Kwanini Serikali inawabagua walimu wenye shahada kwenye ajira?

Kwanini Serikali inawabagua walimu wenye shahada kwenye ajira?

Ndio sikatai tofauti ipo lakini ni kidogo wewe ambacho huelewi ni nini mkuu?

Nyie ndio mnafanya walimu waendelee kulipwa maslahi duni kwasababu ya kutaka kuaminisha jamii kwamba walimu wenye shahada wanalipwa mishahara mikubwa wakati sivyo.
Tofauti ipo umeambiwa.
Mbona u mbishi sana mwalimu?
 
Kuna upungufu mkubwa kwenye diploma na cheti kwenye mashule ya serikali kuliko shahada.
Ila ili.uajiri inakubidi uzingati
Bajeti
Mahitaji
Vipaumbele vya kimkakati.
 
Mkuu kwa upande wa O' level walimu wenye shahada ndio wanafundisha kidato cha 3&4 huku walimu wenye diploma wakifundisha kidato cha 1&2. Mbali na O'level wenye shahada ndio wanafundisha advance na vyuo vya kati kwahiyo kwa kuangalia tu utaona jinsi walivyo na wigo mpana wa ajira lakini serikali haiwaajiri kwanini?
Iyo ni sheria au unahisi...wapo walimu wengi wa diploma wqnafundisha form 3 na form four.
Shahada ni added advantage tu ila shahada wanafundisha olevel na advance ndio kwao
 
Kwa hiyo serikali ya Jk ilikuwa na uhitaji mkubwa na pia ilikuwa na pesa nyingi za kuajiri walimu wote walipokuwa wakimaliza chuo?Hii ni kutetea ujinga.
Walianzisha shule nyingi za kata hivyo zikaitaji walimu wengi kwa wakati mmoja.
Je wakati wa magufuli shule ngapi za kata zimeanzishwa kwa winhi km wakati wa kikwete?
Shule ambazo zina upungufu wa dhati ni za primary kuliko sekondary na za sekondary ni zile za pembezoni zaidi..ijapokuwa waalimu wa sayansi bado tatizo ni kubwa zaidi kwenye levo zote za elimu
 
Hivi bado walimu wenye CHETI wanaajiriwa?? My God!!! No wonder wizi wa mitihani ya darasa la saba umekithiri. Karne ya 21,ya kidigitali unaajiri mwalimu wa CHETI?
Kila.mtu ana umubimu wake mkuu
Nimefanya nimegundua walimu wa cheti na diploma wanaandaliwa/wana fundishwa kuwa waoga na walimu wa shahada wanaandaliwa/ wana fundishwa ujasiri na kujiamini. Kama niko wrong nisahihishe mkuu
ukiacha hayo mambo ila walimu wa diploma na cheti wanavaa unifom vyuoni( sijui siku izi ikoje)wanafundishwa ualimu ila wa degree anafundishwa usimamizi wa elimu.
Sehemu kubwa walimu wa cheti na diploma ni wavumilivu wana adopt mazingira mapema.wazuri kwenye taaluma japo kwenye utawala wanaweza wasiwe wazuri.rate yao ya kuacha kazi ya ualimu ni ndogo kuliko wenye shahada.
Sio wanaopenda kuhoji hoji sana hasa mambo yasiyohusu taaluma.
Pia akipata uzoefu akaenda shahada anakua mwalimu bora zaidi kuliko yule wa shahada akaenda uzamili.

Km walimu mpo mtanisahihisha..naomba kuwasilisha
 
Hiyo ilikuwa zamani mkuu...
Kwa sasa wenye degree wapo wengi sana wanaweza kuwapita hata wenye diploma. Mf. Chuo kimoja tu cha Dar (udsm) kinazalisha zaidi ya walimu 2000 kwa mwaka lakini kati ya hao wanaopata fursa za ajira ni chini ya walimu 500 Wengine zaidi ya 1500 wanaachwa. Kwa muktadha kama huo huwezi kusema ratio iko sawa sawa ikiwa idadi ya waajiriwa ni ndogo mara dufu ya idadi ya wanaoachwa...
Tafuta idadi kamili ya universities hapa nchini kisha tafuta idadi kamili ya colleges hapa nchini halafu urudi tena
 
Haya hayana maana. Lete figures za take home tuthaminishe tuone kama viwango vinatofautiana kwa kiasi mnachotaka kutuaminisha.
Piga kwa muda wako makato % ..kila kwa kukusaidia maana
B1 take home 331,000
C1 ......... 418,000
D1....... 565,000
E1.......742,000
F1.......975,000 .

Pia imeongezeka 58,000 kwa kila daraja kutokana 'na kupunguzwa kwa PAYE (LIKU) hivyo utofauti yake kipato kwa daraja unabaki palepale.
NB: Ukinitag sehemu ambayo nimekuaminisha itakuwa ni vyema kuliko kunikusanya kundi moja 'na hao wako ... Nipo humo nafanya kazi humo mwaka wa 11 .. Najua tofauti zake siwezi kukubali huo ujinga kwamba mwalimu 1 wa degree anaweza kulipa sijui wa5 wa diploma SIJUI cheti haipo hiyo
 
Haya hayana maana. Lete figures za take home tuthaminishe tuone kama viwango vinatofautiana kwa kiasi mnachotaka kutuaminisha.
Tatizo lako unachanganya mikopo yako ambayo ni wewe binafsi na take home ya ngazi nyingine

ukitaka kulinganisha take home za salary chukua mtumishi ambaye hana mkopo wowote wa ngazi fulani na ulinganishe na mtumishi wa ngazi fulani ambae hana mkopo wowote uwe wa benki au bodi ya mikopo

tofauti ya mwl mwenye diploma na shahada ni kama sh.120,000 -150,000
 
Tatizo lako unachanganya mikopo yako ambayo ni wewe binafsi na take home ya ngazi nyingine

ukitaka kulinganisha take home za salary chukua mtumishi ambaye hana mkopo wowote wa ngazi fulani na ulinganishe na mtumishi wa ngazi fulani ambae hana mkopo wowote uwe wa benki au bodi ya mikopo

tofauti ya mwl mwenye diploma na shahada ni kama sh.120,000 -150,000
Ubora sasa wameweka mshahara kubaki 1/3 zamani walikuwa wanafuta kabisa kamshahara kote wanakakopa ... Nakumbuka tulianza degree tgsd take home 258,000 ... Nominal 322,000 .. Kikwete akapamdisha ndani ya miaka mitano ikafika hii 716,000 ndio kameongezeka 760,000 (yaani kikwete miaka mitano katoka 322,000 mpaka 716,000 huyu mwamba miaka mitano katoka 716,000 mpaka 760,000)...mitano tenaaaaa
 
Kuna vyuo vya kati 35 vinavyotoa cheti na diploma nchi nzima.
Makadirio ya wahitimu kwa chuo kimoja ni >500 kwa mwaka...
Piga 500 x 35 = 17500 ...hayo ni makadirio ya chini,
Kwahiyo idadi ya walimu wa cheti na diploma wanaohitimu kwa mwaka ni kubwa kuliko degree,
Sawa ila kumbuka college zipo nyingi za degree Kwa walimu mfano udsm ina duce,muce,na udsm na kila mwaka wanagraduate walimu 5000-6000,pia kuna udom -ualim,st Augustine ,Mwenge ,na vipo vingi Tu pia idadi wanaopata na kuhitimu degree ni wengi Sana pia
 
Sawa ila kumbuka college zipo nyingi za degree Kwa walimu mfano udsm ina duce,muce,na udsm na kila mwaka wanagraduate walimu 5000-6000,pia kuna udom -ualim,st Augustine ,Mwenge ,na vipo vingi Tu pia idadi wanaopata na kuhitimu degree ni wengi Sana pia
Karibu kila wilaya tz kuna chuo kiwe cha private au serikali cha ualimu wa cheti.
 
Jibu lako ni hili hapa.

Walimu hao wenye degree ni wachache ukilinganisha na wenye certificate na ndio maana katika kuajiri utaona wao wachache kwa idadi ila kwenye ratio ni sawasawa tu...

Watu wanabwabwaja tu.
umeongea point.
Lakini pia kitu kingine ukiangalia pia shule anazotakiwa kufundisha mwalimu mwenye degree ni high school na ziko chache sana ukilinganisha na shule wanazofanyia kazi walimu wa diploma na certificate ambazo zipo kwenye kila kata.
 
  • TGTS B1 = 419,000/-
  • TGTS C1 = 530,000/-
  • TGTS D1 = 716,000/-
  • TGTS E1 = 940,000/-
  • TGTS F1 = 1,235,000/-
  • TGTS G1 = 1,600,000/-
  • TGTS H1 = 2,091,000/-
  • TGTS I = 2,810,000/-
Daraja b cheti, c diploma , d degree , DARAJA E 'na kuendelea ni upandaji wa madaraja
Huyo D1 wengine kwa ajira hiz mpya wamesain 756K au 750K...sijajua utofaut ni una nini ndn?
 
Huyo D1 wengine kwa ajira hiz mpya wamesain 756K au 750K...sijajua utofaut ni una nini ndn?
Kila daraja lina mwisho wake "Bar"...
Kuna D1,D2,D3 ambapo kuhama kutoka moja mpaka nyingine ni zile annual increment ambazo zipo kisheria Serikali imegomea kuziongeza .. Ukishapanda annualy mara3 unakuwa umefika mwisho wa daraja lako hivyo unatakiwa kupandishwa daraja na kwenda mshahara mpya mf.E1 unaenda hivyohivyo ... Pia kuna kuna kada mfano afya , engeneer, mining wao hawaanzi 'na D wanaanza 'na F... Pia kuna suala la level yake elimu anaweza kuwa 'na degree lakini hajasoma advance level ataanza chini kuliko yule aliyeenda advance level.
 
Tafuta idadi kamili ya universities hapa nchini kisha tafuta idadi kamili ya colleges hapa nchini halafu urudi tena
Mkuu, Colleges ni nyingi lakini zinazalisha wahitimu kwa kiasi kidogo compared to Universities. Chuo kama udsm na matawi yake kinazalisha walimu zaidi ya 6000 kwa mwaka lakini chuo kama Monduli tc kinazalisha walimu 300 tu kwa mwaka. Kwa kuzingatia uwiano huo utaona vinahitajika vyuo (colleges) visivyopungua vitano ili kufikia idadi ya walimu inayozalishwa na chuo(University) kimoja tu cha Udsm. Hapo sijagusia vyuo vingine vinavyozalisha walimu kwa wingi kama udom, rucu, saut et cetera
 
Iyo ni sheria au unahisi...wapo walimu wengi wa diploma wqnafundisha form 3 na form four.
Shahada ni added advantage tu ila shahada wanafundisha olevel na advance ndio kwao
Sio hisia ndivyo mtaala unavyotaka. Mwalimu mwenye shahada anafundisha kuanzia kidato cha tatu hadi cha sita, vyuo vya kati na vyuo vikuu kama tutorial assistant. Hivyo walimu wa diploma wanaofundisha kidato cha 3&4 ni kwa sababu ya emergency kwa shule ambazo zinakuwa na upungufu wa walimu wenye shahada.
 
Huyo D1 wengine kwa ajira hiz mpya wamesain 756K au 750K...sijajua utofaut ni una nini ndn?
Mkuu, saivi hakuna cha D1. Walimu wapya wameanzia kidato cha tatu cha ngazi ya mshahara (D3) ndio maana ya hilo ongezeko
 
Hivi bado walimu wenye CHETI wanaajiriwa?? My God!!! No wonder wizi wa mitihani ya darasa la saba umekithiri. Karne ya 21,ya kidigitali unaajiri mwalimu wa CHETI?
Cheti kitaendelea kuwepo hata karne ya 30. Ni mgawano wa kazi, wa degree ana majukumu yake, wa diploma ana majukumu yake, vivyo hivyo wa cheti. Hata nchi zilizoendelea wenye cheti unawakuta shuleni wakitekeleza majukumu Yao kwa Raha zao.
 
Back
Top Bottom