Kwanini Rais Samia anatumia ndege za ATCL kwa safari zake hata fupi badala ya ndege ya Rais?

Kwanini Rais Samia anatumia ndege za ATCL kwa safari zake hata fupi badala ya ndege ya Rais?

Jet Gulf Stream 50
This one?

1629279912768.png
 
Nadhani kuliko ipaki iwe mazalia ya Popo na viumbe wengine ni bora ipashwe pashwe

Hapo kwenye gharama za kuiendesha hio hesabu itiwe kwenye Hasara ya Mwendazake
Kama ni hivyo si ile ya Raisi ndio itapaki?

Kama ni kuzipasha moto, wapunguze nauli iwe kama ya Fast Jet, zitatembea sana
 
Si anaitangaza ATCL,
tena kipindi hiki safari zimepungua ni muhim kweli ikulu waichukue wazunguke nayo kuitangaza ATCL
Kwa hiyo ni sawa serikali kuzitumia bila busara?

Hata Ethiopian Airways, Rwandair, ni ndege za serikali.
 
Hao Malawi wana viwanja vikubwa tu, kama kile cha Blantyre na Lilongwe vya kuweza kutua ndege kubwa tu, na hata Air Malawi wana Airbus na Boeing 747 na Bombadier za kutosha zinazofanya safari zake ndani na nje ya nchi...

Hivi Malawi wana uwanja wa ndege kubwa kama airbus yetu kutua? Mi nadhani unatua kwanza Botswana au namibia halafu unavuka na gari Malawi. Mimi nilijua ni hizi cassena ndege za umwagiliaji wa pembejeo ndo zinaweza kutua Malawi.

barafu
J
 
Acha mama angalau aipashe moto Airbus yetu vinginevyo inge-park tu airport hatimaye ipate kutu!
Si watupe basi tuifaidi angalau kwa laki Dar Mwanza kama tatizo ni kuipasha moto!

Hata wakisema hizi ni safari za ilani ya uchaguzi ya CCM hatuna tatizo, tutapanda tu, "Wahi Mwanza na ATCL kwa laki moja!"
 
Nimeona katika picha Rais Samia alitumia ndege ya ATCL Airbus 220 5H-TCH (Dodoma - Hapa Kazi Tu) kwenda Malawi kwenye mkutano wa SADC. Ndege hii ina uwezo wa kubeba abiria kama 120 hivi.

Sio kwamba ninataka tu kumkosoa Rais Samia, lakini najiuliza sana, kwamba ni kwa nini anapofanya safari kama hizi fupi za kwenda hapa karibu Malawi anatumia ndege kubwa ya ATCL badala ya ndege ya Raisi ambayo iliponunuliwa tuliambiwa hata kama ni kula nyasi ili inunuliwe basi tungekula?

Nina uhakika ndege kama Airbus 220 ina gharama kubwa zaidi kumpeleka Samia na ujumbe wake Malawi kuliko angetumia ndege ya Raisi. Na kama watasema walihitaji Airbus 220 kwa sababu ya kuwa na ujumbe mkubwa, ni kwa nini waende na ujumbe mkubwa katika mkutano huu wa SADC wa siku mbili sijui?

Mie nadhani wakati Watanzania tunaambiwa tuvumilie tozo ili kuendeleza miundo mbinu na uchumi kwa ujumla, basi na watu kama Rais Samia wawe na ufikirio wa matumizi ya fedha za serikali kwa kuwa na busara katika vitu kama hivi. Mie sioni sababu ya Rais kutumia ndege za ATCL wakati kuna ndege ya Rais iliyonunuliwa mahsusi kwa ajili ya safari za Rais, na ina uwezo wa kwenda hadi USA.

Na sitegemei watatuambia kwamba hawakuitumia hii Airbus 220 bure bali waliikodi toka ATCL na kulipia, kwa sababu hizo fedha za kukodi pia ni fedha zetu za tozo na zinatuuma.
ATCL haina ndege, ndege ni za Serikali ambazo zinakodishwa.
 
Back
Top Bottom