Ina Maana yule Mtangazaji Siwatu Luanda, yawezekana alikuwa Mzaramu?Majina ya wazaramu Yana message ...
Mara nyingi yalikuwa Yana define watu walivyo hasa ukweni ..
Binti akiolewa jinsi atakavyo pokelewa ukweni ndo atakavyo toa majina Kwa watoto wake....Sikudhani...manake hakudhani Hali iko kama alivyoikuta huko ukweni ..Siwatu...manake familia ya mume sio watu...labda wanamtesa...Sikitu manake hakuna shida atavumilia Tu n.k n.k Siwazuri...,Mateso n.k mostly huwa ni mama alieolewa ana define wakwe au majirani.....wazaramo wenyewe wanajua
Kuna jamaa nilisoma naye anaitwa Tangazo Mwanza.Akina sinaubaya, havijawa, bahati, ...
Ni vile tu wao wanatumia kiswahili. Wengine wanatumia zaidi ya 'kilugha'
Japo ukienda usukumani wapo akina cherehani, bakuli, sahani, majaba
Wapo, Siwatu umewai lisikia?Ila hili sijawah skia "HAVINITISHI"
Ingekua hivyo angeitwa Mwadhani, tafuta maana ya neno mwazani kwa kindengereko au kizaramo.Mwazani huwa ni kifupi cha mwana wa Ramadhani kama baba yake ni ramadhani au kazaliwa mwezi wa Ramadhani kama ilivyo Mwajuma, Mwanaaly, Mwashabani , Mwanaheri, Mwanaenzi, Mwarashi, Mwadawa, Mwamtumu, Mwahija nk.
Mwarami maana yake ni nini? Nilidhani ni la kidini.🤣🤣 wakina somoe, kaisi, sikitua, siwema, mpenzi, Jongo, Lipipa, Litanda, Tabu mfuko, Siwazuri, Sijali, Stumai, Madai, Mwarami 🤣🤣.
Kwa nini apigike, nan anamfanya apigike ?Ni fikirishi sana, nadhani hawawazi madhara yake kwa huyo mtoto, mfano ukimwita SHIDA mtoto si anaweza pigika maisha yake yote?
SiwajibuAmani iwe nanyi
Wakati tunakua, bado Dar es Salaam ilikua na wazaramu wengi na nilibahatika kusoma na watu wenye majina kama SIKITU, SIWATU, SIWAZURI, TABU, MATESO, HAVINITISHI, SIKUDHANI, KIDAWA, CHAUREMBO na majina mengi ya namna hiyo.
Sasa, sijui hekima ya wazee wa kizaramo ilikua ina kusudia nini?
Wakati mwingine, though it is a myth, jina linaweza kubeba au kusadifu aina ya maisha ya huyo mtoto baadae.
Watalaamu embu dadavueni
La kidini hilo.Mwarami maana yake ni nini? Nilidhani ni la kidini.
Asante Mkuu, manake kuna mchagga anaitwa hivyo.La kidini hilo.
Muharami ni sawa na Shaaban na Ramadhani.
Majina ya miezi.
Wapo bunge, mfano Mbunge wa mbagara anaitwa chaurembo.. na kuna Mbunge wa Lindi alikuwa anaitwa Bwege.Majina hayo kuyakuta bungeni au wizarani nipo pale
TAIFA SECONDARY
Sio la kidini.... ila maana yake sijuiMwarami maana yake ni nini? Nilidhani ni la kidini.
Maana nimepata na nila kidini.Sio la kidini.... ila maana yake sijui
Nini maana yake?Maana nimepata na nila kidini.
Ni jina la kidini lenye maana ya Mwezi kama Shabani au Ramadhani.Nini maana yake?
Hayo majina huwa yana maana hawayatoi tu, mfano kama Mimi Dada yangu anaitwa Semeni ni kwa sababu baba yetu alikuwa mweusi sana lakini Dada yangu akatoka mweupe sana sasa maneno yakawa mengi sana ndipo akapewa jina la Semeni. Na Dada yangu mkubwa anaitwa Sikujua ni kwa sababu mama yetu alisumbuliwa sana na uzazi na maneno yakawa mengi maana walimkatia tamaa kabisa lakini baadae akapata mtoto akampa jina la Sikujua. Hivyo kwa Mimi naona hayo majina kwa wao yanathamani kutokana na matukio.Amani iwe nanyi
Wakati tunakua, bado Dar es Salaam ilikua na wazaramu wengi na nilibahatika kusoma na watu wenye majina kama SIKITU, SIWATU, SIWAZURI, TABU, MATESO, HAVINITISHI, SIKUDHANI, KIDAWA, CHAUREMBO na majina mengi ya namna hiyo.
Sasa, sijui hekima ya wazee wa kizaramo ilikua ina kusudia nini?
Wakati mwingine, though it is a myth, jina linaweza kubeba au kusadifu aina ya maisha ya huyo mtoto baadae.
Watalaamu embu dadavueni