Kwanini Tanzania hakuna daily briefing juu ya Corona virus pandemic?

Kwanini Tanzania hakuna daily briefing juu ya Corona virus pandemic?

Kwa kuijua nguvu ya shetani mungu akaona amtupe duniani!
Wewe ni nani upambane na mwenye mamlaka ya vizuri vyote vya dunia hii?

Popobawa ni mjukuu wa shetani akikuchapa nao usipotangaza anaweka kambi.
 
Vipi kuzika watu kisirisiri kama misukule siyo dalili ya uchawi?
Kupenda kutangaziwa watu kufa ni dalili ya uchawi Kama alivyo seme mleta mada utalilia vp usikie watu wanakufa? Kama si uchawi nini? Ukisikia vifo ndio Corona itakimbia ama kweli wafuasi wa shetani wako wengi
 
Vipi kuzika watu kisirisiri kama misukule siyo dalili ya uchawi?
Hivi unavyojua mgonjwa wa Corona akifa anazikwaje? Huoni habari/video watu wanapozikwa nchi zozote au labda ulijua ni hapa tu nenda Google kaangalie nchi yoyote unayotaka utaona wagonjwa walio kufa kwa Corona wanavyo zika afadhali yetu huku mnaruhisiwa familia mpaka watu 10
 
Tanzania haina wagonjwa wengi .ugonjwa umedhibitiwa sana nchini.na hivi karibun shughuli zote zitaendelea kama kawaida heko rais magufuli.2020 ni magufuli
 
They must be mad.

Yaani yale maambukizi waliyotuambia yamefikia stage tunaambukizana wenyewe uswahilini yamekauka ghafla, ok utakuwa muujiza wa yale maombi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
wangangi mmengalia jana BBC SWAHILI kupitia starTv? SERIKALI wameamua kutuzika
 
Hao waliopona pia watutangazie.
Mfano Mtwara wamepona wangapi
Mwanza ,Dsm na mikoa mingine wamepona wangapi.
Mh Ummy najua umebanwa umetoka kwenye misingi na kanuni za Afya umeenda kwenye kanuni za mitishamba na ushirikina.
Akifa ndugu yako ndo utaona
 
Tanzania haina wagonjwa wengi .ugonjwa umedhibitiwa sana nchini.na hivi karibun shughuli zote zitaendelea kama kawaida heko rais magufuli.2020 ni magufuli
Mna akili timamu kweli?Mficha maradhi kifo humuumbua!Acheni kucheza na maisha ya watanzania!Eti maambukizi yameacha kusambaa baada ya hotuba ya Rais,shame!
 
... wale 7 waliotangazwa Zanzibar jana sio watanzania? Anyway, basi tangazeni hao wengi wanaopona!
 
Back
Top Bottom