKITU, SIWATU, SIWAZURI, TABU, MATESO, HAVINITISHI, SIKUDHANI, KIDAWA, CHAUREMBO na majina mengi ya namna hiyo.

Sasa, sijui hekima ya wazee wa kizaramo ilikua ina kusudia nini?

Wakati mwingine, though it is a myth, jina linaweza kubeba au kusadifu aina ya maisha ya huyo mtoto baadae.

Watalaamu embu dadavueni
Nina jamaa yangu anaitwa Mgeni Kifo mtokambali

Sent from my Pixel 3 using JamiiForums mobile app
 
Kwa hiyo kumwita mtoto John, Emmanuel, Abdallah, Mohammed ni sawa.

Ila ukimwita Aishi, Tabu, Ubaya, Apendwae, Aizari, Msiba ,Nyamayao, Cha wote, Mzuri sio sahihi?

Mnajua hata maana na hayo majina mnayojifaharisha nayo?

Mimi katoto kangu ka kike nimekiita SALAMA na WA kiume Aishi akipatikana wa tatu ni TABU.
 
Kwa hiyo kumwita mtoto John, Emmanuel, Abdallah, Mohammed ni sawa.

Ila ukimwita Aishi, Tabu, Ubaya, Apendwae, Aizari, Msiba ,Nyamayao, Cha wote, Mzuri sio sahihi?

Mnajua hata maana na hayo majina mnayojifaharisha nayo?

Mimi katoto kangu ka kike nimekiita SALAMA na WA kiume Aishi akipatikana wa tatu ni TABU.
Huyo CHAWOTE ni mtihani
 
Kuna makabila mengi majina yao yana maana fikirishi . Kuna mtu tafsiri ya jina lake ni mwanjaaa/njaa (nyanzala/ mayala), mtembezi ( nyamisi) cha pombe, chausiku/usiku(nyangeta) shida (makoye), nk
wenye majina yenye maana nzuri angalau ni wanyakyusa na waha
Wanyakyusa, Wapare na Wahaya wana majina yana maana nzuri mara nyingi
 
Back
Top Bottom